Pole sana ndugu,tuna mshukuru Mungu kwa kukunusuru na ajali mbaya,nakuombea upone majeraha uliyoyapata........Jamani tuwe waangalifu sana kwenye bara bara zetu hizi,ajali zimekuwa nyingi sana wakati huu na watu wengi wamepoteza maisha.
Naungana na nyie wadau wote kumpa pole Lunyungu.Nimepata nafasi ya kuteta naye kama alivyo fanya Mzee Jasusi .Lunyungu alikuwa ndani ya mbuga ya Saadan na mwendo wa km 90 kwa saa .Alikuwa na gari aina ya Range Rover Vogue basi ghafla ikafunguka boneti na akapoteza control.Walikuwa ni watu 2 pekee ndani ya gari akitokea Bukoba kupitia Arusha maana alikuwa Biharamulo kuona yanayo tokea huko .
Anasema gari liligonga daraja na kushuka porini katika shimo kubwa likapinduka miguu juu.Ndipo wananchi wa Lugoba wakaanza kupora na kuchukua vitu kama saa , radio ya gari ,na vifaa kadhaa vya gari .
Lunyungu anaumwa bega sasa la kushoto na alipata majeraha kidogo mkono wa kulia na kichwani.Anasema anaikosa sana JF na anawapa shukrani wote sisi kwa kumuombea.anasema namba zake ni
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.