Maalim Seif: Tunataka kiti cha Zanzibar UN kirudishwe

Hakuna dhulma yenye kudumu.

Hongera maalim Seif kutoa duku duku lako hadhwarani tena mchana kweupeeeee. Hilo linakutofautisha wewe na viongozi wengine huko Tanzania.
 
mbona hili ni rahisi sana; Seif na CUF watangaze kujitoa kwenye serikali ya umoja wa kitaifa; wawaongoze watu wa Zanzibar kutoka kwenye Muungano ili hatimaye Zanzibar iwe nchi nje ya Muungano ipate kiti, meza na kalamu kwenye Umoja wa Mataifa.
Mmmm, hii ni rahisi, ila haitaki unafiki. Huku wataka na huku.
 
Afadhali Maalim Seif ameamua kuwa mkweli, wengine woote wanaangalia matumbo yao na wala si Nchi. Mimi binafsi naona Zanzibar waende tu, maana kelele nyingiii, bila sababu.
 
Seif ni mchina wa kisiasa anataka umaarufu amebashiri yatakayojiri 2015 huko Z'bar. Japo mie binafsi sio mwanachama wa CCM ila kwa hali ilivyo 2015 CCM itashinda kihalali na kiulani kwani CUF wameshindwa kwa asilimia 95 kuwapa wazinzibari yale waliyoyatarajia endapo CUF ingeiingia madarakani. Kwahiyo chama cha CUF kinakufakufa. Na hata hawa wanaoitwa wanauamsho ni matokeo ya CUF kushindwa kuwa mbadala wa CCM sasa wananchi wa Z'bar wanatafuta mbadala. CUF kushine bin taaban. Kwahiyo Seif anatoa kauli hiyo ili kujaribu kuwadanganya wazanzibar ambao wameshamsoma na kujua si lolote si chochote ni mchumia tumbo kama nyinyiem manake mie sipo kwahiyo siwezi kusema sisiem. Seif tatizo matatizo ya wananchi acha longolongo.
 
Sasa wanatuomba ruhusa au??? Mbona wanapenda sana kurudia rudia maneno hawa? au kwa sababu wamejawa na maneno mengi basi wanadhani yatawasaidia kuwainua katika madai yao?
Sisi hatuwahitaji wajipange tu wao wajito na maoni ya yatheshimiwa......sasa hizi kelele wanazozianza ni za nini tena? watu tupo busy bana..
 
Assalamu alaykum


Ismail Jussa
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, amefikisha ujumbe wa Wazanzibari wanaotaka Zanzibar yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa ikiwa na kiti chake Umoja wa Mataifa kwenye Ofisi ya Rais (White House) na Wizara ya Mambo ya Nje (State Department) ya Marekani.
 
Hapa Maalim Seif hajawaomba marekani UHURU bali amewapasha kuwa tunakuja UN kwa kutaka kiti chetu kwa hivo marekani wasipinge ombi la Zanzibar katika security council Mupo?. Hii ni "protocl" ya UN. Lolote lile likiletwa na nchi ndogo lazima lipitie SC kupitia taifa moja wapo la SC. Ok.
 
Hivi vituko! Anaiomba Marekani? Wakikataa je? Njia rahisi ni kuleta mswada BLW ili Zanzibar ipige kura ya maoni kutoka kwenye muungano na kuweka utaratibu wa kugawana mali na madeni kati yake na Tanganyika pamoja na mengineyo.

marekani ana kura ya VETO .. UN.. so ni kama kuwapa taarifa nadhani...

 
Wanamuomba Nani.,??

wanawaomba hao Freemansons walioipandisha bendera ya Zanzibar huko New york katika headqurter ya UN 1963
Flags%20of%20Zanzibar%20and%20Kenya%20Raised%20at%20United%20Nations%20Headquarters%20Dec%201963.jpg



UN-SPEACH-FOR-MINISTER-OF-ZANZIBAR-MOHAMMED-SHAMTE 1963

 
Sikujua kuwa Maalim Seif naye pia ni mtu wa kujifurahisha!. Kabla Zanzibar haijaomba hicho kiti chake kule UN, "first it has to exist"!. Katika medani za kimataifa, hakuna nchi inayoitwa Zanzibar!, Zanzibar doesn't exist anymore so does Tanganyika!. Kimataifa nchi ni moja tuu Tanzania, na Zanzibar ni sehemu ya hiyo Tanzania!.

Ili Zanzibar iweze ku reclaim its lost glory, hatua ya kwanza sio kukimbilia kwa big brother na kuomba utambuliwe, bali ni kumwambia partner wako kuwa umemchoka, mvunje kwanza hiyo parneship yenu ya muungano, uwe huru, uwe una exist tena kama zamani, then unabisha hodi UN kwenyewe na sio kwa host wa UN!.

Hivyo ili kukipata kiti chenu, hatua ya kwanza ni kuuvunja muungano na kuirejesha jamhuri ya Watu wa Zanzibar. Kama alivyoshauri Mzee Mwanakijiji pale juu, tumieni BLW, mamlaka hayo mnayo kupitia ile sheria yenu ya kura ya maoni!. Hamna haja ya kuiliza bara lolote, pigine kura ya maoni kuwauliza Wazanzibari kama wanautaka muungano kwa yes or no, watakaojibu no na kama no ndio itashinda, then BLW wanapitisha azimio na taratibu za kuuvunja muungano zinafuatia ikiwemo namna ya kugawana mali!.

Maalim ana bahati sana sasa hivi ni enzi za Dhaifu, ingekuwa ni enzi ya Mwalimu, na ni kweli ameuwasilisha huo huko wa kwanza kushughulikiwa ni Shein, angeulizwa tuu, "jee unataarifa kuhusu waraka huo?, jee ulitoa baraka zako?, kama jibu ni ndiyo, then Shein angetiwa kizuizini (nyumbani) kama Jumbe!, na Maalim angeambiwa ambaki huko huko, na kama hana tujisenti twa Uswiss twa kumsetiri,yule half brother wake Sultani wa Brunei, angaokoa jahazi kumsetiri kama wanavyoifadhili CUF and that would have been the end of the story!.
 
Sikujua kuwa Maalim Seif naye pia ni mtu wa kujifurahisha!. Kabla Zanzibar haijaomba hicho kiti chake kule UN, "first it has to exist"!. Katika medani za kimataifa, hakuna nchi inayoitwa Zanzibar!, Zanzibar doesn't exist anymore so does Tanganyika!. Kimataifa nchi ni moja tuu Tanzania, na Zanzibar ni sehemu ya hiyo Tanzania!.

Ili Zanzibar iweze ku reclaim its lost glory, hatua ya kwanza sio kukimbilia kwa big brother na kuomba utambuliwe, bali ni kumwambia partner wako kuwa umemchoka, mvunje kwanza hiyo parneship yenu ya muungano, uwe huru, uwe una exist tena kama zamani, then unabisha hodi UN kwenyewe na sio kwa host wa UN!.

Hivyo ili kukipata kiti chenu, hatua ya kwanza ni kuuvunja muungano na kuirejesha jamhuri ya Watu wa Zanzibar. Kama alivyoshauri Mzee Mwanakijiji pale juu, tumieni BLW, mamlaka hayo mnayo kupitia ile sheria yenu ya kura ya maoni!. Hamna haja ya kuiliza bara lolote, pigine kura ya maoni kuwauliza Wazanzibari kama wanautaka muungano kwa yes or no, watakaojibu no na kama no ndio itashinda, then BLW wanapitisha azimio na taratibu za kuuvunja muungano zinafuatia ikiwemo namna ya kugawana mali!.

Maalim ana bahati sana sasa hivi ni enzi za Dhaifu, ingekuwa ni enzi ya Mwalimu, na ni kweli ameuwasilisha huo huko wa kwanza kushughulikiwa ni Shein, angeulizwa tuu, "jee unataarifa kuhusu waraka huo?, jee ulitoa baraka zako?, kama jibu ni ndiyo, then Shein angetiwa kizuizini (nyumbani) kama Jumbe!, na Maalim angeambiwa ambaki huko huko, na kama hana tujisenti twa Uswiss twa kumsetiri,yule half brother wake Sultani wa Brunei, angaokoa jahazi kumsetiri kama wanavyoifadhili CUF and that would have been the end of the story!.
Pasco, I can't agree with you more!Thanks. Please, allow me to chip in senti sumuni.

Kama ni kweli Maalim atakuwa ameshindwa kuelewa jambo dogo sana. Farouk Karim na Ally Salehe wame-champion Zanzibar kujitoa Chama cha mpira FAT nyakati hizo. Jitihada zao za kujiunga na mashirika ya kimataifa kama FIFA zimegonga mwambwa kwa sababu alizoeleza Pasco hata pale TFF ilipowaunga mkono.

Falconer; Security council ina wanachama wa kudumu 5 (USA,Russia, China, France na UK). Halafu kuna 10 non-permanent members. Wenye kura ya turufu (Veto ni 5) sasa kama unachosema ni kweli Maalimu inabidi awaone wengine 4 maana wanaweza kupinga tu. Hoja yako! mhh

Mwanakijiji: Hakuna ugomvi na Zanzibar kwahiyo maalimu anatakiwa apeleke mswada kwanza BLW kutaka kura ya maoni au kukataa muungano kwa short kati kama ile ya katiba ya Zanzibar, kuondoa mafuta na gesi(Ahmed Rajab) n.k.
Lakini pia alitakiwa awatumie wabunge 50 wanaowakilisha Zanzibar Dodoma.
Zaidi ya hapo wapo wabunge kutoka BLW wanaoingia Dodoma.
Kinachoshangaza ni kuwa unaomba vipi kiti UN kabla hujawa na nchi?

Nadhani Ahmed Rajab anapata majibu ya akina nani wenye ajenda hii (Raia mwema) licha ya kuwatetea.

Baada ya serikali 3(Ahmed Rajab) kukosa majibu na mkataba kuonekana hauna majibu,kwanini wazanzibar wanahangaika sana? Kwanini wasivunje muungano kesho ili keshokutwa Maalim apite kwa Ban Kimoon akiwa na document za maombi.

Huwezi kuwa na kiti UN, ukawa na BLW, Rais, Mahakama halafu ukadai mkataba. Uhusu nini tena!
Seif ni mwanasiasa wa ajabu sana, wakati anachukua mafao treasury Dar es Salaam wakati huo huo anaomba kiti UN.

Maalimu Seif rudi Nyumbani uvunje muungano, acha kujificha nyuma ya serikali 3 au mkataba wewe na washirazi wenzako
 
Nguruvi3,

..hawa watu hawa!!

..niliwahi kubishana na jamaa yao mmoja hapa JF. wiki nzima tunabishana.

..hoja yake ilikuwa ati Tanganyika haikuwahi kuwa na "kiti" UN.

..madai yalikuwa "kiti" cha Tanzania UN, kilikuwa ni "kiti" cha ZNZ.

..sasa uzi huu unadhihirisha kwamba hata hawajui the simple process ya kuwa mwanachama wa UN.
 
Last edited by a moderator:


marekani ana kura ya VETO .. UN.. so ni kama kuwapa taarifa nadhani...


Kwahiyo Maalim atakwenda kwenyennchi zote tano zenye VETO UN security Council...???
Au ataishia kwa big brother tu.
 
Pasco, I can't agree with you more!Thanks. Please, allow me to chip in senti sumuni.

Kama ni kweli Maalim atakuwa ameshindwa kuelewa jambo dogo sana. Farouk Karim na Ally Salehe wame-champion Zanzibar kujitoa Chama cha mpira FAT nyakati hizo. Jitihada zao za kujiunga na mashirika ya kimataifa kama FIFA zimegonga mwambwa kwa sababu alizoeleza Pasco hata pale TFF ilipowaunga mkono.

Falconer; Security council ina wanachama wa kudumu 5 (USA,Russia, China, France na UK). Halafu kuna 10 non-permanent members. Wenye kura ya turufu (Veto ni 5) sasa kama unachosema ni kweli Maalimu inabidi awaone wengine 4 maana wanaweza kupinga tu. Hoja yako! mhh

Mwanakijiji: Hakuna ugomvi na Zanzibar kwahiyo maalimu anatakiwa apeleke mswada kwanza BLW kutaka kura ya maoni au kukataa muungano kwa short kati kama ile ya katiba ya Zanzibar, kuondoa mafuta na gesi(Ahmed Rajab) n.k.
Lakini pia alitakiwa awatumie wabunge 50 wanaowakilisha Zanzibar Dodoma.
Zaidi ya hapo wapo wabunge kutoka BLW wanaoingia Dodoma.
Kinachoshangaza ni kuwa unaomba vipi kiti UN kabla hujawa na nchi?

Nadhani Ahmed Rajab anapata majibu ya akina nani wenye ajenda hii (Raia mwema) licha ya kuwatetea.

Baada ya serikali 3(Ahmed Rajab) kukosa majibu na mkataba kuonekana hauna majibu,kwanini wazanzibar wanahangaika sana? Kwanini wasivunje muungano kesho ili keshokutwa Maalim apite kwa Ban Kimoon akiwa na document za maombi.

Huwezi kuwa na kiti UN, ukawa na BLW, Rais, Mahakama halafu ukadai mkataba. Uhusu nini tena!
Seif ni mwanasiasa wa ajabu sana, wakati anachukua mafao treasury Dar es Salaam wakati huo huo anaomba kiti UN.

Maalimu Seif rudi Nyumbani uvunje muungano, acha kujificha nyuma ya serikali 3 au mkataba wewe na washirazi wenzako
Mkuu Nguruvi3, Zanzibar kuna vituko vya ajabu!, wengi wanadhani ni Maalim ndie autakaye sana urais wa Zanzibar, hawajui kinachotakiwa sio urais, kinachotakiwa ni kisiwa na kinatakiwa na wenyewe!.

Baadhi tuu ya vituko vya Zanzibar ni kama vifuatavyo!.
  • Kuna mmoja wa marais wao alikuwa ni Mmalawi!, huko Zanzibar alikuwa hana baba, mama, kaka ,dada wala ndugu yoyote, uzuri ni kwamba hakusahau kwao, hivyo wanawe, aliwasomesha kwao Malawi!.
  • Aliyeongoza Mapinduzi ni Mganda!
  • Kuna rais alikuwa na watoto two brothers, mmoja wa watoto akatunukiwa zawadi ya urais kama heshima tuu kumuenzi baba yake!. Kipindi cha miaka kumi ya urais wa kaka mtu kilipotimia, mdogo mtu akaomba urais, huko kwao wakamkemea kuwa wewe umeona rais anayemaliza ni kaka yako, toka ntoke, halafu na wewe unaomba, huu umekuwa usultani?!. Mdogo mtu akajibu kuwa kama kaka ameupata urais kama shukrani ya kumuenzi baba, mwenye atahiki haswa ya urais ule ni yeye, kwa sababu kaka mtu, sii mtoto wa aliyeenziwa, alikuwa ni mtoto tuu wa kufikia, mwanahalisi ni yeye, hivyo sasa ndio apewe yeye ili kumuenzi kihalali!.
  • Kuna Sultani mmoja, alimbaka mjakazi wa mkewe na kumpa ujauzito (kubaka mjakazi sio kosa kama ilivyokuwa kumuua mtumwa), ili kuisetiri aibu ya mwana sultani kwa kijakazi, mjakazi yule akaileshwa ozwa kwa ndoa ya mkeka pahala mpaka alipozaliwa mwana sultani, wengine wote hawamjua kuwa ni mwana sulani, ila kuna wachache wanaijua siri hiyo!, sasa mwana sultani anafanya juhudi za juu chini kuvikomboa viziwa hivyo mikononi mwa ukoloni wa Tanganyika ili avirejeshe kwa sultani!. Huko ndiko zinakotoka fedha za kundi kama Uamsho, wengi wakifikiri ni ukombozi, kumbe Mwarabu anataka kurudi!.
  • Na kuna rais mmoja alioa mpaka chuo cha 5, best wake alikuwa rais wa mchi tajiri ya mafuta, akamsaidia sana huyo rais na alipomaliza tuu term yake ya urais, akamsaidia mpaka mkewe!.
  • Juzi kwenye Shindano Bibi Bomba ya Clouds kulijitokeza Bibi kutoa Zenj, akajitambulisha kuwa yeye ndiye mke wa kwanza wa rais fulani wa Zanzibar na wamezaa nae mtoto wa kiume, mumewe alipopata mke wa Kiarabu, yeye aliachika na kutelekezwa na mwanae mpaka kesho!.
Visa, vijambo na vimambo vya Zenj viko tele, ila kwa leo naomba niishie hapa, Mtoto akililia wembe mpe.. na mkataa pema, pabaya panamwita!, tuharakishe tuwapatia wanachiotaka halafu subirieni hilo tifu!.
 
Back
Top Bottom