Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
Binafsi nimefurahishwa na makala ya mwanakijiji na sishangai anapopata mashambulizi kwani anakabiliana na system iliyotawala kwa miaka zaidi ya 50 mfululizo ambayo imezaa watu wanayoiunga mkono out of mazoea, wengine maslahi, wengine ushabiki na wengi zaidi ujinga (illiteracy/ignorance). Kuna utofauti wa kuunga chama na miiko/misingi yake vis a vis kuunga mkono chama na madudu yake. Hapa nalenga watu wanaokiunga chama na madudu yake. Mimi ni Mwana CCM lakini hiki sio chama ambacho kama ningekuwa nina ‘choice', ningependa kiwe katika hali ya leo. Lazima tukubali ukweli kwamba CCM imekosa mwelekeo. The only excuse we can have ni kwamba chama "hakijakosa mwelekeo" BUT "kinakoseshwa mwelekeo". Wana CCM, hivi ni mambo gani ambayo leo hii tunaweza kusimama majukwaani huko vijijini na kujenga hoja kwamba CCM ni chama chao? Zaidi ya kuja na ‘make up list' ya hapa na pale, kwa kweli hatuna hoja. Tusipoteze muda mwingi kwenda kwa wananchi kuwasemea upinzani, tutumie muda mwingi zaidi kwenda kwa wananchi kurekebisha mapungufu yetu kwa vitendo, hoja na kwa siasa safi.
Makala ya Mwanakijiji inapata upinzani mkubwa kutokana na mtatizo mawili makubwa: Kwanza, wengi tumekuwa wazito kuelewa dhana ya uhuru wa kutoa mawazo. Mimi sioni tatizo kama Mwanakijiji ni mfuasi wa Chadema. Na isitoshe, hata katika siasa za nchi za wenzetu waliokomaa kidemokrasia kwa mfano Marekani, kuna media organizations ambazo zipo aligned na vyama vya siasa na kwa uwazi kabisa. Kwa mfano, makampuni kama FOX, hawa ni republicans, na makampuni kama MSNBC, hawa ni democrats. Lakini pamoja na tofauti zao hizi ambazo hubebwa na utofauti katika ideological following or beliefs, vyama vyote vinasimamia maslahi ya taifa, wanachotofautiana au pishana ni njia ya kufuata towards a better America. Huwa namsoma sana Mwanakijiji hapa JF na kwenye magazeti, na mara nyingi hoja zake huwa ni za maslahi ya taifa kwa kweli kwani zina cut across mtu yoyote mwenye nia njema na nchi yetu. Inawezekana kuna nyakati anaonekana anaegemea upande fulani, lakini kama nilivyokwisha sema, hata kwenye nchi za wenzetu waliokomaa kidemokrasia, hili ni jambo la kawaida.
Pili, wengi wetu humu tupo busy kujaribu ‘to make sense of his (mwanakijiji) language' in the article instead of making sense of the issues that he is trying to address before us. Makala ya Mwanakijiji leaves us with an important question that is in dispute and must be settled. Binafsi ningependa kuiangalia makala ya Mwanakijiji kwa mapana zaidi, hasa kuhusu suala zima la jinsi ya kumpata rais wa Tanzania. Vigezo na utaratibu uliopo ni kama vile Rais wa Tanzania daima atatokea CCM, and to make matters worse, kuna dalili kubwa kwamba CCM na mashabiki wake wanajikita zaidi kuzalisha marais wengi (quantity) kuliko wingi unaoendana na ubora wa marais hao (quality).
Katiba ya sasa ya Tanzania (1977) ni Katiba ya CCM. Pamoja na kufanyiwa amendments za hapa na pale lakini bado ilitungwa ili kuhalalisha supremacy ya CCM. Ndio maana kwa miaka karibia kumi na tatu (1964 – 1977), tulikuwa tunaongozwa na katiba ya mpito na hatukujali hilo kwani Katiba ya TANU, hasa Azimio la Arusha, na uongozi makini wa Nyerere ulifanya wengi wetu tusijali sana hilo kwani Nyerere alikuwa ana deliver. Ilipofika mwaka 1977, Vyama vya TANU na ASP vikaungana na kulazimisha mabadiliko, na hapo ndipo katiba ya nchi ikazaliwa ili kuhalalisha utawala wa chama kimoja (TANU + ASP = CCM), na ndio maana sehemu kubwa ya mgogoro wa katiba yetu ni the "union question". Vinginevyo, baada ya 1977, Katiba ya CCM ikawa Superior kwa Katiba ya Nchi. Ipo mifano mingi juu ya hili lakini kwa haraka haraka niseme tu kwamba - viongozi wengi wa CCM na Serikali kwa ujumla walikuwa mara kwa mara wanakikiuka katiba ya nchi lakini hakuna aliyekuwa anawakemea, lakini ilipotokea kiongozi anakiuka Katiba ya Chama, huyo alionekana muasi, mhaini na kila lililo baya. Muundo huu ukatengeneza mfumo mbovu wa kutuzalishia viongozi, na ni hapa ndipo naungana na mwanakijiji kwamba mfumo wetu wa kutupatia viongozi (CCM) leo hii una matatizo.
Kwahiyo, tafsiri yangu ya hoja ya Mwanakijiji ndio hiyo i.e. ‘kimfumo zaidi' – hasa pale anaposema kwamba haoni jinsi gani CCM inaweza kupata Rais bora ajae ambae atatoka miongoni mwa wabunge (CCM) wa sasa. Tukituliza kidogo akili zetu na kutafakari hili, wengi tutakubaliana na mwanakijiji hata kama haitakuwa mia kwa mia. Nitajaribu kuichambua hoja ya mwanakijiji kwa kutumia Katiba ya sasa ya Tanzania kwani hiyo ndio inatoa vigezo vya mtu kuwa rais bila ya kujali rais anatoka chama gani. Lakini cha kushangaza kidogo ni kwamba katika mijadala kuhusu mapungufu ya katiba yetu, nje ya suala la umri na mgombea binafsi, hatuangalii sana suala hili la sifa ya mtu kuwa rais kwa mujibu wa katiba ya Tanzania (1977).
Kwa mujibu wa katiba ya Tanzania (1977), sifa za mtu kuwa Rais wa Tanzania, awe:
(a) Ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa Sheria ya Uraia;
(b) Ametimiza umri wa miaka arobaini;
(c) Ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;
(d) Anazo sifa za kumwezesha kuwa Mbunge au Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi,
(e) Katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi Mkuu hajawahi kutiwa hatiani katika Mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.
Nitajaribu kujadili vigezo hivi vitano kwa haraka haraka.
· na miaka ishirini na moja, na ambaye anajua kusoma na kuandika katika Kiswahili au Kiingereza;
· ni mwanachama na ni mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;
· katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi hakuwahi kutiwa hatiani katika mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.
Tayari tumeshaona migongano mingi hapo, na kuna sifa nyingine ambayo sijaiweka hapo ambayo, wakati sifa kielimu (mbunge) ni angala darasa la saba, sifa kielimu (rais) ni angalau shahada ya kwanza.
Wengi wetu katika mjadala huu inaonekana hatupo tayari kumfikiria mtanzania ambae hayupo kwenye kundi la sasa la wabunge (CCM); tunaamini kwamba nje ya wabunge waliopo sasa, hakuna mtanzania mwingine mwenye uwezo wa kuwa Rais na Amiri Jeshi mkuu. Na wenye mtazamo huu hawajali kama ubunge wa mgombea ambaye ni chaguo lao, ubunge wa aliupata vipi - kama ulipatikana kihalali au kwa hila, vitisho, rushwa na ujanja ujanja wa kila aina. Kwa wenzetu hawa, hilo kwa sio muhimu!!
Wana CCM wenzangu, tusiogope kushindwa hoja kuhusu CCM kufilisika kihoja mbele ya umma, kwani badala ya kutibu tatizo, tunaficha ugonjwa ambao utakuja kutuadhiri. Tukubali kwamba nchi yetu imeshakomaa kuruhusu demokrasia ya kupokezana vijiti. Wana CCM wenzangu, kushindwa 2015 (kama itatokea) sio mwisho wa dunia, and as a matter of fact, tutakuwa kwenye nafasi bora zaidi ya kujipanga upya tukiwa nje kuliko tukiwa madarakani kwa sababu moja kubwa: Tukipoteza madaraka ya nchi, hapo ndio tutajua kina nani walikuwa wapo CCM kimaslahi na kina nani walikuwa wapo CCM kwa dhati kwani ni dhahiri kwamba wengi watakimbilia upinzani, na hii itawapatia nafasi wale wachache watakaobaki CCM kwani watakuwa na nia ya kweli ya kukirejesha Chama kwenye mstari.
Wana CCM wenzangu, CCM ni chama pekee katika dunia ya tatu kilichokaa madarakani kwa zaidi ya nusu karne, hasa katika mazingira ya liberal democracy. Sasa kama vipo vyama vinavyopoteza madaraka ya nchi kwa kutawala miaka mitano au kumi, sisi ni nani kuwa immune kiasi hicho? Unless madaraka kwetu ni kwa ajili ya kujipatia immunity na ufisadi ili tusifikishwe mbele ya sheria pale chama kingine kitakapochukua madaraka; au unless lengo letu ni kutumikia matumbo yetu na sio wananchi, vinginevyo watanzania wakiamua kututoa madarakani 2015, tukubali maamuzi ya wengi, lakini isiwe mwisho wa dunia kwetu kwani kwa mfano:
Last but not least, niseme tu kwamba pamoja na haya yote, binafsi bado nina jina moja ambalo nina imani mtu huyo ana uwezo wa kulitumikia taifa hili vizuri (ngazi ya Urais) hata kama anatokana na wabunge wa sasa (CCM), kwa sababu amekuwa anapingana na the existing state of affairs (some of which nimezijadili) kwa muda mrefu. Lakini haina maana kwamba yeye ni bora kuliko wengine wa upinzani, na muda ukifika nitamtaja ili tumpime kwa hoja (sio kwa ushabiki, mazoea au maslahi).
Vinginevyo naunga mkono hoja ya Mwanakijiji kwa vigezo nilivyovijadili.
Makala ya Mwanakijiji inapata upinzani mkubwa kutokana na mtatizo mawili makubwa: Kwanza, wengi tumekuwa wazito kuelewa dhana ya uhuru wa kutoa mawazo. Mimi sioni tatizo kama Mwanakijiji ni mfuasi wa Chadema. Na isitoshe, hata katika siasa za nchi za wenzetu waliokomaa kidemokrasia kwa mfano Marekani, kuna media organizations ambazo zipo aligned na vyama vya siasa na kwa uwazi kabisa. Kwa mfano, makampuni kama FOX, hawa ni republicans, na makampuni kama MSNBC, hawa ni democrats. Lakini pamoja na tofauti zao hizi ambazo hubebwa na utofauti katika ideological following or beliefs, vyama vyote vinasimamia maslahi ya taifa, wanachotofautiana au pishana ni njia ya kufuata towards a better America. Huwa namsoma sana Mwanakijiji hapa JF na kwenye magazeti, na mara nyingi hoja zake huwa ni za maslahi ya taifa kwa kweli kwani zina cut across mtu yoyote mwenye nia njema na nchi yetu. Inawezekana kuna nyakati anaonekana anaegemea upande fulani, lakini kama nilivyokwisha sema, hata kwenye nchi za wenzetu waliokomaa kidemokrasia, hili ni jambo la kawaida.
Pili, wengi wetu humu tupo busy kujaribu ‘to make sense of his (mwanakijiji) language' in the article instead of making sense of the issues that he is trying to address before us. Makala ya Mwanakijiji leaves us with an important question that is in dispute and must be settled. Binafsi ningependa kuiangalia makala ya Mwanakijiji kwa mapana zaidi, hasa kuhusu suala zima la jinsi ya kumpata rais wa Tanzania. Vigezo na utaratibu uliopo ni kama vile Rais wa Tanzania daima atatokea CCM, and to make matters worse, kuna dalili kubwa kwamba CCM na mashabiki wake wanajikita zaidi kuzalisha marais wengi (quantity) kuliko wingi unaoendana na ubora wa marais hao (quality).
Katiba ya sasa ya Tanzania (1977) ni Katiba ya CCM. Pamoja na kufanyiwa amendments za hapa na pale lakini bado ilitungwa ili kuhalalisha supremacy ya CCM. Ndio maana kwa miaka karibia kumi na tatu (1964 – 1977), tulikuwa tunaongozwa na katiba ya mpito na hatukujali hilo kwani Katiba ya TANU, hasa Azimio la Arusha, na uongozi makini wa Nyerere ulifanya wengi wetu tusijali sana hilo kwani Nyerere alikuwa ana deliver. Ilipofika mwaka 1977, Vyama vya TANU na ASP vikaungana na kulazimisha mabadiliko, na hapo ndipo katiba ya nchi ikazaliwa ili kuhalalisha utawala wa chama kimoja (TANU + ASP = CCM), na ndio maana sehemu kubwa ya mgogoro wa katiba yetu ni the "union question". Vinginevyo, baada ya 1977, Katiba ya CCM ikawa Superior kwa Katiba ya Nchi. Ipo mifano mingi juu ya hili lakini kwa haraka haraka niseme tu kwamba - viongozi wengi wa CCM na Serikali kwa ujumla walikuwa mara kwa mara wanakikiuka katiba ya nchi lakini hakuna aliyekuwa anawakemea, lakini ilipotokea kiongozi anakiuka Katiba ya Chama, huyo alionekana muasi, mhaini na kila lililo baya. Muundo huu ukatengeneza mfumo mbovu wa kutuzalishia viongozi, na ni hapa ndipo naungana na mwanakijiji kwamba mfumo wetu wa kutupatia viongozi (CCM) leo hii una matatizo.
Kwahiyo, tafsiri yangu ya hoja ya Mwanakijiji ndio hiyo i.e. ‘kimfumo zaidi' – hasa pale anaposema kwamba haoni jinsi gani CCM inaweza kupata Rais bora ajae ambae atatoka miongoni mwa wabunge (CCM) wa sasa. Tukituliza kidogo akili zetu na kutafakari hili, wengi tutakubaliana na mwanakijiji hata kama haitakuwa mia kwa mia. Nitajaribu kuichambua hoja ya mwanakijiji kwa kutumia Katiba ya sasa ya Tanzania kwani hiyo ndio inatoa vigezo vya mtu kuwa rais bila ya kujali rais anatoka chama gani. Lakini cha kushangaza kidogo ni kwamba katika mijadala kuhusu mapungufu ya katiba yetu, nje ya suala la umri na mgombea binafsi, hatuangalii sana suala hili la sifa ya mtu kuwa rais kwa mujibu wa katiba ya Tanzania (1977).
Kwa mujibu wa katiba ya Tanzania (1977), sifa za mtu kuwa Rais wa Tanzania, awe:
(a) Ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa Sheria ya Uraia;
(b) Ametimiza umri wa miaka arobaini;
(c) Ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;
(d) Anazo sifa za kumwezesha kuwa Mbunge au Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi,
(e) Katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi Mkuu hajawahi kutiwa hatiani katika Mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.
Nitajaribu kujadili vigezo hivi vitano kwa haraka haraka.
- Kwanza ni suala la uraia – Siasa za sasa ni zamu ya upande huu au upande ule unatoa mwanya wa kutuletea Ma-rais wabovu ambao wanateuliwa ili kufanikisha zaidi malengo ya kisiasa. Kwa mfano, siasa ya zamu ya bara bila vigezo vingine vya msingi inaweza kutuletea rais wa ovyo lakini pia vile vile siasa ya zamu ya visiwani. Ni muhimu katika kumpata Rais, tukasukumwa zaidi na mahitaji ya watanzania in all spheres (kisiasa, kiuchumi na kijamii) badala ya kusukumbwa zaidi na siasa za muungano.
- Pili ni suala la umri (miaka 40). Hili tumeshalijadili sana hivyo nitaliacha kwa sasa.
- Tatu ni kuhusu mgombea lazima atokane na chama cha siasa – hili pia tumeshalijadili sana, huku wengi wetu tukihimiza umuhimu wa kuruhusu wagombea binafsi. Lakini ningependa kulisemea kidogo. Kwenye mdahalo baina ya Nape, Mnyika, Naibu Katibu Mkuu CUF (jina limenotoka), Nape alijaribu kujenga hoja kwamba hatuna haja ya mgombea binafsi kwani hata nchi kubwa kama Marekani wagombea binafsi hawana nguvu, hivyo kusisitiza msimamo wake kwamba Tanzania hatuna haja ya wagombea binafsi ndani ya katiba mpya. Hili ni suala ambalo hata Nyerere leo hii angepingana na Nape kwani hata yeye hakuona sababu za msingi za kuendelea kulikataa hilo kikatiba. Lakini nikirudi kwenye hoja ya Nape, anasahau kwamba Rais wa kwanza wa marekani ‘George Washington', hakutokana na chama chochote cha siasa, na ilichukua muda mrefu kwa marekani kujenga vyama vya maana. Pamoja na kuibuka kwa vyama viwili vya maana baadae, bado katiba ya marekani iliendelea kuwapa option wananchi kuchagua mgombea binafsi. Kinachofanya wananchi wengi waegemee wagombea wa vyama kuliko wagombea huru ni kwa sababu nchi imegawanyika karibia nusu kwa nusu kiitikadi. Hata hivyo, bado kuna majimbo ambayo wabuge wake wanapita kama wagombea huru. Lakini sisi CCM tunafanya maamuzi juu ya suala muhimu kama hili ina top-down fashion, na mbaya zaidi ni katika mazingira yanayotawaliwa na ombwe la kiitikadi (including CCM). Hivi sio kuwatendea haki watanzania.
- Nne ni kuhusu sifa Rais lazima awe na sifa za kuwa mbunge: Je ni sifa zipi hizi? Kwa mfano katiba ya Tanzania inasema ili mtu kuwa mbunge ni lazima awe:
· na miaka ishirini na moja, na ambaye anajua kusoma na kuandika katika Kiswahili au Kiingereza;
· ni mwanachama na ni mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;
· katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi hakuwahi kutiwa hatiani katika mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.
Tayari tumeshaona migongano mingi hapo, na kuna sifa nyingine ambayo sijaiweka hapo ambayo, wakati sifa kielimu (mbunge) ni angala darasa la saba, sifa kielimu (rais) ni angalau shahada ya kwanza.
Wengi wetu katika mjadala huu inaonekana hatupo tayari kumfikiria mtanzania ambae hayupo kwenye kundi la sasa la wabunge (CCM); tunaamini kwamba nje ya wabunge waliopo sasa, hakuna mtanzania mwingine mwenye uwezo wa kuwa Rais na Amiri Jeshi mkuu. Na wenye mtazamo huu hawajali kama ubunge wa mgombea ambaye ni chaguo lao, ubunge wa aliupata vipi - kama ulipatikana kihalali au kwa hila, vitisho, rushwa na ujanja ujanja wa kila aina. Kwa wenzetu hawa, hilo kwa sio muhimu!!
- Na tano ni juu ya ‘kutiwa hatiani' kuhusu masuala ya kodi. Kwa kweli hapa tunachezeana tu akili kwani tumezidi kushuhudia jinsi gani wanasiasa wengi wanajificha nyuma ya pazia la ‘innocent until proven guilty', huku vyombo vyote vya kufanya kazi ya kutia watu hatiani vipo mifukoni mwao. Hivi kweli are we serious na kuachia maadili ya uongozi yapimwe na masuala ya kodi tu? Fine, tuseme suala la kodi ni muhimu, je nani asiyejua kwamba Azimio la Arusha lilivunjwa ili kuhalalisha wanasiasa kuwa na mshahara zaidi ya mmoja, nyumba za kupanga, na hisa katika publicly traded companies, na nyingi ya kampuni hizi zikiwa mstari wa mbele kuhujumu uchumi wetu?? Na je hivi kuna any transparency katika masuala ya ‘tax returns' miongoni mwa wanasiasa wetu wafanyabiashara? Lakini swali muhimu zaidi hapa ni je, hatia kwa kiongozi nje ya kodi hakuna kweli? What about kujihusisha rushwa na matumizi mabaya ya madaraka? What about kubaka au kutafuta hongo za ngono? What about kuwa raia wa nchi zaidi ya moja kinyume cha sheria? The list goes on and on…
Wana CCM wenzangu, tusiogope kushindwa hoja kuhusu CCM kufilisika kihoja mbele ya umma, kwani badala ya kutibu tatizo, tunaficha ugonjwa ambao utakuja kutuadhiri. Tukubali kwamba nchi yetu imeshakomaa kuruhusu demokrasia ya kupokezana vijiti. Wana CCM wenzangu, kushindwa 2015 (kama itatokea) sio mwisho wa dunia, and as a matter of fact, tutakuwa kwenye nafasi bora zaidi ya kujipanga upya tukiwa nje kuliko tukiwa madarakani kwa sababu moja kubwa: Tukipoteza madaraka ya nchi, hapo ndio tutajua kina nani walikuwa wapo CCM kimaslahi na kina nani walikuwa wapo CCM kwa dhati kwani ni dhahiri kwamba wengi watakimbilia upinzani, na hii itawapatia nafasi wale wachache watakaobaki CCM kwani watakuwa na nia ya kweli ya kukirejesha Chama kwenye mstari.
Wana CCM wenzangu, CCM ni chama pekee katika dunia ya tatu kilichokaa madarakani kwa zaidi ya nusu karne, hasa katika mazingira ya liberal democracy. Sasa kama vipo vyama vinavyopoteza madaraka ya nchi kwa kutawala miaka mitano au kumi, sisi ni nani kuwa immune kiasi hicho? Unless madaraka kwetu ni kwa ajili ya kujipatia immunity na ufisadi ili tusifikishwe mbele ya sheria pale chama kingine kitakapochukua madaraka; au unless lengo letu ni kutumikia matumbo yetu na sio wananchi, vinginevyo watanzania wakiamua kututoa madarakani 2015, tukubali maamuzi ya wengi, lakini isiwe mwisho wa dunia kwetu kwani kwa mfano:
- Ghana, kwa mfano Chama cha NDC kilipoteza madaraka mwaka 1992 kwa chama cha upinzani, lakini kikarudi madarakani mwaka 2008;
- Uingereza, chama cha Labour kilikuwa cha upinzani kwa miaka 17 mpaka pale Tony Blair alipokirudisha madarakani;
- Japan, chama Cha DP kilitawala kwa miaka 50, lakini kikashindwa miaka michache iliyopita, na hivi sasa kinajipanga na kina nafasi kubwa ya kurudi uchaguzi mkuu ujao;
- Zambia, CCM ya Zambia (UNIP) ilitawala kwa miaka 27 na kuja kupoteza uchaguzi kwa Chadema ya Zambia (MMD), ambayo ilitawala kwa miaka 20 kabla ya kupoteza kwa chama kipya (DP) cha Satta ambacho tayari wananchi wengi wanaanza kufikiria tena kuwapa ridhaa yao MMD au UNIP. Hii ni ishara kwamba tatizo linalowakabili waafrika kwa ujumla ni umaskini lakini kuna uhaba wa vyama vyenye itikadi ya kutatua tatizo hili. Ndio maana huwa napingana na mawazo wa baadhi yetu humu kwamba hatuna haja ya vyama vingine vipya kwani CCM na Chadema wametosha.
Last but not least, niseme tu kwamba pamoja na haya yote, binafsi bado nina jina moja ambalo nina imani mtu huyo ana uwezo wa kulitumikia taifa hili vizuri (ngazi ya Urais) hata kama anatokana na wabunge wa sasa (CCM), kwa sababu amekuwa anapingana na the existing state of affairs (some of which nimezijadili) kwa muda mrefu. Lakini haina maana kwamba yeye ni bora kuliko wengine wa upinzani, na muda ukifika nitamtaja ili tumpime kwa hoja (sio kwa ushabiki, mazoea au maslahi).
Vinginevyo naunga mkono hoja ya Mwanakijiji kwa vigezo nilivyovijadili.