Lowasa ndio jembe la CCM, Richmond mwizi alikuwa Kikwete, Lowasa alibebeshwa aibu kulinda heshima ya nchni.
Ndugu yangu chonde chonde chonde! Usidhani tumezaliwa leo. Kama wewe ulikuwa mtoto wakati kashfa hii inatokea, au kama wewe hukuwa na akili timamu au ulikuwa jela kipindi hicho, tuache tuliokuwepo tena tukiwa na akili timamu tutafakari njia nzuri ya kumwadhibu mwizi wetu huyu, maana hadi sasa amekaa mkao wa kusubiri adhabu laini wanaotakiwa kumuadhibu wameshiba dini na sasa wanaona kama vile ni dhambi kumtia adabu. Kitendo hiki cha kumuacha huru ndicho kinachotumiwa na hawa akina Yuda waliotapakaa pote nchini wakidai kuwa hakuhusika. Mungu bahati ametuonyesha katika makashfa mengine anavyoendelea kutoboa hazina ya nchi hiyo hiyo ambayo leo anajifanya kuipenda na kuihurumia.
Hivi kazi ni urais tu? Atuache tupumue na kutafakari mustakabali wa taifa hili! Kila tukijipanga kufanya la maana aliowakodi kumtakasa wanaibuka na hoja tasa ambazo ni kichefuchefu. Huyu bwana maekuwa mbunge toka 1990 na jimbo lake ni miongoni mwa majimbo yanayoshika mkia kielimu. Kwa nini asiwapeleke private schools badala ya kutoa suluhisho la kinafiki na lenye nia ya kuendelea kuifilisi hazina yetu. Maskini populist huyu! Na wapambe wake wanacheka tu na huku wanampotosha!