Mvaa Tai
JF-Expert Member
- Aug 11, 2009
- 6,159
- 4,443
Vigogo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wanaotakiwa wajiuzulu kwa tuhuma za ufisadi wamekutana na uongozi wa juu wa chama chao, na taarifa zinasema bado mvutano haujaisha kati ya pande mbili hizo.
Taarifa za hakika zimeliarifu Raia mwema kwamba walikutana na makamu Mwenyekiti, Pius Msekwa, wiki iliyopita, na kwamba mmoja wao, Edward Lowassa, Bado ana donge.
Habari zinaeleza kwamba Lowassa (Mbunge wa Monduli), Rostam Aziz(Mbunge wa Igunga) na Andrew Chenge (Mbunge wa Bariadi magharibi) waliitwa ofisi ndogo ya CCM, Lumumba Dar es Salaam wakitakiwa kutekeleza uamuzi wa NEC.
Lakini habari kutoka kwa watu wa karibu na Lowassa zinaeleza kwamba mwanasiasa huyo amebainisha kwamba hakubaliani na uamuzi wa NEC.
Mzee (Lowassa) amesema kwamba aliitwa na kwamba alitakiwa kuachana na suala la urais ili mambo yaishe, lakini amewaambia uamuzi wowote kisiasa ni haki yake kikatiba, na hivyo hakubaliani nao anasema Mbunge mmoja ambaye yuko katika kambi ya Lowassa akiongeza:
Ila wajue kwamba wao wakimwaga mboga sisi tunamwaga ugali. Kwa mujibu wa Mbunge huyo, Rostam Aziz na Chenge wanaonekana kulegeza kamba katika suala hilo.
Anasema mbunge huyo Rostam amesema wazi kwamba hawezi kushindana na Rais aliye madarakani hata kama watakuwa wameonewa.
Chenge anakubali tu kwasababu anaona hana jinsi.
Lowassa bado moyo wake ni mzito .Gazeti lilipotaka
Lowassa alizungumzie suala hilo alijibu No coment, No coment, No coment
Taarifa ambazo Raia mwema limezipata zinaeleza kuwa tayari viongozi hao ambao wote ni wajumbe wa NEC na walihudhuria kikao kilichoazimia wajiuzuru, wameshakabidhiwa barua rasmi za kuwataka wajiuzuru zikirejea uamuzi wa vikao vya juu vya CCM.
Source:
Raia Mwema June1-June7, 2011
Taarifa za hakika zimeliarifu Raia mwema kwamba walikutana na makamu Mwenyekiti, Pius Msekwa, wiki iliyopita, na kwamba mmoja wao, Edward Lowassa, Bado ana donge.
Habari zinaeleza kwamba Lowassa (Mbunge wa Monduli), Rostam Aziz(Mbunge wa Igunga) na Andrew Chenge (Mbunge wa Bariadi magharibi) waliitwa ofisi ndogo ya CCM, Lumumba Dar es Salaam wakitakiwa kutekeleza uamuzi wa NEC.
Lakini habari kutoka kwa watu wa karibu na Lowassa zinaeleza kwamba mwanasiasa huyo amebainisha kwamba hakubaliani na uamuzi wa NEC.
Mzee (Lowassa) amesema kwamba aliitwa na kwamba alitakiwa kuachana na suala la urais ili mambo yaishe, lakini amewaambia uamuzi wowote kisiasa ni haki yake kikatiba, na hivyo hakubaliani nao anasema Mbunge mmoja ambaye yuko katika kambi ya Lowassa akiongeza:
Ila wajue kwamba wao wakimwaga mboga sisi tunamwaga ugali. Kwa mujibu wa Mbunge huyo, Rostam Aziz na Chenge wanaonekana kulegeza kamba katika suala hilo.
Anasema mbunge huyo Rostam amesema wazi kwamba hawezi kushindana na Rais aliye madarakani hata kama watakuwa wameonewa.
Chenge anakubali tu kwasababu anaona hana jinsi.
Lowassa bado moyo wake ni mzito .Gazeti lilipotaka
Lowassa alizungumzie suala hilo alijibu No coment, No coment, No coment
Taarifa ambazo Raia mwema limezipata zinaeleza kuwa tayari viongozi hao ambao wote ni wajumbe wa NEC na walihudhuria kikao kilichoazimia wajiuzuru, wameshakabidhiwa barua rasmi za kuwataka wajiuzuru zikirejea uamuzi wa vikao vya juu vya CCM.
Source:
Raia Mwema June1-June7, 2011