Maalim Seif: Nikipewa uenyekiti niko tayari kuhamia CCM

Moses Kyando

Member
Mar 4, 2010
48
7
Kwa mujibu wa mahojiano yatakayorushwa Jumatatu na ITV, Maalimu Seif Sharif Hamad (Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar), amesema yuko tayari kujiunga na Chama Cha Mapinduzi, ikiwa tu atapewa nafasi ya Uenyekiti. Na kwa mujibu wake kwa sasa hakuna jambo la Msingi ambalo serikali ya CCM inafanya makosa.

My take:
Historia inajirudia mashaka yangu ipo siku chama kikuu cha upinzani bara, kitaanza kukiona CCM kizuri ilimradi tu kipewe nafasi serikalini
 
r-COLIN-MYLER-huge.jpg
 
kwanza mkuu hilo gazeti si limefungiwa au..kingine cuf ni ccm b kwa hiyo don't be shocked...
 
Kwa mujibu wa mahojiano yatakayorushwa Jumatatu na ITV, Maalimu Seif Sharif Hamad (Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar), amesema yuko tayari kujiunga na Chama Cha Mapinduzi, ikiwa tu atapewa nafasi ya Uenyekiti. Na kwa mujibu wake kwa sasa hakuna jambo la Msingi ambalo serikali ya CCM inafanya makosa.

My take:
Historia inajirudia mashaka yangu ipo siku chama kikuu cha upinzani bara, kitaanza kukiona CCM kizuri ilimradi tu kipewe nafasi serikalini

Mkuu hiyo ni ndoto, CCM hakiwezi kuwa kizuri hata siku moja. Mbona kule kenya mpaka na leo hii KANU bado haijaonekana nzuri?

kwa upande wa HAMAD mimi sishangai kwa yeye kurudi CCM manake kwa sasa CUF si ni CCM B?
 
Kwa mujibu wa mahojiano yatakayorushwa Jumatatu na ITV, Maalimu Seif Sharif Hamad (Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar), amesema yuko tayari kujiunga na Chama Cha Mapinduzi, ikiwa tu atapewa nafasi ya Uenyekiti. Na kwa mujibu wake kwa sasa hakuna jambo la Msingi ambalo serikali ya CCM inafanya makosa.

My take:
Historia inajirudia mashaka yangu ipo siku chama kikuu cha upinzani bara, kitaanza kukiona CCM kizuri ilimradi tu kipewe nafasi serikalini


Usitake kupotosha watu Mkuu Moses maana hata sisi tumesikia.

Alichosema Maalim Seif ni kuwa "walinambia kuwa sasa tuna Serikali ya Umoja wa Kitaifa, si urudi tu CCM?. Mimi niliwambia labda niwe Mwenyekiti" Au words to that effect.

Sasa ho ni tofauti kabisa na unavyotaka watu waamini.

Nadhani humjui Maalim Seif wewe.
 
huyu self inaonekana si mpinzani wa kweli,ila anapenda madaraka!! watu wanashindwa kuwa na iman na chama chetu cha cuf.
 
Usitake kupotosha watu Mkuu Moses maana hata sisi tumesikia.

Alichosema Maalim Seif ni kuwa "walinambia kuwa sasa tuna Serikali ya Umoja wa Kitaifa, si urudi tu CCM?. Mimi niliwambia labda niwe Mwenyekiti" Au words to that effect.

Sasa ho ni tofauti kabisa na unavyotaka watu waamini.

Nadhani humjui Maalim Seif wewe.

Hata kwa ulivyo andika wewe bado ujumbe ni ule ule kuwa katamka kuwa anaweza kurudi CCM. Every man has his price and he just named his. Sasa wewe sijui unataka watu waelewe vipi.
 
Tanzania hamna mpinzani wa kweli. Watu wapo kimaslahi zaidi. Hata FF akipewa position CDM anabadilisha kabisa mrengo wake!
 
maalim sif mnafiki wa karne-kabla ya mseto alikuwa ba kelele nyingi sana kuhusu amendeleo a zanzibar mara katiba,mara maliasili mara bandari mara mapato ya wazanzibari leo kapewa cheo yuko kimya-anakula kuku tu huku akiwa ana mategemeo makubwa ya pensheni nyumba na ulinzi baada yz kustafu.yeye ameshafikia ,alengonyake-kazi kwao wa mchamba wimw,jangombe watakuwa maskini mpaka watalala na vyura ndani.wazanzibari wakati mwingine they are very foolish.ka nchi kadogo kama wangedhamiria maendeleo ni ,waka mmoja tu.lakini serikali kubwa wanaokula keki ya nchi wachache .
 
Kuna Wazanzibari wengi humu JF walikuwa wanamuona Maalim Seif kama mkombozi wa Zanzibar. Kuna members kama Junius walimuelevate huyu kuwa kama vile ni Mandela wao. Wengine tulishaona na kujua kwamba siku zote huyu mzee kilichokuwa kinamsumbua si ukombozi wa Wazenji bali kukosa uraisi. Kumbe hata kumpa umakamo wa raisi usiokuwa na majukumu yoyote ilitosha kumpoza. Kweli imekula kwa wenzetu. Watafute mpiganaji mwingine huyu washampoteza zamani. I wonder why CCM hawakumpa kacheo huyu mtu tokea 2000 nadhani wali muover-estimate.
 
he is ccm member who was outside their party seeking for leadership.point pekee anayoongea siku izi ni umoja wa kitaifa wala aongelei tena wapemba wanavyotengwa znz
 
Mimi c jawahi msikikia kabisa hata akiongerea swala la muungano au maswala ya karafuu. Ishu za wapemba kutengwa alisha sahau.

wakuu kwa kifupi ni kwamba haya maswara ya serikali za umoja wa kitaifa hayafai africa. Mfano

1. Kule zimbabwe kwa sasa yule mongilai wazimbabwe wanamuona hafai kabisa na msaliti no 1

2. Kule kenya odinga umarufu wake unashuka kila kukicha

3. Huku zenji hamad nazani ndo anajiangamiza hivyo, serikali ya zanzibar ikishindwa kuwaletea wananchi wake maendeleo ni wote watakuwa wamearibu means ccm na cuf
na hata kampeni za uchaguzi ujao c jui hamadi atajinadi vipi kwa sababu yeye naye alishakuwa sehemu ya matatizo ya wazanziba na ccm wameisha pata point za kuongerea uchaguzi ujao huko zenji
 
Kuna watu wanamtetea humu Mh M. Seif, hv kwa kiongoz wa juu wa chama kuzungumza maneno km yale ni sahihi?, tena akasema kwa sasa CCM inafanya vizuri kule zanzibar, nimeamin ukiwa ndan ya serikal kila kitu kwako ni safi. Yule akipewa madaraka CCM anawaacha CUF solemba.
 
Km waasisi wetu {NYERERE & KARUME} wangekuwa na roho km ya Maalim Seif na wengne wa aina yk cjui leo tungekuwa wapi.
 
Tanzania hamna mpinzani wa kweli. Watu wapo kimaslahi zaidi. Hata FF akipewa position CDM anabadilisha kabisa mrengo wake!
nitoke vipi!!! Wako kimadaraka zaidi. Mi nashauri wangempa uenyekiti, akihamia tu wanamnyang'anya tuone kama atarudi CUF.
 
Maalim Seif Hamad akirudi nyumbani CCM siyo jambo la kushangaza. Huyu kisiasa alilelewa na kukulia huko. Akafikia ngazi ya kada wa ngazi ya juu. Huyu bwana alikua ktk sekretarieti ya chama enzi ya mwalimu Nyerere akiwa na akina Kingunge, Salmin Amour,Mwakawago. nk. Alikua waziri kiongozi mwenye nguvu huko Zanzibar. Alifukuzwa kutokana na fitina na majungu ya kugombea madaraka kama sasa tunavyoona wanataka kufukuzana kwa kisingizio cha kujivua gamba. Kama kuna eneo ccm inaweza jifunza ni tukio la kufukuzwa kwa akina Hamad ambavyo limekitesa chama chao Zanzibar na nchi yetu kwa ujumla mpaka tukafikia kuuliwa wananchi wa pemba na kuzalisha wakimbizi kwa mara ya kwanza ktk historia ya nchi yetu.
 
Usitake kupotosha watu Mkuu Moses maana hata sisi tumesikia.Alichosema Maalim Seif ni kuwa "walinambia kuwa sasa tuna Serikali ya Umoja wa Kitaifa, si urudi tu CCM?. Mimi niliwambia labda niwe Mwenyekiti" Au words to that effect.Sasa ho ni tofauti kabisa na unavyotaka watu waamini.Nadhani humjui Maalim Seif wewe.
ww ndio muongo alichoulizwa seif ni kama anaweza kurudi ccm, na akijibu kwamba kama atapewa uenyekiti.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom