regam
JF-Expert Member
- Jan 4, 2011
- 269
- 51
Ndugu wana jf wenzangu naangalia mawaidha ya fisadi wetu lowasa wakati wa uzinduzi wa studio ya wasanii wa tz. Anaendelea kusisitiza eti tz inaongoza kwa kuwa na amani ukilinganisha na majirani zetu. Sasa ninachojiuliza hivi hii amani tunayoambiwa tunayo watz ni ipi? Hivi ni vigezo gani vinavyoonyesha kwamba mtu ana amani? Hivi amani ina maana gani kama hali ya maisha ni ngumu? Mafuta juu, gesi juu, ajira ngumu, mazingira ya kuanzisha biashara magumu? Hivi hii ni amani kweliiiii?