Maana na tofauti ya "waathirika" na "wahanga"

Katavi

Platinum Member
Aug 31, 2009
41,983
12,701
Haya maneno yana maana sawa? Maana yananitatiza matumizi yake.
 
Kwa kingereza ni Victim and Infected

vic·tim⁠ Noun⁠
1. A person harmed, injured, or killed as a result of a crime, accident, or other event or action.

2.infected⁠(Verb)⁠past participle, past tense of⁠in·fect(Verb)
Affect (a person, organism, cell, etc.) with a disease-causing organism
 
Kuna tofauti kubwa sana kati ya haya maneno mawili: Waathirika na Wahanga! Tatizo lililojitokeza ni kuwa waandishi, watangazaji na baadhi ya viongozi wamekuwa wakiyachanganya haya maneno na kuyatumia bora liende! Yaani wakati mwingine natamani Mzee kifimbo cheza akatembeze bakora kule bungeni!

Wahanga ni watu waliojitolea na mara nyingi wakapoteza maisha yao katika hiyo shughuli (au kitu wao wanachokiamini sana): Mfano kuna wahanga wa mapinduzi ya Zanzibar- wao walijitoa muhanga mpaka hayo mapinduzi yakatokea. Hawakujali uhai au afya zao. Pia Kule msumbiji, Angola, nk wanakuwa na watu wao waiojitolea muhanga kwa nchi yao. Miaka ya karibuni kuna wahanga wa CUF pia, wao waliuwawa kwa imani ya chama chao cha siasa, piia wale wa Mwembechai enzi za Mzee Mkapa, na pia wapo hawa wa juzi kule Arusha! wote hao walijitoa muhanga kwa imani zao/ukereketwa wao.

Kuna yule bwana akiitwa Seti Benjamin (kama sikosei), JK Nyerere alipotangaza Azimio la Arusha, yeye na wenzake walitembea kwa miguu kuunga mkono, yeye akafia njiani-alijitoa muhanga na akawa mhanga!

Waathirika ni kama wale wa mabomu kule gongo la mboto au hawa wa mafuriko! Ni kutoelewa tu ndo kunafanya kila waitwe wahanga! Ila, kama yupo ambaye wakati mabomu yanaanza kulipuka alikimbilia kuyazuia au alijaribu kuokoa watu, na katika mchakato huo akaaga dunia atakuwa ni Mhanga, siyo muathirika.

Muathirika / waathirika ni mtu / watu walioathiriwa ni kitu fulani-mvua, vita, mabomu nk.
 
Kuna tofauti kubwa sana kati ya haya maneno mawili: Waathirika na Wahanga! Tatizo lililojitokeza ni kuwa waandishi, watangazaji na baadhi ya viongozi wamekuwa wakiyachanganya haya maneno na kuyatumia bora liende! Yaani wakati mwingine natamani Mzee kifimbo cheza akatembeze bakora kule bungeni!

Wahanga ni watu waliojitolea na mara nyingi wakapoteza maisha yao katika hiyo shughuli (au kitu wao wanachokiamini sana): Mfano kuna wahanga wa mapinduzi ya Zanzibar- wao walijitoa muhanga mpaka hayo mapinduzi yakatokea. Hawakujali uhai au afya zao. Pia Kule msumbiji, Angola, nk wanakuwa na watu wao waiojitolea muhanga kwa nchi yao. Miaka ya karibuni kuna wahanga wa CUF pia, wao waliuwawa kwa imani ya chama chao cha siasa, piia wale wa Mwembechai enzi za Mzee Mkapa, na pia wapo hawa wa juzi kule Arusha! wote hao walijitoa muhanga kwa imani zao/ukereketwa wao.

Kuna yule bwana akiitwa Seti Benjamin (kama sikosei), JK Nyerere alipotangaza Azimio la Arusha, yeye na wenzake walitembea kwa miguu kuunga mkono, yeye akafia njiani-alijitoa muhanga na akawa mhanga!

Waathirika ni kama wale wa mabomu kule gongo la mboto au hawa wa mafuriko! Ni kutoelewa tu ndo kunafanya kila waitwe wahanga! Ila, kama yupo ambaye wakati mabomu yanaanza kulipuka alikimbilia kuyazuia au alijaribu kuokoa watu, na katika mchakato huo akaaga dunia atakuwa ni Mhanga, siyo muathirika.

Muathirika / waathirika ni mtu / watu walioathiriwa ni kitu fulani-mvua, vita, mabomu nk.

Makes sense, muhanga= mtu aliyejitola muhanga.
 
1. wahanga, waathirika wa moja kwa moja
2. waathirika inajumuisha wale wa moja kwa moja na wassio wa moja kwa moja

mfano,

wahanga wa mafuriko ni waliokosa makazi, waliofariki kwa kuzolewa na mafuriko nk. lakini waathirika wa mafuriko ni wale waliopoteza makzi, maisha, mali zao nk pamoja na waliochelewa kufika majumbani au makazini kwao kwa sababu ya mafuriko kukata mawasiliano na wengine wote waliothirika kwa namna moja ama nyingine
 
1. wahanga, waathirika wa moja kwa moja
2. waathirika inajumuisha wale wa moja kwa moja na wassio wa moja kwa moja

mfano,

wahanga wa mafuriko ni waliokosa makazi, waliofariki kwa kuzolewa na mafuriko nk. lakini waathirika wa mafuriko ni wale waliopoteza maisha, mali zao nk pamoja na waliochelewa kufika majumbani au makazini kwao kwa sababu ya mafuriko kukata mawasiliano na wengine wote waliothirika kwa namna moja ama nyingine
Mkuu, hapo nyekundu. kufariki na kupoteza maisha, tafauti iko wapi?
 
Kuna tofauti kubwa sana kati ya haya maneno mawili: Waathirika na Wahanga! Tatizo lililojitokeza ni kuwa waandishi, watangazaji na baadhi ya viongozi wamekuwa wakiyachanganya haya maneno na kuyatumia bora liende! Yaani wakati mwingine natamani Mzee kifimbo cheza akatembeze bakora kule bungeni!

Wahanga ni watu waliojitolea na mara nyingi wakapoteza maisha yao katika hiyo shughuli (au kitu wao wanachokiamini sana): Mfano kuna wahanga wa mapinduzi ya Zanzibar- wao walijitoa muhanga mpaka hayo mapinduzi yakatokea. Hawakujali uhai au afya zao. Pia Kule msumbiji, Angola, nk wanakuwa na watu wao waiojitolea muhanga kwa nchi yao. Miaka ya karibuni kuna wahanga wa CUF pia, wao waliuwawa kwa imani ya chama chao cha siasa, piia wale wa Mwembechai enzi za Mzee Mkapa, na pia wapo hawa wa juzi kule Arusha! wote hao walijitoa muhanga kwa imani zao/ukereketwa wao.

Kuna yule bwana akiitwa Seti Benjamin (kama sikosei), JK Nyerere alipotangaza Azimio la Arusha, yeye na wenzake walitembea kwa miguu kuunga mkono, yeye akafia njiani-alijitoa muhanga na akawa mhanga!

Waathirika ni kama wale wa mabomu kule gongo la mboto au hawa wa mafuriko! Ni kutoelewa tu ndo kunafanya kila waitwe wahanga! Ila, kama yupo ambaye wakati mabomu yanaanza kulipuka alikimbilia kuyazuia au alijaribu kuokoa watu, na katika mchakato huo akaaga dunia atakuwa ni Mhanga, siyo muathirika.

Muathirika / waathirika ni mtu / watu walioathiriwa ni kitu fulani-mvua, vita, mabomu nk.
Maelezo yako yanakubalika kabisa. labda kwa kuongezea tu ni kuwa
Hatma ya Mhanga wa tukio au maafa ni kifo, lakini lazima awepo wakati wa tukio, na hatma ya Mwathirika wa tukio, maafa au ugonjwa huwa yupo hai, amekumbwa na tukio, maafa au ugonjwa. Tukumbuke pia mwathirika si lazima awepo kwenye tukio na mwathirika wa ugonjwa anaweza kufariki lakini hawezi kuwa mhanga isipokuwa kama ulivyosema hapo juu, awe amepoteza maisha katika kuwaokoa wengine.
 
1. wahanga, waathirika wa moja kwa moja
2. waathirika inajumuisha wale wa moja kwa moja na wassio wa moja kwa moja

mfano,

wahanga wa mafuriko ni waliokosa makazi, waliofariki kwa kuzolewa na mafuriko nk. lakini waathirika wa mafuriko ni wale waliopoteza makzi, maisha, mali zao nk pamoja na waliochelewa kufika majumbani au makazini kwao kwa sababu ya mafuriko kukata mawasiliano na wengine wote waliothirika kwa namna moja ama nyingine

Mkuu nadhani unachanganya kidogo hapo vitu viwili.

Mtu akiwa ameathiriwa na kitu fulani bado anaweza akapoteza maisha. Ndiyo maana wagonjwa wa ukimwi tunawaita waathirika ambao baada ya muda huwa wanapoteza maisha yao baada ya hivyo virusi kuwaathiri na kukosa kinga ya mwili. Je hawa nao utawita wahanga wa ukimwi, ati kwa sababu wamepoteza maisha yao? Jib u la haraka ni hapana, ila waliathirika hadi wakapoteza maisha yao! Wagonjwa wa maleria au TB nao ni hivyo hivyo tutawaita waathirika na wanapoaga dunia wanabakia kuwa waathirika waliopoteza maisha yao kwa huo ugonjwa. Kama ni waathirika wa ajali ya gari nao ni hivyo hivyo, au hawa wa mafuriko hata wakiaga dunia wanakuwa ni waathirika waliofikwa na mauti.

Pia ukumbuke kuwa kujitoa Muhanga siyo lazima huyo mtu apoteze maisha yake. Watu kama akina Kimaro (miaka ya mzee Ruksa Chuo kikuu), waligoma na katika uongozi wao na msimamo wao mkali dhidi ya serikali walijitoa muhanga, hadi wakafukuzwa chuo kikuu.

Yaani muathirika au waathirika linatokana na neno athari.


Mtu aliyejitoa Muhanga anakuwa Muhanga / Mhanga. . Huyu anakuwa ama alikuwa anatetea kitu fulani au anasisitizia kitu fulani hadi kufa kwake au hadi afukuzwe chuo au aadhibiwe.
 
choveki nashukuru kwa ufafanuzi huu maana nilikuwa najiuliza nini maana ya mhanga na manusuru (kama linavyotumika hivi sasa). Kwa hiyo manusuru ndio waathirika? Na victim ndio mhanga. Kwa hiyo pia wale waokoaji wa manusuru wa mafuriko ndio wahanga?
 
Muhanga ni aina ya mnyama ambaye aghalabu huishi chini ya ardhi. Makazi yake ni kwenye vichuguu au mashimo ambayo tayari yameshachimbwa na nyoka. Kitendo chake cha kuvamia makazi ambayo tayari yametengenezwa na wanyama wengine ndicho kilichopelekea kuzaliwa kwa sentensi ''kujitoa muhanga''. Kwahiyo mtu anayejitoa muhanga ni yule ambaye yupo tayari, hata ikibidi, kutoa uhai wake ili afanikishe adhma yake.
Baadaye nitawaelezea chanzo cha neno 'muathirika'
 
Back
Top Bottom