Lukuvi na kauli zake

NGULI

JF-Expert Member
Mar 31, 2008
4,803
637
Kwa wafwatiliaji wa mambo ya siasa hasa kipindi hichi cha mabomu huko Mbagala kimecha vinywa wazi hasa kiongozi wa mkoa Mr. Lukuvi anavyo jieleza kwa waandishi wa habari .....aliulizwa mzee mbona madhara yanasemekana ni mengi (hasa lile bomu lilolipuka last wk saa 11 jioni) akasema ni kawaida tu wanasafisha eneo na wananchi wakiona kitu chochote cha chuma watoe taarifa, mtangazi wa TBC akambana zaidi mbona hapa tunaona watu zaidi ya 20 wamelezwa hapa wodini Temeke Hospital? na bado wengine wanaletwa huku? huoni kama madhara ni makubwa akasema wananchi wanatakiwa wazoee kama wale wa air port ya mwl .Nyerere mbona wao hawazimii na ndege zinakelele kama hayo Mabomu? Hichi ni kimeo kingine tena kwenye hii serikali ya CCM mkuu wa mkoa kwa kauli hizi sidhani kama ni sahihi, na sitashangaa kuona nyingine nyingi za ajabu ajabu na hii jamii yetu sio wafwatiliaji wa misemo au semi za viongozi wetu nyingi ni tete sana.
 
Mjomba, hiyo kauli ni ya mbali, mpya kabisa ni kwamba wananchi wa aidha Mbagala au Kipawa wamepanga maandamano ya kumtaka huyo 'mwenye mkoa' ajiuzulu nafasi hiyo fasta.

Tunajua hilo haliwezi kutekelezeka, kama ambavyo utamaduni wa Kibongo ulivyo, Lakini kwa ujumla, Kauli hiyo ni ya Kejeli.

Fikiria mabomu hayo yangelipukia maeneo ya Mikocheni au Masaki na kuua idadi ileile ya watu, na kupiga chini yale mahekalu yao, je unadhani mambo yangekuwa kama hivyo?

Nchi nzima hii tungepelekwa mchakamchaka wa hatari....!

There are classes here, and we have to embark onto class struggle!
 
mjomba, hiyo kauli ni ya mbali, mpya kabisa ni kwamba wananchi wa aidha mbagala au kipawa wamepanga maandamano ya kumtaka huyo 'mwenye mkoa' ajiuzulu nafasi hiyo fasta.

tunajua hilo haliwezi kutekelezeka, kama ambavyo utamaduni wa kibongo ulivyo, lakini kwa ujumla, kauli hiyo ni ya kejeli.

fikiria mabomu hayo yangelipukia maeneo ya mikocheni au masaki na kuua idadi ileile ya watu, na kupiga chini yale mahekalu yao, je unadhani mambo yangekuwa kama hivyo?

nchi nzima hii tungepelekwa mchakamchaka wa hatari....!

there are classes here, and we have to embark onto class struggle!

sijui wamemmchaguaje natamani angetoka hata kesho...huwezi waambia wananchi wazoee mabomu na kusema watoto waliokuwa viziwi mbona ni mia nne tu? Hata kama ni hao je ni ni kidogo? Angekuwa ni mtoto 1 tu ameumia ingekuwaje siangepelekwa usa kutibiwa angepelekwa temeke hospital? Na je wangejibu kwa jeuri kama hivyo??
 
Nimekuwa najiuliza jeuri ya majibu ya huyu jamaa aliyokuja nayo kaitoa wapi, Makao makuu au wapi. Aliwahi pia kuulizwa idadi ya watu waliokuwa wamepoteza maisha akajibu, " haina tofauti sana na ya jana, ameongezeka mmoja tu na kufikia kama ishirini hivi, nikiwa na maana kuwa wanajeshi wanaendelea kubakia wale wale watano hivyo kufanya jumla kuwa 25". Ni kauli ya jeuri, isiyokuwa na hata chembe ya huruma tena iliyotolewa na Lukuvi katikati ya watu wenye majonzi na walohitaji kauli za kuwarejeshea matumaini. Hakika sina uhakika kama atauweza mkoa huu.
 
Huyu baba hana huruma kabisa halafu anaficha ficha mambo, na yule Mganga mkku wa Temeke siku ile ya kwanza ya mabomu anasema majeruhu waliumia umia kidogo wameshaanza kuruhusiwa ,wakati watu wameumia sana na wameonekana mimi sijui huwa wanapewa course ya kusema uongo na serikali sijui.
 
jamani siasa ni ngumu....sana jamani haya kauli zake zitamtoaa...alipo kazi kwake
 
Huyu jamaa atakuwa na matatizo na nina hakika ufikiri baada ya kusema.Kiongozi wa kisiasa ambaye anasema kwanza halafu ndo anaanza kufikiri,hatufai hata kidogo.Si unajua siasa zinategemea sana mdomo na jamaa ndo kusema ameshaonesha kufeli
 
jamani siasa ni ngumu....sana jamani haya kauli zake zitamtoaa...alipo kazi kwake

Hapa hakuna maswala ya siasa, ni ya kiutendaji zaidi. Kama anataka siasa agombee uenyekiti wa CCM Mkoa ili akabwabwaje na akina Tambwe,Msabaha na wanaofanana nao.
 
Issue hapa ni upeo Pengine ile intelligence (sio IQ, labda TQ (Tactical Intelligence), au MQ (Media Intelligence!) ya kutambua kwamba yupo wapi, anaongelea nini, anaongea na nani - ni ndogo. Recall Mramba viz Prez Jet viz Manyasi
 
Mimi sishangai sana ndugu zangu kwani kauli kama hizi ni za kawaida kwa aina hii ya serikali isiyojali watu. Malaika wetu ni kwanza kwenye hili after all kipi huwa kinatokea baada ya kauli hizi tata? Nothing so no one cares.

Waziri anasema hatojiuzulu mpaka ithibitishwe kwamba ni uzembe ndio umesababisha milipuko. Sasa sijuwi ni uthibitisho gani anautaka wakati tayari imethibitishwa kwamba mabomu yalikuwa yameexpire na serikali kuu iliombwa kutoa pesa ya kuyaangamiza ikagoma so uthibitisho gani anautaka daktari huyu anayeandaliwa kuwa rais? Na kwenye kampeni Busanda CCM wanawaambia wananchi wakae mbali na helicopter ya Mbowe itawalipukia kama mabomu ya Mbagala-what a hell is this? Hawa jamaa kwa uzembe wameua raia wasio na hati leo wanaiingiza hii issue kwenye siasa tena? Binafsi nimewachoka hawa jamaa kinoma.
 
Back
Top Bottom