Kuna taarifa kwamba Lowassa amejiingiza kwa nguvu ndani ya UVCCM kwa kuwatumia Katibu Mkuu, Martin Shigella na Mwenyekiti wa zamani, Masauni, na kwa kutumia kikao maalumu kitakachofanyika Jumamosi mjini Dodoma wanataka kumng'oa Benno Malisa katika nafasi yake na kuvunja Baraza la Utekelezaji ambalo ndani yake yumo Ridhiwani Kikwete, akimuona kama mtu hatari kwake na anahofia ndiye nguvu nyuma ya kauli ya vijana waliotoa tamko na ambao wanajipanga sasa kushinikiza mabadiliko makubwa wakitaka mafisadi (akiwamo Lowassa) kuondolewa ndani ya CCM. Hatua hiyo imekuja baada ya kutajwa na UVCCM na sasa anatafuta mchawi maana anasema baada ya kina Mwakyembe kumtaja katika kamati teule, hajawahi kutajwa tena ndani ya vikao rasmi vya CCM na popote na ndio maana akapita na kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama bila kupingwa. hata Bungeni hakuna mwenye ubavu wa kumtaja, na ndio ameshangaa na kushitishwa sana na UVCCM tena Pwani kumtaja hadharani tena kwa jina. Ameshangaa wamepata wapi hizo nguvu.
Kulikua na mkakati na kuwaondoa mafisadi ndani ya CCM kabla ya uchaguzi wa CCM wa mwaka 2012, lakini Lowassa na wenzake wameshituka baada ya Kikwete kugusia hilo katika hotuba yake ya Februari 5, ambapo alisema CCM lazima ijivue gamba na hivyo, kundi la mafisadi wakaanza mikakati kutumia vyombo vya habari na wansiasa kushinikiza kuzuiwa kwa hatua hiyo na kama itabidi eti isubiri hadi 2012. Mpango wa kutaka wasubiri 2012, unalenga kuwa watakuwa wamejiandaa na wanaanza sasa kupanga safu ndani ya uongozi wa CCM (kama walivyopanga ndani ya bunge kuanzia madiwani na uongozi wa serikali za mitaa), mpango ambao umetengewa mabilioni ya fedha na hivyo utakapofika Mkutano mkuu wa CCM 2012, Lowassa na wenzake watakuwa na nguvu kubwa ndani ya CCM, ndani ya Bunge na ndani ya serikali (ndio maana hadi sasa ma-DC na ma_RC hawajateuliwa) na hivyo Kikwete hatakuwa na nguvu tena na yeyote atakayetoa kichwa ataminywa kuelekea 2015.
Mkakati huo unaanza Jumamosi kwa kuvuruga UVCCM (wanaoonekana viherehere sasa) na baadaye Wazazi na UWT haraka iwezekanavyo.
Kulikua na mkakati na kuwaondoa mafisadi ndani ya CCM kabla ya uchaguzi wa CCM wa mwaka 2012, lakini Lowassa na wenzake wameshituka baada ya Kikwete kugusia hilo katika hotuba yake ya Februari 5, ambapo alisema CCM lazima ijivue gamba na hivyo, kundi la mafisadi wakaanza mikakati kutumia vyombo vya habari na wansiasa kushinikiza kuzuiwa kwa hatua hiyo na kama itabidi eti isubiri hadi 2012. Mpango wa kutaka wasubiri 2012, unalenga kuwa watakuwa wamejiandaa na wanaanza sasa kupanga safu ndani ya uongozi wa CCM (kama walivyopanga ndani ya bunge kuanzia madiwani na uongozi wa serikali za mitaa), mpango ambao umetengewa mabilioni ya fedha na hivyo utakapofika Mkutano mkuu wa CCM 2012, Lowassa na wenzake watakuwa na nguvu kubwa ndani ya CCM, ndani ya Bunge na ndani ya serikali (ndio maana hadi sasa ma-DC na ma_RC hawajateuliwa) na hivyo Kikwete hatakuwa na nguvu tena na yeyote atakayetoa kichwa ataminywa kuelekea 2015.
Mkakati huo unaanza Jumamosi kwa kuvuruga UVCCM (wanaoonekana viherehere sasa) na baadaye Wazazi na UWT haraka iwezekanavyo.