rugumye
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 561
- 178
Wanajamii watu wengi hasa walio kwenye sekta binafsi wanaopenda kuandamana kupinga sheria iliyopitishwa na serikali Mnaombwa kutoa mawzo yenu hapa, ni kupinga sheria ya mifuko ya jamii kukalia michango ya wanachama mpaka wafikishe umri wa miaka 55. Inasadikika kuwa serikali yetu imekopa pesa nyingi kutoka katika mifuko hii kiasi kwamba mifuko imeathirika sana. Ili kuweza kupunguza usumbufu, serikali imelazimika kutunga sheria ili iweze kuchota mipesa hii bila matatizo. kama mipesa ile ya EPA iliyokuwa imetulia pale BOT.
Uzoefu kutoka nchi za wenzetu mifuko hii inawasaidia sana wanachama kwaani wanaweza kukopa kujemgewa nyumba, mikopo ya pesa, na fursa nyingi sana tofauti na hapa Bongo. Mfano mimi nilichangia NSSF kwa miaka 8, lakini pesa niliyopata haikuwa na interest (faida) hata kidogo. Nilichopata ilikuwa jumla ya michango yangu niliyokuwa nimechangia tu huku mifuko ikiwa imewekeza pesa yangu kwenye majengo marefu na miradi mingine mingi. (Ushahidi ninao kama NSSF wakiutaka).
Hivyo tusipo simama wenyewe tusifikiri bunge lina jipya kwaani sheria ilipitishwa na hao hao wabunge.
Wajumbe tunaomba mawazo yenu lini tuandamane juu ya swala hili. kuna watu watatafuta kibari kutoka polisi. Ni maandamano ya amani bila fujo.
KARIBUNI.
Uzoefu kutoka nchi za wenzetu mifuko hii inawasaidia sana wanachama kwaani wanaweza kukopa kujemgewa nyumba, mikopo ya pesa, na fursa nyingi sana tofauti na hapa Bongo. Mfano mimi nilichangia NSSF kwa miaka 8, lakini pesa niliyopata haikuwa na interest (faida) hata kidogo. Nilichopata ilikuwa jumla ya michango yangu niliyokuwa nimechangia tu huku mifuko ikiwa imewekeza pesa yangu kwenye majengo marefu na miradi mingine mingi. (Ushahidi ninao kama NSSF wakiutaka).
Hivyo tusipo simama wenyewe tusifikiri bunge lina jipya kwaani sheria ilipitishwa na hao hao wabunge.
Wajumbe tunaomba mawazo yenu lini tuandamane juu ya swala hili. kuna watu watatafuta kibari kutoka polisi. Ni maandamano ya amani bila fujo.
KARIBUNI.