Maadhimisho ya wiki ya Maji....!!

Katavi

Platinum Member
Aug 31, 2009
41,983
12,702
Tuko katika maadhimisho ya wiki ya maji, lakini watu wengi bado hawapati maji safi na salama. Haya ni maji kwa matumizi ya nyumbani kama kunywa, kupikia nk....

P2050154.JPG
 
Yaani vitu hivi sitaki hata kuviona au kusikia, vinanifanya nijione mnyonge
 
maji.JPG


Hayo maji yanayo pita kuna wanachi wametapisha vyoo vyao huko juu huyu mama anachota ya kupikia
 
maji+ya+shida.jpg


Hivi viunga vya magogoni DAWASCO huwa wanakata maji?
Angalia mama anavyo teseka na mtoto mgongoni
 
Maji%20qe.jpg


Umeona foleni hiyo?
Siioni sababu ya kuwa na wizara ya maji wakati wananchi wenyewe wanakosa maji
 
Inasikitisha kwa kweli na hapo tunajinadi na maisha bora kwa kila mtanzania baada ya miaka 50 ya uhuru!
 
mkuu mende0 watawala wangejua ulipo ungeishi kwa shida, na laiti kama wananchi wengi wangebahatika kuona hii walahi kile chama chenye mrengo wa kushoto kingekamata hii nchi, mark my words. anyway inasikitisha sana mkuu. :peep:
 
hiyo foleni ndo moja kati ya mambo yanayo changia binti zetu kuharibiwa
 
Picha nyingine wandugu zinasikitisha
Maji hayo hata kuyaweka tuu mdomoni hayafai ila huko vijijini ndio ya kupikia na kunywa kwa wazazi wetu
Ni aibu miaka hamsini ya uhuru tunashindwa hata kuchimba visima vya maji na kuwawekea wananchi hata pump za kutumia solar angalau wawe na maji ya uhakika
Maji kama hayo hayafai kw amatumizi ya binadam ila ndio kimbilio la wananchi wengi huko vijijini
Tuna waziri wa maji ambaye nafikiri wajibu wake umebaki kuhakikisha kuwa wakazi wa dar tuu ndio wana shida ya maji wala hajui huko vijijini au miji mingine hata tone la maji hawalioni na wanakunywa maji ya madimbwi au mvua ikinyesha ndio suluhisho kwa yale maji yaliyosimama barabarani
 
Back
Top Bottom