BONGOLALA
JF-Expert Member
- Sep 14, 2009
- 16,507
- 11,883
EL amesema hayo mwanza alipokua mgeni rasmi kuchangia kanisa katoliki, kukosekana kwa ajira kwa vijana ni bomu linalotarajia kulipuka wakati wowote hivyo kusababisha vita nchini.
Kuna vijana 2.5m wasio na ajira!
==========
UPDATED:
Na mwandishi wa FikraPevu.com
Mhe. Edward Ngoyai Lowassa (MB), amesema kwamba, amani iliyopo hapa nchini ipo mashakani kutoweka, kutokana na wimbi kubwa la vijana kutokuwa na ajira maalumu, hivyo Serikali inapaswa kuweka mikakati madhubuti ya kuzalisha ajira nyingi kwa vijana.
Amesema, kati ya nguvu kazi ya taifa inayokadiriwa kufikia milioni 25 kwa sasa, kati yake milioni 17.5 ni vijana ambao kimsingi wanakabiliwa na ukosefu wa ajira maalumu, jambo ambalo Serikali inapaswa kulipatia ufumbuzi haraka sana ili kulinda amani ya nchi isiyumbe au kutoweka kabisa.
Lowassa, aliyasema hayo leo Jijini Mwanza, wakati alipokuwa akizungumza kwenye harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa Katoliki, Parokia ya Nyakato Jimbo Kuu la Mwanza.
Lowassa ambaye pia ni mbunge wa Monduli na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM taifa alisema, hali hiyo inachangiwa na uchumi duni wa nchi ikiwa ni pamoja na sera mbovu za elimu zisizozingatia uhitaji wa soko la ajira na vijana wengi kutotaka kuchukuwa masomo ya sayansi na hisabati ambayo yana fursa kubwa ya kupata ajira.
Kiongozi huyo ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika harambee hiyo iliyokusanya sh. milioni 200 na kuvuka lengo la sh. milioni 120, alisema kwa sasa tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana hapa Tanzania limefikia zaidi ya asilimia 30, ikilinganishwa na wastani wa asilimia 21 wa tatizo hilo linalozikumba nchi zote za Bara la Afrika.
"Siku zote nimekuwa nikisema nchi yetu inakabiliwa na tatizo kubwa la ukosefu wa ajira kwa vijana. Hali hii isipopatiwa ufumbuzi na Serikali, amani ya nchi yetu inaweza kuyumba.
"Kati ya vijana 850,000 wanaoingia kwenye soko la ajira baada ya kumaliza masomo yao ya msingi, sekondari na vyuo, ni asilimia tano tu ndiyo wanapata ajira katika sekta rasmi isiyo ya kilimo. Na hii ni hatari sana kwa maendeleo ya taifa letu", alisema Lowassa ambaye alichangia sh. milioni 11 katika harambee hiyo.
Kwa mujibu wa Lowassa ambaye alionekana kushangiliwa kila wakati pale jina lake linapotajwa, vitendo vya rushwa vinavyoonekana kuota mizizi katika sehemu za utoaji ajira rasmi Serikalini na kwenye taasisi za umma, ndiyo chanzo kikubwa cha matatizo kama hayo.
Sababu nyingine alizozitaja Lowassa zinazochangia kukosekana kwa ajira kwa vijana nchini ni pamoja na sera mbovu za ajhira na mitaala ya elimu isiyokidhi mahitaji ya soko la ajira Bara la Afrika na duniani kwa ujumla.
"Kutozingatia mabadiliko ya kiuchumi, kibiashjara, kisiasa, kijamii na kiteknolojia nchini, Afrika Mashariki, Afrika na dunia nzima ndiyo inayozalisha yote haya mabaya", alisema Lowassa ambaye alionekana kuwa kivutio kikubwa kwenye harambee hiyo.
Awali, Makamu Baba Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Mwanza, Askofu Richard Makungu aliwaonya watu wanaowanyooshea vidole wenzao, na kusema vitendo hivyo si vizuri hata kidogo, kwani watu hao wakichunguzwa nao wana mabaya yao, na wala hata choo majumbani mwao hawana kabisa.
Askofu Makungu alisema, vitendo vya kulalamika lalamika ama kwa kuilalamikia Serikali, ofisa, kiongozi au mtu fulani huo ni sawa na ufedhuli mtupu, na kwamba Watanzania waache kusonta vidole watu, ili taifa liweze kupata taranta kutoka kwa Mungu.
Hata hivyo, alisema ujio wa Lowassa katika harambee hiyo ni mzuri sana, na alisema kwa vile kanisa hiolo limejengwa kwa tofali moja moja, basi na waumini wa kanisa hilo watakuwa tofali moja moja kwa Lowassa.
CHANZO: FikraPevu | JamiiForums' News Site
Kuna vijana 2.5m wasio na ajira!
==========
UPDATED:
Na mwandishi wa FikraPevu.com
Mhe. Edward Ngoyai Lowassa (MB), amesema kwamba, amani iliyopo hapa nchini ipo mashakani kutoweka, kutokana na wimbi kubwa la vijana kutokuwa na ajira maalumu, hivyo Serikali inapaswa kuweka mikakati madhubuti ya kuzalisha ajira nyingi kwa vijana.
Amesema, kati ya nguvu kazi ya taifa inayokadiriwa kufikia milioni 25 kwa sasa, kati yake milioni 17.5 ni vijana ambao kimsingi wanakabiliwa na ukosefu wa ajira maalumu, jambo ambalo Serikali inapaswa kulipatia ufumbuzi haraka sana ili kulinda amani ya nchi isiyumbe au kutoweka kabisa.
Lowassa, aliyasema hayo leo Jijini Mwanza, wakati alipokuwa akizungumza kwenye harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa Katoliki, Parokia ya Nyakato Jimbo Kuu la Mwanza.
Lowassa ambaye pia ni mbunge wa Monduli na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM taifa alisema, hali hiyo inachangiwa na uchumi duni wa nchi ikiwa ni pamoja na sera mbovu za elimu zisizozingatia uhitaji wa soko la ajira na vijana wengi kutotaka kuchukuwa masomo ya sayansi na hisabati ambayo yana fursa kubwa ya kupata ajira.
Kiongozi huyo ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika harambee hiyo iliyokusanya sh. milioni 200 na kuvuka lengo la sh. milioni 120, alisema kwa sasa tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana hapa Tanzania limefikia zaidi ya asilimia 30, ikilinganishwa na wastani wa asilimia 21 wa tatizo hilo linalozikumba nchi zote za Bara la Afrika.
"Siku zote nimekuwa nikisema nchi yetu inakabiliwa na tatizo kubwa la ukosefu wa ajira kwa vijana. Hali hii isipopatiwa ufumbuzi na Serikali, amani ya nchi yetu inaweza kuyumba.
"Kati ya vijana 850,000 wanaoingia kwenye soko la ajira baada ya kumaliza masomo yao ya msingi, sekondari na vyuo, ni asilimia tano tu ndiyo wanapata ajira katika sekta rasmi isiyo ya kilimo. Na hii ni hatari sana kwa maendeleo ya taifa letu", alisema Lowassa ambaye alichangia sh. milioni 11 katika harambee hiyo.
Kwa mujibu wa Lowassa ambaye alionekana kushangiliwa kila wakati pale jina lake linapotajwa, vitendo vya rushwa vinavyoonekana kuota mizizi katika sehemu za utoaji ajira rasmi Serikalini na kwenye taasisi za umma, ndiyo chanzo kikubwa cha matatizo kama hayo.
Sababu nyingine alizozitaja Lowassa zinazochangia kukosekana kwa ajira kwa vijana nchini ni pamoja na sera mbovu za ajhira na mitaala ya elimu isiyokidhi mahitaji ya soko la ajira Bara la Afrika na duniani kwa ujumla.
"Kutozingatia mabadiliko ya kiuchumi, kibiashjara, kisiasa, kijamii na kiteknolojia nchini, Afrika Mashariki, Afrika na dunia nzima ndiyo inayozalisha yote haya mabaya", alisema Lowassa ambaye alionekana kuwa kivutio kikubwa kwenye harambee hiyo.
Awali, Makamu Baba Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Mwanza, Askofu Richard Makungu aliwaonya watu wanaowanyooshea vidole wenzao, na kusema vitendo hivyo si vizuri hata kidogo, kwani watu hao wakichunguzwa nao wana mabaya yao, na wala hata choo majumbani mwao hawana kabisa.
Askofu Makungu alisema, vitendo vya kulalamika lalamika ama kwa kuilalamikia Serikali, ofisa, kiongozi au mtu fulani huo ni sawa na ufedhuli mtupu, na kwamba Watanzania waache kusonta vidole watu, ili taifa liweze kupata taranta kutoka kwa Mungu.
Hata hivyo, alisema ujio wa Lowassa katika harambee hiyo ni mzuri sana, na alisema kwa vile kanisa hiolo limejengwa kwa tofali moja moja, basi na waumini wa kanisa hilo watakuwa tofali moja moja kwa Lowassa.
CHANZO: FikraPevu | JamiiForums' News Site