Lowassa kuchunguza Ufisadi Meremeta!

Pengine bunge limeona heri kuwapa kamati ya usalama inayosimamiwa na edward lowasaa kusimamia
ufsadi wa meremeta ili kuficha uovu wao lakini magazeti ya leo yamekuja an mawasali tofauti
je lowaasa mtuhumiwa wa ufisadi wa richmond aliekuwa akipokea million 150 kwa siku kwa malipo feki ya umeme
je ataweza kusaidia kuendeleza wimbi la hamu ya wananchi kutaka akujua nani wahusika wakuu wa meremeta

je ungekuwa lowassa ungebeba mzigo huu??nini mtarajio yako ya kamati hii teule kuchunguza meremeta chini ya e lowassa
ambae hivi karibuni wamefungua bank, community bank arusha kwa ajili ya kupitisha hela zao za kitapeli

kwako mwana jf
 
Binafsi nahisi lowassa anaweza tumia exp yao kuchota hela za richmond kugundua meremeta walikuwa wanakulaje
swali lililopo ni je mbinu hizo chafu zitawekwa hadharani na je kamati hii imepewa muda gani au mpaka 2016??
 
" Rais mstaaf wa Marekani, George Bush, ameteuliwa kuongoza tume ya umoja wa mataifa kushughulikia ukiukwaji wa haki za binadamu uliofanywa na majeshi ya allies huko Iraq. Pamoja na hilo, tume hiyo itachunguza pia uwezekano wa uwepo wa sumu kwenye mabomu yaliyotumika Libya dhidi ya Ghaddafi " !!!

Chanzo: CCN!
 
Hyo ndo nafas ya el kujstakasa.afanye umwakyembe watz 2tasahau na 2tavaa matshet yenye picha yake then atakuwa prezd we2!
 
Lowassa hawezi kuja na kitu chochcote chenye manufaa kwa Taifa hili kuhusu Meremeta kwasababu wahusika wakuu waliokuwa JWTZ wakati huo ni watu waliokuwa karibu nae sana and he depends on them for his political survivor!!
 
BAADA ya Bunge kuikabidhi Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama inayoongozwa na Mbunge wa Monduli (CCM), Edward Lowassa, jukumu la kuchunguza ufisadi wa zaidi ya Sh205.9 bilioni unaodaiwa kufanywa kupitia Kampuni ya Meremeta, wasomi na wanasiasa nchini wamepinga uamuzi huo wakidai kuwa ukweli utapindishwa.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Sengondo Mvungi alisema, “Inakuwaje mtu anatuhumiwa kwa mambo mbalimbali halafu kamati yake inapewa jukumu la kuchunguza suala hilo zito?”
Mvungi ambaye kitaaluma ni mwanasheria alisema kuwa, ni vyema kiongozi akiwa na tuhuma za kifisadi achunguzwe kwanza kabla ya kupewa majukumu.“Hapa ndio utaona jinsi Serikali ya Tanzania inavyougua ugonjwa wa saratani ni lazima ife…, jambo hili katika taaluma ya sheria na katiba tunaliita kuwa ni ‘ishara ya dola inayokufa’,” alisema Mvungi.Aliongeza: “Siku hizi si ajabu kuona jaji anahongwa na Takukuru… Ni wazi kuwa Serikali inayumba”.


Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema, “Jambo linaloibuliwa na kundi jingine na kuhitaji ufumbuzi si vyema likasimamiwa na kundi linalolalamikiwa”.Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni alisema kwa kiasi kikubwa sakata la Meremeta liliibuliwa na wabunge wa upinzani, lakini anashangaa kuona suala hilo linapi pelekwa katika kundi ambalo linaweza kuwa lilihusika.
“Simhukumu Lowassa kuwa ni fisadi…, lakini wakati Serikali inaingia mkataba na kampuni hii yeye alikuwa katika Baraza la Mawaziri, sasa suala hili kurejeshwa tena kwake ni sawa?” alihoji Mbowe.Mbowe alisema kuwa huu ni wakati wa Bunge kutambua kuwa si lazima kila Kamati iongozwe na wabunge wa CCM na kusisitiza kuwa ni vyema ikaundwa Kamati itakayoongozwa na upinzani ili kuchunguza Meremeta.


Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia, alisema si lazima ufisadi wa Meremeta ukachunguzwa na Kamati ya Bunge.
“Takukuru si wapo wanaweza kufanya kazi hii…, hili ni jambo nyeti ambalo linatakiwa kuchunguzwa na watu wenye taaluma kama Takukuru, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mkuu wa Jeshi la Polisi,” alisema Mbatia.
Mbatia alidai kuwa ndani ya CCM hakuna wa kumfunga mwenzake kengele. Alidai kuwa chama hicho kimekithiri kwa ufisadi na kwamba walio salama ni wachache.


Mhadhiri wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Dk Benson Bana, alisema ingawa uamuzi huo wa Bunge utazua maswali mengi kwa wananchi, sheria za Tanzania zinaeleza wazi kuwa mtuhumiwa sio mkosaji.
“Mbona Lowassa anakwenda kanisani na kuchangisha mamilioni ya fedha watu hawasemi lolote?” Alihoji Bana na kuongeza:
“Watanzania wasimhukumu mtu kwa hisia, sidhani kama hata hiyo kamati yake ina watu wasafi…, Lowassa kisheria na kisiasa yuko safi ila kihisia si safi, tunatakiwa kufanyia kazi hali halisi si hisia,”.
Hata hivyo, alisema pamoja na Bunge kupeleka suala hilo kwa kamati inayoongozwa na Lowassa, Serikali pia inaweza kuunda tume yake ya kuchunguza ufisadi huo


Mhadhiri mwingine wa chuo hicho, Bashiru Ally alisema kuwa unyeti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama unaweza kufanya majibu ya uchunguzi huo yakawa wazi au kuwa siri.
 
Mbona hawakupinga hasiwe mwenyekiti wa hiyo kamati! Maana kazi imepewa kamati siyo Lowasa.
 
Wewe unashusha hadhi ya JF, yaani gazeti la mwananchi la Jumapili iliyopita ndio unakuja kuibandika hapa leo? au uliingia kichwa kichwa kwenye website ya Mwananchi ukadhani hii ni habari mpya.
 
Hawa ndio Ma-Profesa ambao wahifika vijijini hupigwa fagio la uso na bibi zao na kuongezewa tusi juu la 'muone mjinga mkubwa huyu' kwa sababu tu ya kung'angania elimu nadharia hata pale ambapo kiongozi fulani vitendo vyake vimeleta madhara makubwa sana hasa kwa walazwahoi katika taifa.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Dk Benson Bana, alisema ingawa uamuzi huo wa Bunge utazua maswali mengi kwa wananchi, sheria za Tanzania zinaeleza wazi kuwa mtuhumiwa sio mkosaji.
"Mbona Lowassa anakwenda kanisani na kuchangisha mamilioni ya fedha watu hawasemi lolote?" Alihoji Bana na kuongeza:
"Watanzania wasimhukumu mtu kwa hisia, sidhani kama hata hiyo kamati yake ina watu wasafi…, Lowassa kisheria na kisiasa yuko safi ila kihisia si safi, tunatakiwa kufanyia kazi hali halisi si hisia,".
Hata hivyo, alisema pamoja na Bunge kupeleka suala hilo kwa kamati inayoongozwa na Lowassa, Serikali pia inaweza kuunda tume yake ya kuchunguza ufisadi huo

Mhadhiri mwingine wa chuo hicho, Bashiru Ally alisema kuwa unyeti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama unaweza kufanya majibu ya uchunguzi huo yakawa wazi au kuwa siri.
 
BAADA ya Bunge kuikabidhi Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama inayoongozwa na Mbunge wa Monduli (CCM), Edward Lowassa, jukumu la kuchunguza ufisadi wa zaidi ya Sh205.9 bilioni unaodaiwa kufanywa kupitia Kampuni ya Meremeta, wasomi na wanasiasa nchini wamepinga uamuzi huo wakidai kuwa ukweli utapindishwa.Spika wa Bunge, Anne Makinda aliamua kuwa Kamati hiyo ya Bunge ifanye uchunguzi huo kwa kuwa ndiyo inayohusika na suala hilo la Meremeta.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Mwananchi Jumapili jana, wasomi na wanasiasa hao walidai kwamba, tatizo sio suala hilo kupelekwa katika kamati hiyo, bali ni mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye walisema hawaamini kama atafanya kazi hiyo vizuri.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Sengondo Mvungi alisema, “Inakuwaje mtu anatuhumiwa kwa mambo mbalimbali halafu kamati yake inapewa jukumu la kuchunguza suala hilo zito?”
Mvungi ambaye kitaaluma ni mwanasheria alisema kuwa, ni vyema kiongozi akiwa na tuhuma za kifisadi achunguzwe kwanza kabla ya kupewa majukumu.
“Hapa ndio utaona jinsi Serikali ya Tanzania inavyougua ugonjwa wa saratani ni lazima ife…, jambo hili katika taaluma ya sheria na katiba tunaliita kuwa ni ‘ishara ya dola inayokufa’,” alisema Mvungi.
Aliongeza: “Siku hizi si ajabu kuona jaji anahongwa na Takukuru… Ni wazi kuwa Serikali inayumba”.
Alisisitiza kwamba, ndani ya kamati hiyo atakayejiona hawezi kufanya kazi hiyo kwa kuwa ana maslahi binafsi na Meremeta aachie ngazi mapema ili kuondoa maswali kutoka kwa wananchi, kinyume chake uchunguzi wa kamati hiyo hautakuwa na faida yoyote.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema, “Jambo linaloibuliwa na kundi jingine na kuhitaji ufumbuzi si vyema likasimamiwa na kundi linalolalamikiwa”.
Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni alisema kwa kiasi kikubwa sakata la Meremeta liliibuliwa na wabunge wa upinzani, lakini anashangaa kuona suala hilo linapi pelekwa katika kundi ambalo linaweza kuwa lilihusika.
“Simhukumu Lowassa kuwa ni fisadi…, lakini wakati Serikali inaingia mkataba na kampuni hii yeye alikuwa katika Baraza la Mawaziri, sasa suala hili kurejeshwa tena kwake ni sawa?” alihoji Mbowe.
Mbowe alisema kuwa huu ni wakati wa Bunge kutambua kuwa si lazima kila Kamati iongozwe na wabunge wa CCM na kusisitiza kuwa ni vyema ikaundwa Kamati itakayoongozwa na upinzani ili kuchunguza Meremeta.
Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia, alisema si lazima ufisadi wa Meremeta ukachunguzwa na Kamati ya Bunge.
“Takukuru si wapo wanaweza kufanya kazi hii…, hili ni jambo nyeti ambalo linatakiwa kuchunguzwa na watu wenye taaluma kama Takukuru, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mkuu wa Jeshi la Polisi,” alisema Mbatia.
Mbatia alidai kuwa ndani ya CCM hakuna wa kumfunga mwenzake kengele. Alidai kuwa chama hicho kimekithiri kwa ufisadi na kwamba walio salama ni wachache.
“Hakika uamuzi huu utazidi kuwachanganya Watanzania, inakuwaje mtu anatuhumiwa kwa mambo fulani halafu anachaguliwa kuwa Mwenyekiti Kamati ya Bunge, halafu kamati yake inapewa jukumu hili?” Alihoji Mbatia
Mwenyekiti wa Chama cha Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, alidai kuwa kamati hiyo haiwezi kuja na majibu ya kuwaridhisha Watanzania.
“Ni usanii mtupu, hata vyombo vingine vya Serikali haviwezi kulichunguza jambo hili kwa kuwa kwa muda mrefu vimekuwa vibaraka wa mafisadi, labda vivunjwe na kuundwa upya,” alidai Mtikila
Mhadhiri wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Dk Benson Bana, alisema ingawa uamuzi huo wa Bunge utazua maswali mengi kwa wananchi, sheria za Tanzania zinaeleza wazi kuwa mtuhumiwa sio mkosaji.
“Mbona Lowassa anakwenda kanisani na kuchangisha mamilioni ya fedha watu hawasemi lolote?” Alihoji Bana na kuongeza:
“Watanzania wasimhukumu mtu kwa hisia, sidhani kama hata hiyo kamati yake ina watu wasafi…, Lowassa kisheria na kisiasa yuko safi ila kihisia si safi, tunatakiwa kufanyia kazi hali halisi si hisia,”.
Hata hivyo, alisema pamoja na Bunge kupeleka suala hilo kwa kamati inayoongozwa na Lowassa, Serikali pia inaweza kuunda tume yake ya kuchunguza ufisadi huo.
Mhadhiri mwingine wa chuo hicho, Bashiru Ally alisema kuwa unyeti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama unaweza kufanya majibu ya uchunguzi huo yakawa wazi au kuwa siri.
“Wanaweza kusema kuna mambo hawawezi kuyasema kwa ajili ya usalama wa nchi, ila binafsi nilidhani suala hili lingepelekwa Kamati ya Nishati na Madini au ile ya Mashirika ya Umma, sijui Spika wa Bunge katumia vigezo gani kulipeleka suala hili katika kamati hii,” alihoji Bashiru.
 
******* woote,kuanzia makinda hadi lowassa,na wasubiri kilichomkuta Gadafi!!nyambaf zao
 
Huyo Dr. Benson Bana anachemsha kama ni muhadhiri anaidhalilisha taaluma yake. Ni kweli mtu hahukumiwi kwa hisia lakini kama serikali haijaweza kumsafisha aidha kwa kumpeleka mahakamani akashinda kesi ni haki ya wananchi kuhisi ni muhalifu maana hata uwaziri mkuu aliacha kwa sababu hizo hizo, kama angekuwa safi asingejiuzulu uwaziri mkuu, kitendo cha kujiuzulu one way or another kinamtia hatiani kijamii sio kisheria, period!

Nchi hii imeoza kuanzia kichwani mpaka mkiani, msomi wa chuo kikuu anaongea namna hii! ati mbona kanisani anatoa michango watu wasiulize, kuna uhusiano gani hapa na jambo linalozungumziwa!
 
Bunge hili lisipokuwa makini litasahau majukumu yake ya kutunga sheria na kubakia na miradi ya uchunguzi isiyo na kikomo..................kazi hii takukuru hawaiwezi kwa sababu kama wangelikuwa wanaiweza tayari wangelikuwa wameifanya......................ukweli ni kuwa Bunge linatakiwa liunde sheria ya kumruhusu mchunguzi kama Ken Starr wa USA aliyemchunguza Clinton kwenye kashfa ya Monica Lewinsky..........................katika kila uchunguzi unaolipulwa na Bunge nchi imani kwenye taasisi za umma inazidi kupotea.............................tatizo la wanasiasa wetu wamelewa madraka kuliona hili................
 
ni kweli LOWASA alijiuzulu kutokana na kashfa ya Rechmond serikalini mi naona kujiuzulu ni ujasiri hasa kwa mazingira ya nchi zetu za Afrika hiyo nisawa na adhabu hata ukifuatilia siasa za japan mawaziri wakuu tofautitofauti wamekuwa wakijiuzulu kutokana na kashfa mabalimbali ndoi huo utamaduni huyo lowasa aliutumia kwakuwa alitoka katika ngazi ya uwaziri mkuu wakati ule na sasa siyo waziri mkuu basi anawezapewa nafasi ilitumuone mara nyingine kufanya kosa si kosa kosa kurudia kosa tuwe na moyo huo waTZ lakini kwa wale wanaoshindwa kujiuzulu hao wachunguzwe na ikithibiti wafikishwe mahakamani au wawajibishwe kwa nguvu ili kuleta imani kwa wananchi. iluendelee kwa haraka utamaduni wa kuwajibika lazima utiliwe mkazo hata kama mtu huyo atahitaji kurudi wananchi ndio wata mhukumu kwa dhambi alizofanya!!pia adhabu zote mbili zinaweza kutumika kuwajibika na kuchunguzwa ikithibiti sheria inachukua mkondo.
 
Kesi ya nyani kapelekewa ngedere unadhani mwisho wake ni nini?
 
Mbona hawakupinga hasiwe mwenyekiti wa hiyo kamati! Maana kazi imepewa kamati siyo Lowasa.

Mkuu hapa umenena. Hii ni Kamati na siyo kapewa mtu mmoja. Ikumbukwe pia kwamba wabunge wenzake walimuamini na KUMCHAGUA kuwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo.
 
Back
Top Bottom