Lunyungu ( JF member) is seriously ill ! - UPDATES

Bado sijaelewa kwa nini binadamu wengine wana roho mbaya kiasi hii,Mtu uko kwenye maumivi yeye anafanya ufisadi hata kwenye afya yako.inatia uchungu.Ni kweli tunahitaji mabadiliko

:A S-danger:Jambo ambalo nilikuwa siamini ni kukosekana kwa maadili katika sekta ya tiba. Matabibu wengi kwenye Hospitali kubwa hawana hata chembe ya utu japo walikula kiapo kutumikia wagonjwa kwa ujuzi wao wote. Sasa sina imani nao na ninaogopa Hospitali hizo maana linalofanyika huko ni uuaji mtupu lakini kwa vile wanalindwa na sheria ndiyo maana hata wanapoua hawaonekani kuwa wametoka nje ya maadili ya taaluma yao. Amin usiamini ndio madaktari wetu na iwapo mtu ataumwa nashauri awe mwangalifu sana. Pole sana Lunyungu na ugua pole. Mwenyezi Mungu ndiye ajuaye yote. Nakutakia upone haraka.
 
Lunyungu, umenipa matumaini kwamba unarejea kwenye hali yako... i smiled when i read this part of your post, sababu kubwa ni kwamba jasiri haachi asili!!!! HUJASAHAU SOCIAL RESPONSIBILITY YAKO mara tu ulipopata kanafuu kadogo

do you have anyone we can contact in Tanzania to support kwa chochote?

Mkuu kwa lolote naomba wasiliana na PakaJImmy yeye anaweza kukusanya lolote kwa niamba yangu .
 
Mkuu Lunyungu,

Naamini mungu ataendelea kukupigania na utarejea katika hali nzuri na utaendelea na mapambano kama kawaida.Inasikitisha kuona kwamba watu wanaacha kufanya kazi kwa misingi ya taaluma zao na kukimbilia kwenye ufisadi tu.

Mungu ni mwema utarudi ukiwa na nguvu na uweza/uwezo zaidi.

Tunakutakia kupona haraka
 
Ndugu zangu wote wana JF nawapa shukrani kwa maombi yenu .Nilifika salama na niko hosp.Nimeona upendo wenu wa kweli kwangu mimi mwana jumuiya hii .FirstLady na Pakajimy mlifanya kazi kubwa . Pakajimy ulianzia nyumbani kwa mchango na hatimaye kuhakikisha kwamba nimepanda ndege usalama . Nasema asante ,

Muhimbili nilinyanyasika , walifikia hatua ya kuficha xrays lwa muda wa siku 3 nikiwa katika maumivu makali na kila nikiuliza naambiwa alioye kupiga hayupo kaemda wizarani.Nikaamua kwenda MOI kupiga upya kwa gharama mpya nako ni Manyanyaso makubwa nimepata .

Wandugu nimeweza kukaa basi nikaona niwatoe hofu .
Wameanza uchunguzi upya hapa . Dawa zangu za maumivu zote wameweka kwenye bin na Xrays zimekuwa rejected wana anza upya . Nimesha chukuliwa specimen puani , kooni na dawa za maumivu nimepewa mpya naenda hadi kufikia kukaa na kuandika .But natumia wheelchair bado naogeshwa na kuvalishwa siwezi kuvifanya hivyo mwenyewe .

Mungu ni mwema kwenye ndege nilikutana na mtanzania mtu mzima anaita ndugu Mahenge yeye alinisaidia kwkenda ****** nk .
Ijumaa naona na mtaalam na mamamuzi zaidi ni siku hiyo na nikiweza kama leo nitawapa taarifa .
Asanteni .Je kuna mtu anatakana namba yangu ? If yes let me know nitawapa .

man, i can feel your pain, your desparation, your hope, and your gratitude to those around you physically, virtually and in prayers. Through hardship of yours i learn a lot. I solemly pray that you recover, bro. And this PJ guy...una utu, bro
 
Pole sana ndugu yetu. Hawa madaktari na manesi wana kiburi cha uzima ndiyo maana hawaoni haja ya kuwahudumia wagonjwa kwa upendo. Mungu yupo upande wetu na ninakuombea upone haraka.
 
Ohh Bwana Yesu, Kutana na maumivu ya ndugu yetu Lunyungu na kuyafuta kwa damu yako. Na ninaamuru uzima katika mwili wake maana kwa kupigwa kwako pale Calvari ulitangaza uzima kwake.
Kwa, jina la Yesu Amina.
 
Hospitali ya TUMAINIA walinipotezea my first born kwa ungese kama waliotaka kumfanyia LUNYUNGU.

Nchi hii maisha yetu yapo rehani mikononi mwa vichaa waliohong vyuoni ili wapate digree zao.

I will walk with my gun my next visit to hospitali
hiyo last stmnt imenifanya nicheke kwa sauti hadi watu wanishangae, kweli tunahitaji mabadiliko!
mkuu Lunyungu, amini umekwisha pona, ni makovu tu yanaishia sasa.
 
Lunyungu,
Mkuu pole sana na Mungu atakulinda bila shaka..
Ili kutuondoa hofu mkuu wa, nauliza tu hukugombea Ubunge maanake..haaa! haaa! haaa!
 
Mwenzenu sijapata taarifa zake wala updates za Member mwenzetu.
Niliibiwa simu nimepoteza namba zake za huko hospitali alipokwenda.
Any updates zake jamani??
 
is doing great, was discharged from the hospital in God willing will soon be here/JF
 
Ni vyema ingeanzishwa thread mpya kwani title ya thread hii inashtua sana, na kama mtu hujaangalia tarehe ambayo mara ya mwisho watu walipost unaweza kufikiri bado hali yake ni mbaya. Naombeni muache kuchangia hapa, kama kuna haja basi new thread yenye title updated ianzishwe. Ikumbukwe kuwa kabla ya leo, mtu wa mwisho alipost tarehe 22/09/2010, sasa sijui kwa nini Msanii umeirudisha humu leo.
 
Nilikuwa sijaiona hii, ni heri Jabulani umesema maana nilistuka hasa sikuwa nimetazama tar. Mungu azidi kumsaidia.
Na kama Ndg Jabulani alivyoshauri ni vyema hii ikafungwa na kuanzishwa thread mpya ya kufuatilia maendeleo yake.
Pole sana ndg yetu Lunyungu!
 
Ndugu wana JF,

T
unasikitika kuwataarifu kuwa mwenzetu Lunyungu ambaye ni JF member, anaugua mno, hawezi kusimama wala kukaa, anaishi kwenye wheelchair.
His lower disc has been compressed ,ana maumivu makali sana na anasubiria operation.

Anasema anawamiss sana JF members na anamiss the forum.
Kwa yoyote anaetaka kuwasiliana nae, namba yake ni 0767 554433.

Uongozi wa Jf na kwa niamba ya members wote wa JF inampa pole sana na inamtakia afya njema na apone haraka.

Mungu mbariki na msaidie Lunyungu.
Hakika Mola amuhafu na manusuru mwenzetu kwa maradhi yamsumbuayo,
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom