kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 266
MAKAMU wa Rais wa Zanzibar, Seif Shariff Hamad, amejibu malalamiko mbalimbali ya wananchi dhidi yake, viongozi na Serikali ya Umoja wa Kitaifa kuhusu kupanda kwa maisha na kutokuwapo kwa serikali ya kitaifa ngazi za chini.
Akihutubia Mkutano Mkuu wa CUF Wilaya ya Mjini jana, Maalim Seif baadhi ya wabunge na wawakilishi wa CUF hawaonekani kwenye majimbo yao tangu walipochaguliwa mwaka jana.
Nimesikia malalamiko kwamba sionekani na kwamba, viongozi tumekaa kimya kuhusu operesheni ya Darajani ambako wafanyabishara waliondolewa. Nafikiri ni vuzuri nyie viongozi mkafanya utafiti kabla ya kutulaumu, alisema Maalim Seif.
Katika kujibu malalamiko hayo, Maalim Seif alisema aliahidi kupunguza bei ya bidhaa hasa chakula iwapo angechaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar.Mimi siyo rais, ni makamu na mshauri tu wa rais. Hata hivyo, sisi viongozi tunafanya kazi ili kuleta unafuu kwa wananchi, alisema.
Kuhusu kupanda kwa bei za bidhaa, Maalim Seif alisema siyo Zanzibar pekee, bali nchi mbalimbali hali ya maisha inazidi kuwa ngumu na kwamba, limesababishwa na kupungua kwa uzalishaji duniani na uharamia wa Wasomali.
Maalim Seif alitaja baadhi ya mikakati ya kupambana na hali ngumu ya maisha kuwa, ni kushawishi wawekezaji kutoka nje kuja kuwekeza Zanzibar, kuimarisha kilimo hasa cha mpunga wa umwagiliaji.
Pia, Maalim Seif alisema miongoni mwa mambo mazuri ambayo Serikali ya Umoja wa Kitaifa inaadaa, ni kuzingatia suala la kubinafsisha soko la Karafuu ili wakulima wawe huru kuuza wanapotaka.Kuhusu muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, alisema katiba imeelekeza kuwa mgawanyo wa nafasi ni ngazi ya mawaziri na naibu mawaziri.
Nafasi nyengine zote zipo chini ya rais kwa mujibu wa katiba. GNU katika kugawana nafasi imeishia juu tu na ndivyo katiba inavyosema, alisema.
Alisema amepunguza kazi na amekuwa haonekani hadharani kwa sababu bado anaumwa, huku akiwataka viongozi wengine wakiwamo wabunge na wawakilishi kuimarisha chama na kuwatumikia wananchi.
Nasikitika, ni kweli viongozi tumelala, sioni harakati ndani ya chama. Vijana na wanawake mmekaa kimya, afadhali ya wanawake. Lazima kazi ya kuimarisha chama iendelee ngazi zote, alisema.
Alisema baadhi ya wabunge na wawakilishi wamekuwa wakifanya kazi nzuri katika majimbo yao, lakini amewaonya ambao bado hawajaonyesha juhudi za kuwatumikia wananchi na kwamba, atawabana wamweleze walichofanya.
Akihutubia Mkutano Mkuu wa CUF Wilaya ya Mjini jana, Maalim Seif baadhi ya wabunge na wawakilishi wa CUF hawaonekani kwenye majimbo yao tangu walipochaguliwa mwaka jana.
Nimesikia malalamiko kwamba sionekani na kwamba, viongozi tumekaa kimya kuhusu operesheni ya Darajani ambako wafanyabishara waliondolewa. Nafikiri ni vuzuri nyie viongozi mkafanya utafiti kabla ya kutulaumu, alisema Maalim Seif.
Katika kujibu malalamiko hayo, Maalim Seif alisema aliahidi kupunguza bei ya bidhaa hasa chakula iwapo angechaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar.Mimi siyo rais, ni makamu na mshauri tu wa rais. Hata hivyo, sisi viongozi tunafanya kazi ili kuleta unafuu kwa wananchi, alisema.
Kuhusu kupanda kwa bei za bidhaa, Maalim Seif alisema siyo Zanzibar pekee, bali nchi mbalimbali hali ya maisha inazidi kuwa ngumu na kwamba, limesababishwa na kupungua kwa uzalishaji duniani na uharamia wa Wasomali.
Maalim Seif alitaja baadhi ya mikakati ya kupambana na hali ngumu ya maisha kuwa, ni kushawishi wawekezaji kutoka nje kuja kuwekeza Zanzibar, kuimarisha kilimo hasa cha mpunga wa umwagiliaji.
Pia, Maalim Seif alisema miongoni mwa mambo mazuri ambayo Serikali ya Umoja wa Kitaifa inaadaa, ni kuzingatia suala la kubinafsisha soko la Karafuu ili wakulima wawe huru kuuza wanapotaka.Kuhusu muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, alisema katiba imeelekeza kuwa mgawanyo wa nafasi ni ngazi ya mawaziri na naibu mawaziri.
Nafasi nyengine zote zipo chini ya rais kwa mujibu wa katiba. GNU katika kugawana nafasi imeishia juu tu na ndivyo katiba inavyosema, alisema.
Alisema amepunguza kazi na amekuwa haonekani hadharani kwa sababu bado anaumwa, huku akiwataka viongozi wengine wakiwamo wabunge na wawakilishi kuimarisha chama na kuwatumikia wananchi.
Nasikitika, ni kweli viongozi tumelala, sioni harakati ndani ya chama. Vijana na wanawake mmekaa kimya, afadhali ya wanawake. Lazima kazi ya kuimarisha chama iendelee ngazi zote, alisema.
Alisema baadhi ya wabunge na wawakilishi wamekuwa wakifanya kazi nzuri katika majimbo yao, lakini amewaonya ambao bado hawajaonyesha juhudi za kuwatumikia wananchi na kwamba, atawabana wamweleze walichofanya.