Mshume Kiyate
JF-Expert Member
- Feb 27, 2011
- 6,766
- 894
Wana JF.
Historia inajibainisha yenyewe kwamba watu makini wa sampuli kama ya Lowassa hawachelei kurejea nafasi za hapo awali.
Na ujio wao huwa ni wa kishindo kikubwa na hicho kishindo ndicho haswa kinawatia viwewe wale mahasimu wake wa kisiasa kutokana na kuona wazi wazi kushindwa kuhimili historia ya utendaji kazi wa Lowassa unaotambulika na kukubalika ndani ya jamaii.
Sote tumeshudia utendaji wa Lowassa kwa nyakati zote tangu mwaka 1975, Mbunge wa Monduli kwa kipindi chote hicho kaweza kufanya mambo yanayoonekana kwa macho ambapo kwa namna mojo ama nyingine yataendelea kuwanafaisha waliopo na vizazi vijavyo.
Lowassa, alipigana vilivyo ongezeko la shule, hakuwapa nafasi ya kupumua wakuu wa mikoa wa wilaya katika ujenzi wa shule hizo.
Hali hiyo ilisababisha ongezeko kutoka 14,257 mwaka 2005 hadi 15,816 mwaka 2010 ambalo ni sawa na ongezeko la wastani wa shule 1559 hali iliyowezesha wanafunzi kuongezeka kutoka 7,541,208 hadi 8,419,305. Haya yote ni matunda ya kazi ya Edward Lowassa.
Tunakumbuka ya kwamba huyu huyu Lowassa aliweza kuvunja mkataba mbovu wa City Water kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla.
Lowassa alipokuwa Waziri wa Ardhi alisimama kidete pale alipogundua Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam wamempa mfanyabiashara eneo la Mnazi Mmoja.
Lowassa hakubaliana na uamuzi huo na kuamuru wananchi wauvunje uzio wake na mabati aliyoweka na hivyo eneo la uwanja kurudi kwa Serikali na Wananchi
Historia inajibainisha yenyewe kwamba watu makini wa sampuli kama ya Lowassa hawachelei kurejea nafasi za hapo awali.
Na ujio wao huwa ni wa kishindo kikubwa na hicho kishindo ndicho haswa kinawatia viwewe wale mahasimu wake wa kisiasa kutokana na kuona wazi wazi kushindwa kuhimili historia ya utendaji kazi wa Lowassa unaotambulika na kukubalika ndani ya jamaii.
Sote tumeshudia utendaji wa Lowassa kwa nyakati zote tangu mwaka 1975, Mbunge wa Monduli kwa kipindi chote hicho kaweza kufanya mambo yanayoonekana kwa macho ambapo kwa namna mojo ama nyingine yataendelea kuwanafaisha waliopo na vizazi vijavyo.
Lowassa, alipigana vilivyo ongezeko la shule, hakuwapa nafasi ya kupumua wakuu wa mikoa wa wilaya katika ujenzi wa shule hizo.
Hali hiyo ilisababisha ongezeko kutoka 14,257 mwaka 2005 hadi 15,816 mwaka 2010 ambalo ni sawa na ongezeko la wastani wa shule 1559 hali iliyowezesha wanafunzi kuongezeka kutoka 7,541,208 hadi 8,419,305. Haya yote ni matunda ya kazi ya Edward Lowassa.
Tunakumbuka ya kwamba huyu huyu Lowassa aliweza kuvunja mkataba mbovu wa City Water kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla.
Lowassa alipokuwa Waziri wa Ardhi alisimama kidete pale alipogundua Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam wamempa mfanyabiashara eneo la Mnazi Mmoja.
Lowassa hakubaliana na uamuzi huo na kuamuru wananchi wauvunje uzio wake na mabati aliyoweka na hivyo eneo la uwanja kurudi kwa Serikali na Wananchi