Lowassa strikes back!

Mimi nadhani hata Muungwana hamtaki swahiba wake kurithi kiti 2015. Angekuwa anataka, angefanya juu chini Dr Bilal (aliyekuwa anapigiwa debe na RA na EL) kupata uteuzi wa kugombea urais wa Zanzibar. Kwani strategy ya RA na EL ilikuwa kwamba kama Rais wa Zanzibar, Dr Bilal angekuwa Vice Chairman wa CCM, nafasi ambayo ingemuwezesha ku-control wajumbe wengi kutoka Visiwani wa NEC na General Congress ya CCM ili (pamoja na wengine wa Bara) kuweka nguvu ya kumpitisha EL mwaka 2015.

Bilal kukosa nafasi hiyo ni pigo kubwa kwa mikakakti ya akina EL na swahiba wake.


Kama ni kweli usemayo, kweli ni pigo kubwa. Lakini hapajaharibika kitu kwani cheo cha Umakamu wa Urais wa Jamhuri ni only one step of becoming full President, according to the Union Constitution. Chochote chaweza kutokea, Mungu apishie mbali!
 
watu mnapenda sana kumdharau kikwete
ukweli ni kwamba lowasa was pushed by his boss (JK)

lowasa asingeweza kujiuzulu mwenyewe na alivyokuwa na uchu wa madaraka
mabalozi mbali mbali walikuwa wameshaanza kulalama juu ya ishu ya richmond na ikizingatiwa G.Bush alikuwa mbioni kuja TZ, JK akaona njia pekee ya kusafisha jina lake ni kumuondoa lowasa, akamwambia jiuzulu na lowasa akawa hana ujanja tena. Hapo JK apporval ratings zake zikaja juu na Bush akawasili kiwetwe akiwa juu na akamwaga misaada lukule.

kabla ya Lowasa kutanga bungeni kujiuzulu lazima alienda kwa JK kumueleza nia yake.
Je inamaanisha lowasa alimuambia JK mimi najiuzulu kukuokoa wewe na serikali yako????
kwanza hawezi kuthubutu kwa ajili kumuambia hivyo JK ni sawa sawa na kumuambia kuwa wewe(JK) ndio wenye makosa na si mimi

na sababu nyingine ni kuwa it was a case of mafahali wawili hawakai zizi moja, lowasa made a big mistake of underestimating kikwete intelligence alikuwa na haraka sana ya kutaka kufika juu.
na kwa mara nyingine july 2015 kikwete atamsukuma tena lowasa na kuhakikisha anakufa kabisa.
lowasa anashindwa kukubali kuwa things will neva be the same again
 
.mzee wapinzani wa mtandawo walikuwa wamejipanga kweli kweli....


Na yeye hakuwa alitakiwa kujipanga kwanza kwa sababu ni mwanasiasa anayejionesha kuwa ni makini lakini vile vile kama Waziri Mkuu kwani kisu kilikuwa kooni mwa serikali yake.
na aina yeyote ya kujitetea asingeeleweka...na rais alishafanywa behind the scene ashindwe au aogope kumtetea

Aina yoyote ya kujitetea? sasa kwanini anajitetea sasa. Kama alishindwa kujitetea wakati ule kwa sababu ya kujipanga au kwa woga ndiyo sababu nyingine inafanya itoshe kabisa kujiuzulu. Kama Waziri Mkuu alitakiwa apiganie kile alichoamini kuwa yuko sahihi, kutofanya hivyo si kosa la Kamati Teule, Mwakyembe au bunge zima. Ni kosa lake yeye la kimkakati na anatakiwa alikumbatie kwa kulikubali.
......so mwanajijiji in general Taarifa za kijasusi alizopewa Lowassa kuhusu hali halisi zilimshtua sana..na zilikuwa za ghafla....ie Plan B ya kina mwakyembe ilikuwa tishio kwa utawala mzima......

Hatujui plan "B", wananchi wanajua kilichofanyika hadharani, kama kungekuwa na plan B Lowassa angeweza kuonesha hadharani na kupata sympathy ya Bunge. Mbona alitoa hoja ya kuzungumza asubuhi ile na kukubaliwa na Spika akaahirisha Bunge kwa siku nzima? Kama angetoa hoja kama nilivyodokeza hapo juu na ingekataliwa, angeomba Bunge liahirishwe ili ajipange kutoa majibu angekataliwa, kama angeomba ajipeleke mwenyewe kwa Kamati Teule ambayo yote ilikuwa pale na angekataliwa na kutaka kura ya imani ipigwe dhidi yake napo angekataliwa basi hapo na hapo pekee tungesema ameonewa. So far, hakuna KUONEWA.
naamini kabisa lowassa angepata taarifa mapema ya kinachopangwa ....angekuwa waziri mkuu hadi leo ...kwani hata angepata taarifa ndani ya masaa 24 au 48 kabla ya tukio ...angekuwa na uwezo wa kubadilisha kabisa..hali ile na kuwapanga waru wa kumtetea na namna ya kujitetea au hata lolote lingeweza kutokea .....

Bado angeweza kufanya hivyo kama angeweza kutumia nafasi yake ya Uwaziri Mkuu kuomba Bunge limpe muda kujibu "madai mazito ya kamati teule" au kuomba "apeleke ushahidi wake kwa kamati teule kabla Bunge halijaipokea rasmi ripoti ya kamati teule". Hakufanya hivyo. Hili ni kosa la Lowassa, na ni yeye pekee wa kulaumiwa na si mwingine.

.ni wazi tume ya mwakyembe ilichomudu ni USIRI mkubwa!!!

Of course.. ndiyo maana ya Kamati Teule. Lakini hakuna lolote ambalo tume ilisema ambalo lilikuwa halijulikani kabla. Niliandika miezi kadhaa kabla kuhusu maswali kadhaa kuhusu Richmond, niliwawekea na picha na taarifa toka Secretary of State wa TX, tukachambua uhalali mzima wa mkataba wa Richmond na kuithibitisha kuwa kampuni ilikuwa feki. Vipi unasema hakuwa anajua kinachofanyika. Kama Waziri Mkuu kwa kutokujua kuhusu Richmond na yeye mwenyewe kuanzisha uchunguzi wake alistahili kujiuzulu kabla ya Kamati Teule kuundwa.
 
..inaelekea wengi wenu mna umri mdogo humu ndani.

..Edward Ngoyai Lowassa ndiye aliyempa Uraisi Jakaya Mrisho Kikwete. kampeni zote chafu, kununua waandishi wa magazeti, etc etc ziliongozwa na kuratibiwa na Lowassa.

..anachotakiwa kufanya Lowassa ni kushinda kura ya maoni ya CCM na baada ya hapo anachukua Uraisi kiurahisi tu.

..kwa mtazamo wenu ni nani aliyeko ktk kamati kuu, na halmashauri kuu za CCM, anayeweza kuzima azma ya Lowassa kumrithi Kikwete?

..je, mna uhakika kwamba ndani ya CCM kuna wanachama wa kutosha ambao wanaona Lowassa hawafai na ni mzigo kwa chama chao.

NB:

..KAMA HAMUMTAKI LOWASSA 2015, BASI MSIMCHAGUE KIKWETE UCHAGUZI HUU WA 2010.
 
watu mnapenda sana kumdharau kikwete
ukweli ni kwamba lowasa was pushed by his boss (JK)

lowasa asingeweza kujiuzulu mwenyewe na alivyokuwa na uchu wa madaraka
mabalozi mbali mbali walikuwa wameshaanza kulalama juu ya ishu ya richmond na ikizingatiwa G.Bush alikuwa mbioni kuja TZ, JK akaona njia pekee ya kusafisha jina lake ni kumuondoa lowasa, akamwambia jiuzulu na lowasa akawa hana ujanja tena. Hapo JK apporval ratings zake zikaja juu na Bush akawasili kiwetwe akiwa juu na akamwaga misaada lukule.

kabla ya Lowasa kutanga bungeni kujiuzulu lazima alienda kwa JK kumueleza nia yake.
Je inamaanisha lowasa alimuambia JK mimi najiuzulu kukuokoa wewe na serikali yako????
kwanza hawezi kuthubutu kwa ajili kumuambia hivyo JK ni sawa sawa na kumuambia kuwa wewe(JK) ndio wenye makosa na si mimi

na sababu nyingine ni kuwa it was a case of mafahali wawili hawakai zizi moja, lowasa made a big mistake of underestimating kikwete intelligence alikuwa na haraka sana ya kutaka kufika juu.
na kwa mara nyingine july 2015 kikwete atamsukuma tena lowasa na kuhakikisha anakufa kabisa.
lowasa anashindwa kukubali kuwa things will neva be the same again
Mi SIDHANI kama kabls ya kujiuzulu kwake Lowassa alikwenda kuongea na mkuu wake, na wakakubalina juu ya kujiuzulu kwake. Ingekuwa wameongea kabla na kukubaliana, Lowassa asingejiuzulu kwa namna alivyojiuzulu. Angejipanga kwa makini hata katika lugha, na kujiuzulu bila jazba.

Lakini ukiangalia namna alivyofanya siku ile inaonesha dhahiri kabisa kwamba jamaa alikuwa hajajipanga kabla kwani - mi nionavyo - ni kama alikurupuka tu. Ona hata lugha yake: "Naachia ngazi, najua kinachotafutwa ni Uwaziri Mkuu". Kwa mtu mkomavu kisiasa na hata kiumri hakutazamiwa ku-react kwa jinsi ile.

Ndo maana mi nakataa dhana kwamba jamaa aliongea kwanza na JK juu ya kujiuzulu kwake, kwani asinge-act vile. Mi naona ni uamuzi aliouchukua ghafla: kwa initiative zake; na ndo mana hata wabunge wote walishangaa na kuzizima. Hawakutegemea ghafla hivo.
 
Kwa wale walioangalia TBC jana watakuwa wamejionea viinimacho vilivyofanywa na Tido mhando ili kumrudisha lowasa kwenye public spot light.

Hivi huyu pinda hana watu wa kumshauri na kumwambia kuwa anatumika na Tido na TBC kwa manufaa ya Lowassa.

Na hata kwenye interview ya Lowassa utaona Tido alikuwa anampiga vijembe Pinda na kusema baada ya Lowassa kuondoka mambo yamepooza huku lowasa akijidai hajui.

Pinda amka kutoka usingizi uliolala.....
 
Bado Pinda anajiona kuwa ni mdogo kwa Lowassa.. si alikuwa chini yake kule Ofisi ya Waziri Mkuu? Au mnafikiri alipendekezwa tu kuushika Uwaziri Mkuu bila Lowassa kujua. Ndiyo maana hautaki tena kwani mwenye nao anauridia baadaye mwaka huu.
 
Inashangaza mbado kuna wananchi misukule bado wanaitetea hii misukule origino pamoja na HASARA KUBWA walituingizia taifani. HII INAGHADHABISHA SANA.
Tatizo la misukule wanategemea master wao awapatie ugali na kila kitu.
Hapo ndo penye tatizo.

Watu wapo tayari kuuza utu wao ilhali wamtumikie SHETANI
 
Bado Pinda anajiona kuwa ni mdogo kwa Lowassa.. si alikuwa chini yake kule Ofisi ya Waziri Mkuu? Au mnafikiri alipendekezwa tu kuushika Uwaziri Mkuu bila Lowassa kujua. Ndiyo maana hautaki tena kwani mwenye nao anauridia baadaye mwaka huu.

mkuu apo kwenye red umeniacha kidogo :A S tongue:
 
Bado Pinda anajiona kuwa ni mdogo kwa Lowassa.. si alikuwa chini yake kule Ofisi ya Waziri Mkuu? Au mnafikiri alipendekezwa tu kuushika Uwaziri Mkuu bila Lowassa kujua. Ndiyo maana hautaki tena kwani mwenye nao anauridia baadaye mwaka huu.
Kwahiyo kujiuzulu kwa EL ilikuwa danganya toto?Naona kama una maanisha Pinda alikuwa akimshikia nafasi EL kwa muda hadi wadanganyike wasahau,ajisafishe then arudi kwenye nafasi yake kabla ya kugombea urais mwaka 2015?
 
Bado Pinda anajiona kuwa ni mdogo kwa Lowassa.. si alikuwa chini yake kule Ofisi ya Waziri Mkuu? Au mnafikiri alipendekezwa tu kuushika Uwaziri Mkuu bila Lowassa kujua. Ndiyo maana hautaki tena kwani mwenye nao anauridia baadaye mwaka huu.
Kwa hiyo alimshikia Uwaziri Mkuu kwa muda? Kama mwendo wenyewe ndio huu watanzania wataanza kuwaabudu wanasiasa kama Miungu yao. ''Allah Lowasa U Akbar, Allah Kikwete U Akbar''. ''Kwa jina la Lowasa na la Kikwete'' Wote tuseme.....
 
Tido aliletwa TBC na Lowassa. Na mkataba wake utakapomalizika anakwenda kuongoza TV ya Lowassa Arusha. So figure.
 
..inaelekea wengi wenu mna umri mdogo humu ndani.

..Edward Ngoyai Lowassa ndiye aliyempa Uraisi Jakaya Mrisho Kikwete. kampeni zote chafu, kununua waandishi wa magazeti, etc etc ziliongozwa na kuratibiwa na Lowassa.

..anachotakiwa kufanya Lowassa ni kushinda kura ya maoni ya CCM na baada ya hapo anachukua Uraisi kiurahisi tu.

..kwa mtazamo wenu ni nani aliyeko ktk kamati kuu, na halmashauri kuu za CCM, anayeweza kuzima azma ya Lowassa kumrithi Kikwete?

..je, mna uhakika kwamba ndani ya CCM kuna wanachama wa kutosha ambao wanaona Lowassa hawafai na ni mzigo kwa chama chao.

NB:

..KAMA HAMUMTAKI LOWASSA 2015, BASI MSIMCHAGUE KIKWETE UCHAGUZI HUU WA 2010.


Bravo Mkuu,

Naona wengi wameshindwa kung'amua hii fomula. Niliposema kuwa EL hakwenda popote nilikuwa namaanisha kuwa ndani ya CCM sasa hivi hakuna mtu mwenye Ubavu wa kumrithi JK kumzidi EL.

Kama vile usiku hufuatiwa na mchana, ndivyo itakavyokuwa 2015, EL ataweka jina na hakika nawaambieni kutakuwa hakuna wa kumpinga...why..simple; WANAMUOGOPA.
 
Kwahiyo kujiuzulu kwa EL ilikuwa danganya toto?Naona kama una maanisha Pinda alikuwa akimshikia nafasi EL kwa muda hadi wadanganyike wasahau,ajisafishe then arudi kwenye nafasi yake kabla ya kugombea urais mwaka 2015?

That is correct - EL will come back: no matter what?
 
Lowasa ameanza kampeni ...................na hapo ni mwanzo tu.

subiri kuona sura ya Lowasa kila kona na pembe ya Tanzania.

matangazo ya tv ya mgombea mmoja mmoja mwaka huu yatashamri kwenye tv na redo

nasema utamjua lowasa kuliko unavyomjua mbunge wa jimbo lako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom