MAGAMBA a.k.a WADHAIFU jana waliandika humu JF kuwa raia walio hudhuria walikuwa chini ya arobaini (40)
Mkuu mbona kawaida sana hakuna jipya..
Mkuu mbona kawaida sana hakuna jipya..
Weka picha ya sinza acha longolongo.
Weye kweli giza, lini CHADEMa ilifanya mkutano sehemu hiyo ikapata idadi kama hiyo?
kwa umati umati huu Mungu ashukuriwe mwelekeo ni mzuri viva piposss pawaaaaaaaaaaaaaaaaaPipozi Pawa Mungu yuko nanyi amini haya nisemayo .It is about time watu wako mbolewe View attachment 57322 wadau. habar zenu binafsi. hii ni picha niliyofanikiwa kuipiga kwa kutumia kisimu changu cha laini mbili. hawa ni sehemu ya wakazi wa Kimanga waliohudhuria 'somo' la mabadiliko lililokuwa likitolewa kwa ufasaha na makamanda wetu, Mh. Godbless Lema, na mtu mzima, miaka 80, Mh. Mzee Philemon Ndesamburo. kwa umati umati huu Mungu ashukuriwe mwelekeo ni mzuri viva piposss pawaaaaaaaaaaaaaaaaa naweza tu kuwahakikishia kuwa hakukuwa na msafara wa aina yoyote kwenda kwenye mkutano ule, mimi huwa nashinda Mawenzi (ambapo msafara wowote wa magari ukiwa unaelekea Kimanga lazima upitie hapo). sikuona mbwembwe za aina hiyo. kila mtu alienda kivyake bila kusukumwa wala kutishwa. Dondoo: 1. Kamanda Lema alizungumzia sana ishu ya udini na namna inavyotumiwa vibaya na watu wa ccm, kwa lengo la kuwagawa na kuwatawala Watanzania. Somo lilieleweka vema, kwa kila muislam na mkristo aliyehudhuria, na kwa wale ambao hamkuhudhuria eleweni hivyo. Lema pia akadai ccm wamekuwa wakieneza propaganda kuwa chadema ni chama cha wachaga, akaeleze kuwa huo ni uwongo uliopindukia, lakini pia akahoji, hivi kipi cha maana basi? kwamba tumkatae mtu kwa uchaga wake, lakini akija mvutabange, mwizi, mbadhirifu wa mali za umma tumchague kutuongoza ati kwa vile siyo mchaga? Alihoji. 2. Ndesamburo aliwalaumu wananchi wa Dar Es Salaam kwa uwoga na kukosa uthubutu. Akarejea jimbo lake la moshi kwa namna ambavyo limekuwa mahala salama kwa watanzania waishio huko, tangu mwaka 2000 lipo chini ya chadema likiwa na huduma zote muhimu za kijamii, na pia ndiyo jiji linaloongoza kwa usafi kulinganisha na majiji mengine. Akaendelea kusema mwaka 2000, mkapa, akiwa Rais alijaribu kutumia vibaya madaraka yake ya urais kwa kumtisha msimamizi wa uchaguzi kuwa wamtangaze mgombea wa ccm kuwa mshindi, lakini vijana wa pipoz pawa walikuwa macho, tayari kwa lolote, askari wakanywea na mzee ndesapesa akaukwaa ubunge. 3. Diwani wa Kipawa ni jembe. Mama anachana kama 2-Pac Shakur. yeye aliwashauri kina mama waamke. wanadanganywa kwa kanga na vilemba vya kuteleza wanaisaliti nchi. Yalikuwa mengi. na ama hakika kufikia mwaka 2015, wengi watakuwa wameamka kutoka usingizini na mabadiliko ya kweli yatafikiwa. Pipozi Pawa Mungu yuko nanyi amini haya nisemayo .It is about time watu wako mbolewe
Hivi wewe hunapajua Tabata Kimanga? Kwanza hakuna uwanja mkutano umefanyika barabarani na barabara za Kimanga ni nyembamba sana na watu wamejibana hapo lazima uone watu wengi.
Wale wazee walokuwa wakilia kutoka na hutuba ya Ndg Lema, nao kama una picha zao ziweke.Na pia Lema alipoacha gari yake kuwahi majukumu ya chama nayo iweke kama ipo, tuacha ubinafsi Lema anakubarika kwani jana gari yake vijana walitakaa kuisukuma ila alikataa, alipopanda bodaboda alishangiliwa sana na watu.Lengo letu jimbo la Segerea 2015 liwe chini ya CHaDEMA.
usihofu nitaziweka mkuu. Hawa magamba nyeupe wao wanaona nyeusi, wala msitumie nguvu nyingi kuwaelewesha. Uwezo wao wa kufikiri umezibwa na gamba.
Sahihisho mkuu,huyo diwani niwa kata ya Kimanga mkuu....nashikuru kwa habari tuliwakilisha vyema.View attachment 57322
wadau. habar zenu binafsi.
hii ni picha niliyofanikiwa kuipiga kwa kutumia kisimu changu cha laini mbili. hawa ni sehemu ya wakazi wa Kimanga waliohudhuria 'somo' la mabadiliko lililokuwa likitolewa kwa ufasaha na makamanda wetu, Mh. Godbless Lema, na mtu mzima, miaka 80, Mh. Mzee Philemon Ndesamburo.
naweza tu kuwahakikishia kuwa hakukuwa na msafara wa aina yoyote kwenda kwenye mkutano ule, mimi huwa nashinda Mawenzi (ambapo msafara wowote wa magari ukiwa unaelekea Kimanga lazima upitie hapo). sikuona mbwembwe za aina hiyo. kila mtu alienda kivyake bila kusukumwa wala kutishwa.
Dondoo:
1. Kamanda Lema alizungumzia sana ishu ya udini na namna inavyotumiwa vibaya na watu wa ccm, kwa lengo la kuwagawa na kuwatawala Watanzania. Somo lilieleweka vema, kwa kila muislam na mkristo aliyehudhuria, na kwa wale ambao hamkuhudhuria eleweni hivyo.
Lema pia akadai ccm wamekuwa wakieneza propaganda kuwa chadema ni chama cha wachaga, akaeleze kuwa huo ni uwongo uliopindukia, lakini pia akahoji, hivi kipi cha maana basi? kwamba tumkatae mtu kwa uchaga wake, lakini akija mvutabange, mwizi, mbadhirifu wa mali za umma tumchague kutuongoza ati kwa vile siyo mchaga? Alihoji.
2. Ndesamburo aliwalaumu wananchi wa Dar Es Salaam kwa uwoga na kukosa uthubutu. Akarejea jimbo lake la moshi kwa namna ambavyo limekuwa mahala salama kwa watanzania waishio huko, tangu mwaka 2000 lipo chini ya chadema likiwa na huduma zote muhimu za kijamii, na pia ndiyo jiji linaloongoza kwa usafi kulinganisha na majiji mengine. Akaendelea kusema mwaka 2000, mkapa, akiwa Rais alijaribu kutumia vibaya madaraka yake ya urais kwa kumtisha msimamizi wa uchaguzi kuwa wamtangaze mgombea wa ccm kuwa mshindi, lakini vijana wa pipoz pawa walikuwa macho, tayari kwa lolote, askari wakanywea na mzee ndesapesa akaukwaa ubunge.
3. Diwani wa Kipawa ni jembe. Mama anachana kama 2-Pac Shakur. yeye aliwashauri kina mama waamke. wanadanganywa kwa kanga na vilemba vya kuteleza wanaisaliti nchi.
Yalikuwa mengi. na ama hakika kufikia mwaka 2015, wengi watakuwa wameamka kutoka usingizini na mabadiliko ya kweli yatafikiwa.
Pipooooooooooooz!