Ma-Doctor na watambuzi hebu nijuzeni

FirstLady1

JF-Expert Member
Jul 29, 2009
16,792
5,373
Hivi kama hapo nyuma ulijifungua kwa Operation na watoto wote watakaofatia inakuwa ni operation pia ?

FL1

 
Sio lazima...inategemea na sababu ya mtu kufanya hivyo mara ya kwanza!!Kama kulikua na complications wataangalia mara inayofuatia ikiwa zitakuwepo au la...kama hazitakuwepo basi unaweza kutumia njia ya kawaida!

Na kama ulifanya vile tu bila kua na matatizo yoyote mara ya pili waweza kuamua kutumia njia ya kawaida.
 
Sio lazima...inategemea na sababu ya mtu kufanya hivyo mara ya kwanza!!Kama kulikua na complications wataangalia mara inayofuatia ikiwa zitakuwepo au la...kama hazitakuwepo basi unaweza kutumia njia ya kawaida!

Na kama ulifanya vile tu bila kua na matatizo yoyote mara ya pili waweza kuamua kutumia njia ya kawaida.

nakushukuru sana my dear Lizzy kwa kunielewesha

Maana naplan sasa nianze mikiki ya kuiongeza dunia ila nikawaza mmh first time haka ka binti kangu kalinitesa mpaka nukasema naapa sitarudia tena Ila sasa nimetamani tena ndo najiuliza hivi next baby mungu akinijaalia itakuwaje tena?
 
Kama alivyokueleza dada Lizzy, kurudia tena kujifungua kwa caesarean section (c/s) kunategemea na sababu iliyopelekea ukajifungua kwa njia hiyo in the first place.

Kuna sababu tunaziita 'absolute indication', ukiwa na hii basi uzazi wako wote utakuwa kwa c/s. Sababu hizi zinajumuisha mwanamke kuwa mfupi sana chini ya 150cm, mara nyingi hawa nyonga (pelvis) yao inakuwa ndogo kuweza kuruhusu an average baby to pass kutonana na kutowiana kati ya kitangulizi cha mtoto na nyonga (cephalo-pelvis disproportion (CPD)); mwanamke mwenye ulemavu unaoathiri sehemu ya nyonga na hivyo mtoto hawezi kupita; na kama ulishajifungua kwa c/s mara 2 au zaidi.

Lakini sabau nyingi za c/s huwa sio lazima zijirudie...mfano mtoto mkubwa, kitovu kutokeza nje ya uke kabla mtoto hajazaliwa (cord prolapse), mtoto kuchoka (hii ni sababu mara nyingi sana), uchungu kuchukua muda mrefu sana (prolonged labor), kifafa cha mimba, kitangulizi cha miguu (breech presentation), kupasuka kizazi etc..

Kwa sababu ambazo si lazima zijirudie, daktari/mkunga anaweza kumpa mama mjamzito nafasi ya kujifungua kawaida kwa uangalizi wa karibu huku ukimpima mara kwa mara mama kuhusu maendeleo yake ya uchungu na uwezo wa kovu la kwenye kizazi lililotokana na c/s ya uzazi uliopita kuhimili uchungu, tunaita 'trial of scar'. Ila sharti hapa ni kuwa mama huyo awe amejifungua kwa c/s si zaidi ya mara moja.
 
Kama alivyokueleza dada Lizzy, kurudia tena kujifungua kwa caesarean section (c/s) kunategemea na sababu iliyopelekea ukajifungua kwa njia hiyo in the first place.

Kuna sababu tunaziita 'absolute indication', ukiwa na hii basi uzazi wako wote utakuwa kwa c/s. Sababu hizi zinajumuisha mwanamke kuwa mfupi sana chini ya 150cm, mara nyingi hawa nyonga (pelvis) yao inakuwa ndogo kuweza kuruhusu an average baby to pass kutonana na kutowiana kati ya kitangulizi cha mtoto na nyonga (cephalo-pelvis disproportion (CPD)); mwanamke mwenye ulemavu unaoathiri sehemu ya nyonga na hivyo mtoto hawezi kupita; na kama ulishajifungua kwa c/s mara 2 au zaidi.

Lakini sabau nyingi za c/s huwa sio lazima zijirudie...mfano mtoto mkubwa, kitovu kutokeza nje ya uke kabla mtoto hajazaliwa (cord prolapse), mtoto kuchoka (hii ni sababu mara nyingi sana), uchungu kuchukua muda mrefu sana (prolonged labor), kifafa cha mimba, kitangulizi cha miguu (breech presentation), kupasuka kizazi etc..

Kwa sababu ambazo si lazima zijirudie, daktari/mkunga anaweza kumpa mama mjamzito nafasi ya kujifungua kawaida kwa uangalizi wa karibu huku ukimpima mara kwa mara mama kuhusu maendeleo yake ya uchungu na uwezo wa kovu la kwenye kizazi lililotokana na c/s ya uzazi uliopita kuhimili uchungu, tunaita 'trial of scar'. Ila sharti hapa ni kuwa mama huyo awe amejifungua kwa c/s si zaidi ya mara moja.

thanks Riwa Nadhani nina urefu mzuri tu wa haja na pia tatizo langu mtoto aligoma kabisa kugeuka na alikaa vibaya tumboni mpaka hatua za mwisho miezi ya saba na nane nikawa chini ya uangalizi wa Ma DR mpaka pale nilipofanikiwa kujipatia kababy kangu salama salimi ingawa kwa operation
Ila sasa napenda kuongeza baby mwingine..Naomba msaada wa kimawazo labda ni mazoezi gani natakiwa kufanya katika kipindi chote hicho ili isijejirudia kama mwanzo
natanguliza shukrani ..
 
thanks Riwa Nadhani nina urefu mzuri tu wa haja na pia tatizo langu mtoto aligoma kabisa kugeuka na alikaa vibaya tumboni mpaka hatua za mwisho miezi ya saba na nane nikawa chini ya uangalizi wa Ma DR mpaka pale nilipofanikiwa kujipatia kababy kangu salama salimi ingawa kwa operation
Ila sasa napenda kuongeza baby mwingine..Naomba msaada wa kimawazo labda ni mazoezi gani natakiwa kufanya katika kipindi chote hicho ili isijejirudia kama mwanzo
natanguliza shukrani ..

tatizo hilo lililopelekea ukafanyiwa c/s sio absolute...sio lazima kuwa next pregnancy mtoto atakaa tena vibaya. hivyo utafanyiawa trial of scar ambapo unazalia hospitali chini ya uangalizi wa karibu wa daktari. wengi tu wameshajifungua kawaida baada ya c/s katika uzazi wa kwanza.
 
Kama alivyokueleza dada Lizzy, kurudia tena kujifungua kwa caesarean section (c/s) kunategemea na sababu iliyopelekea ukajifungua kwa njia hiyo in the first place.

Kuna sababu tunaziita 'absolute indication', ukiwa na hii basi uzazi wako wote utakuwa kwa c/s. Sababu hizi zinajumuisha mwanamke kuwa mfupi sana chini ya 150cm, mara nyingi hawa nyonga (pelvis) yao inakuwa ndogo kuweza kuruhusu an average baby to pass kutonana na kutowiana kati ya kitangulizi cha mtoto na nyonga (cephalo-pelvis disproportion (CPD)); mwanamke mwenye ulemavu unaoathiri sehemu ya nyonga na hivyo mtoto hawezi kupita; na kama ulishajifungua kwa c/s mara 2 au zaidi.

Lakini sabau nyingi za c/s huwa sio lazima zijirudie...mfano mtoto mkubwa, kitovu kutokeza nje ya uke kabla mtoto hajazaliwa (cord prolapse), mtoto kuchoka (hii ni sababu mara nyingi sana), uchungu kuchukua muda mrefu sana (prolonged labor), kifafa cha mimba, kitangulizi cha miguu (breech presentation), kupasuka kizazi etc..

Kwa sababu ambazo si lazima zijirudie, daktari/mkunga anaweza kumpa mama mjamzito nafasi ya kujifungua kawaida kwa uangalizi wa karibu huku ukimpima mara kwa mara mama kuhusu maendeleo yake ya uchungu na uwezo wa kovu la kwenye kizazi lililotokana na c/s ya uzazi uliopita kuhimili uchungu, tunaita 'trial of scar'. Ila sharti hapa ni kuwa mama huyo awe amejifungua kwa c/s si zaidi ya mara moja.
..Riwa kuna wanawake wengine wanadai hawapendi kujifungua kwa njia ya kawaida eti kukwepa maumivu so hupenda kuzaa kwa operation. Nina mtuninaye mfahamu ana watoto wawili wote aliomba mwenyewe azalishwe kwa operation na tumbo ukiliona utadhani binti wa miaka 12...
 
..Riwa kuna wanawake wengine wanadai hawapendi kujifungua kwa njia ya kawaida eti kukwepa maumivu so hupenda kuzaa kwa operation. Nina mtuninaye mfahamu ana watoto wawili wote aliomba mwenyewe azalishwe kwa operation na tumbo ukiliona utadhani binti wa miaka 12...

Yeah, zamani ilikuwa vigumu kidogo, lakini siku hizi na maobstetrician wamejaa tele, na mwanamke ana haki ya kuomba services stahiki...wapo kadhaa ambao wanaopt c/s kuepuka uchungu! na wanahudumiwa, lakini kwenye private hospitals zaidi..
 
hiyo trial of scar uwe na private doc, kwenye hospital za mh jk utaishia kurupture uterus. B careful with ur next pregnancy!
 
hiyo trial of scar uwe na private doc, kwenye hospital za mh jk utaishia kurupture uterus. B careful with ur next pregnancy!

Ahsante Nyalotsi kwa kulileta hili...maana ya trial of scar ni hapo kwenye kupima uwezo wa hilo kovu kwenye kizazi lililotokana na uzazi uliopita kwa operation, na kuona kama litaweza himili uchungu wa uzazi husika. Unahitaji uangalizi wa karibu wa daktari au nesi/mkunga mzoefu ambaye mara kwa mara atapima strength ya hilo kovu against progress ya labor, ili usifikie hali ya kuchanika kizazi (kurupture uterus). Kwa kweli kama hamna uwezekano wa uangalizi wa hali ya juu....don't try the scar!
 
Hivi kama hapo nyuma ulijifungua kwa Operation na watoto wote watakaofatia inakuwa ni operation pia ?

FL1

Hivi wewe ni yuleyule FL1 au ni pacha wako maana yule wa zamani kuna siku kama kichwa changu kizuri ingawa avata mpya ila jina ni lilelile alikuwa akipongwezwa katikia siku yake ya kuzaliwa na kuulizwa umri akasema ana miaka 40 (2years imepita kama sikosei) na tena akasema anakaribia kupata wajukuu. au wajukuu ndo hao watoto wa uzeeni? Ufafanuzi please.

By the way kila la kheri.
 
Hivi wewe ni yuleyule FL1 au ni pacha wako maana yule wa zamani kuna siku kama kichwa changu kizuri ingawa avata mpya ila jina ni lilelile alikuwa akipongwezwa katikia siku yake ya kuzaliwa na kuulizwa umri akasema ana miaka 40 (2years imepita kama sikosei) na tena akasema anakaribia kupata wajukuu. au wajukuu ndo hao watoto wa uzeeni? Ufafanuzi please.

By the way kila la kheri.

hahaha Rubi bado ni ka safari karefu ka kufika 40 mungu anisaidie
Labda wakati najibu hiyo post nilikuwa na hangover
Mbona umepotea sana mpendwa
Miss you big time
 
heeh! mi nilitaka nikuambie unipe dawa ya ku-rewind! all the best. kuna ndugu yangu alijifungua kwa njia ya kawaida a year after kufanyiwa operation ya kutoa mtoto aliefia tumboni wa miezi sita na uvimbe mkubwa sana. tatizo lake alikuwa na maumivu sana ya mshono,ila kujifungua ilikuwa chapchap,uchungu 2 hrs then kitu mwake. kama ukiwa active, unatembea na kupanda ngazi u will be ok. kila la kher mpenzi
hahaha Rubi bado ni ka safari karefu ka kufika 40 mungu anisaidie<br />
Labda wakati najibu hiyo post nilikuwa na hangover <br />
Mbona umepotea sana mpendwa<br />
Miss you big time
<br />
<br />
 
heeh! mi nilitaka nikuambie unipe dawa ya ku-rewind! all the best. kuna ndugu yangu alijifungua kwa njia ya kawaida a year after kufanyiwa operation ya kutoa mtoto aliefia tumboni wa miezi sita na uvimbe mkubwa sana. tatizo lake alikuwa na maumivu sana ya mshono,ila kujifungua ilikuwa chapchap,uchungu 2 hrs then kitu mwake. kama ukiwa active, unatembea na kupanda ngazi u will be ok. kila la kher mpenzi
<br />
<br />

thanks swirry ngoja sasa nianze harakati wish me luck
 
thanks swirry ngoja sasa nianze harakati wish me luck
<br />
<br />
kuna msemo wa kwenye vtab unasema First caeserian section alwayz controverse badala ya alwayz c/s..be careful coz medical issues never read books. unaweza kukutana nayo ww tofaut na wa2 walivyozoea!
 
Mkuu Riwa amechanganua vizuri sana, kwa kuongeza, kanuni nyingine ni kuwa, kama umepata siza mbili (C/S) bila kujali sababu zilizopelekea , uzazi wa tatu lazima iwe C/S!, kwa lugha nyingine ni kuwa kama una 2 previous C/S, hiyo ni ABSOLUTE indication ya C/S kwa mimba inayofuata, na C/S ya tatu inaambatana na kufungwa kizazi permanently hata kama mimba zote umekosa watoto, though in rare circumstances unaweza pewa nafasi nyingine but under very close monitoring.
 
Mkuu Riwa amechanganua vizuri sana, kwa kuongeza, kanuni nyingine ni kuwa, kama umepata siza mbili (C/S) bila kujali sababu zilizopelekea , uzazi wa tatu lazima iwe C/S!, kwa lugha nyingine ni kuwa kama una 2 previous C/S, hiyo ni ABSOLUTE indication ya C/S kwa mimba inayofuata, na C/S ya tatu inaambatana na kufungwa kizazi permanently hata kama mimba zote umekosa watoto, though in rare circumstances unaweza pewa nafasi nyingine but under very close monitoring.

nina moja tu hata hivyo nawashukuru wote kwa ushauri kwa vile ninae Gyna wangu pia iyabidi nijaribu kuongea nae zaidi
Mbarikiwe
 
Hivi wewe ni yuleyule FL1 au ni pacha wako maana yule wa zamani kuna siku kama kichwa changu kizuri ingawa avata mpya ila jina ni lilelile alikuwa akipongwezwa katikia siku yake ya kuzaliwa na kuulizwa umri akasema ana miaka 40 (2years imepita kama sikosei) na tena akasema anakaribia kupata wajukuu. au wajukuu ndo hao watoto wa uzeeni? Ufafanuzi please.

By the way kila la kheri.

Una kumbu kumbu nzuri sana wewe, hata mimi nakumbuka alisema ana 40s tena kuna kipindi alisema hata kuolewa alichelewa. Kweli humu JF kuna watu wala si wa kuwaamini wanachoongea. Sasa una 40 wataka kuzaa mtoto mwingine wa nini?
 
Una kumbu kumbu nzuri sana wewe, hata mimi nakumbuka alisema ana 40s tena kuna kipindi alisema hata kuolewa alichelewa. Kweli humu JF kuna watu wala si wa kuwaamini wanachoongea. Sasa una 40 wataka kuzaa mtoto mwingine wa nini?
Sister Sofia unajua hapa Ndani kuna Ma FL wawili kwa hiyo mmoja anaweza kuongea mkadhani ni mie, hata sikumbuki tena kama nilisema nina miaka 40 labda was joking
mama unajua hapa JF sio kila info ni ya kuamini sana ..kuna wakati mtu anakuuliza katika Jokes na wewe unajibu hivo hivo ,kuna wakati mtu anakuuliza akiwa serious na wewe unajibu hivo hivo..
Lakini mie sio mzee kivile jamani .. bado niko kwenye mkakati wa kuongeza familia..

karibu kwangu Sister Sofia
 
Kama alivyokueleza dada Lizzy, kurudia tena kujifungua kwa caesarean section (c/s) kunategemea na sababu iliyopelekea ukajifungua kwa njia hiyo in the first place. <br />
<br />
Kuna sababu tunaziita 'absolute indication', ukiwa na hii basi uzazi wako wote utakuwa kwa c/s. Sababu hizi zinajumuisha mwanamke kuwa mfupi sana chini ya 150cm, mara nyingi hawa nyonga (pelvis) yao inakuwa ndogo kuweza kuruhusu an average baby to pass kutonana na kutowiana kati ya kitangulizi cha mtoto na nyonga (cephalo-pelvis disproportion (CPD)); mwanamke mwenye ulemavu unaoathiri sehemu ya nyonga na hivyo mtoto hawezi kupita; na kama ulishajifungua kwa c/s mara 2 au zaidi.<br />
<br />
Lakini sabau nyingi za c/s huwa sio lazima zijirudie...mfano mtoto mkubwa, kitovu kutokeza nje ya uke kabla mtoto hajazaliwa (cord prolapse), mtoto kuchoka (hii ni sababu mara nyingi sana), uchungu kuchukua muda mrefu sana (prolonged labor), kifafa cha mimba, kitangulizi cha miguu (breech presentation), kupasuka kizazi etc..<br />
<br />
Kwa sababu ambazo si lazima zijirudie, daktari/mkunga anaweza kumpa mama mjamzito nafasi ya kujifungua kawaida kwa uangalizi wa karibu huku ukimpima mara kwa mara mama kuhusu maendeleo yake ya uchungu na uwezo wa kovu la kwenye kizazi lililotokana na c/s ya uzazi uliopita kuhimili uchungu, tunaita 'trial of scar'. Ila sharti hapa ni kuwa mama huyo awe amejifungua kwa c/s si zaidi ya mara moja.
<br />
<br />
my wyf mara ya kwanza ni operation thn second tym madoctorz wakaniambia lazima iwe operation it waz last year, mke wangu hakuwa na tatizo lolote bt baada tu ya kucheck mshono ndo ikawa tabu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom