Mndundu
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 233
- 34
Irente View Point Hotel iliyopo Lushoto (mazingira ya Nje na Ndani ya Vyumba)
Naomba bei za kulala hapo nataka nije vekesheni Lushoto.
Mzee details zao unaweza kuzipata hapa http://www.irenteview.com/contacts.htm na cost hapa http://www.irenteview.com/booking.htm . Meneja wao bwana Msuya ni mtu poa sana.
Asante Mkuu kwa Picha. Nilishawahi kufika Lushoto zamani saana. Nilipandishwa kwenye basi la East Africa Railway (mabasi meupe na mstari mweusi) na sister wangu tukiwa na mwanae. Tulisafiri na kijana mmoja kama Kondakta wa Bus aliyeonekana kufahamu tunakwenda wapi maana tulikuwa below 5 years. Tulipoingia tu mwanzo wa mji (kulikuwa na barabara ya lami na taa za barabarani) basi likasimama na tukashushwa na hapo kulikuwa na kijana aliyekuja kutupokea. Alituchukua hadi kwa babu mmoja akienda kwa jina la Mzee Mtangi. Nyumba nakumbuka ilikuwa eneo la milimani, nyasi safi kabisaa. Babu alikuwa na kigorofa chake miaka hiyo ya 70 na mke wa Kizungu juu. Tulikaa wiki mbili na tukarudishwa tena Korogwe kwa njia hiyohiyo.
Natamani siku moja nirudi tena nilione hili eneo. Lushoto kwa kweli ni pazuri saana na ukichukulia hali ya hewa na mimea inayoota hapo, kweli mtu unapumzika saafi sana.
Nyumba ya Rais mstaafu kwa mbaaaali na maporomoko ya maji (water fall) yaliyo njia ya kwenda kifungiro
Mafisadi wanajuana kwa ufisadi wao na kulindana.Hapo jirani na nyumba ya Mkapa pia kuna nyumba ya Ngwilizi. Tena inasemekana ndo aliyemtafutia hicho kiwanja.
Mafisadi wanajuana kwa ufisadi wao na kulindana.