Lowassa anasafishwa!

Mkandara .Nina habari za huu mkakati mzito.Na kila nikiangalai naona kila aina ya dalili baada ya rais kuanza kujikanyaga kwenye majukwaa.Lowasa huenda akaenda Ubalozini ama akapata nafasi moja kubwa na ya ulaji lakini anapigania kurudi kwenye siasa ndani ya CCM.

Akimpa nafasi yoyote ile Lowassa basi atakuwa amejichimbia kaburi mwenyewe. Huyu Lowassa hastahili kupewa nafasi yoyote ile, bali anastahili kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma kuhusiana na kashfa za Richmond.

Kwa namna moja au nyingine anahusika na kashfa hiyo ndio maana alikuwa mstari wa mbele kuhakikisha anawanyamazisha wabunge kila walipotaka kujua kuhusiana na kashfa hiyo.
 
............................. Richmond ilikuwa kati ya makampuni yaliyo fail vibaya sana, lakini bado kutokana na shinikizo toka ofisi yake walipewa tender hiyo.
Uhalifu ilianza kabla hata contract haijawa signed na nadhani kama alikuwa hana mkono wake angeanza kuwaambia watu kushiriki kwake kabla/toka siku ya uchaguzi wa kampuni hiyo na sio baada uya kuwa signed................................Swali lilikuwa:- Kwa nini Richmond walipewa Tender hiyo?...Jibu la kamati lilikuwa ni nguvu toka ofisi ya Waziri mkuu. Hadi wakati huu hajajibu kabisa nafasi yake wakati tender ikitolewa..isipokuwa anazungumzia baada ya contract kuwa signed.

Bob Mkandara,

.....Huyu Lowasssa................kama nilivyosema hapo awali.....he is still the weakest link.....hastahili kuingia ktk platform hivi sasa........what is he trying toi tell the Umma wa watanzania???.....ya kwamba eti yeye ni CLEAN na hii sakata ya Richmond????......gimme a BREAK!!!
 
Baada ya kuyaona haya yanayojiri hivi sasa na michezo ya maigizo tunayochezewa na kina Lowassa, nazidi kuiamini nadharia niliyokuwa nayo mwanzo kuwa labda Kamati ya Mwakyembe ilikuwa na melekezo maalumu kutoka mahali fulani kuwa Lowassa asihojiwe, ili kumpa mwanya wa kuendelea na mpango wao fulani.

Na hata ushabiki watu wengi walioonesha kwa PM "mpya" naanza kuhisi ni yaleyale mambo ya "kipya kinyemi ingawa ........".

Kazi ipo!
 
Nimesikiliza Mahojiano,

Nadhani other than makosa madogo madogo ya Mh. Lowassa kama binadamu... ilikuwa ni muhimu kwetu kujua upande wake,,, ambao tumeufahamu...

Kuna jambo Mh. Lowassa amelisisitiza nalo ni Kamati aliyounda iliyochini ya Mwanasheria Mkuu ilikuwa Bogus... hivyo kwa maneno haya ya Mh. Waziri mkuu mstaafu... tunaomba Mwanasheria Mkuu wa Serikali aachie kazi yetu jamani... huyu mheshimiwa anataka mpaka aaambiwe je wajameni?

Mh. Mgonja, hata kama unajiamini sana,,, soma nyakati... it is time to go mzee
 
Unajua, ingekuwa mimi ni EL na nina nia ya kurudi kwa nguvu, ningekubali kuwajibika na kutotota hata sababu moja kujitetea kuwa sihusiki.

Ningesema " Kwa nafasi yangu kama Waziri Mkuu, nilipaswa kuwa makini katika kufuata taratibu za sheria na utendaji katika kutafuta mzabuni wa umeme huu wa muda. Nakiri kufanya uamuzi kwa pupa ya kutaka kutatua tatizo bila kuwa makini. Kwa hili na mzigo wote ambao nimeupa Taifa kutokana na maamuzi yangu, naomba radhi kwa Taifa kwa kushindwa kulitumikia ipaswavyo na kulilinda kutokana na uhujumu, kwa mujibu wa katiba na kiapo changu kama Mbunge, Waziri Mkuu na Mwana CCM. Naomba Watanzania wanipe imani yao kuwa nitaliwakilisha jimbo langu la Monduli kwa umakini kwa kujifunza kutokana na makosa niliyofanya ambayo yamepita. Kidumu Chama cha Mapinduzi"

Kwa mtaji huo, watu tutasahau kuwa yeye ni "fisadi" tutasema kafanya uungwana na ikifika 2015 na matunda ya yeye kuwa Mbunge mahiri bungeni, anaukwaa Ugombea uraisi kupitia CCM.

Lakini, huyu ni Lowassa hivyo......
 
Unajua, ingekuwa mimi ni EL na nina nia ya kurudi kwa nguvu, ningekubali kuwajibika na kutotota hata sababu moja kujitetea kuwa sihusiki.

Ningesema " Kwa nafasi yangu kama Waziri Mkuu, nilipaswa kuwa makini katika kufuata taratibu za sheria na utendaji katika kutafuta mzabuni wa umeme huu wa muda. Nakiri kufanya uamuzi kwa pupa ya kutaka kutatua tatizo bila kuwa makini. Kwa hili na mzigo wote ambao nimeupa Taifa kutokana na maamuzi yangu, naomba radhi kwa Taifa kwa kushindwa kulitumikia ipaswavyo na kulilinda kutokana na uhujumu, kwa mujibu wa katiba na kiapo changu kama Mbunge, Waziri Mkuu na Mwana CCM. Naomba Watanzania wanipe imani yao kuwa nitaliwakilisha jimbo langu la Monduli kwa umakini kwa kujifunza kutokana na makosa niliyofanya ambayo yamepita. Kidumu Chama cha Mapinduzi"

Kwa mtaji huo, watu tutasahau kuwa yeye ni "fisadi" tutasema kafanya uungwana na ikifika 2015 na matunda ya yeye kuwa Mbunge mahiri bungeni, anaukwaa Ugombea uraisi kupitia CCM.

Lakini, huyu ni Lowassa hivyo......


Lowasa ananua mengi kwenye huu U RDC. Anasema alimwita Waziri husika akamkatalia ndipo akaitwa Katibu Mkuu Hazina , mwanasheria na Luhanjo .Mbona haya hatukuwahi kuyasikia jamani ? All in all he is very much trying for a come back . Nauliza kwa muda huu akiwa Monduli , ile mvua yetu itakuja lini ?
 
naamini wapo hata humu ambao huwa ni vigeugeu na walwah tunayo majina tunsubiri wale sikukuu kisha tuwataje peupeee...
 
Baada ya kuyaona haya yanayojiri hivi sasa na michezo ya maigizo tunayochezewa na kina Lowassa, nazidi kuiamini nadharia niliyokuwa nayo mwanzo kuwa labda Kamati ya Mwakyembe ilikuwa na melekezo maalumu kutoka mahali fulani kuwa Lowassa asihojiwe, ili kumpa mwanya wa kuendelea na mpango wao fulani.

Na hata ushabiki watu wengi walioonesha kwa PM "mpya" naanza kuhisi ni yaleyale mambo ya "kipya kinyemi ingawa ........".

Kazi ipo!

Ukimsikiliza kwa makini Lowasa utapata tafakuri nyingi sana. Mojawapo kuna kila dalili kuwa some one was out there trying to find possible means to clean the government. It also seems that the Mwakyembe committee had many of the conlcusions at hand prior to their investigation and used the investigation to justify them. Furthermore, there is a clear sign that it is not all good in CCM following Lowasa's resignation (or dismissal?). In this context it is difficult to avoid to contemplate that the committee was used consciously or otherwise to try to clear CCM government woes.

That said, kitendo cha kamati kutokumhoji Lowasa kitaendelea kubaki kuwa ni doa sio tu katika report yao lakini pia katika harakati zetu za kujenga demokrasia hasa msingi wa kumpa nafasi kila mtu kusikilizwa. Pamoja na haya, Lowasa hana uwezo wa kujisafisha na mazingira ya ufisadi yanayomzunguka. Nyerere alikuwa wa kwanza kutustua sote kuwa Lowasa alikuwa ni fisadi hatari, lakini rafiki yake JK akaziba masikio akampa nafasi Lowasa ili awathibitishia watanzania kwamba madai ya Nyerere yalikuwa ni hisia tu na hayakuwa na ukweli wowote. Lowasa ameshindwa kutumia nafasi aliyopewa na rafiki yake kujisafisha, badala yake yeye akaitumia kujichafua zaidi na kututhibitishia kuwa Nyerere was more tha right. Sasa hizi giliba za kuwatumia wananchi wa Monduli kumwandalia mapokezi makubwa haziwezi kubadilisha mawazo yetu, tulishaamua. Anachotakiwa kufanya Lowasa ni kukaa kimya ili tumsahau. Uzuri ni kwamba sisi watanzania ni wepesi wa kusahau na inawezakana huko mbele CCM yake hata wakampa madaraka makubwa tu bila matatizo yeyote na wala watanzania wasilalamike.
 
Hizi habari kama ni za kweli inabidi uweke wazi majina ya waliopokea rushwa na waliotoa rushwa kwani yote hayo ni makosa ya jinai, kutoa na kupokea. habari kama hizi ni nzito sana inabidi uziweke wazi, yaani utuwekee wazi majina na magazeti yaliyowaajiri ukisema kijujuu tu "waandishi", hapo naona inakuwa kashfa kwa waandishi wote wakati tunawajua waandishi wengi sana ambao ni wazalendo wa kweli na wanapinga na wako weupe kwenye kashfa namna hizi. Tunaomba weka wazi hao waandishi mafisadi na magazeti yao.

VIJANA wa TAKAKURU haya tena leads hizo, maana kwa jinsi nilivyoona mkilumbana humu JF hamna hata kazi za kufanya, haya changamkieni tenda zinaweza zikawa-save mkawemo kwenye chombo kipya ambacho kipo njiani kinapikwa.
 
baadhi ya magazeti ya kufuatilia hasa ktk feature stories,
Habari corporation, Uwazi, Tanzania Daima (culumnist), Nipashe list inaendelea.....

kuna baadhi ya waandishi wa makala ambao wamelipwa huko ili kutumia kalamu zao kuupaka rangi ufisadi ili ionekane as kuonewa na kijicho.

Ninaamini pia kuwa baadhi wa wanene fulani hasa ktk kurugenzi ya Nishati wanahaha kuokoa shingo zao panga lisiwapitie. mmeyasikia ya BOT? walioidhinisha mijihela ya richmond awamu ya pili wameshatimuliwa na wengine watafuata.
 
Hii habari ina ukweli sana tu. Maana mienendo ya magazeti inajionyesha. Maro ooh mtabiri katabiri nini maro lile. Hizi ni dalili kuwa JK anawaza kumrudisha kundini kondoo wake aliyejitosa porini. Lowassa hasafishiki hata kwa magadi na chlorine!

Kwako JK; ni vizuri nikuonye kama mtu mzima. Mheshimu Makamu wako wa rais na hasa mawazo yake. Tabia yako uliyokuwa nayo ya kumfunika wewe na Lowassa kwa sababu zenu, uiache sasa. Msikilize waziri mkuu pia.

Kwa hao wanaojiona CCM sana huko Arusha; kwa kitendo chenu cha kumwekea mwizi 'kapeti jekundu' eti anakwenda kusema ukweli kwa wananchi wake. Ni kipi kilimshinda asiseme bungeni akasikika na watanzania? Mimi wala sijasikia jipya kwenye maongezi yake. Yakiwakuta msianze kulia ooh watanzania tusaidieni wakati mmeonyesha wazi lengo lenu la kumsafisha mwizi
 
Kisheria Tume ilipaswa kumuita na yeye atoe maelezo yake ambayo kimsingi yangepaswa kuwemo ndani ya ripoti nyeti ya Mh mwakyembe.
hii inafanya jamii kmhukumu moja kwa moja kupitia matokeo ya ripoti ile, lakini je yeye mwenyewe anasemaje?

kwa mujibu wa mahojiano yake yaliyorushwa na TVT na kupatikana kwa Mhshimiwa sana Mwanakijiji lowasa anasema nanukuu...
“Lakini inafahamika kwamba mara mbili nilijaribu kuonya kuhusu mradi huo wa Richmond, uliokuwa uzalishe umeme wa dharura. Kwanza mwishoni mwa Septemba 2006 niliandika kwa Waziri wa Nishati na Madini, nilitaka Richmond ichunguzwe na Serikali ijiridhishe kama kampuni hiyo ina uwezo, na mara ya pili, ni Oktoba mwaka huo huo, alipoitisha kikao cha wakuu wa idara, kama ya Usalama na vyombo vingine, kutaka kujua hali ya mambo ilikuwaje,”

Kwa mujibu wa watu wa karibu waliohojiwa na gazeti la This Day ambalo lilikuwa la kwanza kutilia mashaka Kampuni hii, Lowasa hawajibiki na ulaji wa pesa ya Richmond ila kuna watu walitumia mgongo wake tuu.
 
Tumwamini nani? Tume , Lowasa au watetezi wake? Tafuta riport ya Mwakyembe.
 
Simba jike umeunguruma kikweli na ninakukubali sana
Vipi kuhusu kitwana CHENGEye aliyebakia kulinda minofu ya bwana mkubwa?? nadhani iwe njia njema kuwashtaki kwa wananchi wale viongozi ambao wanakwiba amali zetu
Pia Muungwana (JK) ipe meno zaidi Tume ya Maadili maana kutoa mapendekezo tu haitoshi, iwe tume huru inayofanya kazi kikamilifu bila ya kuogopa kisheria maana naamini kuwa endapo wangepewa nafasi hawa wa-maadili tungekuwa na viongozi safi. Na ni mapendekezo mangapi ya Tume ambayo yamefanyiwa kazi??? kumbuka wanafanya kazi chini ya kiapo hawa watu.
 
Ama kweli waandishi wetu wamefika pabaya na ndiyo hao hao walianza kwa kutuandikia kuwa Lowassa ni nabii na Sokoine anayekuja kuikomboa Tanzania na watu wake. Hivi kweli hata nafsi za haziwasuti kweli? Wenye akili na ufahamu mkubwa tunatambua kuwa hao ndiyo miongoni mwa waandishi ambao wamejengewa nyumba na kununuliwa magari, na zaidi sana hata kuahidiwa au kusomeshwa kabisa wao, wake zao na watoto. Ndio hao hao ambao Lowassa aliagiza kuwekewa umeme kwa siku moja na kafanikiwa.
Kama waandishi nao wanakuwa namna hiyo iweje kwa watu wengine, nani atawaetea wana wa nci hii tajiri lakini yenye watu masikini wa kutupwa kwa kuwa tu kna Lowassa na wengine wa aina yake wanatuibia na kukomba kila kilicho chetu kwa faida ya matumbo yao, wake zao, wachumba zao, mashangingi yao na shemeji zao. Twafile nyambara
 
ni aibu tupu
hata wanahabari ambao ndio tunawaamini nao wamezolewa na kimbunga hiki cha mafisadi wenye nchi, na kutuacha peke yetu sisi wananchi?
inasikitisha.
naamini sio wote.
 
Tumwamini nani? Tume , Lowasa au watetezi wake? Tafuta riport ya Mwakyembe.

tea niamalizia ushauri wako kwa kuwambia waisome kwa makini ripoti ya mwakyembe au la wataishia kulalama ktk vyombo vya habari.
NAJIULIZA HUU NI UJASIRI WA AINA GANI KUMTETEA MHALIFU AMBAYE BADO HATA AHAFUNGULIWA JALADA?? acheni vyombo vya serikali vifanye kazi kisha ndipo mkatoe ushahidi wenu wa kuwa huyu kaonewa na yule kafanyiwa halali
msinisukume nikaanza kufoka hapa, ebo!
 
Back
Top Bottom