Lukuvi ujasiri huu uwe endelevu

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Maoni ya Mhariri

Lukuvi ujasiri huu uwe endelevu
Imeandikwa na Mhariri; Tarehe: 22nd May 2009

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi, anaonekana 'kutema cheche' hasa kutokana na kukerwa na mambo kadhaa aliyoyakuta mkoani Dar es Salaam, alikohamishiwa hivi karibuni akitokea Dodoma ambako anasema ameacha huruma aliyokuwa nayo.

Kauli ya Lukuvi inaonyesha ujasiri fulani kwa dhamira yake ya kutaka kuweka mambo sawa katika mkoa huu wenye mambo mengi na wakazi wengi wa rangi, tabia, itikadi, makabila na dini tofauti; hali inayosababisha uangalifu mkubwa katika kukabiliana na matatizo yaliyopo.

Mkuu wa Mkoa anaona wazi kero ya wafanyabiashara wa kigeni kuvamia biashara za wenyeji, ambazo hazistahili utaalamu kutoka nje kuziendesha, ikiwa ni pamoja na uuzaji wa karanga na hata maua tena katikati ya Jiji.

Anasema waziwazi kuwa atapambana na watendaji wake wabovu, kwani hakuja Dar es Salaam kujenga urafiki usio na tija kwa wananchi anaowaongoza, hivyo amedhamiria kubanana nao katika kazi za kupambana na kero za wananchi.

Kero nyingine anayosema inamchefua pia ni ya uchafu ambao unaanza kukithiri katika kona mbalimbali za Jiji la Dar es Salaam licha ya kuwapo magari mengi ya kusomba taka ingawa nayo yanaonekana kuwa taka kutokana na ubovu na uchafu wao.

Tunasema kauli ya Lukuvi ni ya kijasiri kwa kuzingatia waliomtangulia ambao nao walikuwa wakiingia Dar es Salaam, kwa 'gia' kama yake lakini baada ya muda gia hiyo imekuwa ikishindwa kuliwezesha 'gari la maendeleo' kupanda kilima hata kidogo.

Tulishasema huko nyuma, kuwa Dar es Salaam ndio uso wa nchi, ambapo wageni wengi kama si wote waingiao nchini, huanzia kabla ya kwenda mikoani, hivyo hakuna namna yoyote ya kukwepa kuiona Dar es Salaam na uchafu na miundombinu yake duni.

Kwa kuzingatia hilo, Rais anapomteua Mkuu wa Mkoa wa kuiongoza Dar es Salaam, anatarajia kuwa na kiongozi atakayeweza kuuosha uso wa nchi kwa maji na sabuni ukatakata. Mwosha uso wa sasa ni Lukuvi.

Tunamwamini kuwa ni mchapakazi ambaye ameshawahi kuishi Dar es Salaam na kuongoza wizara kwa nafasi ya unaibu ambako pia alifanya vizuri lakini baadaye akaondolewa na kuwa mkuu wa mkoa, hivyo ni wazo ana uchungu na watu wa Dar es Salaam na mkoa wenyewe.

Anaelewa pia kuwa Dar es Salaam haina miundombinu mizuri hususan ya barabara na hivyo anahitaji kuja na mikakati itakayosaidia kuboresha miundombinu hiyo huku akichelea kutoa ahadi za takwimu ambazo hatimaye kwa mwaka wake huu mmoja, atashindwa kuzitekeleza.

Kama walivyo wananchi wa Dar es Salaam, sisi tunaahidi kumpa ushirikiano kama kweli ataonyesha dhamira ya vitendo ya kulisaidia Jiji hili kuondokana na kero hizo na hasa atakapopambana na viongozi 'Waswahili' wenye visingizio na wanaotanguliza posho kwa kila kitu.

Kwa kuwa kupanga ni kuchagua, Lukuvi ana changamoto kubwa ya kutoa kipaumbele kwa miradi muhimu ambayo itakuwa ndiyo inayolenga kukabiliana na kero za wananchi na kuzimaliza, ili Dar es Salaam ianze kuonekana kama miji mingine yenye hadhi yake Afrika, kwa kuanzia.

Ingawa hajabainisha staili yake ya kuongoza, tuamini tu kuwa anaongoza kwa vitendo virefu na si maneno, hivyo tuna matumaini makubwa kuwa yaliyoshindikana kwa Abbas Kandoro yatawezekana kwa Lukuvi.
 
Niliwahi kuandika hapa siku za nyuma kwamba Kandoro kama Mkuu wa Mkoa wa Dar alizembea katika kusimamia usafi wa Dar. Baadhi ya watu wakadai kwamba hiyo ni kazi ya mkurugenzi wa jiji. Sasa Dar imepata mtu ambaye inaelekea ana nia ya kuhakikisha Dar inakuwa safi na inapendeza na hayo magari ya kubeba taka ambayo nayo ni uchafu yaondolewe haraka na hao wenye mikataba ya kuzoa takataka jijini wapewe miezi mitatu ya kununua magari mapya vinginevyo mikataba waliyopewa ya kubeba taka ifutwe mara moja.

Tuna matumaini hii kauli ya Lukuvi haitakuwa nguvu ya soda maana tumeshaona kampeni nyingi za kulisafisha jiji la Dar ambazo zilifanikiwa na baada ya muda jiji likarudi tena katika hali ya uchafu uliokithiri na waa kutisha
.
 
Maneno matupu mkuu wangu huyu Kateuliwa hakuchaguliwa!..hivyo hana homa JK yuko majuu..
 
Maneno matupu mkuu wangu huyu Kateuliwa hakuchaguliwa!..hivyo hana homa JK yuko majuu..

Mkuu Mkandara, tutayatumia maneno yake mwenyewe kumweka kiti moto pili itakapobainika kwamba kumbe alikuwa anafanya USANII TU ili akonge nyoyo za Wakazi wa Dar ambao wengi wao wanakerwa na wamechoshwa na uchafu uliokithiri.
 
Lukuvi kaletwa kwa ajili ya uchaguzi wa 2010, haya mengine maigizo tu.Mji umemshinda Makamba na makaratee yake yote.
 
huyu si alikuwa Dodoma na hakuna chochote cha maana amefanya huko,hawa wazee wapo serikalini kabla hatujazaliwa mnategemea leo watafanya nini?
 
nimekuwa nikiwaza kuhusu umuhimu wa huyu bwana kuhamishiwa DSM, nikikumbuka kidogo historia yake tangu alipokuwa waziri.anyway, kwa kuwa wantanzania wote tumeshakuwa so saturated na maneno ya hawa wanasiasa, na imani yatu imepotea kabisa, nimeamua kumpa chance kuangalia matendo yake.kwa maneno anaonekana kuwa ana nia, lakini haya tumeyazoea, na sababu za kushindikana tunaweza pia kumtajia hata sasa hivi kabla ya siku mia alizojiwekea.kero zetu hapa ni nyingi, 99% zinachangiwa na uzembe wa utekelezaji wa sheria ndogondogo za miji.Hawa jamaa hawajui kuwa tatizo la miji ni kubwa inabidi mtu uache porojo? inatakiwa utumie wataalamu kila nyanja, (bila wanasiasa) anyway, tumpe hizo siku 100 tangu ateuliwe kaziomba mwenyewe na hatuna cha kumfanya hata atakaposhindwa kufanya kazi yake tutalalamika tu kama kawaida yetu. Hatuna cha kumfanya!! au tunacho?Anyway kero yangu kubwa ni ujenzi holela, hakuna anaejali, japo ni hatari kwa afya, hivi huu mji una ramani?je inajulikana nyumba zinatakiwa ziwe vipi kwa eneo gani?je matumizi ya nyumba hizo yamewekewa mipaka?je idadi ya wakazi imewekewa mipaka?je huduma za hayo majengo zina utaratibu maalum?ni haki au ni msaada?je mipango iliyopo inazingatia afya kwa kiasi gani?najua wataalamu wa haya wako wengi tu wameajiriwa ila siasa na uzembe hasa wa viongozi ndio kikwazo.vikao kwa wingi na warsha na semina.mimi ningeomba waanze kwa kuhakikisha hakuna mtu anahamia yeye au biashara yake katika sehemu ambayo haiko kwenye standard endelevu
 
Hakuna kitu hapo nawaambie, huyu jamaa ni garasa kabisa....Ukitaka kujua ni garasa angalia kauli zake alizokuwa anazitoa kwa kukurupuka kwenye mabomu ya Mbagala...........!!! Aliwahi kusema eti nchi nzima hakuna matenti mpaka waagize nje ya nchi! Matenti yanauzwa mtaa wa Jamhuri na kwingine kwingi tu! Pia tuna kiwanda cha maturubai kiko Morogoro! Hii inaonyesha jinsi gani hayuko "informed"! Huo ni mfano mdogo tu kati ya michemsho mingi aliyoitoa wakati wa sakata la Mbagala! Mpaka sasa hivi wahanga wa Mbagala hatima yao haijulikani.....!!!

Mji wa Dar una matatizo makubwa ya miundombinu yanayochangiwa kwa kiasi kikubwa na rushwa pamoja na uzembe wa watendaji wa jiji. Vibali vya majengo makubwa vinatolewa kiholela bila kujali uwezo wa miundombinu ya maji taka na maji safi, maegesho ya magari, umeme na barabara! Matokeo yake katikati ya jiji sasa hivi hakufai kabisa!

Hayo magari mabovu ya takataka ni ya makampuni ambayo naamini aidha yanatoa 10% ya mauzo kwa watendaji wa jiji, ama watendaji hao wa jiji wana hisa katika makampuni hayo kwa kupitia mlango wa nyuma. Sasa unategemea nani atakemea hilo?
 
Niliwahi kuandika hapa siku za nyuma kwamba Kandoro kama Mkuu wa Mkoa wa Dar alizembea katika kusimamia usafi wa Dar. Baadhi ya watu wakadai kwamba hiyo ni kazi ya mkurugenzi wa jiji. Sasa Dar imepata mtu ambaye inaelekea ana nia ya kuhakikisha Dar inakuwa safi na inapendeza na hayo magari ya kubeba taka ambayo nayo ni uchafu yaondolewe haraka na hao wenye mikataba ya kuzoa takataka jijini wapewe miezi mitatu ya kununua magari mapya vinginevyo mikataba waliyopewa ya kubeba taka ifutwe mara moja.

Hayo magari mabovu ya takataka ni ya makampuni ambayo naamini aidha yanatoa 10% ya mauzo kwa watendaji wa jiji, ama watendaji hao wa jiji wana hisa katika makampuni hayo kwa kupitia mlango wa nyuma. Sasa unategemea nani atakemea hilo?
Makampuni na CBO zinazo zoa taka katika Jiji hilo hawana ubavu wa kununua magari mapya ya kufanyia kazi hiyo. Hii inatokana na uwezo mdogo kifedha wa asasi hizo au sababu alizotaja Nd. Masaki hapo juu.

Aidha kazi ya kuliweka na kusimamia Jiji hilo katika masuala ya usafi lipo chini ya Mkurugenzi wa Jiji, kwani ni yeye ambae huingia mikataba na wasafishaji na sio Mkuu wa Mkoa. Mkuu wa mkoa anaweza kutoa kuongea lolote lakini utekelezaji utabaki kule kule kwa Mkurugenzi na Maafisa wake.

Cha msingi ni kwa Mkuu huyo wa Mkoa kukaa pamoja na Halmashauri, na kuajua nini cha kufanya. Ikumbukwe kuwa Mkurugenzi nae hubanwa na kufuta matakwa ya Madiwani wake. Otherwise hapata kuwepo na uendelevu wowote katika kauli yake na Jiji litaendelea kunuka tu.
 
Last edited:


Kero nyingine anayosema inamchefua pia ni ya uchafu ambao unaanza kukithiri katika kona mbalimbali za Jiji la Dar es Salaam licha ya kuwapo magari mengi ya kusomba taka ingawa nayo yanaonekana kuwa taka kutokana na ubovu na uchafu wao.

.

Sawa tunakubaliana nae na aendelee hivyo hivyo ila sasa hizi taka zinasombwa zinapelekwa wapi au ndio zinakwenda kule kule mbagala kwa walala hoi.
 
KAZI ANAYO ila kama ana nia basi huenda akafanikiwa kwa kiasi.Tatizo ninaloliona mimi ni kama walioko chini yake wataweza kumpa support inayostahili kufikia azma.Kama waliopo hawana nia wala utashi wa kuleta mabadiliko, au wameweka maslahi binafsi mbele na hivyo wakavuta miguu basi Mkuu huyu atajikuta mpweke na hatafanikiwa.

Tuchukulie suala la mgambo wa jiji kukimbizana na mama/babalishe na kuwanyang'anya masufuria ya ubwabwa au kuwatoa kitu kidogo, kupambana na wamachinga wanaozunguka na mitumba na bidhaa nyingine kwenye mabegi kisa kuwatoa kitu kidogo badala ya kupambana na uchafu - hapa tunaona kabisa kuwa watendaji wanakimbizaUtakuta pengine wakubwa wao nao "wanakula mezani kwao" na inajulikana hivyo wanakosa uhalali wa kuwaadabisha hao mgambo.

Matokeo mazuri itategemea utendaji wa idara zote husika.Njia mojawapo kama inawezekana ni kuwaondosha wale watendaji waliokuwepo na kuleta wengine - hao wapangiwe malengo.Lakini je hili linawezekana?

BTW zile semina elekezi Ngurdoto na yaliyofuata baada ya hapo- hakuna performance goals kwa wakuu hawa? Utendaji wao unapimwa vipi?
 
Jamani

Tumpe muda Lukuvi kwani ndio kwanza ana Mwezi moja ndani ya Ofisi kwa sijakosea.

Mi nafikiri atafanya na kuliweka Jiji la DSM safi, salama na kuwa kivutio cha Watalii
 
Hakuna kitu hapa, huu ni usanii tu kama kawaida ya Awamu ya Nne. Kuletwa kwake Dar ni katika kupangua safu kwa finali za 2010!!!! Anajua kucheza usanii maana mkoa wa Dar es Salaam ni complicated kama ilivyo Mara.

Kwanza kitendo cha kuwaambia victims/wakazi wa Mbagala kwa bombs kuwa wazoe milio ya mabomu kama walivyozoea wakazi wa jirani na uwanja wa ndege milio ya ndege basi, nilimdharau mpaka mwisho. Je unaweze kulinganisha hatari ya mabomu, kishindo chake, sumu yake, n.k na mlio wa ndege!!!!???? Ubongo wake kiwango cha kufikiri ni kidogo na hana busara. Anatakiwa aende Mbagala akaombe msamaha kabisa.

Kuhusu usafi, kweli jiji ni chafu kwa sasa!!! Ila mnasahau kuwa hiyo ni biashara ya viongozi wa jiji/mkoa na hao wenye contract??? Asilimia kubwa ya magari au contract za kubeba uchafu/taka Dar ni biashara ya Kingunge et al......Kwanza magari aliyo nayo ni machache na chakavu, angalao siku za karibuni ameongeza magari ila bado hayatoshi, usimamizi pia ni mbovu maana kwa mfano manispaa ya temeke taka/uchafu unaazagaa kwenye mitaa kwa wiki nzima maana wanapita once a week kukusanya taka na magari yakiharibika basi hata mwezi hawapiti kabisa!! Hivyo unakuta tu kwenye mitaa wakazi wamepanga mapipa yamejaa, wanongeza mifuko ambayo pia kunguru wanafurahi maana inakuwa rahisi kusambaza taka hizo.

Pia ili usafi we effective inabidi kila mtaa waweke mapipa ya kumwaga chafu, ila tena nimesahau kuwa biashara ya plastic haitayaacha!!!! Sisi wana jamii nao ni tatizo!!!
 
msijali hiyo ni nguvu ya soda tu...bado hajajua atoke vipi?? yupo kisiasa zaidi hapa mjini....will see his true colour soon...
 
huyu si alikuwa Dodoma na hakuna chochote cha maana amefanya huko,hawa wazee wapo serikalini kabla hatujazaliwa mnategemea leo watafanya nini?

Mkuu Koba,

Nia yangu sikuleta malumbano bali kuweka rekodi sawasawa.

Hebu tueleze wewe umezaliwa lini na huyu Mheshimiwa alikuwa na wadhifa gani serikalini wakati huo unazaliwa?
 
MH. LUKUVI NA NDUGU YAKE KANDORO WOTE NI WAMWAGITO SASA SIJUI KAMA MWAGITO HUYU KALETWA ILI AREKEBISHE KAZI YA NDUGU YAKE, HAWA JAMAA NI WANYALUKOLO(DUGU MOJA) HIVYO NAFKIRI WATAKUWA WAKIPEANA USHAURI JUU YA JIJI HILI LA DAR ISO SALAMA, LABDA BW. LUKUVI ATAJITAHIDI KUBORESHA BAADHI YA MAMBO YALOMKWAZA KANDORO, LAKINI ISIWE TU KWA TAMAA YA KUTAKA KUFANYA BILA TAHADHARI, WAHEHE WANA MSEMO' U WALI WAWULIGE SEFU' yaani uroho wa wali ulimuua bw. SEFU'
 
Back
Top Bottom