Nimekuwa nikifuatilia sana vyombo vya habari vinavyopinga Lowassa(Mwanahalisi na Raiamwema) na vinavyo msapoti(Rai na Mtanzania). Nimefuatilia sana wanasiasa wanaompinga na kumsapoti. Mwisho nimebaini kuwa Lowassa ni tishio kubwa kwa wanaoutaka urais wa muungano ndani ya chama chake na kwa upande wa upinzani. Ana nguvu kubwa sana serikalini na katika chama. Ni bingwa wa kuratibu mtandao kisomi. Ni mtendaji na haogopi. Na iwapo ataamua kugombea, hatakuwa na mpinzani mwenye nguvu ndani ya chama chake na hata ktk uchaguzi mkuu. Sote tumeshuhudia jinsi alivyoweza kuukwaa uenyekiti wa kamati ya bunge ya mambo ya nje, ulinzi na usalama bila mtu yeyote kutia mguu kumpinga. Na sasa tumeshuhudia jinsi anavyopata sapoti kutoka kwa Mhe Beatrice Shelukindo na mumewe William Shelukindo. LOWASSA NI TISHIO