LOWASSA kuiambia CCM "Mwenye Nguvu Mpishe"

Kashaijabutege

JF-Expert Member
Oct 20, 2010
2,696
740
Edward Ngoyai Lowassa (fisadi pacha) amerudi kwa kishindo kutoka ughaibuni alikoenda kwa ajili ya matibabu ya macho. Amewajulisha adui zake wa kisiasa, nafikiri ndani ya CCM, kuwa yuko tayari kwa "mapambano". Alikunja ngumi kama ishara ya kuonesha kuwa yuko "fit and fine" (buheri wa afya); na akatamba kuwa atayathibitisha hayo huko Arumeru Mashariki.

Nape na wenzake wamekuwa wakipiga kelele kwa kumtaja Lowassa kuwa ni kati ya "wanachama wachafu" wanaopaswa kuacha nafasi za uongozi ndani ya CCM, kama njia mojawapo ya kukisafisha chama; au kama wenyewe wanavyosema, "kujivua gamba". Rostam Aziz, aliyekuwa Mbunge wa Igunga, yeye katangulia kujivua nafasi zake zote za uongozi katika chama ili "aachane na siasa uchwara". Pacha mwingine Andrew Chenge, maarufu kama Mzee wa Vijisenti, yuko kimya anasubiri yeyote amguse ili alianzishe; yaani wamwage ugali, naye amwage mboga. Lowassa yeye amewazidi wote kwa ujasiri. Ana roho ya paka. Ameonesha wazi kuwa anataka kuwa "Rais ajaye". CCM kimeonesha kumgwaya. CCM kiko kimya.

Lowassa aliporudi jana, ametamka wazi wazi kuwa anayemzushia kuwa afya yake ina mushkeli basi akaone kuwa yuko "fit and fine" huko Arumeru Mashariki. Ninahisi alimaanisha kwenda kumpigia debe mkwewe, ambaye amempigania kwa "remote ya rushwa" mpaka akapata nafasi ya kugombea kwa tiketi ya CCM.

Ni wazi kuwa CCM, hii ya sasa, haitakuwa na uwezo wa kumzuia mtu iliyemtangaza mchafu kupanda jukwaani kumnadi mgombea wao. Nape na "walokole" wenzie watafyata mkia. Nina imani kuwa Jumamosi hii, watatuma ujumbe mzito wa kwenda kumpa pole "mzee" na safari na kumtaka hali, na ZAIDI, kumuomba asaidie kutoa chochote ili wakabiliane na "chama ambacho William Sarakikya hakipendi". Watamsifu; watamwambia uko "fit and fine"; mzee unaonekana "una afya kuliko wakati mwingine wowote". Watampamba; naye atawapa chochote. Mwisho kabla ya kuaga watamwomba wiki ijayo akawasidie jukwaani. Watamwambia "mzee tumechunguza na kuona unakubalika". Atacheka kidogo, na atawajibu "sawa".

Lowassa wiki ijayo atapanda jukwaani. Atamnadi mkwewe. Nape na wenzie watakula matapishi. Watakaa kimya. Ila moyoni watajisemea "MWENYE NGUVU MPISHE".

Mie nikimwona Lowassa jukwaani wiki ijayo nitakumbuka maneno ya kwenye kitabu cha KULI; "YANA MWISHO".
 
Lowassa si fisadi kama unavyotaka kutuaminisha. 2015 utajuta.
Ndugu unajitahidi kumfagilia Lowassa lakini atakuwa kiongozi tu wa CCM na sio Rais wa Tanzania. Na kama huamini utaona kama Ocampo hatatia team hapa bongo. Tusubiri tuone.
 
Ndugu unajitahidi kumfagilia Lowassa lakini atakuwa kiongozi tu wa CCM na sio Rais wa Tanzania. Na kama huamini utaona kama Ocampo hatatia team hapa bongo. Tusubiri tuone.
2015 Lowassa atakuwa His Excellency, The President Of United Republic Of Tanzania. Ukweli mchungu eeh, utaumeza tu.
 
"Niko fit and fine kuliko wakati mwingine wowote ule na niko tayari kwa mapambano"-ENL
 
Upuuzi tu hakuna kitu!!

Stroke imemkomesha huyu masai!!
Akubali tu kuwa ni mgonjwa lakini anaendelea vizuri!!
 
mtu alie fiti anatembe kama amekakamaa huyo atakuja kufia jukwaani
 
Aliyekuwa wa kwanza kumchafua mh. Lowasa ndiye atakayemchana nyewele na kumpa mh. Lowasa kioo ajiangalie kama kweli amependeza na atamfungulia mlango na Lowasa atatoka kwenda kugombea urais kwa tiketi ya CCM.
 
Edward Ngoyai Lowassa (fisadi pacha) amerudi kwa kishindo kutoka ughaibuni alikoenda kwa ajili ya matibabu ya macho. Amewajulisha adui zake wa kisiasa, nafikiri ndani ya CCM, kuwa yuko tayari kwa "mapambano". Alikunja ngumi kama ishara ya kuonesha kuwa yuko "fit and fine" (buheri wa afya); na akatamba kuwa atayathibitisha hayo huko Arumeru Mashariki.

Nape na wenzake wamekuwa wakipiga kelele kwa kumtaja Lowassa kuwa ni kati ya "wanachama wachafu" wanaopaswa kuacha nafasi za uongozi ndani ya CCM, kama njia mojawapo ya kukisafisha chama; au kama wenyewe wanavyosema, "kujivua gamba". Rostam Aziz, aliyekuwa Mbunge wa Igunga, yeye katangulia kujivua nafasi zake zote za uongozi katika chama ili "aachane na siasa uchwara". Pacha mwingine Andrew Chenge, maarufu kama Mzee wa Vijisenti, yuko kimya anasubiri yeyote amguse ili alianzishe; yaani wamwage ugali, naye amwage mboga. Lowassa yeye amewazidi wote kwa ujasiri. Ana roho ya paka. Ameonesha wazi kuwa anataka kuwa "Rais ajaye". CCM kimeonesha kumgwaya. CCM kiko kimya.

Lowassa aliporudi jana, ametamka wazi wazi kuwa anayemzushia kuwa afya yake ina mushkeli basi akaone kuwa yuko "fit and fine" huko Arumeru Mashariki. Ninahisi alimaanisha kwenda kumpigia debe mkwewe, ambaye amempigania kwa "remote ya rushwa" mpaka akapata nafasi ya kugombea kwa tiketi ya CCM.

Ni wazi kuwa CCM, hii ya sasa, haitakuwa na uwezo wa kumzuia mtu iliyemtangaza mchafu kupanda jukwaani kumnadi mgombea wao. Nape na "walokole" wenzie watafyata mkia. Nina imani kuwa Jumamosi hii, watatuma ujumbe mzito wa kwenda kumpa pole "mzee" na safari na kumtaka hali, na ZAIDI, kumuomba asaidie kutoa chochote ili wakabiliane na "chama ambacho William Sarakikya hakipendi". Watamsifu; watamwambia uko "fit and fine"; mzee unaonekana "una afya kuliko wakati mwingine wowote". Watampamba; naye atawapa chochote. Mwisho kabla ya kuaga watamwomba wiki ijayo akawasidie jukwaani. Watamwambia "mzee tumechunguza na kuona unakubalika". Atacheka kidogo, na atawajibu "sawa".

Lowassa wiki ijayo atapanda jukwaani. Atamnadi mkwewe. Nape na wenzie watakula matapishi. Watakaa kimya. Ila moyoni watajisemea "MWENYE NGUVU MPISHE".

Mie nikimwona Lowassa jukwaani wiki ijayo nitakumbuka maneno ya kwenye kitabu cha KULI; "YANA MWISHO".


hawezi kua Rais wala mgombea wa CCM 2015 hata kama asipokufa now and then
 
14 " ‘Ninapomwambia mwovu: "Hakika utakufa," naye kwa kweli ageuke na kuiacha dhambi yake na kuendelea kutenda haki na uadilifu, 15 naye mwovu arudishe kitu kile kilichowekwa rehani, alipe vitu vile vilivyochukuliwa kwa unyang'anyi, naye kwa kweli atembee katika sheria za uzima kwa kutotenda ukosefu wa haki, hakika ataendelea kuishi. Yeye hatakufa. 16 Hakuna yoyote kati ya dhambi zake alizozitenda itakayokumbukwa juu yake. Yeye ameendelea kutenda haki na uadilifu. Hakika ataendelea kuishi.' Ezekieli 33.14
 
Edward Ngoyai Lowassa (fisadi pacha) amerudi kwa kishindo kutoka ughaibuni alikoenda kwa ajili ya matibabu ya macho. Amewajulisha adui zake wa kisiasa, nafikiri ndani ya CCM, kuwa yuko tayari kwa "mapambano". Alikunja ngumi kama ishara ya kuonesha kuwa yuko "fit and fine" (buheri wa afya); na akatamba kuwa atayathibitisha hayo huko Arumeru Mashariki.

Nape na wenzake wamekuwa wakipiga kelele kwa kumtaja Lowassa kuwa ni kati ya "wanachama wachafu" wanaopaswa kuacha nafasi za uongozi ndani ya CCM, kama njia mojawapo ya kukisafisha chama; au kama wenyewe wanavyosema, "kujivua gamba". Rostam Aziz, aliyekuwa Mbunge wa Igunga, yeye katangulia kujivua nafasi zake zote za uongozi katika chama ili "aachane na siasa uchwara". Pacha mwingine Andrew Chenge, maarufu kama Mzee wa Vijisenti, yuko kimya anasubiri yeyote amguse ili alianzishe; yaani wamwage ugali, naye amwage mboga. Lowassa yeye amewazidi wote kwa ujasiri. Ana roho ya paka. Ameonesha wazi kuwa anataka kuwa "Rais ajaye". CCM kimeonesha kumgwaya. CCM kiko kimya.

Lowassa aliporudi jana, ametamka wazi wazi kuwa anayemzushia kuwa afya yake ina mushkeli basi akaone kuwa yuko "fit and fine" huko Arumeru Mashariki. Ninahisi alimaanisha kwenda kumpigia debe mkwewe, ambaye amempigania kwa "remote ya rushwa" mpaka akapata nafasi ya kugombea kwa tiketi ya CCM.

Ni wazi kuwa CCM, hii ya sasa, haitakuwa na uwezo wa kumzuia mtu iliyemtangaza mchafu kupanda jukwaani kumnadi mgombea wao. Nape na "walokole" wenzie watafyata mkia. Nina imani kuwa Jumamosi hii, watatuma ujumbe mzito wa kwenda kumpa pole "mzee" na safari na kumtaka hali, na ZAIDI, kumuomba asaidie kutoa chochote ili wakabiliane na "chama ambacho William Sarakikya hakipendi". Watamsifu; watamwambia uko "fit and fine"; mzee unaonekana "una afya kuliko wakati mwingine wowote". Watampamba; naye atawapa chochote. Mwisho kabla ya kuaga watamwomba wiki ijayo akawasidie jukwaani. Watamwambia "mzee tumechunguza na kuona unakubalika". Atacheka kidogo, na atawajibu "sawa".

Lowassa wiki ijayo atapanda jukwaani. Atamnadi mkwewe. Nape na wenzie watakula matapishi. Watakaa kimya. Ila moyoni watajisemea "MWENYE NGUVU MPISHE".

Mie nikimwona Lowassa jukwaani wiki ijayo nitakumbuka maneno ya kwenye kitabu cha KULI; "YANA MWISHO".


Duuh umenikumbusha mbali sana! Ila ni kweli kila kitu kina mwisho tupende tusipende
 
Ocampo atakuja kumkamata Ali Hassan Mwinyi kwa mauaji ya kimbari ya mwaka 1987 katika eneo la Mkomazi game reserve, kwa eti sababu ya kuunda mbuga aliamura majeshi yaue, yachome miji, ubakaji na vitendo vingine vingi vya uvunjaji mbaya wa haki za binadamu... naona na mwanae anatumaliza kwa mabomu Dar na hata ndoto ya kujiuzulu hamna.
Ndugu unajitahidi kumfagilia Lowassa lakini atakuwa kiongozi tu wa CCM na sio Rais wa Tanzania. Na kama huamini utaona kama Ocampo hatatia team hapa bongo. Tusubiri tuone.
 
Dah nilimuona akitembea kwa tahadhari kama vile anashuka ngazi au tumbo limechafuka...
 
dah nilimuona akitembea kwa tahadhari kama vile anashuka ngazi au tumbo limechafuka...


sisiemu wote ni wawa kuny .nga tu hakuna aliye msafi hata mmoja. Waliibia taifa mpaka limebaki mifupa nashangaa tuvyoendelea kuwa chekea was..zi hawa wasio na chembe hata moja ya huruma kwa walalahoi
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom