"Alisema wametumia nguvu za wastani kuwatawanya wana CUF na watu tisa wanashikiliwa na jeshi hilo na hakuna aliyejeruhiwa katika maandamano hayo, na Polisi kupitia Idara yake ya Upelelezi inafuatilia suala hilo ili kuangalia hatua gani itachukua kutokana na kukiukwa kwa amri yao"
Haya maneno ya Kova yananipa wasiwasi. Hivi toka lini polisi wakawa hivi? Washindwe kuzuia maandamano toka buguruni mpaka mjini, wanasindikiza tuu na hakuna mtu aliyejeruhiwa pamoja na polisi kufwatua risasi za moto? Nina wasiwasi hii ni mbinu ya kutaka kuinyanyua tena CUF dhidi ya Chadema. Haiwezekani polisi FFU wawe wanawasindikiza waandanaji, tena nasikia aliyekuwa anatoa matangazo ya polisi alikuwa ni dereva wa polisi, siku zote tunajua huwa ni mkuu wa kikosi cha FFU. Kwangu mimi huu ni mchezo wa kuigiza (Filamu kama magazeti mengi yalivyosema)
Haya maneno ya Kova yananipa wasiwasi. Hivi toka lini polisi wakawa hivi? Washindwe kuzuia maandamano toka buguruni mpaka mjini, wanasindikiza tuu na hakuna mtu aliyejeruhiwa pamoja na polisi kufwatua risasi za moto? Nina wasiwasi hii ni mbinu ya kutaka kuinyanyua tena CUF dhidi ya Chadema. Haiwezekani polisi FFU wawe wanawasindikiza waandanaji, tena nasikia aliyekuwa anatoa matangazo ya polisi alikuwa ni dereva wa polisi, siku zote tunajua huwa ni mkuu wa kikosi cha FFU. Kwangu mimi huu ni mchezo wa kuigiza (Filamu kama magazeti mengi yalivyosema)