lugha ya kiingereza ni kikwazo

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
MCHEZAJI filamu za Bongo, Mohamed Miwkongi maarufu kwa jina la Frank, amesema kuwa lugha ya kiingereza ni kikwazo kikubwa na huwapiga chenga wasanii wengi wa filamu za Bongo.
Frank alisema kuwa wasanii wengi wa filamu za bongo hawaelewi vizuri kimombo na hushirikishwa kwenye filamu bila ya kujua maudhi na maana ya majina ya filamu hizo.

Frank alisema kuwa waigizaji wengi wanaokautana na matatizo hayo ni
wale wanaoshirikishwa kwenye filamu zenye majina ya Kiingereza.

"Wasanii wengi wanashiriki tu kwenye filamu, lakini hadi anamaliza
kucheza kipande chake hajui maudhui ya filamu yenye wala maana ya jina
la filamu aliyocheza," alisema Frank.

"Utakuta msanii anaambiwa kuna filamu inaitwa Avenger au Off Side
tunaomba ushiriki, tunakubali bila ya kujua maudhui (mtiririko) waala
maana ya jina",

"Ukikutana na msanii atakuambia kuna Avenger inakuja", alisema Frank.

"Ukimuuliza maana ama maudhui yake hajui," aliongeza Frank.

Frank alisema kuwa kwakuwa wasanii wengi wa Tanzania lugha ya Kiingereza imewapiga chenga, ni vyema kwa waandaaji wa filamu hizo kuwaeleza kwanza maana ama maudhui ya filamu hizo kabla ya kuwapa sehemu za kucheza ili waweze kuelewa kinachoendelea.
 
Tatizo si kiingereza peke yake. Hata ufahamu wa mambo mbali mbali huwa ni mdogo. Ni vizuri wakaenda shule badala ya kutegemea vipaji tu. Waigizaji hawa wangekuwa walau wanakuwa hata na digrii moja, ingeweza kuboresha kazi zao kwa ujumla.
 
Mimi naona kama wamekaa kifedha zaidi na kutaka maisha mazuri bila shule wengi wanapenda mambo makubwa sana kwa wakati mfupi kwa hiyo tukisema waende shule sidhani kama watakua na muda wa kusoma zaidi ya kudesa au kununua pepa au kukatisha masomo kabisa ni wachache sana wenye upeo wa kuona mbali ambao huwa wanasoma na kufikia mahala pazuri wewe chunguza mifano ya wasanii wengi ukianza na wanamuziki utakuta ni wachache sana waliosoma!wengi shule wanaipa kisogo
Tatizo si kiingereza peke yake. Hata ufahamu wa mambo mbali mbali huwa ni mdogo. Ni vizuri wakaenda shule badala ya kutegemea vipaji tu. Waigizaji hawa wangekuwa walau wanakuwa hata na digrii moja, ingeweza kuboresha kazi zao kwa ujumla.
 
Mimi naona kama wamekaa kifedha zaidi na kutaka maisha mazuri bila shule wengi wanapenda mambo makubwa sana kwa wakati mfupi kwa hiyo tukisema waende shule sidhani kama watakua na muda wa kusoma zaidi ya kudesa au kununua pepa au kukatisha masomo kabisa ni wachache sana wenye upeo wa kuona mbali ambao huwa wanasoma na kufikia mahala pazuri wewe chunguza mifano ya wasanii wengi ukianza na wanamuziki utakuta ni wachache sana waliosoma!wengi shule wanaipa kisogo

Wasanii wa bongo. Lakini wale wa majuu wengi wana tu-degree.
Nafikiri hapa, tutakuja kuwa na picha nzuri sana tutakapopata wasanii ambao shule wameenda kabla ya kujikita kwenye movies.
 
Nadhani ni muhimu hawa wasanii wachukulie fani zao kwa umakini zaidi na kama usanii ndio wanaotaka itawalizimu warudi kwenye vyuo mbali mbali ili waweze kujikwamua katika swala hili zima la kimombo.
 
Back
Top Bottom