Lt. Gen Abrahaman Amir Shimbo kustaafu kesho

Mnadhimu mkuu wa jeshi (chief of staff) lt. gen Shimbo ataagwa rasmi kesho.

Kamanda huyu anastaafu kwa mujibu wa sheria za jeshi za kutimiza umri wa kustaafu baada ya kuongezewa muda wa kustaafu kipindi cha nyuma japo umri wake wa kustaafu ulishafika.

Shughuli ya kumuaga itafanyika kesho makao makuu ya jeshi, Upanga.

Ikumbukwe, alipata wadhifa wa unadhimu wa jeshi mwaka 2007 ambapo yeye na CDF Davis Mwamunyange walichukua madaraka kutoka kwa general Waitara.

Nitawajuza yatakayojiri kesho kwenye shughuli ya kumuaga huyu chief of staff.

Source: MOSHE DAYAN

Natumai JK ata "balance" uwiano wa Dini Jeshini kwa kumteua mnadhimu mwingine mwenye jina linalofanania na la Abdulrahman
 
Ndio maana nikasema tufikirie kidogo kama ishu kama hizi zikiendeshwa kwa mihemuko tutakuwa kila siku tunakula za uso mahakamani. Hoja yangu haikuwa ameiba ama hajaiba, amehifadhi fedha au hajahifadhi. Mashaka yangu yalikuwa kwa wale waosema ni trilioni nne nikaeleza trilioni nne ni sawa na bajeti ya Wizara ya ulinzi kwa muda zaidi ya miaka 5 ambayo inazidi hata miaka aliyokaa kwenye wadhifa wake!!

Hata hayo mabilioni yaliyopo Uswis changanya na za Kenya Na Uganda hazifikii hizo trilioni 4! Au labda tueleze wewe Zilizoko Uswis (pesa za Watanzania ni sh. ngapi).....?

Sina undugu na Shimbo zaidi ya kumuona kwenye kioo tu ila kwa hilo najaribu kufikiri as GT.
mkuu hata mimi najua Trillion 3 ni pesa nyingi lakini ukisikia hii nchi bado ni masikini wakati watu wanafanya kazi usiku na mchana ndipo linakuja jibu kuwa pesa zipo ila ziko sehemu.
Sisi hapa kisiwani na wilayani kwetu bajeti ya afya inawezekana haifiki hata million 500, na ndio maana siku ya kwanza niliposikia mtu mmoja kuwa ana US $1m tena kwenye akaunti moja tu ambazo ni zaidi ya mara tatu ya mahitaji ya wilaya nzima sikuamini habari hizo but all over the sudden yeye akasema hivi ni "vijisenti". Kwa maana hiyo siwezi kukataa uwepo wa pesa kama hizo japo ushahidi hauko wazi.
Nasikia Mobutu alikuwa na pesa Uswisi karibia $60,000,000 lakini alivyokufa walisema ni $6,000,000 tu. Kwa hiyo ni bora ukakumbuka kuwa pesa nyingi ambazo viongozi mafisadi (hasa Afrika) huficha nje ya nchi mara nyingi wanazila hao wenye mabenki maana wenye nazo 'mambo yakiharibika' hawana ujasiri wa kwenda kuzidai

 
kwenye kuagwa tutasikia "luteni mwadilifu" pamoja na ufisi wote.
 
Afande! alikuwa anatania tu! Mapumziko mema baada ya utumishi wako uliotukuka Afande!
Umri wangu wa kustaafu bado sana. Ila nasikitika kwa sababu
mara nyingine nimekuwa karibu na kamanda Shimbo ambaye
anasikitishwa sana na shutuma hizi ambazo hazina ukweli.
Nataka ufahamu kuwa kamanda Shimbo alikuwa Muadilifu sana.
 
Umri wangu wa kustaafu bado sana. Ila nasikitika kwa sababu
mara nyingine nimekuwa karibu na kamanda Shimbo ambaye
anasikitishwa sana na shutuma hizi ambazo hazina ukweli.
Nataka ufahamu kuwa kamanda Shimbo alikuwa Muadilifu sana.

Afande samahani mbona hata wapiganaji wadogo wanajua huu wizi? Afande mng'ate sikio private mmoja hapo nje uone atakachosema! Afande sitachangia post zako usijestaafu na mimi Afande nina familia bado changa sana Afande!
 
anahitaji ulinzi mkubwa akistaafu if he is to survive in the streets,alitutia hofu 2010 tunamsubiri kwa hamu kitaa.
 
Itakuwa Lt.Gen Moshe Dayan wa bongo lakini sio Israel.
Hahahaahhahahaahaaaaaa..,
Comrade ndahani.., mm appointment za namna hii sizipendi..,

I am a typical battlefield commander sio staff officer.., si unanijua tena MOSHE DAYAN....,
 
Kwa uzoefu wake akaanzishe kampuni ya Ulinzi..itamlipa sana! Nchi hii bwana.

Nikimkumbuka Shimbo na vitisho vyake 2010 najisikia bado kutetemeka kwa hasira. I don't even wish him well on his retirement!
 
Ngoja nipeleke maombi ya hiyo kazi pale Upnga wanaweza huwezi jua bahati yangu msiilalie mlango wazi!
 
mzee mpuuzi sana yule...ameshirikiana na jk katika mambo mengi ya hovyo sana..na ni huyu huyu aliyesababisha mkuu wa majeshi mwamunyange aondoke bila kuaga na hakujulikana aliko baada ya huyu mzee kufanya mambo ya hovyo na jk kuyakubali kama yalivyo.....
 
Hizo ela alizochakachua kama kweli anaweza kutumia million arobaini kwa siku zaidi ya miaka 30 na bado haziishi
 
Ametumikia nchi kwa uadilifu mkubwa..karibu nyumbani arusha mkuu

Hana uadilifu wowote bali mla rushwa mkubwa. afunguliwe mashtaka ya uhujumu uchumi, sioni la kumkumbuka zaidi ya wizi wa mali za umma, anafaa kugombea uongozi CCM kwa wezi wenzie
 
Back
Top Bottom