Maandamano CUF hakuna aliyejeruhiwa!!!!!!!!!!!!!! Ni mchezo wa kuigiza

chidide

Member
Nov 11, 2010
91
9
"Alisema wametumia nguvu za wastani kuwatawanya wana CUF na watu tisa wanashikiliwa na jeshi hilo na hakuna aliyejeruhiwa katika maandamano hayo, na Polisi kupitia Idara yake ya Upelelezi inafuatilia suala hilo ili kuangalia hatua gani itachukua kutokana na kukiukwa kwa amri yao"
Haya maneno ya Kova yananipa wasiwasi. Hivi toka lini polisi wakawa hivi? Washindwe kuzuia maandamano toka buguruni mpaka mjini, wanasindikiza tuu na hakuna mtu aliyejeruhiwa pamoja na polisi kufwatua risasi za moto? Nina wasiwasi hii ni mbinu ya kutaka kuinyanyua tena CUF dhidi ya Chadema. Haiwezekani polisi FFU wawe wanawasindikiza waandanaji, tena nasikia aliyekuwa anatoa matangazo ya polisi alikuwa ni dereva wa polisi, siku zote tunajua huwa ni mkuu wa kikosi cha FFU. Kwangu mimi huu ni mchezo wa kuigiza (Filamu kama magazeti mengi yalivyosema)
 
"Alisema wametumia nguvu za wastani kuwatawanya wana CUF na watu tisa wanashikiliwa na jeshi hilo na hakuna aliyejeruhiwa katika maandamano hayo, na Polisi kupitia Idara yake ya Upelelezi inafuatilia suala hilo ili kuangalia hatua gani itachukua kutokana na kukiukwa kwa amri yao"
Haya maneno ya Kova yananipa wasiwasi. Hivi toka lini polisi wakawa hivi? Washindwe kuzuia maandamano toka buguruni mpaka mjini, wanasindikiza tuu na hakuna mtu aliyejeruhiwa pamoja na polisi kufwatua risasi za moto? Nina wasiwasi hii ni mbinu ya kutaka kuinyanyua tena CUF dhidi ya Chadema. Haiwezekani polisi FFU wawe wanawasindikiza waandanaji, tena nasikia aliyekuwa anatoa matangazo ya polisi alikuwa ni dereva wa polisi, siku zote tunajua huwa ni mkuu wa kikosi cha FFU. Kwangu mimi huu ni mchezo wa kuigiza (Filamu kama magazeti mengi yalivyosema)

Ungefafanua hiyo story ili na wengine tusio na habari ya hayo maandamano tujuwe kilichoendelea.
 
"Alisema wametumia nguvu za wastani kuwatawanya wana CUF na watu tisa wanashikiliwa na jeshi hilo na hakuna aliyejeruhiwa katika maandamano hayo, na Polisi kupitia Idara yake ya Upelelezi inafuatilia suala hilo ili kuangalia hatua gani itachukua kutokana na kukiukwa kwa amri yao"
Haya maneno ya Kova yananipa wasiwasi. Hivi toka lini polisi wakawa hivi? Washindwe kuzuia maandamano toka buguruni mpaka mjini, wanasindikiza tuu na hakuna mtu aliyejeruhiwa pamoja na polisi kufwatua risasi za moto? Nina wasiwasi hii ni mbinu ya kutaka kuinyanyua tena CUF dhidi ya Chadema. Haiwezekani polisi FFU wawe wanawasindikiza waandanaji, tena nasikia aliyekuwa anatoa matangazo ya polisi alikuwa ni dereva wa polisi, siku zote tunajua huwa ni mkuu wa kikosi cha FFU. Kwangu mimi huu ni mchezo wa kuigiza (Filamu kama magazeti mengi yalivyosema)

kaka nakubaliana na wewe..ilikuwa full usanii..
 
Duh! Ukiwaambia ni wageni wa siasa za upinzani watapandisha mizuka sasa hivi!

Hivi lazima kila maandamano watu wafe? Au mlitaka yatokee ya Mwembechai mfurahi na roho zenu?
 
Ila nyinyi mnaokaa kwenye computer na kupepewa na viyoyozi vya serikalini huku mkishabikia Chadema ndiyo hamuwezi kufanya maandamano. Maandamano yanafanywa na watoto wa "Uswahilini" kutoka Manzese, Ilala, Kigogo, Mburahati, Keko, Buguruni, Tandika, Temeke, Mbagala na seheme zingine. Siyo huko kwenye kila baada ya nyumba mbili kuna baa ya kutumbulia pesa za rushwa!
 
kwani ajenda kuu ni ipi na toka lini cuf ilikufa?? Suala la katiba mpya nani kalianzisha? Kudandia treni kwa mbele kuna hatari sana. Waacheni wapambanaji waukweli wafanye kazi.
 
Walikuwa wanawasindikiza na hawakutumia nguvu nyingi hata kama waandamanaji walikuwa hawajaruhusiwa kuandamana kwa kuwa tu kwa sasa CUF ni watawala pamoja na CCM upande wa Zanzibar,hivyo kama wangetumia nguvu nyingi kuwazuia ingeathiri ndoa yao ya utawala.
 
Ila nyinyi mnaokaa kwenye computer na kupepewa na viyoyozi vya serikalini huku mkishabikia Chadema ndiyo hamuwezi kufanya maandamano. Maandamano yanafanywa na watoto wa "Uswahilini" kutoka Manzese, Ilala, Kigogo, Mburahati, Keko, Buguruni, Tandika, Temeke, Mbagala na seheme zingine. Siyo huko kwenye kila baada ya nyumba mbili kuna baa ya kutumbulia pesa za rushwa!

Mbona kina Maalim hawakuwepo? Wao si wapo kwenye ma benz nowdays then wanawatuma watoto wa ilala!!!!
 
...issue hapa ni kwamba, Polisi wakisema maandamano au mkutano wa CDM hayana kibali hivyo yasiwepo angali nguvu inayotumika kuhakikisha hayafanyiki sasa ona ya CUF Kova alisema maandamano hayana kibali na ni batili na watu wasijitokeze sasa ona nini walifanya. Ndio hapo tunaposema CUF inatolewa kwenye wapinzania wa kweli. toka ndoa yao kule zanzibar, CUF kwishnei bana. CCM haiwaogopi CUF hata kidogo ndio maana wakitaka maandamano na mikutano ya wazi watafanya tu maana ni maigizo hayawatishi mafisadi CCM.
 
Najua hili limewachoma sana wana CDM kuona mnazungumza maneno wenzenu wanafanya vitendo. Hivi tuwe wakweli CDM iliwahi wapi kufanya siasa za kutumia umma? Ama ndio mnajaribu, sasa CUF wameonyesha kuwa wao wanatenda hawazungumzi na kuonyesha walivyo ngangari kapewa kijana Mtatiro tu kufanya kazi wakti wake wa CDM wakikimbilia kupeleka hoja binafsi! Mnalo leonu CDM kama hamtaamka, nawaambia tu hata kama Mod na Invisible hapa ni watu wa CDM ambao wataishia kuminya hii thread ama kuni ban. Lakini yote sawa mkifanya naweka jina lingine
 
Kupinga sera mbovu za serikali kwa maandamano ni moja ya njia za kufikisha ujumbe si lazima watu wafe au wajeruhiwe badala ya kuibeza CUF tunapaswa kuwapongeza wanachama wa CUF waliojitokeza, tukumbuke kuwa CCM imeweza kuwanunua Lipumba na Hamadi lakini haitaweza kuwanunua wanachama wa CUF.
 
Haya maandamano ya CUF yamepangwa na Rostam Aziz. Lengo ni kuwafanya wana JF na Watanzania wengine watumie muda mwingi kujadili maandamano na katiba mpya ili wasahao hoja ya haraka na kubwa iliyo mbele yetu -- KUPINGA malipo ya kifisadi ya 185.5 bilioni/- kwa DOWANS. Tayari wanasiasa maarufu wa upinzani wamepigwa STOP na Rostam kupinga suala hili huku wengine wakiwa na kazi maalumu ya kuitisha serikali iilipe DOWANS haraka sana eti ili "kuepusha" hasara zaidi kwa taifa.
 
Najua hili limewachoma sana wana CDM kuona mnazungumza maneno wenzenu wanafanya vitendo. Hivi tuwe wakweli CDM iliwahi wapi kufanya siasa za kutumia umma? Ama ndio mnajaribu, sasa CUF wameonyesha kuwa wao wanatenda hawazungumzi na kuonyesha walivyo ngangari kapewa kijana Mtatiro tu kufanya kazi wakti wake wa CDM wakikimbilia kupeleka hoja binafsi! Mnalo leonu CDM kama hamtaamka, nawaambia tu hata kama Mod na Invisible hapa ni watu wa CDM ambao wataishia kuminya hii thread ama kuni ban. Lakini yote sawa mkifanya naweka jina lingine

Hakun lolote. Ilikuwa ni action movie tu!!!! Hivi unafikiri wangekuwa CDM ndiyo wanafanya maandamano unafikiri police angawaachia hata watoke kwenye hivyo viwanja vya ofisini kwao. Waliwachia kwa vile ni CUF na watu walikuwa wachache. Ngoja CDM siku watakapoandamana uone number za watu zitakavyojitokeza na jinsi gani police watareact.
 
Hakun lolote. Ilikuwa ni action movie tu!!!! Hivi unafikiri wangekuwa CDM ndiyo wanafanya maandamano unafikiri police angawaachia hata watoke kwenye hivyo viwanja vya ofisini kwao. Waliwachia kwa vile ni CUF na watu walikuwa wachache. Ngoja CDM siku watakapoandamana uone number za watu zitakavyojitokeza na jinsi gani police watareact.

CDM hawawezi kufanya maandamano. Hawana uongozi na hawana historia ya kimapinduzi. Mapinduzi hayafanywi ukiwa umekaa kwenye kompyuta na kopo la bia pembeni. Na ndiyo maana CCM wanawaogopa CUF lakini hawasumbuliwi kichwa na CDM. Endeleeni tuu kuamini kwamba mabadiliko yanaletwa na phd.
 
Najua hili limewachoma sana wana CDM kuona mnazungumza maneno wenzenu wanafanya vitendo. Hivi tuwe wakweli CDM iliwahi wapi kufanya siasa za kutumia umma? Ama ndio mnajaribu, sasa CUF wameonyesha kuwa wao wanatenda hawazungumzi na kuonyesha walivyo ngangari kapewa kijana Mtatiro tu kufanya kazi wakti wake wa CDM wakikimbilia kupeleka hoja binafsi! Mnalo leonu CDM kama hamtaamka, nawaambia tu hata kama Mod na Invisible hapa ni watu wa CDM ambao wataishia kuminya hii thread ama kuni ban. Lakini yote sawa mkifanya naweka jina lingine
Hivi CUF hiyo katiba mpya mnaidai kwa CHADEMA?Kama ndio mbona CHADEMA haina dola?Mimi nionavyo kwa ujinga wangu sote CHADEMA,CUF,MREMA,CHEYO,MBATIA,ASKOFU PENGO,MUFTI SIMBA,MZEE MKAPA,MZEE MWINYI,JAJI MSTAAFU KISANGA n.k. Tuunganishe nguvu zetu kwa pamoja kuiandama serikali ya CCM ikubali hili vugu vugu na kutupa katiba mpya,tuweke ubinafsi pengine wa kudai mimi ndio nilianzisha tunahitaji nguvu ya pamoja otherwise watawala watapata mwanya wa kuminya kilio hiki.Pia zipo taarifa za" kung'atwa sikio" kwamba maandamano ya CUF nyuma yake yuko ROSTAM akicheza ngoma ya siasa kujaribu kuwaondoa watanzania kwenye issue moto ya malipo ya DOWANS ambayo mwanasheria mkuu amefunga mjadala wake na kudai serikali itailipa DOWANS.Lakini kama nilivyosema ni taarifa za kung'atwa sikio,hivyo unatakiwa kupima mwenyewe.
 
Jamani wana JF Naomba mnipe majibu ya maswali yangu machache..

1.Hivi huyo Rostam Aziz ana ulinzi wowote (Bodyguards) anavyokuwa kwenye shughuli zake za kawaida hapa jijini? Mimi binfsi sijawahi kumuona mitaani huyu Fisadi..ila nadhani tumemlalamikia vya kutosha na hata mwanasheria mkuu wa serikali katusaidia ku-prove kwamba Dowans ni yake.

2.Pia ningependa kufahamishwa mahali anapokaa (hapa jijini) na sehemu ambazo mara nyingi hupendelea kutembelea.
 
Hivi CUF hiyo katiba mpya mnaidai kwa CHADEMA?Kama ndio mbona CHADEMA haina dola?Mimi nionavyo kwa ujinga wangu sote CHADEMA,CUF,MREMA,CHEYO,MBATIA,ASKOFU PENGO,MUFTI SIMBA,MZEE MKAPA,MZEE MWINYI,JAJI MSTAAFU KISANGA n.k. Tuunganishe nguvu zetu kwa pamoja kuiandama serikali ya CCM ikubali hili vugu vugu na kutupa katiba mpya,tuweke ubinafsi pengine wa kudai mimi ndio nilianzisha tunahitaji nguvu ya pamoja otherwise watawala watapata mwanya wa kuminya kilio hiki.Pia zipo taarifa za" kung'atwa sikio" kwamba maandamano ya CUF nyuma yake yuko ROSTAM akicheza ngoma ya siasa kujaribu kuwaondoa watanzania kwenye issue moto ya malipo ya DOWANS ambayo mwanasheria mkuu amefunga mjadala wake na kudai serikali itailipa DOWANS.Lakini kama nilivyosema ni taarifa za kung'atwa sikio,hivyo unatakiwa kupima mwenyewe.

kaka huyo aliyekung'ata sikio bila shaka ni MBOWE. Wakuu mnasemaje????
 
Kama ulimsoma vizuri maralai Sugu Aka JMK kuwa kama kweli Chadema ni wanaume waandamane tuone, wangekuwa chadema mambo mengi wangezua kwanza wangeanza kuwa.
1. Wangewachonganisha na watz kuwa CDM wanataka kumwaga Damu.
2. Wangeaakikisha watu wanajeruhiwa vibaya na kuonyesha dunia kuwa CDM wakosa ustraabu.
3. Serikali ingeandaa utaratibu wa kukifuta kwa kumshawishi Tendwa kuwa CDM ni Chama cha Kiuni na chenye fujo.
ndio maana CDM inataka kuja na People of Power kuiondoa serikali dhaifu na kuibomoa ngome ya mafisadi wakiongozwa na RA, EL, Cheng na Mkonoo N
 
CDM hawawezi kufanya maandamano. Hawana uongozi na hawana historia ya kimapinduzi. Mapinduzi hayafanywi ukiwa umekaa kwenye kompyuta na kopo la bia pembeni. Na ndiyo maana CCM wanawaogopa CUF lakini hawasumbuliwi kichwa na CDM. Endeleeni tuu kuamini kwamba mabadiliko yanaletwa na phd.

Hakuna lolote Nancy. Tatizo la nchi yetu ni tabaka la wafanyakazi. Wanaelekea kuridhika sana na hivyo vihera wanavyopa vya udokozi. Harakati za mapinduzi popote duniani zimeletwa na wafanyakazi. Lakini TZ itakuwa kinyume. Nafikiri mtu wa social science anaweza kufanya research hapa akatoka na PhD yake kwa hii study ambayo ni tofauti na trend zote duniani ambako mapinduzi ya kweli yamekuwa yakiongozwa na jeshi au vyombo vya wafanyakazi. Si umeona Mgaya mwenyewe kisha ingia mitini.
 
Najua hili limewachoma sana wana CDM kuona mnazungumza maneno wenzenu wanafanya vitendo. Hivi tuwe wakweli CDM iliwahi wapi kufanya siasa za kutumia umma? Ama ndio mnajaribu, sasa CUF wameonyesha kuwa wao wanatenda hawazungumzi na kuonyesha walivyo ngangari kapewa kijana Mtatiro tu kufanya kazi wakti wake wa CDM wakikimbilia kupeleka hoja binafsi! Mnalo leonu CDM kama hamtaamka, nawaambia tu hata kama Mod na Invisible hapa ni watu wa CDM ambao wataishia kuminya hii thread ama kuni ban. Lakini yote sawa mkifanya naweka jina lingine

Huna hoja wewe.kumbe unajibadilisha majina hapa?umeingia lini kuandika hapa.Huku CDM wasomi ni wengi kuliko mbumbumbu na waganga wa kienyeji.

 
Back
Top Bottom