Lucchese DeCavalcante
JF-Expert Member
- Jan 10, 2009
- 5,471
- 734
MHUSIKA katika kiwanda cha filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu' (pichani), ameangusha bonge la ‘pati ya bethdei' ya kutimiza miaka 18 inayodaiwa kugharimu takribani shilingi milioni 3.
Tukio hilo lilichukua nafasi maeneo ya Sinza-Madukani, Dar es Salaam Jumapili iliyopita ambapo lilihudhuriwa na ‘mashostito' wa karibu wa msanii huyo.
Chanzo hicho kilitambaa na mistari kuwa, marafiki hao walipigwa na butwaa kwa kitendo cha Lulu kugharamia bethdei hiyo kiasi kikubwa cha fedha ukilinganisha na kipato chake.
"Kusema kweli Lulu alifanya kufuru ya aina yake, sisi wenyewe hatukuamini kwani viwalo peke yake viligharimu shilingi laki 7 kwa hesabu za haraka.
"Nakwambia tulijiachia, haijawahi kutokea kwani kinywaji cha bei ya chini kabisa kilikuwa ni cha ‘buku' nne," kilisema chanzo hicho ambacho ni rafiki wa karibu wa Lulu aliyehudhuria sherehe hiyo.
Hata hivyo, chanzo hicho kiliongeza kwamba, mpango mzima ulihudhuriwa na mastaa kiduchu huku mama mzazi wa Lulu akiwa hana habari.
Baada ya kuzitia kibindoni ‘nyiuzi' hizo, Risasi Mchanganyiko lilimvutia waya Lulu na kummwagia ishu nzima ‘pwaa' ambapo alidai kuwa hakumbuki kama kilifika kiasi hicho.
Alisema: "Ninachokumbuka mimi niligharamia fedha taslimu zaidi ya shilingi milioni 2.3, sina hakika kama zilifika ‘em 3'."
Aliendelea kudadavua: "Sikuwaalika wasanii wenzangu wengi kwa sababu siyo marafiki zangu, nimejuana nao kwa ajili ya kazi tu."
Jumapili ya Aprili 17, mwaka huu, Lulu alikuwa akisherehekea kutimiza miaka 18 aliyotimiza katikati ya wiki iliyopita hivyo kutamba kwamba amewanyamazisha watu waliokuwa wakimsema mara kwa mara kuwa haruhusiwi kufanya mambo ya kikubwa.