Nyepesi nyepesi zinazojiri kutoka NEC ya CCM Dodoma jana Spika Samwel Sitta kawekwa mtu kati kwa namna anavyolipeleka Bunge mpera mpera.
Miongoni mwa wachangiaji waliomshambulia wazi wazi ni Mwenyekiti wa CCM Shinyanga ambae bila kumung'unya maneno alimwambia Sitta alirudishe kadi ya CCM. Kwa ujumla wachangiaji wengi wameonyeshwa kutoridhiswa na utendaji wa Sitta isipokuwa wawili tu Eng Stellah Manyanya na Mh John Shibuda.
Chungu kimefunikwa na kikao kinaendelea leo ambapo tusishangae kusikia Sitta kasitishwa U-Spika.
Stay tuned...
MHH kama hawa jamaa wanaona Sitta anafanya vibaya kule Dom na kukibeba chama cha kijani kwa sana bado hawataki wanataka awape tonge mdomoni? Lakini si kosa lao kosa ni chama hicho kutokuwa na wasomi wenye vision kwani kama umesoma lakini elimu uliyonayo haikusaidii means hukusoma.
Wacha tuone mwishowake.