Crashwise
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 22,227
- 8,735
M4C ipo Simanjiro, Jana walifanya mkutano kwenye kijiji cha Sukro, masaini Kabisa. Leo watafanya kwenye kijiji cha Terat ambayo ni centre kubwa kulinganisha na Sukro. Ni operesheni ya siku Tatu Mpaka Kesho ikiongzwa Joshua Nasari na Milya, na Paulina Gekul MB viti Maalum mkoa wa Manyara. Wamasai wameamka sana, wengine Hata kiswahili hawajui hivyo wanalazimka kupiga na kimasai au kutafsiri. Wanachama zaidi 110 hivi walijiunga chadema Jana. Wengi wanamlalamikia na kujutia kuwa na Sendeka Kama MB wao. Kwa Kweli Hali ni mbaya. Hakuna maji, Barabara, huduma za afya, umeme, minadani hakuna vyoo.