nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
- Monday, November 28, 2011, 6:34
- Mtanzania-Habari
- Atumia biblia kubeza wanaomchafua kisiasa
- Asema Mungu yu pamoja naye, adai anapumua
Na Pendo Mangala,Singida
Alisena kutokana na kuwepo na mambo mengi ya siasa, amekuwa akichafuliwa jina lake kupitia vyombo, lakini anamshukuru Mungu amemlinda na kumfariji wakati wote.
Alisema siku zote watu wengi wamekuwa wakimfuatilia katika mambo ya kisiasa, huku wakimtuhumu kuwa ni fisaidi, lakini kwa kuliamini neneo la Mungu ambalo limekuwa msada mkubwa kwake.
"Siku moja tulikuwa tumekaa na mke wangu, tunaangalia runinga kipindi cha magazeti, kukawepo na taarifa nyingi za hovyo kuhusu mimi ambazo baadhi ya taarifa hizo mtangazaji alishindwa kuzisoma,"alisema Lowassa.
Alisema kufuatia kuwapo kwa taarifa hizo, mke wake aliingia ndani na kuchukua Biblia na kumsomea neno kutoka kitabu cha Isaya 40-10.
Maneno hayo ya Biblia yanasema "Usiogope kwa maana mimi ni pamoja nawe,usifadhaike kwa maana mimi ni Mungu wako nitakutia nguvu,naam nitakusaidia, naam nitakushika kwa mkono wa kuume wa hai yangu"
Pia kitabu cha Warumi 8 mstari wa 31 ambao unasema ‘basi tuseme nini juu ya hayo?Mungu akiwapo upande wetu ni nani aliye juu yetu,
"Kwakweli baada ya maneno haya yalinifariji sana na kunitia nguvu na sasa ninaishi kwa amani,"alisema Lowassa.
Hata hivyo, aliwashukuru viongozi mbalimbali wa dini wakiwemo Waislamu kwa maombi yao ambayo wamekuwa na upendo juu yake kwa kumuombea kila siku.
Kwa upande wake, Askofu wa Dayosisi, Eliufoo Sima alisema madai ya maskini nchini ni mengi ambayo ni pamoja na mahitaji ya kila siku ambayo wangependa viongozi wayashughulikie kwa umakini mkubwa.
Alisema kama viongozi hao watashughulikia mtatizo ya wananchi, watakuwa wamepiga hatua kubwa ya kuondoa manung'uniko miongoni mwa watu ambayo yaanaharibu jamii ya Kitanzania.
Katika harambee hiyo ya ujenzi wa kanisa, Lowassa alichangia Sh 10 wakati kiasi cha Sh 138 zilipatikana kutoka kwa watu mbalimbali.
Wiki iliyopita, Lowassa alivunja ukimya wakati alipopata nafasi ya kuzungumza katika mkutano wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kutoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali zikiwemo tuhuma za yeye kudaiwa kuwa ni fisadi.
Alikanusha kuhusika na tuhuma hizo na kutaka wale walioneza tuhuma hizo kwa kutumia rasimalia za chama hicho, wachukuliwe hatua akiwemo Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.