Elections 2010 Maana ya kampeni - kwa nini nichaguliwe mimi na si mpinzani wangu ?

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,064
22,756
Inaonekana Tume ya Uchaguzi kwa sababu wanazozifahamu wameamua kutoa tafsiri mpya kwa maana ya kampeni ya Uchaguzi. Ninavyoelewa mimi kufanya kampeni ni kujinadi kwa wapiga kura kwa nini wakuchague wewe na si mpinzani wako.

  • Kujinadi kunajumuisha kutaja sifa zako na uwezo wako kwa nini utakuwa kiongozi bora kuliko mpinzani wako na hivyo unastahili kura zao.
  • Kujinadi pia kunajumuisha kutaja mapungufu ya mpinzani wako kwa nini hana sifa ya kuwa kiongozi bora na hivyo hastahili kura yao.
Tume ya Uchaguzi kupitia sheria ya uchaguzi inamtaka mgombea asiongelee mapungufu ya mpinzani wake - ni wapi duniani sheria hii inatambulika na kutumika kwaniinazua maswali mawili;

  • Kwa mtu anayeutafuta uongozi kampeni itafanyika vipi kama sheria inamzuia kutaja kwa nini yeye anafaa zaidi kuliko kiongozi aliyeko madarakani ?
  • Ataelezeaje atakavyotekeleza mambo tofauti kama hakuonyesha mapungufu ya kiutekelezaji na uwezo mdogo wa kiongozi anayetaka kumwondoa ?
Je kuna mambo Tume ya Uchaguzi isingependa wananchi wapiga kura wayafahamu kuhusu utawala wa sasa ? wanachojaribu kuficha ni kitu gani na kwa maslahi ya nani ? Jaji Lewis Makame, huwatendei haki wazalendo wa nchi hii. Je ni dhambi kuwatahadharisha wananchi kuwa mgombea fulani asipewe kura kwa sababu kadhaa ?
 
Back
Top Bottom