JIULIZE KWANZA
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 2,569
- 499
Nashukuru kwa ushauri in fact sio ushauri mmbaya ila nijibu Swali moja tuu. Je Unajua operation sangra na M4C vinavoendelea Moro na kwingineko? Chadema nzima iko vijijini ni Lema peke Yake Ndio anapiga jaramba ughaibuni sasa sioni kinacho haribika kwa Lema pekee kutokuweko vijijini ilihali uongozi wote uko vijijini kwa sasa. Ingekuwa Hakuna mtu aliyeenda kujenga chama vijijini na badala Yake wawe na Lema uko wote apo ningekugongea like mpaka za ziada ila kwa hili ndugu nisamehe sijashawishika nasisitiza Asante kwa ushauri
Ubishi ni kipaji kama vilivyo vipaji vingine vyote ambavyo mwanadamu kajaaliwa na Mungu, narudia tena hiki cdm wanachofanya si sahihi, lazima tuwashauri kuwa raslimali chache walizonazo wahakikishe wanazitumia vizuri, na nguvu zao waelekeze vijijini maana huko ndio kuna wajinga wengi wa elimu ya urai na ccm wanautumia ujinga wa hao wa vijijini kama mtaji wao wa kisiasa. sasa kama huu ushauri unuona hauna mashiko au unakuhalalishia kuwa mimi ni ccm.sina cha kufanya kwani hayo yatakuwa matatizo yako.