Maalim Seif adai waziri wa Zanzibar hana makosa, safari ya meli ilianzia Tanganyika!!

JokaKuu

Platinum Member
Jul 31, 2006
30,442
55,017
..someni hapo kwenye RED.

..meli hiyo ni mali ya waZNZ.

..imesajiliwa na serikali ya waZNZ.

..kwanini Maalim Seif atubebeshe mzigo wa lawama kwa kuzama kwa meli hiyo??!!

..anadai waziri wa Zanzibar hapaswi kubeba lawama kwasababu safari ya meli haikuanzia ZNZ[read ilianzia Tanganyika].

Makamu wa Kwanza wa Rais alitumia fursa hiyo kutoa mkono wa pole kwa wananchi walioathirika kutokana na ajali mbaya ya boti ya Mv. Skagit ilisababisha vifo vya watu kadhaa.


Amewataka wananchi kuweka imani zao kuwa suala hilo limetokana na mipango ya Mwenyezi Mungu, na kwamba hakuna mtu angeweza kulizuia lisitokee. Katika hatua nyengine Maalim Seif amempongeza aliyekuwa Waziri wa Miundombinu na Mawasilino Mhe. Hamad Massoud Hamad kutokana na kitendo chake cha kijasiri cha kuamua kujiuzulu nafasi hiyo.


Amesema kitendo hicho cha kuwajibika kisiasa kimemjengea heshima yeye mwenyewe, chama chake na taifa kwa ujumla, kitendo ambacho linapaswa kuingwa na viongozi wengine wa nchi iwapo litatokea jambo lolote linalogusa maslahi ya wananchi. "Mhe. Hamad amekuwa mwalimu wa viongozi wa Afrika, kwani viongozi wa Afrika hawana utamauni huo hata likitokea jambo gani, lakini yeye ameamua kujisafisha licha ya kuwa hakuwa na kosa kwa sababu safari ili haikuanzia Zanzibar", alifahamisha Maalim Seif


Kwa upande wake Mwakilishi wa Jimbo la Ole Mhe. Hamad Massoud Hamad ambaye alikuwa akishikilia nafasi hiyo ya uwaziri, amesema aliamua kuachia nafasi hiyo siku chache baada ya tukio, ili kujijengea heshima kisiasa. "Niliamua kujiuzulu nafasi ile kwa nia njema, sikulazimishwa wala kupokea shinikizo kutoka kwa mtu yoyote", alisema Hamad Massoud.
 
Jokakuu,
Huyu maalim Seif unajua wakait mwingine ana Ujinga wa kuzaliwa. hata ndege zinapokaribia anga za tanzania ni jukumu la tanzania kuiongoza ndege sio Jukumu la kule ilipotoka. kama hali ya hewa zanzibar vilikuwa mbaya taarifa inatolewa na zanzibar kwamba meli haziruhusiwi kutia nanga hivyo aidha safari zinaahirishwa ama zina pewa njia mpya..

Meli ilionodka dar salama na hali hakikuwa mbaya zaidi ya upepo ambao usingewez akuizuia kuondoka na ndio maana iliondoka na salama. Tatizo lilikuwa Zanzibar kwenyewe ilipozamia na ndio siku zote ajali hutazamwa ilipotokea.. Hivyo kama sababu ilikuwa muundo mbaya wa meli ambayo kwanza navyosikia ilikuwa Pantoni ikabadilishwa na kufanyiwa marekebisho iwe meli ya abiria. Hii pekee ilitakiwa kufanyiw auchunguzi mkubwa sana kina nani walihusika , kutazama kwa makini hilo Pantoni liliweza vipi kubadilishwa na kuweza kufanya safari ndefu za kwenda na kurudi kati ya Zanzibar na Dar..
 
Jokakuu,
Huyu maalim Seif unajua wakait mwingine ana Ujinga wa kuzaliwa. hata ndege zinapokaribia anga za tanzania ni jukumu la tanzania kuiongoza ndege sio Jukumu la kule ilipotoka. kama hali ya hewa zanzibar vilikuwa mbaya taarifa inatolewa na zanzibar kwamba meli haziruhusiwi kutia nanga hivyo aidha safari zinaahirishwa ama zina pewa njia mpya..

Meli ilionodka dar salama na hali hakikuwa mbaya zaidi ya upepo ambao usingewez akuizuia kuondoka na ndio maana iliondoka na salama. Tatizo lilikuwa Zanzibar kwenyewe ilipozamia na ndio siku zote ajali hutazamwa ilipotokea.. Hivyo kama sababu ilikuwa muundo mbaya wa meli ambayo kwanza navyosikia ilikuwa Pantoni ikabadilishwa na kufanyiwa marekebisho iwe meli ya abiria. Hii pekee ilitakiwa kufanyiw auchunguzi mkubwa sana kina nani walihusika , kutazama kwa makini hilo Pantoni liliweza vipi kubadilishwa na kuweza kufanya safari ndefu za kwenda na kurudi kati ya Zanzibar na Dar..

Jamani yule waziri alijiuzuru kwa sababu ya wizara yake kuruhusu meli isiyo na viwango ku-operate na wala si kwa sababu ya ajali hiyo. Mbona wakati wa ajali ya Mv Spice hakujiuzuru?

Maalim anataka tu kumsafisha, kwanza hakuwepo, alikuwa amelazwa, wanasiasa bwana!
 
..someni hapo kwenye RED.

..meli hiyo ni mali ya waZNZ.

..imesajiliwa na serikali ya waZNZ.

..kwanini Maalim Seif atubebeshe mzigo wa lawama kwa kuzama kwa meli hiyo??!!

..anadai waziri wa Zanzibar hapaswi kubeba lawama kwasababu safari ya meli haikuanzia ZNZ[read ilianzia Tanganyika].

Sheria za usalama wa meli duniani zina ainisha kuwa lawama huenda kwenye bandari iliyotoka meli mara ya mwisho ikitokea hitilafu ya usalama wa hiyo meli. Siyo ilipoandikishwa.

Dunia nzima, hilo linajulikana, meli inaweza kuwa ni ya nchi fulani lakini toka iondoke bandari iliyosajiliwa inaweza kupita mwaka isirudi iwe kazini, na kila bandari duniani inabeba jukumu la kuikaguwa na kuhakikisha usalama ikiwa bandarini kwake.

Ni kama ndege, kama haikidhi usalama wa kuruka au wakaguzi wanaona italeta madhara basi hawairuhusu kuondoka mpaka amma itengenezwe itengemae au hali ya hewa iruhusu au isimamishwe na kuwa scrap bila kuihusisha nchi iliyosajiliwa.

Mzigo wa hii meli, tukitaka tusitake unadondokea bandari ilipoanza safari yake ya mwisho. Iwe ni kwa ubovu wa hiyo meli au hali ya hewa ilikuwaje wakati inaruhusiwa kuondoka.

Hawezi kutoka inspector Zanzibar kukaguwa kila meli iliyosajiliwa Zanzibar kila inapokuwa bandari za nje.

Port State Control (PSC) is the inspection of foreign ships in national ports to verify that the condition of the ship and its equipment comply with the requirements of international regulations and that the ship is manned and operated in compliance with these rules.
psc.jpg
Many of IMO's most important technical conventions contain provisions for ships to be inspected when they visit foreign ports to ensure that they meet IMO requirements.
These inspections were originally intended to be a back up to flag State implementation, but experience has shown that they can be extremely effective, especially if organized on a regional basis. A ship going to a port in one country will normally visit other countries in the region before embarking on its return voyage and it is to everybody's advantage if inspections can be closely co-ordinated.

Soma zaidi: IMO | Port State Control
 
Hapa mwenye makosa ni msajili wa meli ambaye alisajili meli mbovu isiyokidhi viwango vya usalama kubeba abiria. Kuongelea masuala ya wapi kiliondokea kuelekea Zanzibar ni upuuzi ambao ni mwanasiasa asiye makini pekee anaweza kuusema.
 
Hapa mwenye makosa ni msajili wa meli ambaye alisajili meli mbovu isiyokidhi viwango vya usalama kubeba abiria. Kuongelea masuala ya wapi kiliondokea kuelekea Zanzibar ni upuuzi ambao ni mwanasiasa asiye makini pekee anaweza kuusema.

Soma hizo kanuni za International Maritime Organization kabla hujakurupuka: IMO | Port State Control
 
Soma hizo kanuni za International Maritime Organization kabla hujakurupuka: IMO | Port State Control

Wewe ndio unakurupuka. Na kwa kuonyesha jinsi ulivyo mkurupukaji ume "copy" na ku "paste" link ambayo inaongelea port state control. Kwa taarifa yako hiki ulicho bandika hapa kinaongelea ukaguzi wa meli za kigeni zinazotia nanga bandari za ndani ya nchi. Labda kama unasema Zanzibar ni nchi ya kigeni kwa Tanganyika.

Hakuna nchi duniani yenye registry mbili isipokuwa ni Tanzania tu. Na bahati mbaya zaidi hiyo ya pili ya hiki kinachoitwa na wanasiasa kuwa ni "nchi" ya Zanzibar haipo unguja wala pemba na wala hawana control nayo kwa sababu wametoa hiyo kazi kwa mkandarasi aliye Dubai. Huu ndio ninaouita upuuzi wa wanasiasa.
 
Baada ya Seif kugeuzwa nyumba ndogo ya CCM ameishiwa kila kitu. Alichobaki nacho ni mshipa kukosa aibu wa kujikomba kwa kila kitu ili aweze kupata marupurupu. Amepewa nafasi isiyo na kazi zaidi ya kuwa kama fanicha nyumbani. Angalia balozi Idd Seif anayeitwa makamu wa pili anavyofanya kila kitu huku Seif akiachwa uani. Kweli walijua kumtenda. Amegeuka kituko karibu katika kila kitu. Kweli mshahara wa usaliti aibu.
 
Zomba,

..it will be interesting kusikia wahusika toka bandari za ZNZ na Dsm wana maelezo gani.

..lakini ukumbuke kwamba mamlaka ya ZNZ ndiyo iliyosajili meli 2 ambazo zimepata ajali mwaka huu.

..mwisho, kuna maelezo ya ziada hapa ambayo yanaelekeza kwamba "primary responsibility" iko upande wa ZNZ.

This ensures that as many ships as possible are inspected but at the same time prevents ships being delayed by unnecessary inspections. The primary responsibility for ships' standards rests with the flag State - but port State control provides a "safety net" to catch substandard ships.
 
Zomba,

..it will be interesting kusikia wahusika toka bandari za ZNZ na Dsm wana maelezo gani.

..lakini ukumbuke kwamba mamlaka ya ZNZ ndiyo iliyosajili meli 2 ambazo zimepata ajali mwaka huu.

..mwisho, kuna maelezo ya ziada hapa ambayo yanaelekeza kwamba "primary responsibility" iko upande wa ZNZ.

This ensures that as many ships as possible are inspected but at the same time prevents ships being delayed by unnecessary inspections. The primary responsibility for ships' standards rests with the flag State - but port State control provides a "safety net" to catch substandard ships.

Hata isajiliwe New York. Dhamana ni bandari iliyotoka, soma kanuni za IMO, nimeweka link juu huko, tusiongee ushabiki. Kwenye kosa tubainishe ili tusiendelee kuwa na makosa. Ukificha maradhi kifo kitakuumbuwa.

Na ile iliyozama Lake Victoria ikauwa mamia kama si maelfu ilisajiliwa Zanzibar?
 
Hata isajiliwe New York. Dhamana ni bandari iliyotoka, soma kanuni za IMO, nimeweka link juu huko, tusiongee ushabiki. Kwenye kosa tubainishe ili tusiendelee kuwa na makosa. Ukificha maradhi kifo kitakuumbuwa.

Na ile iliyozama Lake Victoria ikauwa mamia kama si maelfu ilisajiliwa Zanzibar?

Iwe bara au visiwani wote ni wazembe walohusika na usajili pamoja na wanaosimamia suala nzima,kuanzia Mr Dhaifu na nyinyiemu wote pamoja nawe.Lakini hatushangai ndo utawala wenu wa kuua.
 
Iwe bara au visiwani wote ni wazembe walohusika na usajili pamoja na wanaosimamia suala nzima,kuanzia Mr Dhaifu na nyinyiemu wote pamoja nawe.Lakini hatushangai ndo utawala wenu wa kuua.

Mlitaka Kikwete aende bandarni akasimame akaguwe kila jahazi na meli na Mwakyembe afanye kazi gani? Na waziri wenu kivuli anaepaswa kusimamia haya madudu alikuwa wapi? anachangisha M4C halafu zikajenge mbezi kwa nanihii?
 
Mlitaka Kikwete aende bandarni akasimame akaguwe kila jahazi na meli na Mwakyembe afanye kazi gani? Na waziri wenu kivuli anaepaswa kusimamia haya madudu alikuwa wapi? anachangisha M4C halafu zikajenge mbezi kwa nanihii?

aaah! malizia mkuu, mbezi kwa josephin au? kuchimba kisima cha ges kilwa! usiogopee za kawaida tu hizo
 
Zomba
hizo provisions za IMO ulizocopy na kupaste zinahusiana sana na ocean going vessel, si kwa usafiri wa ndani. Usikurupuke soma kwanza.
 
Hata isajiliwe New York. Dhamana ni bandari iliyotoka, soma kanuni za IMO, nimeweka link juu huko, tusiongee ushabiki. Kwenye kosa tubainishe ili tusiendelee kuwa na makosa. Ukificha maradhi kifo kitakuumbuwa.

Na ile iliyozama Lake Victoria ikauwa mamia kama si maelfu ilisajiliwa Zanzibar?

Zomba,

..ungesoma post yangu sidhani kama ungetoa majibu hayo.

..yaani ZNZ wasajili meli mitumba au mbovu halafu wategemee zitakaguliwa na bandari za mataifa mengine!!

..again, kanuni ya IMO uliyoinukuu ilimaliza kwa maneno haya hapa chini. zingatia hapo kwenye RED.


This ensures that as many ships as possible are inspected but at the same time prevents ships being delayed by unnecessary inspections. The primary responsibility for ships' standards rests with the flag State - but port State control provides a "safety net" to catch substandard ships.
 
Back
Top Bottom