Maalim Seif Atikisa Zanzibar, Mabomu Yarindima Kuwatawanya Wafuasi Wake

Huo muda unaousema sisi tunaishi leo na kama jambo halinifai leo kwa kigezoili lichochote basi haina maana yeyote kwangu sababu hatutakuwepo kipindi hicho
Mkuu, wanao na vizazi vyako bila shaka watakuwapo, wataipeleka nchi pahala ambako wewe ulishindwa na nadhani watafaidi kwa niaba yako. Ni kweli tunatamani tufanye mambo mazuri zaidi ili tuishi kwa neema lakini lazima tukubali kuna muda lazima ufike hata kama kwa wakati huu tumeshindwa kwa bahati mbaya ama kwa kukwamishwa na yeyote. Inajulikana pia kwamba haiwezekani kwa vyovyote vile CCM wawepo madarakani milele lakini si lazima watoke 2020 na si lazima watoke wewe ukiwa hai ili upate madaraka ati kwa sababu ndo uliyeanzisha harakati za mageuzi.
 
Kwa
Maalim Seif angekusanya familia yake yoote ikae mbele na yeye atangulie ili mabomu yakipigwa nao waone uchungu wa majeraha. sio kutumia watoto wa wengine kwa faida zao za kisiasa. ni ujinga huu. zama zake zimeshapitwa na wakati. tangu 1992 ??? yupo tuu.yupo tuu. mmhh wajameni
Kwani walimu aliwahi kuitanguliza familia yake mbele zaidi ya wazee wa karikoo
 
Mkuu, wanao na vizazi vyako bila shaka watakuwapo, wataipeleka nchi pahala ambako wewe ulishindwa na nadhani watafaidi kwa niaba yako. Ni kweli tunatamani tufanye mambo mazuri zaidi ili tuishi kwa neema lakini lazima tukubali kuna muda lazima ufike hata kama kwa wakati huu tumeshindwa kwa bahati mbaya ama kwa kukwamishwa na yeyote. Inajulikana pia kwamba haiwezekani kwa vyovyote vile CCM wawepo madarakani milele lakini si lazima watoke 2020 na si lazima watoke wewe ukiwa hai ili upate madaraka ati kwa sababu ndo uliyeanzisha harakati za mageuzi.

Pamoja na kusema mambo mazuri lakini sababu tulizonazo nchi za ki Afrika kukandamiza demokrasi na watu wetu hazina mashiko zaidi ya kung'ang'ania madaraka e.g. Zanzibar na Uganda
 
Hivi yeye aliwahi hata kupigwa risasi ya mguu ama kama kawa anafurahi kila siku wanaoumizwa ni watoto wa wenzie? miaka 30 bado mtu unapigania kitu ambacho hata impact bado huioni lakini bado tu umo, huo ni ukichaa. Mbona Mwl. Nyerere aliweza ndani ya miaka 15 tayari akawa amemaliza kazi ya kuipata Tanganyika iweje huyu Maalim anashindwa hata kusonga mbele hatua moja? leo Cuf imebaki haina wabunge Zanzibar alafu unasema jamaa ana umuhimu, upi huo? hata ukiona mwanao kawa was mwisho kila leo alafu anakwambia eti kisa darasani kwao wenye akiri ni wengi basi jua hapo umechemka, na ukimkubalia basi nyote mnakuwa vilaza, kama baba kama mtoto.

Mtaisoma namba,,,dhulma mbaya.Dhulma haina tafauti na rushwa....,kurudiwa uchaguzi na kukataa matokeo ya uchaguzi wa mwanzo imefanya CCM ichimbie kaburi lake mwenywe zanzibar,Mimi na wengine kama mimi ni CCM wa damu ,lakini kwasababu ya dini yangu ya kiislam inayopinga dhulama ya aina yoyote, tumekuwa tunawaonea huruma CUF kwa yaliyotokea....
 
Huyu jamaa wakati nchi iko kwenye harakati za kujenga uchumi yeye anaingiliaa,awekwe kizuizini tu amezidi.

Uchumi haujegwi kwa dhulma,uchumi unajengwa na watu kama watu wameibiwa haki yao uchumi huo utajengeka kivipi,,,
 
Kazi gani wamekuja kuomba chakula kwako? Acha demokrasia itamalaki.. Hujalazimishwa kwenda kumlaki maalim wenye mapenzi nae acha waende inshort jihusishe na mambo ya ccm cuf hachana nao
TADEA, UPDP, CCM, UDP, ADC, ACT, CHADEMA, NCCR, CUF, JAHAZI ASILIA nk. Vyote hivyo ni vyama vyetu vya kitaifa na kwa 100% vinatuhusu sote kwa ujumla wetu. Ndo maana Seif Hamad anapita mitaa yote bila kujali itikadi ya wanaoishi huko. Kwa mawazo yako ya kujimilikisha hiyo CUF yako angewaiteni nyumbani kwake ama angewafuateni huko majumbani kwenu ili awahabarishe na hizo habari za kunyang'anywa urais badala ya kufanya hotuba kwenye hadhara isiyohusu wana CUF pekee. Lakini pia siyo lazima waje kula kwangu ama waombe kwangu, ni vyema wakawekeza muda wao katika kazi za kuwaingizia kipato ili wawe na maisha bora kuliko ndoto za kufikiria kumchagua seif ili awapeleke ktk maisha bora.
 
Angalia avatar yako ni ? tizo la wewe kufikiri vizuri. Kupigania jambo halina mwisho hasa unapopambana na wakoloni weusi wanaojiona wateule wasiotakiwa kupingwa hata kama hawana hoia
nasema hivi kwa nini wakati wa maandamano wanawaambia watoto wao na familia wasitoke ndani ? hivi unaelewa? kwanza nikuulize umeshawahi shiriki maandamano yoyote ya kisiasa. au na wewe ndio kati ya wale wanaoambiwaga wasitoke nje
 
Hii nchi ina nifanya ninenepe kutokana na mambo yake japo hali ngumu..!!
 
Uzuri ni kwamba dhambi ikikomaa sana huzaa mauti na hilo kila mmoja wetu analifahamu ,tutavuna tulichokipanda
 
Mkuu, wanao na vizazi vyako bila shaka watakuwapo, wataipeleka nchi pahala ambako wewe ulishindwa na nadhani watafaidi kwa niaba yako. Ni kweli tunatamani tufanye mambo mazuri zaidi ili tuishi kwa neema lakini lazima tukubali kuna muda lazima ufike hata kama kwa wakati huu tumeshindwa kwa bahati mbaya ama kwa kukwamishwa na yeyote. Inajulikana pia kwamba haiwezekani kwa vyovyote vile CCM wawepo madarakani milele lakini si lazima watoke 2020 na si lazima watoke wewe ukiwa hai ili upate madaraka ati kwa sababu ndo uliyeanzisha harakati za mageuzi.

Kweli hiari yashindwa utumwa. Ndugu yangu umejikubalisha kutetea dhulma kwa njia ya philosopy ya kutaka watu wasidai haki. Maalim kama kadhulumiwa unataka akae kimya apakate miguu kama wewe eti CCM itaondoka muda ukifika.

historia ya mapambano haiko hivyo. ikiwa kumkatisha tamaa maalim haijasaidia tokea 1995 hadi leo ambapo dhulma zenu ziko wazi dunia nzima unaomba poo kwa maalim sasa asifanye tena mapambano, mmeshaanza kuchoka siyo?

Maalim endeleea mpaka uingie kaburini hata kama wabaya wako watakuuwa. endelea kupigania haki yako na dunia inakuona.

Mwisho wa ubaya aibu.
 
Hakuna anayemkatisha tamaa Hamadi isipokuwa ni vyema sote tukajua kwamba demokrasia haina cut off date kwamba sasa ama leo hiki lazima kiwe hivi ili kukithi matakwa ya demokrasia.
 
TADEA, UPDP, CCM, UDP, ADC, ACT, CHADEMA, NCCR, CUF, JAHAZI ASILIA nk. Vyote hivyo ni vyama vyetu vya kitaifa na kwa 100% vinatuhusu sote kwa ujumla wetu. Ndo maana Seif Hamad anapita mitaa yote bila kujali itikadi ya wanaoishi huko. Kwa mawazo yako ya kujimilikisha hiyo CUF yako angewaiteni nyumbani kwake ama angewafuateni huko majumbani kwenu ili awahabarishe na hizo habari za kunyang'anywa urais badala ya kufanya hotuba kwenye hadhara isiyohusu wana CUF pekee. Lakini pia siyo lazima waje kula kwangu ama waombe kwangu, ni vyema wakawekeza muda wao katika kazi za kuwaingizia kipato ili wawe na maisha bora kuliko ndoto za kufikiria kumchagua seif ili awapeleke ktk maisha bora.

Wakati mnafanya hadaaa zenu . Watu wako level nyengine za mapambano. Katika hali ya kuishawishi dunia juu ya ubaya wa dhulma zenu. Kumbuka awali mlikuja na udini, na usultani yakaja maridhiano wazungu wakatoa pesa zao na katiba ya zanzibar ikabadilishwa ili kuondoa sintofahamu. kumbe hujuwi hawa wazungu walikuwa wanawachora.

Ukaja uchaguzi wa wazi wa trh 25 oktoba 2015, mukafuta na kuja na figisu zenu, watu wamepeta ushahidi juu ya dhulma zenu. Leo mnapiga kelele eti Seif haitakii mema nchi hii Ebo?

CCM ikubali kuwa imeshindwa na dhulma haisaidii kwa kutaka kunyamazisha watu kudai haki zao. Maalim ni mlengwa wa wazi kadhulumiwa kamwe hawezi kunyamaza kama CCM mnavyotaka.

Mlidhani uchafu wenu wa Machi, 20 utapita bure? mlikosea.

Kubalini mchezo uendelee hivyo hivyo na muwe wavumilivu kwa sababu mlichaguwa kulinywa vumilieni
 
Hakuna anayemkatisha tamaa Hamadi isipokuwa ni vyema sote tukajua kwamba demokrasia haina cut off date kwamba sasa ama leo hiki lazima kiwe hivi ili kukithi matakwa ya demokrasia.

Sasa wewe hapa unazumngumza nini? Maalim kadhulumiwa hilo lijuwe. unataka asitembelee wanachama? unataka asikemee dhulma? Unataka wananchi wasiwe na mapenzi naye na kwa hivyo wasimshangilie? tatizo nini?

Unaonesha chuki zako za wazi kwa Maalim lakini unajificha nyuma ya neno MUDA. unachaguwa na kutaka kumchagulia Maalim njia ya kudai haki yake unayoona inakufaa wewe sio? By the way hio njia anayofanya ni ya kidemokrasia hofu yako nini?

Au nawe ni wale walioapa Maalim asiwe rais nchi hii mpaka afe? mko kwenye jitihada za kumark time ili iwe hawezi tena kwa umri wake sio na sasa unaona jamaa hachoki? ndio ukaomba poo kwa kiroja c " MUDA ukifika" ?

maalim endelea na mapambano ya kudai haki yako na ya maamuzi ya Wazanzibari kwa njia za amani.
 
Uzuri ni kwamba dhambi ikikomaa sana huzaa mauti na hilo kila mmoja wetu analifahamu ,tutavuna tulichokipanda

Watatumia hata mitishamba kuwasemea. Naona mzee mrema hatoshi. Dhulma ni dhulma tu lakini hii ya Oktoba 2015 imezidi. Maalim kawashika mbaya na anachokipigania kina ungwa mkono na ulimwengu wote wa kidemokrasia.

Acha tuvune tulichopanda. Watawala wanahadaa Watanzania kwa uchafu wa Machi, 20 halafu wanataka kutuaminisha kilichofanywa cha kufuta maamuzi ya walio wengi hapo tarehe 25 oktoba 2015 kuwa ni haki .

Hesabu inakataa na kwa hili Maalim asilaumiwe. By thge way hajafanya geni kabisa anatembelea wanachama na wananchi wanamshangilia kwa mapenzi yao dhambi iko wapi?

Kuhusu maneno nyinyi wengine mlitegemea nini ? ende akamsifu Shein sio ? badala ya kumwita dikteta na mpora madaraka?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom