Maalim Seif: CHADEMA wako sahihi kwenye suala la posho

Tuache unafiki, kwenye ukweli tusimamie huo ukweli.
Maalim alipigia kelele posho zake kwa sababu ilikuwa ni haki (MAFAO) yake kisheria as aliwahi kuwa WAZIRI KIONGOZI wa serikali ya Zanzibar. Alikuwa analipwa kama kiongozi wa juu mstaafu. Posho zinazopigiwa kelele na CHADEMA ni posho ambazo unamlipa mbunge wakati hicho unachomlipia ni sehemu ya kazi yake. Mbona polisi, walimu au madaktari hawalipwi wakati wanatekeleza majukumu yao?

Nakuunga mkono. Ukweli ni ukweli. Seif alikuwa waziri kiongozi nako kuna haki zake. Anachosema maalim Seif, ndio ukweli. Kwa nini mbunge alipwe posho kwa kazi anayolipwa mshahara? Chadema wako sahihi na Maalim Seif yuko sahihi. Katika hili tuungane kwani ni njia ya ukombozi kujiepusha na unyonyaji unaofanywa na viongozi wa kisiasa. Waziri Mkuu mstaafu posho yake sawa na 80% ya Waziri Mkuu aliye madarakani. Mbona wastaafu wengine hawapati 80% ya ngazi waliyokuwa nayo. Wanachukua posho na malipo ya kustaafu wanajipendelea. HUO NI WIZI TU.
 
Wana JF,

Jana kwa mara ya kwanza nilikubali kwamba makamu wa kwanza wa RAIS wa zanzibar ni mwanasiasa aliyebobea anayeamini katika ukweli.Kwa wale walioangalia taarifa ya habri ya ITV saa mbili usiku,akihojiwa na Suleiman Semunyu kuhusu msimamo wake wa posho za wabunge;Alisema bila kumung'unya maneno kwamba chadema wako right na wanatetea haki za umma.

Alisema si haki kwa mtu kulipwa posho kwa kazi aliyoajiriwa pale anapotimiza majukumu yake ya ajira.Aliongeza kwamba serikali inatakiwa ijipange sawasawa kukabiliana na hoja za chadema,vinginevyo kamwe hawataeleweka kwa wananchi.

Baada ya kumsikiliza maalim Seif niliwaonea huruma kina Hamad Rashid ambao wanapita huku na huko kuilaani Chadema...

Tujadili wadau.

Maalim Seif kichwa sana tunamhitaji cdm ili alete changamoto maana yeye ni hazina kwa siasa za tanzania na itatusaidia kupata wafuasi wengi pemba.

Pipooooozzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzz
 
Nakuunga mkono. Ukweli ni ukweli. Seif alikuwa waziri kiongozi nako kuna haki zake. Anachosema maalim Seif, ndio ukweli. Kwa nini mbunge alipwe posho kwa kazi anayolipwa mshahara? Chadema wako sahihi na Maalim Seif yuko sahihi. Katika hili tuungane kwani ni njia ya ukombozi kujiepusha na unyonyaji unaofanywa na viongozi wa kisiasa. Waziri Mkuu mstaafu posho yake sawa na 80% ya Waziri Mkuu aliye madarakani. Mbona wastaafu wengine hawapati 80% ya ngazi waliyokuwa nayo. Wanachukua posho na malipo ya kustaafu wanajipendelea. HUO NI WIZI TU.

Hapo kwenye nyekundu cdm tungehakikisha kina lissu na zitto wanabadilisha sheria ya kiiunua mgongo cha ubunge ili pesa zinazookolewa zisaidie maendeleo maana ukifanya hesabu ya pesa itakayokuwa saved kwa wabunge wote ni mara elfu ya pesa za posho na mara mia tano ya pesa za shangingi. Ni imani yangu tumeanza na kastep kadogo tutakandamiza soooon ilitusionekane wanafiki.

Pipozzzzzzzz
 
hata maalimu sasa anazinduka kweli tukiendelea hivi tutafika mbali zaidi
 
Tuache unafiki, kwenye ukweli tusimamie huo ukweli.
Maalim alipigia kelele posho zake kwa sababu ilikuwa ni haki (MAFAO) yake kisheria as aliwahi kuwa WAZIRI KIONGOZI wa serikali ya Zanzibar. Alikuwa analipwa kama kiongozi wa juu mstaafu. Posho zinazopigiwa kelele na CHADEMA ni posho ambazo unamlipa mbunge wakati hicho unachomlipia ni sehemu ya kazi yake. Mbona polisi, walimu au madaktari hawalipwi wakati wanatekeleza majukumu yao?


Kwani haki ya mfanyakazi si mshahara wake? sasa hii kusema posho hii iwepo na hii isiwepo kunakujaje? CHADEMA wanataka posho kwa ajili ya kazi yako isitolewe mbona hizo posho zote ziko kwa ajili ya kazi umayoifanya? Unapolipwa mshahara iwe umemalizana na haki yako lakini kutokana na sababu mbalimbali ndio inawekwa posho. Sijasikia mtu asiekuwa mbunge akalipwa posho ya ubunge hivyo hivyo ikiwa kwa daktari au mwalimu.
Tukija kwa Bunge , mbunge anapolipwa 2,500.000 halafu anapewa mtiririko wa posho hadi kufikia milioni 7 na zaidi. sasa tunapojidai kukubali baadhi ya posho na kukataa nyengine haiwezekani, ikiwa tunataka tuondoe posho basi tuondowe posho na kubaki na mishaharatu.
Huyo Sefu ni muongo kwani ana mlolongo wa maposho na hayo anayapata kwa sababu ya kazi yake na asingepata kama asingepata huo umakamo wa Rais. kiongozi unaposhangiria kuondoshwa viposho vidogo vidogo vya wafanyakazi wa umma huyo ana matatizo kwani hao Wabunge na viongozi kama Seif wakiondoshewa posho ya vikao hawana tabu kwa vile wana maposho mengine yanayowaendeshea maisha yao kwa raha. Kwao wao posho la umeme , watumishi, gari bure na msururu wa mafao ambayo mfanyakazi wa kawaida anatakiwa ayatolwe kutoka kwenye mshara wake.
 
Tuache unafiki, kwenye ukweli tusimamie huo ukweli.
Maalim alipigia kelele posho zake kwa sababu ilikuwa ni haki (MAFAO) yake kisheria as aliwahi kuwa WAZIRI KIONGOZI wa serikali ya Zanzibar. Alikuwa analipwa kama kiongozi wa juu mstaafu. Posho zinazopigiwa kelele na CHADEMA ni posho ambazo unamlipa mbunge wakati hicho unachomlipia ni sehemu ya kazi yake. Mbona polisi, walimu au madaktari hawalipwi wakati wanatekeleza majukumu yao?

Kwa hiyo zingine haziko kisheria? Suala ni kwamba tuangalie sheria hizo ambazo zinatoa posho ambazo si sahihi. Tusijikite kwenye posho za vikao tu tukasahau posho za viburudisho kwa mawaziri na viongozi wengine wa serikali pamoja na miposho lukuki inayolipwa kwa mujibu wa sheria. Inaweza kuwa posho inalipwa kwa mujibu wa sheria lakini kimantinki siyo halali.
 
Kwa hiyo zingine haziko kisheria? Suala ni kwamba tuangalie sheria hizo ambazo zinatoa posho ambazo si sahihi. Tusijikite kwenye posho za vikao tu tukasahau posho za viburudisho kwa mawaziri na viongozi wengine wa serikali pamoja na miposho lukuki inayolipwa kwa mujibu wa sheria. Inaweza kuwaa posho inalipwaa kwaa mujibu wa sheria lakini kimantinki siyo halali.


Nakubaliana nawe kabisa hili suwala la kungangania sitting allowance na kusahau millioni mbili za vinywaji ni ukosefu wa kutumia akili. sitting allowance ni posho pekee ambalo halina daraja kwani hata mtumishi wa nafasi ya chini anaweza akafaidika nayo, lakini kuna maposho yaliyo makubwa wanasiasa wa upinzani wanayanyamazia.
 
Nimeangalia na nimemuona Mheshimiwa Zitto yumo sasa.
Naomba utupe ufafanuzi kwanini hasa mbunge apewe posho la aina yoyote iwapo tayari ameshapangiwa mshahara wake. Mtumishi wa Serikali mbona huwa anategemea maisha yake kwa mshahara wake tu?
 
Hongera Seif kwa kusema ukweli!!

Leo Maalim Seif anaonekana shujaa na mtu mzuri kwa sababu hoja zake zimeoana na za chadema. Huko mbele akiwa na msimamo tofauti lakini ambao ni imani yake ya dhati ataitwa kila aina ya majina, kenge, mamluki, chatu n.k. Ndugu zangu tujifunze kukubali kutofautiana bila kutukanana. Kulazimisha maoni yako yakubalike na kutawala ni udikteta!
 
Jamani Seif naye ni binadamu hata kama aliharibu huko nyuma, mtu aliyemkomavu wa kisiasa utamtambua tu, alilolisema lazima tumpongeze, mbona wengi wanaujua ukweli kuhusiana na posho hizo lakini wanaonekana kuvaa miwani ya mbao namba moja akiwa mtendaji mkuu wa serikali mtoto wa mkulima lakini yeye mwenyewe bepari
namkubali maalim seif huwa mkweli na muwazi na hamungunyi maneno na ameungana na chadema moja kwamoja kua suala la posho serikali ilishugulikie,bravo maalim seif.
 
Leo Maalim Seif anaonekana shujaa na mtu mzuri kwa sababu hoja zake zimeoana na za chadema. Huko mbele akiwa na msimamo tofauti lakini ambao ni imani yake ya dhati ataitwa kila aina ya majina, kenge, mamluki, chatu n.k. Ndugu zangu tujifunze kukubali kutofautiana bila kutukanana. Kulazimisha maoni yako yakubalike na kutawala ni udikteta!

Umenena kweli mkuu. Uungwana ni kutofautiana bila kutukanana. Humu ndani kuna watu wanaamini kwamba wao kwao hoja ni matusi. Mtu anatoa hoja lakini badala ya kujibiwa kwa hoja utaona watu wanaandika mara unatumia makalio kufikia, mara mjinga, mara umetumwa na waume zako!! Haya yote ya nini? Kama mtua ametoa pumba basi wewe toa hoja itayoonyesha kwamba alichokisema mwenzio si hoja bali kioja. Ukitukana inakuwa hadithi ya kumfukuza chizi ambaye hana nguo amekuta unaoga mwaloni akachukua nguo zako na kuanza kukimbia nazo. Watu watashindwa kutofautisha chizi na mzima!
 
Nakubaliana nawe kabisa hili suwala la kungangania sitting allowance na kusahau millioni mbili za vinywaji ni ukosefu wa kutumia akili. sitting allowance ni posho pekee ambalo halina daraja kwani hata mtumishi wa nafasi ya chini anaweza akafaidika nayo, lakini kuna maposho yaliyo makubwa wanasiasa wa upinzani wanayanyamazia.

Mkuu kwenye kekundu hapo; unaweza kweli kutamka ng'ambo? Made in Muhutwe au Kemondo Bay?
 
Umenena kweli mkuu. Uungwana ni kutofautiana bila kutukanana. Humu ndani kuna watu wanaamini kwamba wao kwao hoja ni matusi. Mtu anatoa hoja lakini badala ya kujibiwa kwa hoja utaona watu wanaandika mara unatumia makalio kufikia, mara mjinga, mara umetumwa na waume zako!! Haya yote ya nini? Kama mtua ametoa pumba basi wewe toa hoja itayoonyesha kwamba alichokisema mwenzio si hoja bali kioja. Ukitukana inakuwa hadithi ya kumfukuza chizi ambaye hana nguo amekuta unaoga mwaloni akachukua nguo zako na kuanza kukimbia nazo. Watu watashindwa kutofautisha chizi na mzima!

Mzee nimekukubali. Humu JF sasa hivi kuna elemenet za kitotot zinanyemelea na unashangaa wengine ni very seasoned members lakini hufanya mambo kama vile ni chipukizi. No body will take us seriously if we let this trend grow unabetted. Let's nip it in the bud.
 
hata maalimu sasa anazinduka kweli tukiendelea hivi tutafika mbali zaidi
mkuu kwa taarifa yako tu maalim seif alishazinduka zamani kuliko unavyofikiria wewe,maalim seif ndie muanzilishi wa vuguvugu la upinzani ktk eneo lote la maziwa makuu zaid yamiaka 23 iliyopita tokea miaka ya 87 amka kama umelala.
 
mkuu kwa taarifa yako tu maalim seif alishazinduka zamani kuliko unavyofikiria wewe,maalim seif ndie muanzilishi wa vuguvugu la upinzani ktk eneo lote la maziwa makuu zaid yamiaka 23 iliyopita tokea miaka ya 87 amka kama umelala.

Tupe source of this information, kwa mfano wikipedia inayompa sifa hizo.
 
mkuu kwa taarifa yako tu maalim seif alishazinduka zamani kuliko unavyofikiria wewe,maalim seif ndie muanzilishi wa vuguvugu la upinzani ktk eneo lote la maziwa makuu zaid yamiaka 23 iliyopita tokea miaka ya 87 amka kama umelala.

Nakumbuka alivyomtesa Marehemu Idrisa Abdulwakil baada ya Maalim kutoteuliwa kugombea kumrithi Mzee Ruksa! Baada ya kutoteuliwa Maalim alianza kuwa mpinzani ndani ya CCM, sijui alikuwa anapigania Demokrasia au alikuwa mroho wa madaraka?
 
Humu JF kuna siasa za kichekesho. Kiongozi anapimwa uzuri au ubaya wake kwa namna anavyokubaliana au kutofautiana na msimamo wa CDM. Leo huyu Maalim amekuwa shujaa lakini huko nyuma alikuwa hovyo. Huko mbele akitoa msimamo unaokinzana na CDM basi moto utamuwakia.
 
Back
Top Bottom