Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Tangu nchi yetu ipate uhuru takribani miaka 50 iliyopita, imepata mafanikio mengi ya kujivunia. Pengine makubwa kuliko yote ni; amani, utulivu, na mshikamano wa wananchi bila yakujali rangi, kabila na dini. Tunu hizo zilijengwa kwa umahili mkubwa wakati wa awamu ya kwanza ya uongozi. Hivi sasa kuna kila dalili zinazodhihilisha wazi kwamba tunu hizo zinazidi kupotea hatua kwa hatua; na hivyo bila ya kuchukuliwa tahadhali uenda tukajikuta tunatumbukia kwenye shimo. Ni kutokana na sababu hiyo natoa maoni kwamba, katika kuhadhimisha miaka 50 ya uhuru, badala ya kuteketeza raslimali nyingi kwenye sherehe, ingelikuwa vyema ukaandaliwa utaratibu wa wananchi wenyewe kufanya tathmini ya kina, ili kubaini ni wapi sisi kama taifa tumekwenda kombo, na ni hatua zipi zinahitajika kurekebisha hali hiyo.