Lulu na Gigy Money ndani ya mtifuano

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Sep 21, 2011
16,510
28,416
LULU.jpg


MASTAA wawili wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Gift Stanford ‘Gigy Money’ wamejikuta wakiingia kwenye mtifuano mkali baada ya kutoleana maneno machafu.

Ishu ilianzia kwa Gigy ambaye alisema mwanadada Lulu hajui kuvaa, huwa anavaa matangazo, hii ni baada ya kuulizwa na kituo kimoja cha runinga kwamba ataje mastaa kumi wanaojua kuvaa.
Lulu aliamua kumjibu kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa Kijamii wa Instagram kuwa bora asijue kuvaa lakini hawezi kuvaa matambara kama yeye.

“Gigy alikasirishwa sana na kitendo cha Lulu kumwambia anavaa matambara alijikuta akipaniki na yeye akaendelea kushilikilia msimamo kwamba anavaa nguo za matangazo hivyo ni bora yeye anayevaa matambara anayonunua mwenyewe kuliko yeye,” kilisema chanzo.

Gigy alipoulizwa kulikoni, alisema amekasirishwa sana na kitendo cha Lulu kumwambia anavaa matambara wakati yeye alizungumza kama anavyoona kwani mavazi anayovaa hayaendani na mazingira.


maxresdefault.jpg


“Matambara ni ya kwangu na haya ni maisha yangu siyo yeye anayevaa nguo za matangazo eti anajiona naye anavaa maana naona Lulu ameunda na kampeni na makundi kwa ajili ya kunishambulia, mimi ni jeshi la mtu mmoja hawaniwezi,” alisema Gigy Money.

Source: Tanzania Today
 
upumbavu na kufake bongo hautaisha,huwa ctegemei KBS kwa watoto wa kiume kurushiana matope km haya,vidume tusake hela tuwaachie haya hawa wasiojielewa.
 
Ni kweli giggy kamuumbua...Lulu anatangaza na kufanya show off na dukani huko ana madeni kibao.Afadhal gig ye ananunua kwa uwezo wake japo sio za bei ghali
Sio vema kumshambulia Elizabeth Michael aka Lulu,huyo ni mpwa wangu na usemayo yote ni uongo sababu mpwa ana fedha kedekede na ana mijumba kibao na mibiashara kibao na mzuri kwa kila kitu,.,.,, eti ooh ana madeni kibao madukani,.,.,looh ama wanawake kwa kuoneana wivu hajambooo.
 
Hivi bado mna entertain haya maswala wanatunga haya mabifuu kama shishi na vee money ileee wameplan sembuse nahao wakina lulu na giggy halafu hakuna lamaana wanachogombania ila nashangaa mnawapa sapoti huu uzi sidhani kama uanamaana yeyote humu
 
Nafkiri kama sio collo ni nyashinski wa kleptomaniac kuna puch anasema:
Lazima nikutukane ndio ujulikane........ Need to say more?
Its simply publicity stunt
 
Back
Top Bottom