Hapa mpiga filimbi,Hivi huu ni uwanja ule ule tulioona picha zake jana?
Asante Mchukia Fisadi yaani nimesoma maelezo yako kama vile namsikiliza Rwakatare shukrani inaonyesha jinsi watu tunavyoitakia mema nchi yetu.Thanks Quinine.
Kwenye ile thread yangu ya jana nilionyesha uzinduzi wa CUF na leo nimeonyesha wa Chadema. Hali unayoona inaashiria nini? Ni msg tosha kwa Sisi Mafisadi kwamba watu wamechoka na hawadanganyiki tena. Wako tayari kukitosa chama hicho mwaka 2010.
Mark you kwamba mkutano huu haukuwa kati kati ya mji bali umefanyika nje kidogo ya mji kwenye viunga vya mji. Lwakatare amesema watu wasogope kwenda kupiga kura kwa kuogopa kuwa zitaibiwa, maana safari hii anawahakikishia kuwa hakuna hatakura moja itakayoibiwa maana Chadema wamejiandaa kukabiliana kwa hali yoyote na hali hiyo iliyotokea 2005.
Na ametahadhalisha wale wanaotoa vitisho kwamba baada ya kupiga kura watu warudi majumbani kwamba hiyo si kauli ya kisheria maana sheria inawataka watu wakishapiga kura wakae mita 200 toka kituo cha kupigia kura. Amesema kama waheshimiwa wanaotoa kauli hizo wanataka zitekelezwe waitishe bunge na kuibadili sheria hiyo ili isomeke kama wanavyotaka, la sivyo watu watafanya kama sheria isemavyo yaani kukaa mita 200 hadi matokeo yatakapotangazwa. Ameonya wale wanaojifanya kuwa ni maaskari wanaojaribu kufanya fujo ili kuleta vurugu katika matokeo wawe waangalifu maana watu wamejiweka tayari kwa lolote kulinda matokeo yao. Na kwamba hata yeye akishindwa kihalali ataheshimu maamuzi ya wapiga kura kwa kukubali kuwa kashindwa. Lakini akawataka na wagombea wenzake kufanya hivyo bila hila wala kuoneana.
Ameomba Takukuru kama kweli wamemaanisha kuondoa rushwa katika uchaguzi waanze sasa badala ya kuonekana kwamba moto waliokuwa nao ulikuwa ni wa zoezi la kura za maoni ya Sisi M tu. Amewaambia kuwa anaelewa kuwa kwa sasa kuna rushwa inatembea jimboni na ni vema wafuatilie kwa uangalifu.
Amesema kuwa ameazimia kuifanya Manispaa ya mji wa Bukoba kuwa chini ya uongozi wa Chadema na kuleta mabadiliko makubwa ya kiutendaji katika manispaa hiyo. Amesema anategemea mabadiliko hayo atayaongoza yeye akishirikiana na madiwani wa Chadema kama watapewa ridhaa kuongoza manispaa hiyo. Kuongeza nguvu katika hoja hiyo katoa mifano ya Halmashauri zilizokuwa chini ya Chadema kama Kigoma, Karatu na Tarime walivyofanikiwa kuanzisha mifuko ya elimu kusaidia wasioweza kulipia watoto karo mashuleni pamoja na huduma zingine kama afya n.k.
Ni udini tu walionao hawana siasa kitu ,yaani tusubiri ushindi wa kimbunga wa CCM ,si mumepeleka mashitaka kwa Tendwa .sasa subirini jiwe la CCM ,mnapigwa na chini kushinda walivyokoseshwa CUF 2005:glasses-nerdy:
Ni udini tu walionao hawana siasa kitu ,yaani tusubiri ushindi wa kimbunga wa CCM ,si mumepeleka mashitaka kwa Tendwa .sasa subirini jiwe la CCM ,mnapigwa na chini kushinda walivyokoseshwa CUF 2005:glasses-nerdy:
Unajua The Invincible watu wanaoeneza udini kama uliyemjibu hapo juu wamebaki kuonekana kama vituko maana watu wamewachoka hawawajali tena wala hawana interest nao. Mtu anaingiza udini sehemu isiyo hata na elements za dini, tuendelee hivi hivi mtu akilete udini anaachwa peke yake.He he heee!
Aiseee!
Ni udini tu walionao hawana siasa kitu ,yaani tusubiri ushindi wa kimbunga wa CCM ,si mumepeleka mashitaka kwa Tendwa .sasa subirini jiwe la CCM ,mnapigwa na chini kushinda walivyokoseshwa CUF 2005:glasses-nerdy:
Ni element za ufisadi zinamsumbua tu.kagasheki aondolewe ana mbwembwe sana yule mzee