Lowassa, Malecela na Sitta kunyimwa nishani maana yake nini?

Tofautisha Waziri Mkuu mstaafu na Waziri Mkuu aliyefukuzwa. Warioba hakustaafu kwa kashfa, na hata baada ya kuondoka madarakani ameendelea kutumiwa vizuri sana Kimataifa. Hebu tueleze huyu fisadi Lowasa anatumiwa na nani baada ya kufukuzwa?
Madisadi na UVCCM arusha pia na Rostam
 
Jana katika kuazimisha miaka 50 pamoja na mambo mengine Rais alitoa nishani kwa watu mbali mbali waliolitumikia taifa. Kwa upande wa maspika wa Bunge wamepewa Pius Msekwa na Anna Makinda.

Swali ninalojiuliza, hivi Sitta hakustahili kupata nishani? Kwa nini amenyimwa yeye aliyekuwa spika kwa miaka mitano akapewa Anna Makinda ambaye ametumikia nafasi hiyo kwa mwaka mmoja tu sasa?

MAKINDA ANA MIEZI KAMA KUMI NA MOJA TU WALA SIO MWAKA........!!!! Hii ni hatari kabisa!!
 
Jana katika kuazimisha miaka 50 pamoja na mambo mengine Rais alitoa nishani kwa watu mbali mbali waliolitumikia taifa. Kwa upande wa maspika wa Bunge wamepewa Pius Msekwa na Anna Makinda.

Swali ninalojiuliza, hivi Sitta hakustahili kupata nishani? Kwa nini amenyimwa yeye aliyekuwa spika kwa miaka mitano akapewa Anna Makinda ambaye ametumikia nafasi hiyo kwa mwaka mmoja tu sasa?

Hata mimi hili limenipa shida inaonyesha kupata nishani inahitaji uwe mfuasi mwongofu wa CCM. Sisi kama wananchi tulikuwa na mtazamo chanya juu ya uongozi wa Sita kwani hadi leo hii bunge lipo hai kutokana na mwanzo mzuri ulioonyeshwa na Sita. Bunge lilipata heshima yake. Lakini Watanzania hatutakiwi kujua ukweli. Hiyo ndiyo CCM nashindwa kuelewa inakuwaje mtu mwenye akili timamu kuisapoti CCM. God bless Tanzania
 
Hata Pinda hakupewa. Huenda utendaji wake haumridhishi Rais.


Ahaaaaaaaahaaaaaaaaa!!! Hapa umenifumbua macho kidogo, kama speaker wa miezi kumi tu anatunukiwa na je vipi kuhusu waziri wetu mkuu ambaye yuko katika utumishi zaidi ya miaka mitatu???? Du! Maswali ni mengi sana hap....................!!!! Ndio maana Kijana Zitto kasema vigezo vilivyotumika havijulikani ni vipi??
 
Kumnyima Sitta nishani na kumpa Makinda nadhani kila mzalendo atalishangaa hili na historia ya ukweli huu itakuja hukumu walitoa nishani hizo. Unaweza mchukia mtu lakini unapo mnyima haki yake Mungu husimama katikati ya wewe na huyo uliye mnyima haki. Na hukumu ya Mungu huwa ni ya haki ili kila mwenye mwili atambue kuwa kila mwandamu aliumbwa na yeye kwa sura na mfano wake.
 
Mimi kwa upande wangu nafikiri Sitta alistahili tuzo maana wakati akiwa spika Bunge lake lilikuwa bunge lenye haki bila upendeleo wa chama tawala pia sijaona umuhimu kwanini Anna Makinda amepewa tuzo wakati ni puppet na ameshindwa kumudu Bunge? Naamini Aboud Jumbe Mwinyi alistahili tuzo la heshima ya juu kama marais wastaafu kwa sababu zifuatazo ni yeye aliyeleta demokrasia zaidi Zanzibar kuruhu baraza la wawakilishi kuwepo, kuwa na Waziri Kiongozi wa kwanza mwenye mamlaka Brigedia Ramadhani Haji pia kukubali maoni ya mwalimu kuunganisha TANU na ASP na kuzaliwa CCM

Karume alikuwa dikteta hakustahili hilo tuzo kwanza alikuwa muujai aliwaua Kassim Hanga na wengine, pia kutaka kumuua Professa Abrahman Babu pia hakuruhusu bunge isipokuwa kulikuwa na kundi la watu wanane likiongozwa na Kanali Seif Bakari ndilo lilikkuwa linatunga sheria za nchi. Na hata kama watu wanasema aliwezesha Tanganyika na Zanzibar kuungana hakuwa na jinsi maana ni Nyerere alliyemuweka madarakani baada ya kufanya juu chini na kumpokonya madaraka John Okello aliyefanya mapinduzi

Lakini Jumbe aliruhusu wabunge wawakilishi kuwepo, akaruhusu ASP kuungana na TANU na kuzaliwa CCM wakati Karume alikataa aliogopa nguvu zake kumalizwa na Nyerere. hata kama wanasema machafuko ya kisiasa ya mwaka 1984 Jumbe alikuwa upande wa wengi wenye kutaka serikali tatu kwani ni dhambi kusema vile? hata kama CCM wanaona ni dhambi aliyoyafanya ni mengi kuliko hilo leo ASP na TANU zisingeungana na kuzaliwa CCM sijui kama Tanzania ingekuwepo maana sasa hivi wabara huwacontrol wazanzibar kupitia vikao vya CCM kwahiyo ni Jumbe ndio kafanya Muungano uzidi kuwepo na anastahili tuzo la juu na yeye ni bora kuliko Karume
 
MAKINDA ANA MIEZI KAMA KUMI NA MOJA TU WALA SIO MWAKA........!!!! Hii ni hatari kabisa!!

Hata baada ya kutumia udikteta kupitisha mswada wa katiba bado anatunukiwa nishani; well may be she scored high kwasababu hiyo maana kila kitu kibaya kwa wananchi the opposite is true kwa utawala wa CCM nyakati hizi.
 
[QUOTEna bado hakuna mtu aliyekuwa tayari kutoa sababu za kutopewa nishani[/QUOTE]

Lowassa ni aidha Mwizi au Mzembe kwa kusaini mkataba na kampuni hewa.Hata hivyo hakustaafu,amejiuzulu.Hafai kabisaaaaaaa.
 
Kumnyima Sitta nishani na kumpa Makinda nadhani kila mzalendo atalishangaa hili na historia ya ukweli huu itakuja hukumu walitoa nishani hizo. Unaweza mchukia mtu lakini unapo mnyima haki yake Mungu husimama katikati ya wewe na huyo uliye mnyima haki. Na hukumu ya Mungu huwa ni ya haki ili kila mwenye mwili atambue kuwa kila mwandamu aliumbwa na yeye kwa sura na mfano wake.
Ame kumbe nawe umeona yakhe jamaa ana chuki za wazi wazi hazifichiki kama pembe la ng'ombe
 
[QUOTEna bado hakuna mtu aliyekuwa tayari kutoa sababu za kutopewa nishani

Lowassa ni aidha Mwizi au Mzembe kwa kusaini mkataba na kampuni hewa.Hata hivyo hakustaafu,amejiuzulu.Hafai kabisaaaaaaa.[/QUOTE]

Ahaaaaaaaaa! VIPI KWA MTOA NISHANI..................................????
 
Jk mwenyewe amepata hiyo tuzo kwanini Lowassa apate na wote wamekutana zamani
 
sitta haitaji nishani ya kikwete, aliitesa serikali yake fisadi na anendelea. Mzee Sitta nishani unayo tayari.
 
Kama sifa ni kwa walioitumikia Tanganyika/Tanzania kwa uadilifu Gavana wa Kwanza BOT Mtanganyika alistahili kupata nishani hiyo.
 
sherehe ni za uhuru wa tanganyika, hizo nishani wazanzibar wameingiaje?

Umesema kitu ambacho wengi wanahoji huku mtaani. Hivi Dr. Mohamed Shein alichangia nini kwenye harakati za uhuru wa Tanganyika? Na kama kama kweli alitoa mchango, ni mkubwa kuliko Chief Adam Sapi Mkwawa? Au Chief Fundikira? Tusubiri miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar kama watakuwa na list wa wabara!

Kusema la ukweli hii list ya watunikiwa ina walakini mkubwa.
 
Baada ya sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara kumalizika ktk uwanja wa Taifa (Uwanja wa Uhuru), kulifanyika sherehe nyingine ktk viwanja vya Ikulu Dar es salaam, sherehe hiii ilikuwa ni ya kuwatunuku NISHANI viongozi mbali mbali wastaafu waliolitumikia Taifa hili.

Nishani hii yenye HESHIMA kubwa iliyopewa jina la Mwl. J. K. Nyerere ilitolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Mh. Jakaya Mrisho Kikwete. Aliwatunuku Marais wote wastaafu, Makamo wa Rais wote wastaafu, Mawaziri Wakuu wote wastaafu, na viongozi mbali mbali. Idadi ya Nishani zilizotolewa ilikuwa ni 40.

Sherehe hizi zilizoanza majira ya saa kumi jioni zilifana sana ktk viwanja hivyo vya Ikulu, nyuso za waliotunukiwa zilionekana kujaa furaha kubwa sana, na ni dhahiri zilionesha ni kiasi gani pengo la Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere lilivyo.

JAMBO lililoushtua umati mkubwa ulioalikwa kuhudhuria na kupamba sherehe hii ilikuwa ni pale jina la Mh. Edward Ngoyai Lowasa kutokuwepo ktk orodha ya viongozi hao. Watu waliokuwa wamejikusanya ktk makundi mbali mbali walisikika wakisema kuwa "huu ndio mwisho wa Lowasa ktk medani za siasa". Wengine walisikika wakisema kuwa "Lowasa hakupaswa kukimbilia ktk kipindi maalum kilichorushwa na TBC1", kwani kufanya hivyo ni kuonesha Umma wa Watanzania kuwa anashindana na viongozi wake Wakuu, yaani Waziri Mkuu na Rais.

Baada ya mahojiano na TBC1, wananchi wengi kutoka ktk viunga vyote nchini walilipuka kwa mshangao dhidi ya kituo hiki cha habari kinachomilikiwa na Serikali kutojua au kwa makusudi kuvunja itifaki. Wengi wamekosa imani na chombo hiki, na kuona kama ni cha Mh. Edward Lowasa.

Ninaamini kuwa tutapata mawazo mengi mazuri juu ya matukio hayo mawili yaliyotokea jana, na hasa ukizingatia kuwa, mara kadhaa Mh. Lowasa amekuwa akitamba hadharani kuwa Rais Kikwete ni rafiki yake aliyetoka nae mbali, na wawili hao hawakukutana mitaani. Lakini jambo jingine hapa ni kuwa, CCM inajiandaa na uchaguzi wa viongozi wake ktk nafasi mbali mbali mwaka kesho. Uchaguzi huu utaunda timu ya ushindi wa chama hicho kikongwe utakaofanyika mwaka 2015. Kuna tetesi kuwa Mh. Lowasa anautamani saana URAIS, na hivyo ANAJIANDAA KUGOMBEA.

Viongozi wastaafu ambao bado wanaendelea na nyadhifa nyingine serikalini nao hawakupewa nishani maana si wastaafu, na Lowassa si mstaafu ni "mjiuzulu".



Kutoka gazeti la Mwananchi Disemba 11, 2011:

Ni kweli EL sio mstaafu, kwa sababu kujiuzulu na kustaafu ni vitu tofauti.

Lakini mimi naamini kuwa hizo sio sababu za kutopewa tuzo kwa vile kila siku tunaimbiwa wimbo kuwa huyu bwana ni mstaafu.

Nafikiri huu ni mkakati wa makusudi kati ya marafiki hawa wawili ambao ni ''to keep low profile'', kutotibua mambo kabla ya wakati.

Pamoja na kuwa timu ya EL imekuja na malalamiko kwa nini hakupewa tuzo. Kishindo kingekuwa kikubwa zaidi iwapo angepewa tuzo hiyo kitu ambacho hao waheshimiwa wasingependa kitokee wakati huu. Ingetokea ingeharibu mafanikio ambayo EL amepata mpaka sasa ya kukamata ''media''.

Mpaka sasa mtu anayeonekana tishio kwa EL ndani ya magamba ni Sam 6. Kwa hiyo kumpa tuzo kungeongeza umaarufu zaidi kwa timu pinzani.

Inaelekea walipanga vizuri mkakati wao ila kutoa tuzo kwa Ana Makida ndio kitu pekee kilichowaumbua na kufunua hila dhidi ya sam 6.

Kwa hili walitekwa na dhamira ya kumpandisha hadhi Ana Makida mbele ya jamii hasa kutokana na malalamiko mengi juu yake kuhusiana na jinsi anavyoendesha chombo cha kutunga sheria na kusahau kuwa watu tayari wanayo rekodi ya sam 6 amabyo watatumia kupima hao maspika wawili....
 
... Hao viongozi wawili hawana afya ya kutosha kuzozana kwa muda mrfeu ... hakuna shaka afya zao ndizo zitakzo amua mwisho wa sakata hili muda sio mrefu ... stay tuned!!!!

hujaelweka mkuu, afya zao kimwili au kisiasa?? fafanua kaka!!
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom