Maamuzi magumu: The biggest joke of the century

Kwanza naungana na mjumbe aliyetangulia hapo juu Sn2139 kuwa kwa siku mbili tatu zilizopita umejishushia heshima mbele ya members wengi waliokuwa wanakuheshimu nikinukuu swali lako moja ulilomuuliza Slaa 'Kabla ya wewe kukuita fisadi tuambie huo mshahara wako kweli unatoa kodi kama si fisadi ni nani' tuachane na hayo.

Nampongeza sana Mh.Lowassa kwa kuwaonyesha wabunge wenzake na watanzania kuwa si lazima kila siku kuipongeza serikali kuna wakati inatakiwa kukosolewa inapokwenda kinyume na kikosoa si kuwa umekuwa mpinzani. Kwenye maelezo yako umesema Lowassa alisema maamuzi magumu ni pamoja na kutafuta madeni zaidi nafikiri hiyo sentensi si ya Lowassa ni yako mzee sijawahi kuisikia kutoka kinywani mwa Lowassa.

Ukisoma vizuri ujumbe wako sehemu nyingi unailaumu serikali kwa kutotekeleza wajibu wake umesema haina cha kuonyesha, umeme hakuna ukusanyaji kodi umeoza lakini cha ajabu unaishia kumlaumu Lowassa kana kwamba yeye bado yuko madarakani unashindwa sijui kama ni technical kuwa pin point wahusika wakuu wanaosababisha hayo yote.

Lengo lako lilikuwa kuonyesha Lowassa amekosea aliposema serikali inashindwa kufanya maamuzi magumu lakini umeshindwa kujenga hoja na matokeo yake umeanza kumvika Lowassa matatizo ya serikali kana kwamba yeye ndiye ameyasababisha ili kufikia malengo yako yaliyoshindwa ya kumlaumu Lowassa. Binafsi nilipoona heading 'Maamuzi magumu the biggest joke' nikadhani unaongelea ugumu wa CCM kujivua gamba kuwa ni joke of the Century.

- Kasome tena hotuba ya Lowassa mkuu, huwa hatukurupuki!

Willie @ NYC, USA.
 
Dogo, tatizo lako unachanganya chuki zako pamoja na hisia zako za ovyo, na hapo ndipo unaposhindwa hata kabla ya kuanza.
umeonyesha kiwango kikubwa cha kutokuwa na akili, huu ni grade A upupu.
Babako Malecela hakuwa na akili, na wewe umeamua kumuunga mkono kwa kutokuwa na akili. Hiki ni kilio tosha ndani ya familia yenu

- Ndio uzuri wa Demokrasia, kila mwananchi anaruhusiwa kutoa maoni yake regardless ya tija yake wka taifa, maana ni haki yake kusema anything! ha! ha! ah!, I love it!

Willie @ NYC, USA.
 
Katika kipindi hiki cha miaka 6 sasa, nawachukulia watu wawili kama HEROS: Dr. Slaa na Lowassa.

1. Dr. Slaa
Huyu amekuwa na ujasiri wa kipekee, pengine hata kuhatarisha maisha yake kwa kuanika ni jinsi gani Tanzania imegeuzwa kuwa shamba la bibi. lakini kubwa sana kwa matendo yake na ujasiri wake, amewapa watanzania ufunuo na ujasiri wa kukabiliana (walau kwa sauti) na utawala wa mbovu na usiofuata sheria wala kutii haki za binadamu. Utawala huu umetumia CCM kama BRAND NAME lakini hauna uhusiano wowote na CCM (chama cha wakulima na wafanyakazi)

2. Lowassa
Huyu ame-demonstrate in practicle terms everything wrong in the current governance system. Na kupitia bunge ameweka wazi how Boys II Men system functions - you just do it potelea mbali. i.e umeme uwake usiwake lakini Richmond must get the contract, rada must be bought, BOT must release the amounts we want, tutajenga majengo kila kata na kuyaita shule walimu wawepo wasiwepo that is someone else's problem, bungeni hatuhitaji spika tunataka 'mwanamama' na ili kupata ndiyoooo za kutosha tutatumia fursa ya viti maalum na kuweka 'watu wetu'

Mh. Pinda can rants all he likes but Lowassa rules! Na kwa maoni yangu, kwa Pinda anaweza kuwa the most disfunctional leader katika mustakabali wa ccm na taifa. Sijui ni tricks gani amefanya au sijui ni maneno gani alisema kwenye 'semina elekezi' lakini chini ya uongozi wake amewanyamazisha wabunge wote wa ccm na kwa ushiriakano wa karibu na 'mwanamama/spika' ameguza bunge kuwa taasisi ya serikali.

Demokrasia in reverse!
 
Kwangu mimi CCM chairman and MPS ndio the biggest joke of the century; First: pale Lowassa anapomkebehi yeye na serikali yake na bado hana chakumfanya. 2.Pale MPS wanapomsafisha Chenge mchana kweupe ili hali kesi ya Rada iko wazi. 3. Wanapopoteza resources and energy kwenye propaganda ya kujivua gamba wakati wanajua haiwezekani and the list goes on

- Strong!; SALUTE!

Willie @ NYC, USA.
 
William, i agree with you... Maamuzi magumu has been the biggest joke of our government this year

kusema ukweli hata ile tu kumuacha EL, RA na AC kwenye bunge ni ishara tosha kwamba serikali yetu ilifanya maamuzi magumu sana kkuwaachia, pia serikali imeendelea kufanya maamuzi magumu sana ya kuendelea kunyonya maskini kwa kusamehe kodi kwa matajiri na wawekezaje wezi kama barrick
 
Kituko kingine ni cha jana Andrew Chenge anasafishwa na Waziri wa Utawala Bora, Tundu Lissu anasoma barua yenye ushahidi, Wabunge wote wa CCM wanapiga kura ya Sioooooooooo! Lowassa yupo sahihi, Kikwete hawezi wala hana ubavu wa kufanya maauzi magumu. AAnze na Chenge basi kama Lowassa ni kisiki cha mpingo. Sometimes huwa natamani kuukana uraia wa Tanzania kwa sababu mambo yanayofanyika hpa hayawezi kufanywa kokote kule duniani. Natoa wito CCM ama wawatose hao mapacha watatu au wanyamaze milele na kukubali kuitwa mafisadi
 
Katika kipindi hiki cha miaka 6 sasa, nawachukulia watu wawili kama HEROS: Dr. Slaa na Lowassa.

1. Dr. Slaa
Huyu amekuwa na ujasiri wa kipekee, pengine hata kuhatarisha maisha yake kwa kuanika ni jinsi gani Tanzania imegeuzwa kuwa shamba la bibi. lakini kubwa sana kwa matendo yake na ujasiri wake, amewapa watanzania ufunuo na ujasiri wa kukabiliana (walau kwa sauti) na utawala wa mbovu na usiofuata sheria wala kutii haki za binadamu. Utawala huu umetumia CCM kama BRAND NAME lakini hauna uhusiano wowote na CCM (chama cha wakulima na wafanyakazi)

2. Lowassa
Huyu ame-demonstrate in practicle terms everything wrong in the current governance system. Na kupitia bunge ameweka wazi how Boys II Men system functions - you just do it potelea mbali. i.e umeme uwake usiwake lakini Richmond must get the contract, rada must be bought, BOT must release the amounts we want, tutajenga majengo kila kata na kuyaita shule walimu wawepo wasiwepo that is someone else's problem, bungeni hatuhitaji spika tunataka 'mwanamama' na ili kupata ndiyoooo za kutosha tutatumia fursa ya viti maalum na kuweka 'watu wetu'

Mh. Pinda can rants all he likes but Lowassa rules! Na kwa maoni yangu, kwa Pinda anaweza kuwa the most disfunctional leader katika mustakabali wa ccm na taifa. Sijui ni tricks gani amefanya au sijui ni maneno gani alisema kwenye 'semina elekezi' lakini chini ya uongozi wake amewanyamazisha wabunge wote wa ccm na kwa ushiriakano wa karibu na 'mwanamama/spika' ameguza bunge kuwa taasisi ya serikali.

Demokrasia in reverse!

- Maneno mazito sana hayo mkuu!, ya CCM as a brand name ninaamini wahusika wameyasikia!

Willie @ NYC, USA
 
FACEBOOK: by William Malecela on Tuesday, July 5, 2011 at 8:40pm[/h]

The biggest political joke this week, ilikuwa ni ushauri wa maamuzi magumu kwa Serikali kwa Kiongozi aliyetuingiza taifa hasara ya USD $ 170 Million kwa ajili ya umeme wa dharura wa Megawati 100 ambao haupo. Sasa cha ajabu sana ni wananchi na baadhi ya Wabunge wa CCM waliosimama na kumshangilia sana, ninasema hawa wote tunahitaji kuwakamata na kuwachapa bakora sana, kama Mwalimu alivyokuwa akiwafanyia maviongozi magoi goi kule Ikulu zamani. I mean what happened to this Nation? Tumelogwa na nani hasa? Hili taifa kama ni maamuzi magumu tunatakiwa kuyafanya kwa kusimamia Sheria kwanza, ambako ndiko hasa kwenye ubovu na huyu Kiongozi akiwa ni mfano hai wa hilo la kutoheshimu sheria!

- Kutoheshimu sheria sasa kumetufikisha mahali ripoti ya W/B inasema 20% ya bajeti yetu kila mwaka inaishia kwenye Rushwa, mfano mwingine kati ya kesi 10,000 zilizofikishwa Takukuru toka ianzishwe ni 5% tu zilizofikishwa kwenye Sheria, zingine zimeishia hewani kwa sababu ya Rushwa, Wakulima wetu wa Mbao hishia kupata only 5% ya kilimo chao huku 95% zikienda kwa Viongozi wa juu na makampuni husika kupitia Rushwa. Mh. Lowassa anasema maamuzi magumu ni pamoja na kutafuta madeni zaidi, huku akijua wazi kwamba toka ashike madaraka ya juu mpaka leo, deni la taifa limeongezeka kwa kasi kubwa sana kutoka USD $ 6.1 Billion mpaka sasa USD $ 10.2 Billion, huku Serikali ikiwa haina cha maana cha kuonyesha na hasa umeme ambao aliufanyia maamuzi magumu. Huko kwenye ukusanyaji kodi ndio kabisaa kumeoza, kila mwaka TRA wanashindwa kukusanya Shillingi Billion 100 kwa sababu ya Rushwa, matokeo ni kuongezeka kwa inflation 8%!

Masikini ya Mungu hili taifa nani atatuokoa? maana hakuna wa kumsaidia mwingine I mean haiwezekani binadam akashindwa kuona na kufikiri pia, kwamba what Mh. Lowassa said is the biggest political joke of all our times na the saddest thing kuna waliomshangilia, dawa ni kukamata wote na kuchapa viboko mbele ya gademu public!

- Tanzania; maamuzi magumu yaanzie kwenye utawala unaoheshimu sheria kwanza!

Mungu Aibariki Tanzania!


William Malecela @ NYC, USA.

Inaonekana mheshimiwa umekerwa vilivyo na matukio ya hivi karibuni kuhusu suala la maamuzi magumu. Mimi sioni ajabu kwa wabunge wa CCM wakiwemo wale tunaodhani kuwa ni wasomi kumshangilia Lowassa kwa yale aliyoyasema bungeni. Kwanza ni kwa sababu ya utamaduni wa CCM wa "ndiyo mzee" ambapo kila kinachosemwa na viongozi na wana CCM wengine hata kama ni utumbo basi kwa utamaduni wao watashangilia na kurukaruka kama mazuzu. Pili ni kutokana na ukweli kuwa CCM ya sasa haina itikadi, dira wala sera (sera zao zote wanacopy za W/B na IMF). Wamekuwa wakihubiri "ujamaa na kujitegemea" kwa nadharia na maandiko yao lakini wanafanya wizi na ufisadi kwa vitendo. Baya zaidi ni kuwa CCM siyo chama kimoja tena bali ni genge la maslahi lenye watu waliojiunga na wanaoendelea kuwemo ndani ya chama kwa maslahi binafsi zaidi kuliko yale ya Taifa. Kwa sasa CCM imegawanyika katika makundi kinzani ambayo kila moja lina malengo yake na Lowassa ni mmoja wa vigogo wa kundi ambalo, kabla halijaparaganyika, lilifanikiwa kumweka madarakani mtu mwenye mamlaka ya kufanya maamuzi magumu zaidi katika nchi

Ni kwenye CCM pekee unapoweza ukakuta maprofesa, wasomi wa ngazi ya PHd, walioghushi vyeti vya elimu, wafanyabiashara, wachungaji, wauza madawa ya kulevya, wezi, wasiokuwa na shughuli maalumu, wakulima (ambao siku hizi wamepungua sana) na wafanyakazi wakiendesha vikao vyao vya juu vya chama bila mgongano wa mawazo, fikra wala itikadi. Zaidi wanakuwa wakirukaruka kushangilia kila linalosemwa na viongozi utadhani ni mazuzu ambao wamepeleka bongo zao kwenye likizo. Kimsingi kinachoendelea CCM ni usanii na unafiki wa kumtumikia kafiri upate ujira wako. Kwa ufupi ningeshangaa sana kama wabunge wa CCM wasingeshangilia aliyokuwa akisema Lowassa kuhusu maamuzi magumu. Kama ni suala la taifa zima kulogwa basi mchawi wetu ana jina lenye herufi tatu na mavazi yake ni ya njano na kijani.

Mimi nakubaliana na Lowassa kuwa moja ya VIASHIRIA vya matatizo ya nchi hii ni uzito wa kufanya maamuzi magumu yenye kuzingatia maslahi ya taifa kwa wakati. Nachelea kuamini kuwa maamuzi yote kuhusu Richmond yalifanywa na Lowassa peke yake kwa nafasi yake kama waziri mkuu bila kumshirikisha na wala kupata baraka za mwenyekiti wa baraza la mawazi. Na huwa ninajiuliza sana kwa nini Dr. Mwakyembe hakutaka kumhoji Lowassa kwenye kamati yao? Ni nini hasa alikuwa anataka kuficha? Je alipokiri kuwa alificha baadhi ya mambo kuiokoa serikali alimaanisha nini?

Nimetumia neno VIASHIRIA kwa sababu kwa mtazamo wangu kutokufanya maamuzi kunaashiria kuwepo tatizo kubwa zaidi ambalo moja ya athari zake ni hili la maamuzi magumu. Kwa mtazamo wangu hata kamati ya Bunge chini Dr. Mwakyembe ilishindwa kufanya maamuzi magumu walipoamua kwa makusudi kabisa kuficha baadhi ya mambo kwenye ripoti yao ili kulinda heshima ya serikali iliyopo madarakani. Hii maana yake ni kuwa hata Bunge chini ya Samuel Sitta lilishindwa kufanya maamuzi magumu kwenye sakata la Richmond kuanzia kwenye ripoti ya kamati mpaka kumaliza mjadala. Hivyo bunge ni sehemu ya ufisadi wa Richmond. Tusipotibu chanzo hata tukiwachapa viboko hawa wabunge kama unavyoshauri haitasaidia. Viboko vinavyowafaa hawa ni kubwagwa kwenye uchaguzi na kupelekwa mahakamani kujibu tuhuma dhidi yao.

Mimi naona tatizo letu siyo la mtu mmoja mmoja bali ni la kimfumo zaidi na linaanzia kwenye Katiba ambayo kimsingi imegeuza nchi kuwa kama duka la mtu binafsi. Kwa mujibu wa Katiba yetu ya sasa maamuzi yote magumu nchi hii yanapaswa kufanywa na mtu mmoja ambaye ni rais. Kama rais hatanyi maamuzi hakuna jinsi ya kumlazimisha kisheria kuyafanya. Ndio maana mpaka leo hii Hosea bado ni mkuu wa TAKUKURU pamoja na kuwa Bunge lilishauri achukuliwe hatua kwa kificha ufisadi wa Richmond. Kwa nini? Kwa sababu aliyemteuwa hajaamua kumuondoa na hakuna yeyote, hata kama ni Bunge, anayeweza kumlazimisha kufanya hivyo. Kwa mujibu wa katiba yetu raisi ni mfalme (imperial president) ambaye ana nguvu zaidi ya alizo nazo malkia wa uingereza. Yeye ni mkuu wa serikali na taasisi zake zote ndani na nje ya nchi, mkuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, sehemu ya bunge tena yenye nguvu zaidi, na mkuu wa mahakama.

Kinachotakiwa sasa ni watanzania wote na hasa wasomi washiriki kikamilifu kuhakikisha kuwa tunapata katiba ambayo itamuondolea rais ufalme abaki kuwa mtumishi wa watu na baada ya hapo tuimarishe vyombo vingine vya dola kama mahakama na bunge ili viwe huru kuisimamia serikali bila ya kuogopa kushughulikiwa na huyu mfalme wetu. Katiba hii pia itatoa fursa sawa kwa vyama vyote vya siasa ili wananchi wawe na nguvu za kuondoa madarakani chama kinachoshindwa kufanya maamuzi magumu kwa maslahi ya nchi kama tunavyoona sasa.
 
Inaonekana mheshimiwa umekerwa vilivyo na matukio ya hivi karibuni kuhusu suala la maamuzi magumu. Mimi sioni ajabu kwa wabunge wa CCM wakiwemo wale tunaodhani kuwa ni wasomi kumshangilia Lowassa kwa yale aliyoyasema bungeni. Kwanza ni kwa sababu ya utamaduni wa CCM wa "ndiyo mzee" ambapo kila kinachosemwa na viongozi na wana CCM wengine hata kama ni utumbo basi kwa utamaduni wao watashangilia na kurukaruka kama mazuzu. Pili ni kutokana na ukweli kuwa CCM ya sasa haina itikadi, dira wala sera (sera zao zote wanacopy za W/B na IMF). Wamekuwa wakihubiri "ujamaa na kujitegemea" kwa nadharia na maandiko yao lakini wanafanya wizi na ufisadi kwa vitendo. Baya zaidi ni kuwa CCM siyo chama kimoja tena bali ni genge la maslahi lenye watu waliojiunga na wanaoendelea kuwemo ndani ya chama kwa maslahi binafsi zaidi kuliko yale ya Taifa. Kwa sasa CCM imegawanyika katika makundi kinzani ambayo kila moja lina malengo yake na Lowassa ni mmoja wa vigogo wa kundi ambalo, kabla halijaparaganyika, lilifanikiwa kumweka madarakani mtu mwenye mamlaka ya kufanya maamuzi magumu zaidi katika nchi

Ni kwenye CCM pekee unapoweza ukakuta maprofesa, wasomi wa ngazi ya PHd, walioghushi vyeti vya elimu, wafanyabiashara, wachungaji, wauza madawa ya kulevya, wezi, wasiokuwa na shughuli maalumu, wakulima (ambao siku hizi wamepungua sana) na wafanyakazi wakiendesha vikao vyao vya juu vya chama bila mgongano wa mawazo, fikra wala itikadi. Zaidi wanakuwa wakirukaruka kushangilia kila linalosemwa na viongozi utadhani ni mazuzu ambao wamepeleka bongo zao kwenye likizo. Kimsingi kinachoendelea CCM ni usanii na unafiki wa kumtumikia kafiri upate ujira wako. Kwa ufupi ningeshangaa sana kama wabunge wa CCM wasingeshangilia aliyokuwa akisema Lowassa kuhusu maamuzi magumu. Kama ni suala la taifa zima kulogwa basi mchawi wetu ana jina lenye herufi tatu na mavazi yake ni ya njano na kijani.

Mimi nakubaliana na Lowassa kuwa moja ya VIASHIRIA vya matatizo ya nchi hii ni uzito wa kufanya maamuzi magumu yenye kuzingatia maslahi ya taifa kwa wakati. Nachelea kuamini kuwa maamuzi yote kuhusu Richmond yalifanywa na Lowassa peke yake kwa nafasi yake kama waziri mkuu bila kumshirikisha na wala kupata baraka za mwenyekiti wa baraza la mawazi. Na huwa ninajiuliza sana kwa nini Dr. Mwakyembe hakutaka kumhoji Lowassa kwenye kamati yao? Ni nini hasa alikuwa anataka kuficha? Je alipokiri kuwa alificha baadhi ya mambo kuiokoa serikali alimaanisha nini?

Nimetumia neno VIASHIRIA kwa sababu kwa mtazamo wangu kutokufanya maamuzi kunaashiria kuwepo tatizo kubwa zaidi ambalo moja ya athari zake ni hili la maamuzi magumu. Kwa mtazamo wangu hata kamati ya Bunge chini Dr. Mwakyembe ilishindwa kufanya maamuzi magumu walipoamua kwa makusudi kabisa kuficha baadhi ya mambo kwenye ripoti yao ili kulinda heshima ya serikali iliyopo madarakani. Hii maana yake ni kuwa hata Bunge chini ya Samuel Sitta lilishindwa kufanya maamuzi magumu kwenye sakata la Richmond kuanzia kwenye ripoti ya kamati mpaka kumaliza mjadala. Hivyo bunge ni sehemu ya ufisadi wa Richmond. Tusipotibu chanzo hata tukiwachapa viboko hawa wabunge kama unavyoshauri haitasaidia. Viboko vinavyowafaa hawa ni kubwagwa kwenye uchaguzi na kupelekwa mahakamani kujibu tuhuma dhidi yao.

Mimi naona tatizo letu siyo la mtu mmoja mmoja bali ni la kimfumo zaidi na linaanzia kwenye Katiba ambayo kimsingi imegeuza nchi kuwa kama duka la mtu binafsi. Kwa mujibu wa Katiba yetu ya sasa maamuzi yote magumu nchi hii yanapaswa kufanywa na mtu mmoja ambaye ni rais. Kama rais hatanyi maamuzi hakuna jinsi ya kumlazimisha kisheria kuyafanya. Ndio maana mpaka leo hii Hosea bado ni mkuu wa TAKUKURU pamoja na kuwa Bunge lilishauri achukuliwe hatua kwa kificha ufisadi wa Richmond. Kwa nini? Kwa sababu aliyemteuwa hajaamua kumuondoa na hakuna yeyote, hata kama ni Bunge, anayeweza kumlazimisha kufanya hivyo. Kwa mujibu wa katiba yetu raisi ni mfalme (imperial president) ambaye ana nguvu zaidi ya alizo nazo malkia wa uingereza. Yeye ni mkuu wa serikali na taasisi zake zote ndani na nje ya nchi, mkuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, sehemu ya bunge tena yenye nguvu zaidi, na mkuu wa mahakama.

Kinachotakiwa sasa ni watanzania wote na hasa wasomi washiriki kikamilifu kuhakikisha kuwa tunapata katiba ambayo itamuondolea rais ufalme abaki kuwa mtumishi wa watu na baada ya hapo tuimarishe vyombo vingine vya dola kama mahakama na bunge ili viwe huru kuisimamia serikali bila ya kuogopa kushughulikiwa na huyu mfalme wetu. Katiba hii pia itatoa fursa sawa kwa vyama vyote vya siasa ili wananchi wawe na nguvu za kuondoa madarakani chama kinachoshindwa kufanya maamuzi magumu kwa maslahi ya nchi kama tunavyoona sasa.

- Agreed 100%!, SALUTE!

Willie @ NYC, USA.
 
Tanzania; maamuzi magumu yaanzie kwenye utawala unaoheshimu sheria kwanza

Ndio, lakini hii ya utawala inasumbua kwani iko vacuum ya uongozi. Naamini kwamba after the passing on of Mwalimu (RIP), tatizo la UONGOZI BORA limekuwa hadi kufikia chronic proportions.
Kwa hiyo licha ya issues za law and order, WATANZANIA WANATAKIWA WAFANYE UAMUZI MGUMU kuondokana na mfumo uliofikisha nchi hapa ilipo. Sote tunajua pia tunahitaji KATIBA mpya na yatakayokuwa ndani ni pamoja na sheria hizo hizo za law and order pamoja na good governance.

Haitawezekana kutumia akili za hao hao waliotufikisha hapa kuondokana na upuuzi na matatizo waliyosababisha wao. Never!
 
Dogo, tatizo lako unachanganya chuki zako pamoja na hisia zako za ovyo, na hapo ndipo unaposhindwa hata kabla ya kuanza.
umeonyesha kiwango kikubwa cha kutokuwa na akili, huu ni grade A upupu.
Babako Malecela hakuwa na akili, na wewe umeamua kumuunga mkono kwa kutokuwa na akili. Hiki ni kilio tosha ndani ya familia yenu
.
Sidhani kama kichwa yako itakuwa sawa,sidhani,bado sidhani.
 
Taifa hili linaelekea pazuri...km kaka William,ambaye kwa namna moja ama nyingine CCM imekusababisha usimame ulipo ama kukutengenezea njia,ama combination ya vyote hivyo na sasa umeanza kuikinai,vipi ambao maisha yao na ndoto zao zimeingia kichakani km si mwituni kabisa kwa sababu ya CCM hiyo hiyo..

Lowasa ni mkosaji,tena sana,lakini kuna facts za kuangalia hapa! kwamba wakati akifanya huo "uhalifu" (km unavyoonekana na wengi wanaoaminishwa hivyo" alikua chini ya mamlaka!..Well,tumesikia mengi yakisemwa na mengine hisia zetu zinztupeleka kuamini kua kuna mtu zaidi ya Lowasa nyuma ya yote na ndio maana mhalifu huyu atabakia Innocent kwa kua ili awe na hatia inabidi itifaki iwekwe kando na sheria na kanuni zitumike kushughulikia wote...Yes!

Kwa kua nchi hii hakuna sheria,(msiniulize kwanini?) na kila mtu anajiamulia kufanya atakalo basi kaka William ni kosa kama makosa mengine kufanya watu wengine kukuunga mkono kwenye chuki binafsi ama personal interests! Nafikiri bwana Lowasa ataendelea kua tu mhalifu asiye na hatia hadi pale sheria sitakapoanza kutumika na mamlaka husika kutokua taasisi za watu binafsi na kutofanya kazi kwa shinikizo la vyama vya siasa!
 
Jambo la msingi lililopo ni kuondoa hii system nzima ya magamba maana kwa vyovyote iwavyo wao kama wao hawatakubali kukata tawi walilolikalia. CCM kama chama au taasisi wanafaidika sana na hii hali na kamwe hawatakubali kuachana nayo.
Katiba mpya moto wake unakwenda ukififia watu wamekwishaanza kusahau,tunahitajika wanajamii kila siku na kila wakati tunapopata fursa tudai katiba mpya na hili ndilo litakuwa ni jibu la matatizo yetu kama nchi.
 
GreatThinkers,

Kwanza naomba nikupongeze sana sana Willie, Sikuwahi kuwa ktk rithym moja na wewe, mara nyingi nakuona jamvini na kwa kweli kwa hili naomba nikupe pongezi tena.
Ni ukweli usiopingika kuwa Lowassa alishiriki kwa ukaribu sana kuiingiza mkenge nchi yetu na sasa bado tunaumia kwa maamuzi yake hayo magumu ya kujilimbikizia mimali.
Negotiation team aliyoiunda ndiyo ambayo ilicheza ule mchezo mbaya kwa kofia yake, huku akijitokeza mara moja moja kushinikiza RichardMonduli"richmond" ipewe zabuni.

anayetakiwa kuchukua maamuzi magumu ni sisi wananchi, wananchi ambao tunaumia kila kukicha huku wengine wakineemeka, tumefika mahali mtu anaamua kuongeza mkataba hata kama ni mbovu mfano TICTS,
Almanusra tuingizwe mkenge mwingine wa Mvua za kutengeza na lile jambo alikuwa amelikomalia bila kutokea mapinduzi ya uongozi alikuwa anadeal nao.
Tunayo mifano hai, hata hapa Tanzania tunayo mashaka makubwa ule mradi wa maji Shinyanga na Kahama, juu ya Contract ya mabomba mengi na makubwa yaliyokuwa yanatokea hapa Dar REs Salaam na kwenda kanda ya ziwa, kila kitu kimegubikwa na usiri mkubwa.
Tunatambua kwa undani sana tu kwa nini barabaa ya kupitia mbugani wanaig'ang'ania yeye na MKULU, nani asiyejua GRUMET na Mahoteli wanayojenga ndani ya hifadhi, itaharibu kabisa Ecologia na mfumo mzima wa wanyama kwenda Masai na Serengeti, kuna uwezekeno mkubwa wa barabara hiyo kuanzia lamadi kupitia kwetu Maswa hatimaye Mbulu na kuingia Arusha.Lakini hayo yote walafi hawayaoni wanataka kutimiza malengo ya miradi yao
Ufike wakati sisi wenyewe tunaoona na kutambua haya yuingie vijijini kuamsha watanzania juu hili.

Willie, Maamuzi magumu ni lazima yafanywe na wananchi wenyewe, si unaona mwenyewe magamba yanavyotamba hadi bungeni licha huku jasho letu lote linaishia kulipa mikataba yao feki

Rudi nyumbani Tanzania, Fimbo ya mbali kaka yangu haiui nyoka, njoo tuunganishe nguvu. Asante kwa thread yawezekana umeondoka Tz kwa sababu umekatishwa tamaa, ila njoo tupambane.
 
ni janga la taifa serikalini na kwenye vyama kukiwa kumejaa wezi tuuuu, hakuna wa kumfunga paka kengele, viongozi kibao wamejaa mascandal, iliyobaki ni kulindana tu,kila mtu anamuogopa mwenzie. wakuamua sasa ni sie tu.
 
- Maneno mazito sana hayo mkuu!, ya CCM as a brand name ninaamini wahusika wameyasikia!Willie @ NYC, USA
Hawa jamaa wameweka pamba masikioni mwao ndugu Willi. Tangu kuanza kulalamikiwa hakuna mabadiliko....kutochukua maamuzi magumu.... They dont dare, na alieyasema haya anawajua wenzie hawadhubutu.... CCM do it now and lets see umedhubutu.
 
EL ni mkweli, viongozi wengi ni wanafiki sana. Ujumbe anaotupa EL ni kwamba kama wananchi wanadhani yeye ni mbaya, fisadi na hafai, basi kuna wabaya zaidi yake. EL anatuambia yeye ni bora kuliko wengine-and that is a bitter truth for us as a nation. Kama tunapinga ufisadi na mambo mengine yanayoturudisha nyuma kama taifa, hatuwezi kuanza na kumaliza na kina EL and Co, tusafishe nyumba yote. La sivyo, tutakuwa tunawasaidia majambazi wapya wanaopigana na majambazi wa zamani ili na wao wafaidi keki ya taifa.
 
Back
Top Bottom