masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 17,857
- 13,140
Nimefuatilia matamshi ya kiongozi huyu wa CCM aliyelazimika juiuzulu Uwaziri Mkuu, na sijapendezwa na matamshi yake yanayoendelea kusikika katika vyombo vya habari, hata leo.
Mwalimu alifanya kazi kubwa kuondoa dhana ya kufikiri"kikabila" ili waTanzania tuwe na umoja.
Hivyo basi kumsikia kiongozi aliyewahi kushika wadhifa wa pili wa juu kabisa katika Taifa letu akipigia debe kabila lake -kiitikadi na kimkakati, basi nafikiri there is something seriously wrong hapa.
Kwa siku kadhaa sasa Lowassa amekuwa akipigia debe wazi wazi kabila lake(wengine wanasema si lake) la kimasai ili waingizwe katika katiba ya JMT.
Hii ni hatari.
Wachagga nao wakitaka waingizwe kwenye katiba, Wahaya je? na Wanyakyusa au hata Wagogo itabidi lipigwe debe ili kila kabila litambuliwe kikatiba.
Gazeti la Mwananchi la leo linasema Lowassa anataka kuongoza ujumbe wa wamasaai kumwona Rais JK!!
Huo nafikiri hautakuwa ujumbe wa mwisho maana kutakuwa na ujumbe wa Wachagga, wa Wasandawe na Wadigo kumwona Rais kwa mustakabali wao!!
Hatujasahau hata kidogo spidi aliyotumia Lowassa kuwaweka "wa kwao" katika sehemu nyingi na nyeti alipokuwa Waziri Mkuu.
Utetezi wa Ole Naiko wa TIC ulijieleza katika hili wakati Lowassa akijiuzulu uwaziri Mkuu.
Mlolongo huu wa mawazo ndiyo hata Mwalimu aliwahi kusema mtu kafilisika kisiasa, mtu huyo hana political base, anatafuta unyasi ili apate uhalali wa kisiasa.
Mbaya zaidi ni matokeo yake katika siasa za jamii ya kiTanzania.
Lowassa I did not think that you stoop so low!!