Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,756
Inaonekana Tume ya Uchaguzi kwa sababu wanazozifahamu wameamua kutoa tafsiri mpya kwa maana ya kampeni ya Uchaguzi. Ninavyoelewa mimi kufanya kampeni ni kujinadi kwa wapiga kura kwa nini wakuchague wewe na si mpinzani wako.
- Kujinadi kunajumuisha kutaja sifa zako na uwezo wako kwa nini utakuwa kiongozi bora kuliko mpinzani wako na hivyo unastahili kura zao.
- Kujinadi pia kunajumuisha kutaja mapungufu ya mpinzani wako kwa nini hana sifa ya kuwa kiongozi bora na hivyo hastahili kura yao.
- Kwa mtu anayeutafuta uongozi kampeni itafanyika vipi kama sheria inamzuia kutaja kwa nini yeye anafaa zaidi kuliko kiongozi aliyeko madarakani ?
- Ataelezeaje atakavyotekeleza mambo tofauti kama hakuonyesha mapungufu ya kiutekelezaji na uwezo mdogo wa kiongozi anayetaka kumwondoa ?