Lowassa vs Sumaye

wakati wa mchakato wa uchaguzi wa mwaka 2005, nakumbuka kila mtanzania alikua anakereka na kustaajabika kuwa aliyekuwa waziri mkuu wa serikali ya ccm 1995-2005 mh frederick sumaye alikua anataka kugombea urais kwa kupitia ticket ya ccm.

Mapungufu yake mengi tuliyaona na kuyajua, tuhuma kubwa zikiwa alikuwa akichukua mashamba ya watu kwa nguvu au kwa njia ambazo hazikua halali [these were mere allegations].pia na hela alizotumia wakati wa safari moja alienda marekani naomba mnisaidie kwa kumbukumbu nzuri.

Upande mwingine alichomoza el, ambapo ni kama watanzania tulijisahau sijui au ah? Au ndo ujinga wetu?, maana ni kama alionekana ni mtu msafi kwa mda wa kipindi kile cha mchakato wa uchaguzi 2005. Watu wote tulijua kuwa atakuja kuwa waziri mkuu lakini wachache tuliohoji umakini wake na utendaji wake kazi, hususan tukikumbuka el alikataliwa na alikuwa hakubaliki na mw nyerere kwa kuwa na utajiri mkubwa pasipo kawaida.

Wakati ule [2005] ulikua ukiwalinganisha el na fs ni kama lowasa ali edge ahead, na honestly media ilikua sana against fs.

Sasa tunajua a-q if not z ya el, je kuna ya fs ambayo hatuyajui ambayo yana uzito unao fanana na el au kumzidi.

Tukipima mizani yao nani kamzidi mwenzake mpaka sasa kwa ufisadi?

Nani anaweza ku-come back au anaweza kuwa the come back king, maana najua wote wana hamu ya kuingia kwenye uwanja wa siasa ila maji yamewazidi shingo...


hivi tanzania hii hatuna viongozi wengine zaidi ya lowasa na sumaye mpaka tufikirie come back yao, wao wamepita na mda wao umekwisha waje wengine afterall wote wanakashfa kibao ya nini kuwafikiria, warudi vijijini kwao wakalee familia na kulima.
 
Katika Elimu ya siasa kuna kitu kinaitwa "machivelian politics". Machiveli alikuwa mwanasiasa zamani huko Italia na alikuwa anatumia siasa za kupakazia mahasimu wake kisiasa na hivyo kuwaangusha kirahisi. JK/EL na mtandao wao walitumia mbinu kama hivo kwanza kwa kumlega Sumaye na hapo baadae Salim A. Salim. Tatizo la Sumaye ni kwamba ilimchukua muda mrefu kungamua kwamba uongo ukisemwa mara kwa mara dhidi yako mwishowe uchukuliwa kama ukweli.machoni kwa umma. Kama Sumaye angekuwa fisadi kama walivyotuhumu wanamtandao tungeshaona dalili za ufisadi. Sijui kama kuna mtu amefuatilia maisha ya Sumaye baada ya 2005. Ni mtu wa kawaida kabisa na yule mzee hana kubwa sana kimaisha. Bahati nzuri kuna rafiki yangu yuko karibu na Mheshimiwa huyu wa zamani anasema Sumaye hana mali. Kosa lake lilikuwa ni kudharau wapinzani wake na mbinu zao untl when it was too late.Ni kama kukumbuka shuka wakati tayari kumepambazuka!
 
ila naanza kupata imani EL alimchafua mwenzake zaidi ila si kama alivyochafuliwa...FS si mchafu inavyodhaniwa...kama mtu anayo data zake atupe..maana miaka imepita hatajwi..majinayanayotokea ni chenge, EL ,a RA...
 
Kama ni suala la kuwalinganisha hawa wawili, ni bora Mhe. FS kuliko EL kwa sababu ufisadi wa FS tulio wengi tuna usikia tu na hata sijui kama ana mali za kutisha sna kama huyo Mhe. EL.Kwa kipindi hiki ambacho FS amekaa nje ya system angekuwa ameonekana kama angekuwa na mali nyingi.
 
Nilikua najiuliza imekuaje Sumaye akawa anasemwa sana kwa ufisadi wa mapori tu ilihali kuna mafisadi papa kama akina vijisent tulikua hatuwasikii kabisa?

Baada ya kusoma post zilizotangulia hapo juu nimepata mwanga kuwa ulikua ni mchezo mchafu wa EL kummaliza. Hizi media zetu nazo kwa kweli zinachangia sana kuwaenzi mafisadi, hazitendi haki.
 
kitu ambacho siwaelewi watanzania wenzangu ni kwanin munaintatein A COME BACK OF THESE F*C*E**!they have screwed us enough!why don't you guys post something to discourage them NEVER TO BOUNCE BACK!what the hell are you guys doing?

.....................lol!
 
Kuna siku nilikaa na rafiki yangu mmoja, akanambia kwa jinsi nilivyo makini ningekuwa waziri bora sana tz kuliko hawa waliopo... mara kumi zaidi. lakini sifikirii kuingia kwenye siasa. na nadhani kuna watendaji wengi wazuri wako tz, vijana wazalendo lakini wataanzaje anzaje kama siasa zenyewe ndio hizo za kupakaziana! na ukiingia lazima uegemee kwenye kundi la akina fulani, iwe ni mtandao n.k.

Pili, hata kwa hao waliopo, hakuna kiongozi aliye mfano bora na ambaye yupo tayari kuwa groom vijana ili wawe makamanda safi wa kupeleka nchi kwenye neema! nakumbuka mwanahabari mmoja makini pia, wakati akihojiwa alisema... tatizo la kuto groom viongozi lilikuwa moja ya weakness ya baba wa taifa... alipokufa... hakuna hata wa kurithi na kudumisha miongozo yake! Yote aliyoyajenga na kuyapigania, yanaparaganyika sasa!!!

Tanzania nakulilia!!
 
Lowassa amekubuhu kwa propaganda, na hiyo ndio ilimpa advantage ya kummaliza sumaye wakati ule,siwezi kusahau alivyofanya utaalamu wa kuchanganya picha yake ya kichwa na mkulima aliye shambani amevaa mabuti kisha akasema eti ni sumaye yuko shambani kwake kibaigwa!
 
Mundu said:
Kuna siku nilikaa na rafiki yangu mmoja, akanambia kwa jinsi nilivyo makini ningekuwa waziri bora sana tz kuliko hawa waliopo... mara kumi zaidi. lakini sifikirii kuingia kwenye siasa. na nadhani kuna watendaji wengi wazuri wako tz, vijana wazalendo lakini wataanzaje anzaje kama siasa zenyewe ndio hizo za kupakaziana! na ukiingia lazima uegemee kwenye kundi la akina fulani, iwe ni mtandao n.k.

Pili, hata kwa hao waliopo, hakuna kiongozi aliye mfano bora na ambaye yupo tayari kuwa groom vijana ili wawe makamanda safi wa kupeleka nchi kwenye neema! nakumbuka mwanahabari mmoja makini pia, wakati akihojiwa alisema... tatizo la kuto groom viongozi lilikuwa moja ya weakness ya baba wa taifa... alipokufa... hakuna hata wa kurithi na kudumisha miongozo yake! Yote aliyoyajenga na kuyapigania, yanaparaganyika sasa!!!

Tanzania nakulilia!!

Mundu,

..mbona kuna vijana wengi tu wamejitosa kwenye siasa?

..Zitto,Masha,Adam Malima,Stella Manyanya,Muhonga, wote naweza kuwaweka ktk kundi la vijana.

..kuhusu kuwa groomed nafikiri Mwalimu ali-groom wanasiasa wengi tu kuja kushika nafasi za juu. labda tatizo hakutamka hadharani "fulani ndiyo mrithi wangu."

..chukulia mwanasiasa kama John Malecela. hata kama Mwalimu alikuja kukosana naye baadaye, lakini zile nafasi za ndani na nje alizoshika nadhani zilikuwa maandalizi tosha ya kuwa Raisi.

..hata JK naye toka kuwa Naibu Waziri, baadaye Waziri wa Nishati na Madini, halafu Waziri wa Fedha[kijana kuliko wote Tz], na mwisho Waziri wa Mambo ya Nje, naamini pia ilikuwa ni nafasi ya kujifunza na kujiandaa kuja kuwa Raisi.

..kama unaona tuna viongozi wabovu siyo kwasababu ya walinyimwa nafasi ya kujiandaa au hawakuwa groomed, ni kwasababu wahusika hawakuwa serious kutumia nafasi walizopewa kujifunza.
 
Nilikua najiuliza imekuaje Sumaye akawa anasemwa sana kwa ufisadi wa mapori tu ilihali kuna mafisadi papa kama akina vijisent tulikua hatuwasikii kabisa?

Baada ya kusoma post zilizotangulia hapo juu nimepata mwanga kuwa ulikua ni mchezo mchafu wa EL kummaliza. Hizi media zetu nazo kwa kweli zinachangia sana kuwaenzi mafisadi, hazitendi haki.

Mkuu mkuki ulikuwa kwa nguruwe , sasa unarudi kwa binadamu.
Na aliyeua kwa upanga atakufa kwa upanga huo huo-vyombo vya habari mmefanya kazi yenu.
 
mimi ningemchagua fredrick Sumaye, nimemwona kwa mda mrefu for sure hayupo kama alivyokuwa anapambwa, beni kwa upande flani serekali yake ilikuwa na matatizo,watu wengi sana walichukua mali kwa kutumia jina la sumaye,na sababu mkubwa hahojiwi mtu unabaki ooh hii ni ya Sumaye lakini amemtumia fulani aendeshe. most f them are lies, sumaye angekuwepo kipindi huru kama hiki cha sasa hopeful angeweza kufanya mambo makubwa,my opinion na kutokana na thread basi!!
 
Pinda ndo safi maana yeye si fisadina anatuonea donge tunaovaa suti zetu kwa kuwa nchi hii ni masikini hivyo tuvae mashati ya batiki

Usishabikie kona wala penalt waweza fungwa goli la kisigino. Mwizi wa mbuzi ni yule aliyeshikwa na ngozi.
 
Mundu,

..mbona kuna vijana wengi tu wamejitosa kwenye siasa?

..Zitto,Masha,Adam Malima,Stella Manyanya,Muhonga, wote naweza kuwaweka ktk kundi la vijana.

..kuhusu kuwa groomed nafikiri Mwalimu ali-groom wanasiasa wengi tu kuja kushika nafasi za juu. labda tatizo hakutamka hadharani "fulani ndiyo mrithi wangu."

..chukulia mwanasiasa kama John Malecela. hata kama Mwalimu alikuja kukosana naye baadaye, lakini zile nafasi za ndani na nje alizoshika nadhani zilikuwa maandalizi tosha ya kuwa Raisi.

..hata JK naye toka kuwa Naibu Waziri, baadaye Waziri wa Nishati na Madini, halafu Waziri wa Fedha[kijana kuliko wote Tz], na mwisho Waziri wa Mambo ya Nje, naamini pia ilikuwa ni nafasi ya kujifunza na kujiandaa kuja kuwa Raisi.

..kama unaona tuna viongozi wabovu siyo kwasababu ya walinyimwa nafasi ya kujiandaa au hawakuwa groomed, ni kwasababu wahusika hawakuwa serious kutumia nafasi walizopewa kujifunza.
Mkuu Joka kuu!!

..Zitto,Masha,Adam Malima,Stella Manyanya,Muhonga ukisha wataja hao nadhani itabidi ukune kichwa ili uongeze majina mengine matano tu ya vijana kama hao katika siasa! Simply, vijana wamegoma.

Kuna methali ya kiswahili isemayo kuwa ' mbwa wa msasi mkali ni mkali pia' mwalimu alikuwa ni msasi mkali, lakini mbwa wake hawa ni Koko kabisa! kwahiyo ile hofu yangu kuwa mwalimu alikuwa na weakness ya ku-groom leaders wa baadaye ina jaza maji (it holds water)

jamani hata kama watu hawako serious kama unavyodai, ndo hakuna hata mmoja katika uongozi wote wa mwalimu wa miaka 24 toka uhuru ambaye ame lelewa vizuri na mwalimu? Kila mmoja anaimba wimbo mzuri wa tumuenzi mwalimu, je ni nani amevaa viatu vyake kwa sasa
 
wakati wa mchakato wa uchaguzi wa mwaka 2005, nakumbuka kila mtanzania alikua anakereka na kustaajabika kuwa aliyekuwa waziri mkuu wa serikali ya CCM 1995-2005 Mh Frederick Sumaye alikua anataka kugombea urais kwa kupitia ticket ya CCM.

Mapungufu yake mengi tuliyaona na kuyajua, tuhuma kubwa zikiwa alikuwa akichukua mashamba ya watu kwa nguvu au kwa njia ambazo hazikua halali [These were mere allegations].Pia na hela alizotumia wakati wa safari moja alienda marekani naomba mnisaidie kwa kumbukumbu nzuri.

Upande mwingine alichomoza EL, ambapo ni kama watanzania tulijisahau sijui au ah? au ndo ujinga wetu?, maana ni kama alionekana ni mtu msafi kwa mda wa kipindi kile cha mchakato wa uchaguzi 2005. Watu wote tulijua kuwa atakuja kuwa waziri mkuu lakini wachache tuliohoji umakini wake na utendaji wake kazi, hususan tukikumbuka EL alikataliwa na alikuwa hakubaliki na Mw Nyerere kwa kuwa na utajiri mkubwa pasipo kawaida.

wakati ule [2005] ulikua ukiwalinganisha EL na FS ni kama lowasa ali edge ahead, na honestly media ilikua sana against FS.

sasa tunajua A-Q if not Z ya EL, je kuna ya FS ambayo hatuyajui ambayo yana uzito unao fanana na EL au kumzidi.

Tukipima mizani yao nani kamzidi mwenzake mpaka sasa kwa ufisadi?

Nani anaweza ku-come back au anaweza kuwa the come back king, maana najua wote wana hamu ya kuingia kwenye uwanja wa siasa ila maji yamewazidi shingo...
Majembe yetu UKAWA
 
Back
Top Bottom