Lowassa apanda chati kuelekea uchaguzi mkuu 2015

Hiyo ni REDET RIPORT iliyofanywa na Dr. Bana and Assistant Researcher Ritz!Haya Banaa we are waitn:rockon:
 
Ninaamini kama Lowassa angekuwa Waziri Mkuu bado hadi leo, ule mradi wa maji wa Ziwa Victoria usingekuwa umeishia Shinyanga pekee, bali ungekuwa umeishafika katika wilaya za Nzega, Igunga na mikoa ya Singida na Dodoma.
 
Eti katika kila watanzania kumi saba wanamuunga mkono Lowasa! Tatizo lenu Watu wa CCM mambo ya kwenye vikao vyenu mnachukulia ndio maamuzi ya Watanzania wote.
Jana tuu mlikuwa mnapita nchi nzima mnamwita gamba na kwamba lazima ajivue mwenyewe la sivyo mtamvua. Kikao cha NEC kamuumbua Mwenyekiti wenu kuwa mbona naye alihusika kwenye Richmond mkaona ohho! mambo yameharibika sasa tumwite JEMBE! loh mna mambo nyie!
Kweli ukizama baharini hata unyasi utaukimbilia ukidhani utakuokoa. RIP CCM
 
Ungesema kati ya watanzania wana CCM 10 siyo kati ya Watanzania 10. Hiyo ratio ya kimagamba haiapply kwa watanzania wote wenye vyama tofautitofauti na wasio na vyama.

Ni pigo kwa Chadema sijui mtamsimamisha nani Zitto, Mbowe au Dr Slaa.
 
Eti katika kila watanzania kumi saba wanamuunga mkono Lowasa! Tatizo lenu Watu wa CCM mambo ya kwenye vikao vyenu mnachukulia ndio maamuzi ya Watanzania wote.
Jana tuu mlikuwa mnapita nchi nzima mnamwita gamba na kwamba lazima ajivue mwenyewe la sivyo mtamvua. Kikao cha NEC kamuumbua Mwenyekiti wenu kuwa mbona naye alihusika kwenye Richmond mkaona ohho! mambo yameharibika sasa tumwite JEMBE! loh mna mambo nyie!
Kweli ukizama baharini hata unyasi utaukimbilia ukidhani utakuokoa. RIP CCM

Mkuu viwanda vyako vya uongo unavyo vingapi.
 
Hivi si huyu jamaa alituhahidi Mvua kutoka Indonesia? Labda akichaguliwa mvua itanyesha mwaka mzima.
 
sasa naanza kuamini rais ajaye lazima atoke kaskazini tuu......MAGAMBA PROPAGANDA ZENU ZA UKANDA NA MFUMO KRISTU NDIO KWISHA TENA........
 
Ninaamini kama Lowassa angekuwa Waziri Mkuu bado hadi leo, ule mradi wa maji wa Ziwa Victoria usingekuwa umeishia Shinyanga pekee, bali ungekuwa umeishafika katika wilaya za Nzega, Igunga na mikoa ya Singida na Dodoma.

Usisahau ndiye alie-sign MoU
 
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, Lowassa aliweka kambi mikoa ya kusini akisaidiana na wananchi waliokumbwa na mafuriko makubwa.
 
Naunga mkono hoja ndani ya CCM raisi anyefaa ni LOWASA lakini ndani ya Tanzania raisi anyefaa ni Dr Slaa
 
Lowassa ndio kiboko yenu nyie, ndio maana hofu limewajaa, mkwe wake kushindwa haihusiani kabisa, nikuulize,wewe dada yako akiposwa na wewe unavishwa pete?

Mgombea mwenza wake atakuwa huyu hapa kwenye picha...
attachment.php
 

Attachments

  • DOWANS.JPG
    DOWANS.JPG
    63.7 KB · Views: 230
Usisahau ndiye alie-sign MoU

Mkuu Lowassa amekuwa mtu tegemo katika shughuli za kijami iwe Msikitini au Kanisani yupo bega kwa bega na Masheikh na Maaskofu. Tofauti na viongozi wengine wa kisiasa.
 
Ninaamini kama Lowassa angekuwa Waziri Mkuu bado hadi leo, ule mradi wa maji wa Ziwa Victoria usingekuwa umeishia Shinyanga pekee, bali ungekuwa umeishafika katika wilaya za Nzega, Igunga na mikoa ya Singida na Dodoma.

Naona umekusanya nondo. Bahati mbaya zitakuwa monotonous kwasababu utalazimika kuzirudia hizo hizo kila siku
 
Wanabodi,

Wakati mchakato wa Uchaguzi ndani ya Chama cha Mapinduzi CCM unaendelea kuanzia ngazi ya shina hadi taifa. Mbunge wa Monduli Edward Lowassa anaonekana kupanda chati kwa kasi ya ajabu na kuonekana ana nafasi kubwa katika mbio za urais 2015.

Uchambuzi wa kisiasa unaonesha karibu kila kona ya nchi hii, katika watanzania 10 utakaowahoji kuhusu ni nani hasa anayefaa kumrithi Rais wa sasa Kikwete, saba kati yao wanamtaja Lowassa wakidai ni "Jembe" linalopigania haki na maendeleo ya kila Mtanzania.

Makundi makubwa yanayotajwa katika mnyukanakano huo ni pamoja na kundi la Lowassa, Samwel Sitta, na Bernad Membe. Kila mmoja anapambana kufa na kupona kuhakikisha kwamba wanaingiza watu wao muhimu katika vikao vya (NEC) na ndani ya Jumuiya za chama hicho, UVCCM, UWT, na Wazazi, katika makundi yote hayo Lowassa anaonekana kuwa ni mtu makini ana nafasi kubwa ya kupenya na kupererusha bendera ya chama hicho.

Kusimama kwa Lowassa kama mgombea Urais ni pigo kubwa kwa vyama vya siasa hasa Chadema, CUF na NCCR Mageuzi. Kutokana na rekodi ya Lowassa, ni mtu wa kufuatilia kila jambo analoamini katika dhamira yake kwamba linafaa kwa ajili ya maendeleo ya wananchi ni mwenye hulka ya kusaidia na kuchangia shughuli za kijamii bila kujali itikadi za kisiasa wala dini, tofauti na viongozi wengine wa kisiasa amekuwa mtu tegemeo katika shughuli za kijamii iwe za kanisani au msikitini.

Ukitaka kumjua Lowassa ni kiongozi wa namna gani, tembelea jimboni kwake Monduli ukaone namna alivyowezesha makundi ya vijana na wazee kiuchumi.

Hakuna jipya hapa,ni walewale walamba viatu
 
Kinachonifurahisha mimi licha ya kelele zote na propaganda za udini na ukabila wa CCM, lakini Rais ajaye ni lazima atoke kaskazini na ni lazima awe Mkristo, hapa mmejikaanga kwa mafuta yenu wenyewe.

Nadhani Pasco anafanya kazi nzuri sana kama ameweza kumsajili na Ritz kwenye kikosi kazi cha kuelekea 2015, narubungo uko wapi?

Asante mkuu,umemaliza kila kitu.
 
Last edited by a moderator:
Ndio maana kinana ameng'atuka.! Labda baada ya kuona kambi ya lowsa inazidi kuota mizizi.!
 
Mkuu Ritz sikujua na wewe unasapoti kambi ya lowassa,hivi na madudu yote ya Richmond na mvua za kutengeneza unafikiri anaweza kupenya??
Keshaingizwa kwenye payroll,pesa haina dini wala kabila mkuu!

Anasema eti asilimia 70(saba kati ya kumi) sijui ya watu gani hao,eti wanamtaka Lowassa,sijui utafiti wa wapi?Kanisani ama miskitini?lol!
 
mwekeni huyo mwizi muone mtakavyoanguka. Unaleta utafiti wa kivulini unataka tuamini. mleteni tu bwana gamba aliyeshindikana muone kama atashinda kwa makundi mlivyogawanyika.
 
Back
Top Bottom