Lowassa amtwisha zigo waziri nundu

Noti mpya tz

JF-Expert Member
Mar 23, 2011
974
244

search0.png

Sat 26 Mar 2:37PM









rss.png

RSS







Home
arrow.png
Habari
arrow.png
Habari za Siasa
arrow.png
Lowassa amtwisha zigo Waziri Nundu


BOOKMARK THIS PAGE




.buttonheading { float: right; padding-left: 19px; width: 92px; }.buttonheading a { font-weight: bold; text-decoration: none; }
bot_tabimg.gif

Lowassa amtwisha zigo Waziri Nundu Send to a friend Saturday, 26 March 2011 10:02 0diggsdigg

Patricia Kimelemeta
KAMATI ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, imemtaka Waziri wa Uchukuzi, Omary Nundu, kuwasilisha barua ya kupinga ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa eneo la Taveta, Kenya kwa sababu umekiuka mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Hatua hiyo imefikiwa baada kamati hiyo jijini Dar es Salaam jana, kujadili suala la Ulinzi na Usalama kupitia Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, alisema kitendo cha Kenya kujenga kiwanja hicho karibu na Uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia), ni kwenda kinyume na mkataba wa EAC na Tanzania haijatendewa haki.

“Kwa mujibu wa kanuni za Bunge, namtaka Waziri wa Uchukuzi, kuwasilisha pingamizi kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki kupinga ujenzi wa kiwanja cha ndege, kwa sababu umekiuka sheria na taratibu za makubaliano,” alisema Lowassa. Aliongeza kuwa eneo hilo kuna kiwanja cha Kia, hivyo huwezi kufanya uwekezaji wa aina moja eneo hilo na kwamba, hiyo sawa na kuvunja makubaliano hayo suala linaloweza kuzusha mgogoro.

Lowassa alisema kutokana na hali hiyo, waziri anatakiwa kuwasilisha taarifa yake kwenye kamati hiyo atakapotekeleza agizo hilo, ili wajumbe wa kamati na wabunge wa EAC waweze kupata taarifa.

Kutokana na hali hiyo, kamati hiyo inatakiwa kusubiri taarifa kutoka kwa waziri nwenye dhamana ili kuendelea na hatua stahiki ya pingamizi hilo. Akichangia hoja, Mjumbe wa kamati hiyo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Maswa, John Shibuda, alisema serikali isipokuwa makini kwenye suala hilo, Tanzania itakuwa jamvi la wageni.

“Tanzania ni jamvi la wageni sasa, watu wanatoka huko waliko na kukimbilia huku, niwaambie laiti hayati Mwalimu Julius Nyerere angekuwa hai, angetuchapa viboko kwa sababu sisi ndio tunaotetea maslahi ya wananchi wetu, lakini ndio wa kwanza kukubali mambo kama haya,” alisema Shibuda.

Hata hivyo, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, alisema wizara yake inatengewa bajeti ndogo ambayo inafanya washindwe kutekeleza majukumu hayo ipasavyo. “Bajeti iliyopita ya wizara ni Sh3 bilioni, ambazo huwezi kufanya shughuli yoyote ile ikilinganishwa na wizara yenyewe ni nyeti, kutokana hali hiyo tunaomba serikali kupitia kamati hii iweze kutuongezea fungu,” alisema Sitta. Mwisho
 
Back
Top Bottom