Lowassa ana dhambi nyingine zaidi ya Richmond?

Kweli lowasa ni jembe na ni mtu mwenye ujasiri na msimamo ndio maana tunataka apokee hii nchi 2015 kwa sababu nchi imeyumba sana na uchumi umedorora sana kumbe ata nyerere alijua lowassa ana kiburi na ana msmamo​
 
Ccm fahamuni kuwa kumuweka lowasa kuwa mgombea wenu mjihesabu kushindwa katika uchaguzi mkuu ujao. Taarifa ndo hiyoo. Watanzania wameamka sanaa na dharau yeyote katika ukweli huu mmeanguka tena vibaya. Muache ushabiki wa mtu angalieni maslahi ya taifa kwanza. Tupo wengi ndani ya ccm tusiomuafiki lowasa hata kama anapesa nyingi za kutuhonga kama alivyokwishafanya kwenye wajumbe wengi wa nec ya ccm kiasi cha kila mmoja anamsubiria yeye tu. Mtu huyu hafai...ukweli ndo huo. Mmeze! Msimeze! Shauri yenu. Tafuteni watu makini wasimamie rasilimali za taifa letu walete upinzani wa dhati kutoka kwa upinzani. Mtu huyo akisimama kila mpiga kura aone kuwa anafaa na hana mawaa yoyote.
 
Mwenye data za ufisadi ni Samuel Sitta, Sitta akiongea mbingu zitafunguka. Ndio maana Mamvi anamwogopa Sitta kama mungu baba!!!
 
unakemea tabia ya kusema uongo wakati na wewe mwenyewe unaotumia huohuo????
Kweli Biblia imesema 'kila mtu anaongea uongo dhidi ya jirani yake'
 
We Ngamia,
Kwanza tuambie ni upi unafiki wa Kasori. Kaandika hapo facts, zisute. Lowassa hajachukua ranch ya taifa? Lowassa hajachukua majumba huko Arusha? Kwa nini Lowassa alikacha ule mkutano pale Msasani? Lowassa muongo, Lowassa mwizi, Lowassa hafai hata kuwa katibu kata katika serikali ya Tanzania. Hapo unafiki uko wapi? Unafiki ni ninyi ambao mnayaona madudu ya Lowassa lakini kwa sababu anawapa chochote au mnakula naye mnaona ni mtu anayefaa sana. Jibu hoja zake, siyo hii ya kuanza kuita mwingine kuwa mnafiki ili hali unafiki unajidhihirisha usoni mwako.
Lowassa anawaumiza sana CCM ,ukitaja tu neno au jina LOWASSA hadi Rais wa nchi anashtuka ,taasisi zinashtuka hivi ni kwa nn,inawezekana mti wenye matunda ndio unaopigwa mawe
 
Nikiwa kama mtanzania ninaetafakari juu ya hali ya siasa tz, ninasimama ktk ukweli kusema zaidi ya Richmond hakuna ruhwa yenye mashiko ya kumuhukumu roho ya paka Lowasa!

Mwenye ushahidi wa ufisadi mwingine wa Lowasa auweke hapa! Kama si zaidi ya propaganda za wapinzani wake kisiasa!
unaweza ukatengua kauli yako mkuu!!
 
Ccm fahamuni kuwa kumuweka lowasa kuwa mgombea wenu mjihesabu kushindwa katika uchaguzi mkuu ujao. Taarifa ndo hiyoo. Watanzania wameamka sanaa na dharau yeyote katika ukweli huu mmeanguka tena vibaya. Muache ushabiki wa mtu angalieni maslahi ya taifa kwanza. Tupo wengi ndani ya ccm tusiomuafiki lowasa hata kama anapesa nyingi za kutuhonga kama alivyokwishafanya kwenye wajumbe wengi wa nec ya ccm kiasi cha kila mmoja anamsubiria yeye tu. Mtu huyu hafai...ukweli ndo huo. Mmeze! Msimeze! Shauri yenu. Tafuteni watu makini wasimamie rasilimali za taifa letu walete upinzani wa dhati kutoka kwa upinzani. Mtu huyo akisimama kila mpiga kura aone kuwa anafaa na hana mawaa yoyote.

CCM waliusikiliza vyema ushauri wako.... Chama sikivu
 
1. Edward N. Lowasa, Mbunge wa Monduli kwa tiketi ya CCM na mjumbe wa mkutano mkuu wa halmashauri ya ccm,

Makosa:

Huyu ndie MWIZI wa WEZI nchini, anahusika na ufisadi katika mradi wa Richmond ambayo leo inaitwa Syimbion, ambayo leo inalipwa mamilioni na TANESCO,

Amelihujumu shirika la umeme nchini kwashinikiza shirika litegemee zaidi umeme wa mafuta badala ya kuendelea kuzalisha umeme wa maji ama gesi, hii imefuatia baada ya yeye kuwa na hisa kubwa katika makampuni makubwa ya uugizaji na usambazaji mafuta nchini

Kitendo hiki kimelisababishia Taifa ya hasara kubwa kupindukia ambapo SERIKALI inatumia BILIONI TANO kila jua linapozama kulipia umeme huo, huku TANESCO ikizalisha MILIONI KUMI na TANO kwa siku,

Lowasa huyo huyo akiwa ndie mwanahisa mkuu wa VODACOM TANZANIA kwakutumia ushawishi wake wa pesa ndani ya chama na serikali, ameweza kupenyeza nguvu yake katika Chama na serikali na kuwaambia chama lazima kijitafutie pesa kwaajili ya uchaguzi ujao 2015, hivyo kila MTANZANIA ni lazima achangie chama kupitia KODI ya SIMU,

Wabunge wa ccm wote wamekubaliana na wazo hilo na hata baadhi ya wataalamu wa kodi na biashara nchini wasiojua mchezo wamekubali bila kujua bibi yangu Maseto kule Nyololo simu yake huwa inaisha hata miezi sita bila kuweka vocha hata ya miatano tu,

Ni Lowasa huyuhuyu sasa anatumia wanaccm kuvuruga mchakato wa katiba mpya, anatumia kila hila kuvuruga na kuwagawa wanaccm, amewarubuni wanachama wa ccm wale wenye maruhani zaidi kwakuwaahidi kuwa yeye atakuwa Rais na atawapa vyeo hivyo wanamsikiliza hata akimeza mate tu,

Huyo ndie Lowasa ambae nzi akitua usoni pake wanaccm wanagombania kwenda kumuua nzi huyo,

Hivyo mamlaka ya m/kiti na Rais wa Nchi yangechukua mkondo wake kwa kumfukuza uanachama na kumpeleka gereza kuu ISUPILO,

Abdallah Bulembo,

Huyu amekuwa mstari wa mbele kuvuruga mchakato wa katiba mpya na anatumiwa na Lowasa kama kipaza sauti muhimu mithiri ya spika za minanda,

Vile vile amemudhihaki m/kiti wa chama na rais wa Jamhuri ya Muungano

Hivyo mamlaka ya m/kiti na Rais wa Nchi yangechukua mkondo wake kwa kumfukuza uanachama na kumpeleka gereza kuu LILUNGU,


Steven Wassira,

Huyu ni MFUASI wa LOWASA na amejipanga kutokea Ikulu akihakikisha kuwa anamyumbisha Rais Jakaya Kikwete na kuona nchi haitawaliki kwa amani kabisa,

Tangu awe waziri amekuwa ni mtu wakupingana na mkuu wake wa kazi tu, akijifanya anapambana na upinzani kumbe kinyume chake anaihujumu serikali ya Jakaya kikwete,

Huyu ni mhaini ambaye anastahili kuwajibishwa kihaini kama ilivyo ada ya wahaini,

Hivyo mamlaka ya m/kiti na Rais wa Nchi yangechukua mkondo wake kwa kumfukuza uanachama na kumpeleka gereza kuu LUANDA,


Mathias Chikawe,

Ni mtovu wa nidhamu, amemuhujumu Rais waziwazi bila aibu akimtishia kuwa asipo saini mswaada wa sheria ya katiba mpya atakuwa anatangaza "vita" na Bunge, hilo tu linatosha kusema huyu ni MHAINI mkubwa aliyesimama mbele ya kamera za nchi na kumkanya rais,

Hivyo mamlaka ya m/kiti na Rais wa Nchi yangechukua mkondo wake kwa kumfukuza uanachama na kumpeleka gereza kuu UKONGA,


Job Ndugai

Huyo ni kibaraka wa Lowasa, huyu anatumika kuruga bunge na kuihujumu ccm, matukio yanayojitokeza wakati yeye akiongoza Bunge nanampeleka moja kwa moja kwenye makosa ya uhaini,
Hivyo mamlaka ya m/kiti na Rais wa Nchi yangechukua mkondo wake kwa kumfukuza uanachama na kumpeleka gereza kuu CHUMVINI,



William Lukuvi

Huyu anainajisi serikali kwakuendesha mauaji nchini kwakutumia jeshi la polisi,

Kauli zake bungeni kuwa wapinzani wanajilipua wao na mabomu na matokeo ya polisi kufikishwa mahakamani kwa makosa ya mauaji vinamwangushia moja kwa moja kwenye makosa ya uhaini na kutaka kuiangusha serikali ya Jakaya Kikwete,

Hivyo mamlaka ya m/kiti na Rais wa Nchi yangechukua mkondo wake kwa kumfukuza uanachama na kumpeleka gereza kuu KITAI,

Mwigulu Lameck Nchemba,

Huyu ndie GAIDI namba moja nchini,

Nikibaraka wa Lowasa, huyu anafanya kazi ya uasi chini ya Lukuvi, akisimamia vikundi vya mauaji viitwavyo GREEN GURD,

Amefanya mauaji Igunga, Arumeru, Soweto, Morogoro na Iringa,

Mauaji haya yameiyumbisha serikali ya ccm na kuhatarisha uhai wa Rais wa jamhuri ya Muungano,

Amekua akiendesha mauaji ya viongozi wa dini zote mbili nchini na kusingizia kuwa kuna uhasama wa kidini,

Hivyo mamlaka ya m/kiti na Rais wa Nchi yangechukua mkondo wake kwa kumfukuza uanachama na kumpeleka gereza kuu BUTIMBA,


William John Malecela

Huyu ni kibaraka asiyejua anamwadu nani katika ccm, yeye yupo nyuma ya Bulembo kama waleti, anafanya uhaini mitandaoni kwa kueneza mgawanyiko ndani ya ccm na serikali yake,

Hivyo mamlaka ya m/kiti na Rais wa Nchi yangechukua mkondo wake kwa kumfukuza uanachama na kumpeleka gereza kuu KIMBIJI,


Licha ya kumpongeza mh rais kwa kugundua njama za wahaini hawa na kurudisha mswada bungeni, ninamshauri achukue hatua madhubuti kama nilivyopendekeza hapo au zaidi,

CCM bila hao hapo juu inawezekana tu,
Tanzania bila ccm inawezekana tu!
 
Back
Top Bottom