Nimeongea naye anasema hakuumia sana. Alikuwa anarudi DSM kutoka Arusha bonnet la gari likafunguka na akagonga mti na gari kupinduka. Nimemshauri akaangaliwe na madaktari kwa sababu hata kama hana majeraha ya mwili anaweza kuwa na internal bleeding.
Muda si mrefu nimeongea na mdau wa JF Lunyungu akaniarifu kuwa kapata ajali mbaya maeneo ya Bagamoyo baada ya gari alilokuwa akiendesha kupinduka vibaya.
Kwa wale wenye kuhitaji kuongea naye naweza kuwapa namba yake katika PM.
Pole sana Lunyungu kwa majeraha yoyote uliyoyapata kutokana na ajali hiyo mbaya. Tunamuomba Mungu akupe ahueni ya haraka ili urudi katika shughuli zako za kila siku haraka iwezekenavyo.
Pole sana Kamanda.
Wajua ajali watu watatafsiri mambo mengi ok wewe usijali zaidi ya watu kukupa support pole sana na uendelee na libeneke letu.
ajali ni ajali lakini Yesu yupo nawe atakulinda na damu yake utapona
Hii pia inatukumbusha kuwa kwa binadamu anything can happen any time. Kwa wale wenye imani ni vizuri kila siku kujikabithi mikononi mwa Muumba na zaidi ya hayo tuendelee kujitahidi kuwa waangalifu tunapotumia vyomba vya usafiri.
- Kamanda pona haraka urudi kwenye mapambano, maana ndio kwanza yameanza, Mungu sio fisadi kama tulivyoongea juzi ukiwa Biharamulo kwamba huu ni mwanzo tu wa vita vya kweli vya kuleta mabadiliko kwa taifa letu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.