Maamuzi mabaya ya serikali ndiyo yamesababisha mgomo

TWIZAMALLYA

JF-Expert Member
Oct 1, 2011
397
81
Wanajamiiforums wenzangu jana nilimsikia waziri mkuu akisema kuwa madaktari wakigoma watakuwa wamevunja miiko ya kazi yao. Inaonyesha kuwa serikali haijakubaliana na madai ya hawa watu na haijaona kuwa katika saga hili ni serikali ndio chanzo cha matatizo haya katika maamuzi yao ya ovyo ambayo kimsingi wanatakiwa waangalie kwa undani mkubwa madhara ya maamuzi yao ambayo ndio yamepelekea hawa madaktari wakiuke miiko ya kazi zao.Hoja kuwa waziri Mponda na naibu wake Nkya ni wageni pale wameyakuta matatizo hayo,kitu ninachojiuliza kwa nini Waziri mkuu hajaueleza umma wa Wadanganyika ni jinsi gani Dk mponda ameshiriki kutafuta namna ya kutatua matatizo aliyoyakuta?.Ni dhahiri kabisa kuwa hakufanya chochote ndio maana Madaktari hawamtaki. Sasa badala ya kuendeleza ule Utamaduni wa kubebana ni wakati umefika sasa wa ku-face reality,Waziri Mponda aondoke ili kuepusha vifo vya watu wengi.Huyu mponda ana uzuri gani mpaka Serikali inamng'ang'ania in the expense of poor Tanzanian?
 
Back
Top Bottom