Lowassa akiwa Rais...

nyerere anavyosema hivyo kua mtu anatumia pesa ili kuingia ikulu of coz u have to spend money kama unataka kua Rais waulize akina obama/romney watakuambia jinsi wanavyotumia hela nyingi ili wapate kura za wananchi...tatizo la hapa bongo sio lowasa au viongozi wengine bali ni wananchi..mwananchi ukipewa baiskeli ukakataa au ukipewa kanga au shs 10000 ukakataa basi hamna mtu atakae honga...
 
Maadam wanaomchagua rais wa Tanzania ni Watanzania wenyewe na sio hao watu wa nje, na rais huyo atakayechaguliwa ni rais wa Tanzania na sio rais wa hao watu,
then haya ni mambo yetu ya ndani, hayaruhusiwi kuhojiwa na yeyote ambaye sio Mtanzania!, hayamhusu!.

Watu wasimshangae Al Bashir mwenye arrest warrant ya ICC au Uhuru Kenyatta aliyepo kizimbani!?. Washangae nini kwa EL?!, kwa kosa gani?!,

Kama ni rushwa ndani ya CCM, its the order of the day!. Hata JK amekiri wazi kukerwa na matumizi ya rushwa nje nje na wazi wazi kwenye uchaguzi wa jumuiya za CCM as dhaifu as he is, he did nothing zaidi ya kuelezea kukwerwa!. Kama ni kweli wanachotaka wana CCM ni pesa!, na EL anayo hiyo pesa na kawapa!, then he is the best CCM has!.

Kama walichotaka CCM ni reflection ya wanachotaka Watanzania!, then come 2015, Watanzania watapatiwa na wenyenacho kile wanachokitaka na watawapatia hao wenye nacho asante wanayoitegemea na itakuwa kama inavyotakiwa kuwa!. Nawahurumia sana wasio nacho!, uchaguzi 2015 sio wa Mkono mtupu!.
P.
 
Naungana na mchangiaji hapo juu kuwa CCM yote ni wala rushwa tu japo nasikia wapo waadilifu wachache ila sijui wanafanya nini katikati ya kundi la mbwa mwitu,tumemsikia Mh. Sumaye, tumemsikia Mh.Rais na wengine wengi tu ndani ya CCM wakilalamikia rushwa, lakini kinachotushangaza ni kuwa wengi wanalalamika baada ya kuwa wameshindwa katika chaguzi mbalimbali, enzi ya Mh Mkapa ukisema sana unaambiwa una wivu wa kike na mimi leo nikisikia mtu ndani ya CCM analalamika eti kwa sababu kashindwa uchaguzi basi namuona ana wivu wa kike.

Kinachonifurahisha juu ya bwana mkubwa EL ni kuwa sijawahi hata siku moja kumsikia akilalamikia rushwa ndani ya chama chake (ninaweza kusahihishwa) sasa huwa najiuliza yeye mwenzetu vp, haioni au yeye hana wivu wa kike kama wenzake?

Kinachofanya LOWASA kutaka kwenda ikulu kwakeli anakijua mwenyewe labda na mkewe au kama kuna mwingine anayejua aje atuambie, maana jamaa ana kila sababu ya kuchunguzwa na kuhojiwa na TAKUKURU au hata USALAMA WA TAIFA IKIBIDI lakini nani atathubutu hata kumuita kumuuliza kitu, na hii yote ni kwasababu wanasutwa na ule msemo wa BWANA YESU ASIYE NA DHAMBI AWE WA KWANZA KUTUPA JIWE wandugu, ndani ya CCM sijamuona msafi, kama wapo wasafi basi wana kasoro na kasoro yao ni ulafi kwani wanashindwa kukemea rushwa ili matunzo kutoka SERIKALINI yaendelee.

Kuhusu marais huko nje watamwangaliaje, my friend! viongozi wa AFRICA hawana soni na hii ndio inafanya kila mtu katika AFRICA anataka urais, maana unajiuliza kama fulani kaweza mimi nashindwa nini? wanajuana, na kwavile WANANCHI na sisi tuna hizo chembe chembe za rushwa katika damu basi tunafurahia khanga, kofia na ubwabwa wa leo wa kesho utajiseti wenyewe, si tunaona hata hapa JF watu wanavyotokwa na mapovu kumtakatisha LOWASA.
 
Duh! na wewe ndiye uliyewahi kuandika hapa jamvini siku chache zilizopita kwamba ni Mzalendo ambaye unataka kutetea maslahi ya nchi na si mfuasi wa chama chochote kile cha siasa. Halafu unaandika ***** kama huu!!! Mtanzania mzalendo kamwe hawezi kuandika pumba kama hizi kuelekea katika uchaguzi wa 2015. Kweli njaa mbaya sana!!! unaweza kumuuza hata mzazi wako ili kuganga njaa!!!

Maadam wanaomchagua rais wa Tanzania ni Watanzania wenyewe na sio hao watu wa nje, na rais huyo atakayechaguliwa ni rais wa Tanzania na sio rais wa hao watu,
then haya ni mambo yetu ya ndani, hayaruhusiwi kuhojiwa na yeyote ambaye sio Mtanzania!, hayamhusu!.

Watu wasimshangae Al Bashir mwenye arrest warrant ya ICC au Uhuru Kenyatta aliyepo kizimbani!?. Washangae nini kwa EL?!, kwa kosa gani?!,

Kama ni rushwa ndani ya CCM, its the order of the day!. Hata JK amekiri wazi kukerwa na matumizi ya rushwa nje nje na wazi wazi kwenye uchaguzi wa jumuiya za CCM as dhaifu as he is, he did nothing zaidi ya kuelezea kukwerwa!. Kama ni kweli wanachotaka wana CCM ni pesa!, na EL anayo hiyo pesa na kawapa!, then he is the best CCM has!.

Kama walichotaka CCM ni reflection ya wanachotaka Watanzania!, then come 2015, Watanzania watapatiwa na wenyenacho kile wanachokitaka na watawapatia hao wenye nacho asante wanayoitegemea na itakuwa kama inavyotakiwa kuwa!. Nawahurumia sana wasio nacho!, uchaguzi 2015 sio wa Mkono mtupu!.
P.
 
nyerere anavyosema hivyo kua mtu anatumia pesa ili kuingia ikulu of coz u have to spend money kama unataka kua Rais waulize akina obama/romney watakuambia jinsi wanavyotumia hela nyingi ili wapate kura za wananchi...tatizo la hapa bongo sio lowasa au viongozi wengine bali ni wananchi..mwananchi ukipewa baiskeli ukakataa au ukipewa kanga au shs 10000 ukakataa basi hamna mtu atakae honga...

Usitake kuhalalisha uozo wa mfumo wa marekani na ule wa kwetu kisa kutaka EL aonekane hana shida. Kama ndiyo hivyo, tangazeni pia kuwa ushoga halali tz, kwani Obama kashasema hivyo.
Mwl.Nyerere aliposema tuwaogope watu sampuli ya EL alijua Kuwa Marekani wanatumia pesa kukampeni na sio kuhonga. Tena wenzetu kule vyanzo vya fedha zao viko wazi. Je, vyanzo vya fedha anayotumia EL viko wazi?
 
nimefurahi sana kugundua kuwa kumbe huyu bwana huenda kweli akawa Raisi ajae, Maana Membe sioni akizungumziwa, Kila siku EL, Inaonyesha anamvuto wa kisiasa.
 
Lowassa afya yake inampa matatizo ataweza hayo ya kuzuia rushwa?

Huyu mheshimiwa ataachia mwenyewe, sio mchezo kila mwezi Ujerumani.

Fikirieni magamba wengine kama kushinda kwenyewe ni kwa "kishindo".

CCM hawazungumzii kura,wanasema "tutashinda kwa kishindo".

CCM, CCM inatuzingua wadanganyika.
 
Watanzania tukumbuke maneno ya mwalimu Nyerere (nadhani alikuwa nabii pia,sijui) kwamba mtu anayetumia fedha kutaka kwenda ikulu mtu huyo niwa kumwogopa kama ukoma. Watanzania tumwogope EL kama ukoma. Tumesoma, tumesikia na wengine tumeona jinsi jamaa anavyotumia fedha kutaka kwenda ikulu. Ikulu panapaswa kuwa patakatifu...na pasafishwe pawe hivyo. Pale siyo pango la wanyang'anyi.

Ikitokea tukamchagua EL kuwa prezidaa wa TZ, watu huko nje watauliza hivi hawa jamaa hawakuwa na mtu mwingine isipokuwa huyu? Yamkini watu wa taifa hilo ni walamba rushwa walioshindikana.Hakuna mwenye nafuu. (unafahamu hata katika kundi la wapumbavu lazima awepo kiongozi) kwa hiyo, itakuwa kiongozi wa wala rushwa ni huyu, duh! Sipati picha.

Siku akikemea rushwa na ufisadi itabidi avae miwani ya mbao. Kwa kweli atakuwa hana budi kuvaa miwani ya mbao.

Akiwa kamam mwenyekiti wa kamati ya bunge ya usalama hajawahi kutoa kauli yoyote kuhusu mauaji ya kiholela Sorry! yaliopangwa dhidi ya raia, kwa kifupi hata wazo la yeye kugombea urais mi naona tulichukulie kama jinai
 
Duh! na wewe ndiye uliyewahi kuandika hapa jamvini siku chache zilizopita kwamba ni Mzalendo ambaye unataka kutetea maslahi ya nchi na si mfuasi wa chama chochote kile cha siasa. Halafu unaandika ***** kama huu!!! Mtanzania mzalendo kamwe hawezi kuandika pumba kama hizi kuelekea katika uchaguzi wa 2015. Kweli njaa mbaya sana!!! unaweza kumuuza hata mzazi wako ili kuganga njaa!!!
Mkuu BAK, hili la njaa, nakubaliana na wewe, ni kweli njaa mbaya!. Ila pia nasisitiza kuwa niko kwa maslahi ya taifa na nina tatizo moja kubwa!, wengi humu jf ni wishful thinkers!, mimi ni realist, nikisema ukweli daima, no matter how ukweli huo ni mchungu, siupaki siagi na jam ili uwe mtamu!.
  1. Jee ni uongo kuwa Watanzania ndio wanaipenda rushwa na kuikumbatia?!.
  2. Jee kuna ubishi kuwa Watanzania walio wengi ni masikini wa kutupwa?!.
  3. Jee ni uongo kuwa rushwa its the order of the day kwenye uchaguzi wa CCM?!
  4. Jee ni uongo kuwa JK did nothing kuhusu rushwa ndani ya CCM zaidi ya kuelezea kukerwa kwake?!.
  5. Jee ni uongo kuwa wanaogaiwa pesa za rushwa, wanazifurahia na kumpigia kura mtoaji?!.
  6. Jee ni uongo kuwa hicho ndicho Wapiga kura wa Tanzania wanachokitaka?!.
  7. Jee ni uongo kuwa serikali ya CCM imetenga Sh. Bilioni 400 za ruzuku ambazo watazigawa kwa wananchi?!.
  8. Jee wananchi hao baada ya kugaiwa fedha hizo, hawataishukuru serikali yao kwa kuwajali?!.
  9. Jee shukrani hizo hazitakuwa reflected kwenye matokeo ya uchaguzi wa 2015?!.
  10. Jee ni uongo kuwa mimi nina waandaa members humu kwa ushindi wa CCM, 2015 ambao ndio reality hivyo kujikuta wako tayari wameandaliwa kisaokolojia kukubali matokeo!, kuliko kuwaacha wakiwa na "wishful thinking" za "great expectations kuwa 2015 mambo yatabadilika", na ikitokea mambo yake yale, watu wale wale, na chama kile kile, si wangeishia kwenye despair, frustrustion na psychoilogigal depression?!.

Kama hoja zozote kati ya hizo ni uongo, then nipinge kwa hoja na sio kuniita "mganga njaa" tuu!.
P.
 
Mkuu BAK, hili la njaa, nakubaliana na wewe, ni kweli njaa mbaya!. Ila pia nasisitiza kuwa niko kwa maslahi ya taifa na nina tatizo moja kubwa!, wengi humu jf ni wishful thinkers!, mimi ni realist, nikisema ukweli daima, no matter how ukweli huo ni mchungu, siupaki siagi na jam ili uwe mtamu!.
  1. Jee ni uongo kuwa Watanzania ndio wanaipenda rushwa na kuikumbatia?!.
  2. Jee kuna ubishi kuwa Watanzania walio wengi ni masikini wa kutupwa?!.
  3. Jee ni uongo kuwa rushwa its the order of the day kwenye uchaguzi wa CCM?!
  4. Jee ni uongo kuwa JK did nothing kuhusu rushwa ndani ya CCM zaidi ya kuelezea kukerwa kwake?!.
  5. Jee ni uongo kuwa wanaogaiwa pesa za rushwa, wanazifurahia na kumpigia kura mtoaji?!.
  6. Jee ni uongo kuwa hicho ndicho Wapiga kura wa Tanzania wanachokitaka?!.
  7. Jee ni uongo kuwa serikali ya CCM imetenga Sh. Bilioni 400 za ruzuku ambazo watazigawa kwa wananchi?!.
  8. Jee wananchi hao baada ya kugaiwa fedha hizo, hawataishukuru serikali yao kwa kuwajali?!.
  9. Jee shukrani hizo hazitakuwa reflected kwenye matokeo ya uchaguzi wa 2015?!.
  10. Jee ni uongo kuwa mimi nina waandaa members humu kwa ushindi wa CCM, 2015 ambao ndio reality hivyo kujikuta wako tayari wameandaliwa kisaokolojia kukubali matokeo!, kuliko kuwaacha wakiwa na "wishful thinking" za "great expectations kuwa 2015 mambo yatabadilika", na ikitokea mambo yake yale, watu wale wale, na chama kile kile, si wangeishia kwenye despair, frustrustion na psychoilogigal depression?!.

Kama hoja zozote kati ya hizo ni uongo, then nipinge kwa hoja na sio kuniita "mganga njaa" tuu!.
P.

  1. Nakubaliana kiasi na hoja zako. Ila najiuliza sasa. Je, si mpango mahususi wa CCM kuwafanya watz wawe maskini daima ili wautumie umasikini huo kuwanunua?
  2. Je, si kweli kwamba tangu uhuru TANU na baadaye CCM na serikali zake waliamua kutofundisha "Katiba ya Nchi" na badala yake wakafundisha katiba ya chama ili kuwapumbaza watz wasijue mamlaka yao kama waajili wa serikali?
 
Watanzania tukumbuke maneno ya mwalimu Nyerere (nadhani alikuwa nabii pia,sijui) kwamba mtu anayetumia fedha kutaka kwenda ikulu mtu huyo niwa kumwogopa kama ukoma. Watanzania tumwogope EL kama ukoma. Tumesoma, tumesikia na wengine tumeona jinsi jamaa anavyotumia fedha kutaka kwenda ikulu. Ikulu panapaswa kuwa patakatifu...na pasafishwe pawe hivyo. Pale siyo pango la wanyang'anyi.

Ikitokea tukamchagua EL kuwa prezidaa wa TZ, watu huko nje watauliza hivi hawa jamaa hawakuwa na mtu mwingine isipokuwa huyu? Yamkini watu wa taifa hilo ni walamba rushwa walioshindikana.Hakuna mwenye nafuu. (unafahamu hata katika kundi la wapumbavu lazima awepo kiongozi) kwa hiyo, itakuwa kiongozi wa wala rushwa ni huyu, duh! Sipati picha.

Siku akikemea rushwa na ufisadi itabidi avae miwani ya mbao. Kwa kweli atakuwa hana budi kuvaa miwani ya mbao.
Mkuu mimi nasema katika katiba mpya kuwe na kipengele cha maadili kuwa mtu yeyote aliyepata kuwa na kashifa ya rushwa, kukosa maadili asipendekezwe na chama chochote kugombea uraisi!!! Tena basi iundwe tume maalumu ya kitaifa ya kuchunguza uadilifu wa kila kiongozi na wanaotaka kuwa viongozi!! Integrity special commission for vetting all the government CEOs from all institutions must be formed in the new constitution!!!

 
Atahalalisha rushwa na kuijengea hoja iingie kwenye katiba mpya!
 

Usitake kuhalalisha uozo wa mfumo wa marekani na ule wa kwetu kisa kutaka EL aonekane hana shida. Kama ndiyo hivyo, tangazeni pia kuwa ushoga halali tz, kwani Obama kashasema hivyo.
Mwl.Nyerere aliposema tuwaogope watu sampuli ya EL alijua Kuwa Marekani wanatumia pesa kukampeni na sio kuhonga. Tena wenzetu kule vyanzo vya fedha zao viko wazi. Je, vyanzo vya fedha anayotumia EL viko wazi?
Mkuu hata Marekani wamechoka rushwa, chukua mfano wa one dolla kampain ya Obama walimwezesha kwa fedha zao akaingia ikulu mtoa rushwa labda republican Mitt Romney!!!

 
Mkuu hata Marekani wamechoka rushwa, chukua mfano wa one dolla kampain ya Obama walimwezesha kwa fedha zao akaingia ikulu mtoa rushwa labda republican Mitt Romney!!!

Wenzetu wanatawaliwa na sheria zinazombana mgombea kutumia fedha halali katika siasa. Tumeona mawaziri wakuu na marais huko wakiwajibishwa ama kwa kupata fedha kifisadi ili kuzitumia katika kampeni zao kisiasa. Je, hatuwezi kufanya kama wao?Mfano mzuri, hata CCM wanadai kuwa wagombea wa nafasi mbalimbali ndani ya chama watakaobainika kutumia rushwa katika kampeni watachukuliwa hatua za kinidhamu. Hatuoni hayo yakitendeka.
 
SALAAM KWA MH. EDWARD LOWASA NA WENZAKE KUHUSU KUSEMA UKWELI (TRUTH) NA SUALA ZIMA LA UADILIFU NA UWAJIBIKAJI WA VIONGOZI TANZANIA

Nimemsoma Askofu Mokiwa kuhusu uadilifu na uwajibikaji wa viongozi wa serikali. Nianze kwa nukuu ya Sir Francis Bacon; samahani kwa kuileta kwenu kwa kiingereza, One of the schools of the Grecians, examines the matter of Truth and is at a stand to think what should be in it, that men should love lies, where neither they make for pleasure, as with poets, nor for advantage, as with the merchants but it is for the lies sake.
TRUTH is a naked and open daylight that does not show the masks, and mummeries and triumphs, of the world half so stately and daintily as could lights. Truth may perhaps come to the price of a pearl, that shows best by day but it will not rise to the price of a diamond or carbuncle, that shows best in varied lights. A mixture of a lie does ever add pleasure…Truth is the sovereign good of human nature.

The first creature of God, in the works of the days was the light of the sense; the last was the light of reason and his Sabbath work ever since is the illumination of his Spirit. First he breathed light upon the fore of the matter or chaos, then he breathed light into the fore of man and still he breathes and inspires light into the face of his chosen. It is a pleasure , to stand upon the shore and to see ships tossed upon the sea, a pleasure to stand in the window of castle and to see a battle, and the adventures thereof below. “But no pleasure is comparable to standing upon the Vantage ground of TRUTH (a hill not to be commanded and where the air is always clear and serene) and to see the ERRORS, wanderings, and mists, and tempests in the valley below, so always that this prospect be with pity and not with swelling or pride. Certainly, it is heaven upon earth, to have a man’s mind more in charity, rest in providence and turn upon the POLES OF TRUTH.”
To pass from theological and philosophical truth, to the truth of civil business, it will be acknowledged, even by those who do not practice it, that clear and sound dealing, is the honor of man’s nature; and that mixture of falsehoods, is like a alloy in coin of gold and silver, which may make the metal work the better but it embaseth it. For those winding and crooked courses, are the goings of the serpent, which goes barely upon the belly and not upon the feet. There is no vile , that does so cover a man with SHAME as to be found FALSE and PERTIFIDIOUS”. Mwisho wa kunukuu.

Naam, tazama ahadi ya 8 ya mwanachama wa CCM, inasema, “ NITASEMA KWELI DAIMA, FITINA KWANGU MWIKO” mwisho wa kunukuu.
Ndugu zangu waheshimiwa wote waliotajwa katika sakata la Richmond napenda wasome kwa kurudia mara kadhaa nukuu hiyo niliyoanza nayo hapo juu katika mstakabali mzima wa kutukuza kwa unyenyekevu kitu kinaitwa kusema UKWELI (TRUTH). Wahenga walisema UKWELI UNAUMA. Ni vizuri tu wote tukakubaliana hivyo. Huo ndio ustaarabu. Ndio utu kusema ukweli. Tuhuma hizo nzito zinazowakabili wakizijibu pasipo kukiri kitu kinaitwa UKWELI na badala yake wakaendekeza majigambo , uwongo na tukafanya hivyo mahali pasipo husika hawalitakii Taifa letu la Tanzania mema. Katika hili hawatakiwi kutumia jaziba au hasira. Tena wakumbuke kuwa Mh. Edward Lowasa, na Karamagi na Msabaha walipewa nafasi halali Bungeni. Pale walichokifanya kwa bahati mbaya walitawaliwa na jazba na hasira “ ANGER ”. Ndugu zangu, kuhusu hasira naomba niwaase kama mtaalam mmoja kwa jina SENECA alivyosema kuwa ukikumbwa na hasira (samahani kwa kunukuu kwa kiingereza)“there is no other way but to meditate and ruminate well upon the effects of anger, how it troubles man’s life. The best time to do this is to look back upon anger when the fit is thoroughly over. Anger is like ruin, which breaks itself upon that, it falls. The scripture teaches us to possess our souls in patience. Whosoever is out of patience is out of possession of his soul. Men must not turn bees” Mwisho wa kunukuu.

Katika makala yangu iliyopita Salaam kwa Mawaziri wa Mhe. J.Kikwete kuhusu uadilifu na uwajibikaji kwa sehemu kubwa nilizungumzia juu ya mawaziri bila kumtaja Mheshimiwa Edward Lowasa. Mb wa Monduli. Kwa haya aliyoyafanya baada ya kuomba kwa Spika Bungeni na kupewa nafasi ya kwanza ajieleze kuhusu ufisadi wa Richmond, namtafadhalisha asome na kurudia mara kadhaa nukuu niliyoanza nayo hapo juu sambamba na hiyo ya mtaalamu SENECA. Napenda niseme kuwa kwa yale aliyosema Bungeni na Monduli na katika mahijioano ya TVT, bwana Lowasa nasema “si mkweli hata chembe moja”. Waandishi wa habari wengu tu wamekwisha mchambua kwa usahihi jinsi asivyokuwa mkweli, asivyo muadilifu anavyopenda kusifiwa kwa gharama yoyotena asivyolitakia mema Taifa letu. Narudia, asome kwa utulivu nukuu zote mbili nilizoanza nazo hapo juu. Kama Mwanasheria Mkuu, Mwanyika na wenzake Lowassa hakuridhika na ushauri wao juu ya Richmond na kuona kuwa ulikuwa na madhara kitaifa, kwanini hakutafuta ushauri wa ziada? Je? Hizo ndizo rasilimali watu pekee nchini katika ushauri wa kiserikali? Je, Vyuo Vikuu na Mahakama Kuu hakuna wataalam wa kisheria wa kuisaidia serikali? Did he leave any stone un-turned?

Kwa mapenzi mema na nchi yetu na mwana (CCM) napenda niwape mfano hai wa Bwana Lowasa asivyo muadilifu na asivyopenda kuwajibika kichama CCM na kiserikali. Tanzania nzima mtakumbuka kuwa huyu mheshimiwa Edward Lowasa alikuwa ni mmoja wa wagombea wa nafasi ya Urais mwaka 1995 na akaenguliwa kwa hoja nzito ya kutokuwa muadilifu na marehemu Baba wa Taifa Mwalimu J.K. Nyerere, kwa ukweli (wala sio tuhuma) kuwa alikuwa amejilimbikizia mali nyingi kwa kipindi kifupi ndani ya CCM na Serikali.Muda mfupi alikuwa ni mtumishi wa CCM, muda mfupi kama Mkurugenzi wa kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha.

Mfano hai wenyewe uko hivi; tufuatane kwa kuusoma tafadhali:-
Mara baada ya kurudi Butiama, 1995, baada ya kuenguliwa kugombea nafasi ya urais, siku moja mapema asubuhi Bwana Lowasa alonipigia simu na kusema yafuatayo: “Bwana Kasori, naomba uende kumwambia Baba wa taifa Mwalimu Julias Kambarage Nyerere, aende Monduli kusaidia kusafisha jina langu ili nisikose ubunge kutokana na yale aliyonisema Dodoma”. Nilishikilia mkono wa simu (TTCL) kwa zaidi ya nusu saa tukiwa tunazungumza na hatimaye mimi nilipata ujasiri wa kumwambia Bwana Lowasa kuwa siwezi kwenda kusema maneno hayo kwa Baba wa taifa na kwamba akitaka aje Butiama na nitamruhusu waongee ana kwa ana. Nikanyamaza na hatimaye yeye akawa wa kwanza kukata simu. Hiyo ikawa itifaki njema kwangu!

Kesho yake tena asubuhi nilipokea simu, safari hii akawa ni mheshimiwa Mzee Rashidi Mfaume Kawawa. Kwa maneno yake alisema “Bwana Kasori,jana ulizungumza na Edward Lowasa; naomba ufikishe ombi lake kwa Baba wa taifa tafadhali”. Kutokana na heshima ya Mheshimiwa Mzee Kawawa, nilikubali na nikaenda na kabla ya hapo nilimuomba Mzee Kawawa akae karibu na simu ili nimpe jibu muda si mrefu.

Nilimueleza Baba wa Taifa kuwa “Mheshimiwa Edward Lowasa kupitia kwa Mhe. Mzee Rashidi Mfaume Kawawa anaomba usaidie kusafisha jina lake kule jimboni kwake Monduli ili asikose ubunge kutokana na yale uliyomsema katika Kamati Kuu ya CCM Dodoma”. Jibu la Baba wa Taifa alilonipa ni kuwa “Nenda umwambie Mzee Rashidi Mfaume Kawawa asiwe mjinga kama Lowasa”!

Watanzania wote, leo March19, 2008, nawaomba radhi kuwa jibu hilo kwa uzito wa maneno hayo kuwa “Kawawa asiwe mjinga kama Lowasa” kweli kwa kuzingatia heshima kati ya wazee hao wawili; “Kawawa sikumwambia hivyo”! Badala yake nilimdanganya (nawaomba radhi tena watanzania) jibu nililompa Mzee Kawawa ni kuwa juma lililokuwa linafuata tungekuwa Dar es Salaam na kwamba aje Msasani aongee na Baba wa Taifa. Mhe. Kawawa alikubali. Nikarudi kwa Baba wa taifa kusema uongo (naomba radhi tena) kuwa “Mzee Kawawa ameomba mzungumze tatizo la Lowasa tutakapofika Dar es Salaam”. Baba wa taifa alikubali na akaagiza nimuombe Mhe. mzee Kawawa kuwa Lowasa na Guninita na wapambe wengine wa Lowasa wote wafike Msasani.

Siku ya siku ikafika. Tukawepo Msasani na Mhe.mzee Kawawa akaja. Lowasa hakuwepo! Sababu anazijua mwenyewe.(muulizeni maana nasema ukweli). Mkutano ulipoanza mzungumzaji wa kwanza nikawa mimi, kueleza lengo la mkutano. Mzungumzaji wa pili alikuwa Baba wa Taifa na swali la kwanza ni kuuliza Lowasa yuko wapi?. Bila kupoteza wakati Mwalimu alisema “Rashidi , huyu Kasori ananiambai eti niende Monduli nikasafishe jina la Mhe. Lowasa eti asikose ubunge kwamba nilimchafulia Dodoma katika Kikao cha Kamati Kuu ya CCM. Kutokana na ombi lako nilimtuma akuambie usiwe mjinga kama Lowasa. Kasori alikuambia eh?”. Oneni , huko nyuma tayari nilishasema uongo kwa kutosema maneno hayo kwa Mhe. mzee Kawawa. Kweli hilo kurudiwa na Baba wa Taifa kwa Mzee Kawawa mbele yangu lilisababisha kalamu yangu kuanguka, nikatetemeka na nikatokwa na jasho jingi mbele ya hao wazee!!! Bila kutegemea na kwa mshangao mkubwa Mhe. mzee Kawawa alikubali kwa kuitikia “NDIO ALINIAMBIA”. Mwalimu akacheka sana!!!! Sababu sijui hadi leo kwa nini alicheka sana.

Kwa kuendelea, Mwalimu alimwambia Mzee Kawawa kuwa “Kasori ana umri mkubwa kuliko Lowasa. Kasori alipata taabu sana kufikisha kwangu ombi la Lowasa na aliniambia kuwa jana yake alikuwa amekataa ombi la Lowasa. Sasa nasema kuwa kwa umri wangu mimi mzee, Lowasa ni mtoto wangu tena mdogo sana. Kwa heshima mliyonayo kwangu na kwa chama cha Mapinduzi mtanishangaa sana mkisikia niko Monduli eti nipo kwenye majukwaa nasafisha jina Bwana Lowasa asikose ubunge. Kweli Lowasa ni jasiri sana kusema maneno hayo. Hayo ningeambiwa na Kasori tu ningesita kumuamini. Lakini kwamba hata wewe Rashidi ulitumiwa kusema maneno hayo! Huyu Lowasa ni jasiri sana!!. Lakini kwa nini hajatuambia ukweli kuhusu mali hizo ambazo ni nyingi kuliko mimi ambaye nimekuwa Rais wenu kwa kipindi kirefu? Sasa Bwana Rashidi, nakuomba hivi, kamwambie mwenyekiti wa CCM Mhe. Mwinyi aitishe wajumbe wote wa Kamati Kuu, chagueni tarehe na mahali popote Tanzania, mimi nitakuja kumsafisha Bwana Lowasa na nitagharamia mkutano huo kwa hela zangu. Kamwe msitumie hela za chama wala serikali. Monduli sitokwenda,umesikia eh?”. Mkutano ukaisha hapo Msasani. Hadi uchaguzi 1995, unafanyika na kumalizika Baba wa Taifa hakwenda Monduli. Alichukia sana tabia za Lowasa na alimfahamu kama mtu muongo na mwenye kiburi. Hadi Baba wa Taifa anafariki,sikuwahi na hata niandikapo makala hii sijasikia wala kusoma popote ambapo Lowasa anakanusha alivyolombikiza mali akiwa mtumishi wa CCM na serikali kwa muda mfupi kiasi cha kumzidi Rais wa Kwanza !!!

Sasa anatuhumiwa na vyombo vya habari kununua sehemu ya Ranchi za Taifa kwa kuandika majina ya wanafamilia! Kama hilo nalo ni kweli, ningekuwa mimi nisingeota tena kugombea URAIS n.k Tanzania. Bora kuendelea na biashara kwa uwazi kuliko kupitia mgongo au wa serikali au wa chama ( CCM). Huo ndio ushauri wangu kama mwana CCM kwa Lowassa.

Angalia tunavyofanya “total transgression of CCM regulations and ethics.” Kamati kuu 1995 ilimwona Mhe. Lowassa hana uadilifu. Mhe. Mkapa baada ya kuingia madarakani baada ya muda si mrefu sijui ni kwa kikao gain cha CCM na taasisi ipi ya serikali akamwona Lowassa ni safi na akamweka katika safu yake ya baraza la mawaziri. Huyu bwana akaendelea na huo usafi hadi akaukwaa uwaziri mkuu 2005. Yote haya yanatia shaka kama kweli ndani ya CCM na Serikali tuna benki sahihi za takwimu za mienendo kitabia ya wanachama na watumishi wetu kama si kubebana kwa majina tu! Nilinunua gazeti la mzalendo nikampa Baba wa Taifa na aliposoma kuwa Lowassa ni Waziri alimaka AHH!! Katika hili nabaki nimeduwaa hasa tunapopeana madaraka makubwa ya kuendesha nchi kimzaha tu. Tukumbuke kuwa kwa kila kitu na kwa dini yoyote Mungu huweka wazi mambo mahali na kwa muda atakao yeye.( Time and space) ya Mwalimu J.K Nyerere juu ya Lowassa tuliyapuuza. Sasa Mungu kayaanika! Basi tuone hizi tuhuma za RICHMOND n.k, Mikataba ya Madini, EPA zitakavyoshughulikiwa.

Ni huyu Lowasa leo anasema kanyimwa “Natural Justice” hakuulizwa na kamati , kaonewa, kamati ya Mwakyembe inauonea wivu uwaziri mkuu wake na ni mahiri wa kuchukizwa mikataba mibovu na kudhalilika! Oh kweli? Hivi Lowassa amewahi kusoma wasifu wa kila mmoja wa hao? Bila kupima uzito, busara na hekima ya maneno yake anasema ameachia ngazi kama alivyofanya Mhe.Alli Hassan Mwinyi, Peter Kisumo, Peter Siyovelwa n.k. Hivi CCM yetu hawa ndiyo viongozi tulio nao ngazi za juu? Wasio sema ukweli? Tukumbuke na kukiri kwa dhati wajibu wa wanachama wa CCM , katika katiba (ccm) inasema 15 (7) “ kuwa tayari kujikosoa na kukosolewa…

Watanzania wenzangu haya anayosema Lowasa yanafanana na nukuu niliyoanza nayo? Fikiria nairudia tena “For those winding and crooked courses, are the goings of the serpent, which goes basely upon the belly and not upon the feet! There is no vile that does cover a man with shame as to be found false and pertifidious” Niharakishe kusema hapa kuwa viumbe vyote ambavyo havikupenda kusema ukweli Mungu aliviadhibu kwa kuvifanya vitembelee matumbo yao milele nyoka wakiwemo! Lowasa, Mwanyika, Hosea na wenzake naomba kama nilivyoanza, tafadhali wasome hiyo nukuu mara kadhaa na waielewe na kuizingatia. Watanzania wanawashangaa, wanadharau na kuchukizwa na viongozi wasiopenda kusema ukweli kwa maisha magumu waliyo nayo ambayo wao wanawazomea kwa dharau kuwa ni wavivu na wachovu wa kufikiri. Wanasahau kuwa hawa watu wa kawaida ndio wanaozalisha kile kinacholipa mishahara na marupurupu yao. Kama viongozi wakuu wa CCM, katika hili daima kumbukeni wajibu wenu kwa mujibu wa katiba ya CCM, ibara ya 15 (4) kuwa wakati wote mkweli, mwaminifu na raia mwema wa Tanzania. Onekaneni hivyo kwa vitendo tafadhali. Utaratibu huu wa kusema uongo unadhoofisha amani na utulivu Tanzania.

Hayo niliyasema niko tayari kuyasema bungeni akiwepo Lowasa ikibidi. Hatuwezi kukubali nchi hii kuendelea kuwa na viongozi wa aina hii. WAWE WAKWELI, WASEME UKWELI TU. WANAPOKOSEA HARAKA NA KWA UKWELI NA UNYENYEKEVU WAOMBE RADHI KWENYE VYAMA VYAO, SERIKALINI NA KWA WANANCHI. NI UPUUZI WA HALI YA JUU KUJITETEA OVYO NA KUINGIZA UKABILA ( LOWASSA NA OLE NAIKO) HATA KWA MAKOSA YALIYO DHAHIRI.

Katika mahojiano na TVT Lowassa alikiri kuwa alishindwa kuvunja mkataba wa RICHMOND. Sababu alizitaja. Sawa. Waziri mkuu kama mtendaji mkuu wa Serikali, kwa mujibu wa kanuni za kudumu za utumishi wa umma ( Toleo 1994), kifungu F33, makosa yake kiserikali ni haya yafuatayo; 33( xi) omission which is against public interest. 33(xiii) negligence occasioning loss to the employer ( yaani serikali na taifa kwa ujumla). 33( xiv) gross negligence in the performance of duty. Kama mtendaji mkuu wa shughuli zote nzito za serikali bwana Lowassa hana namna ya kujitetea kwa makosa hayo yaliyodhahiri ambayo TANESCO imeendelea kudhoofishwa na RICHMOND kwa yeye kuogopa kutumia utaalam nje ya wale aliowaamini. Mbona tuna vyuo vikuu, je, aalivitumia kikamilifu? Mbona kwa maswala yasiyo na maslahi ya maana tumezoea sasa kukodi wataalam wa nje? Kwanini hakujiridhisha katika maeneo yote hayo? Tatizo hili ni kubwa sana maana watanzania sasa wanatozwa viwango vikubwa sana kulipia umeme ikiwa ni pamoja na sehemu za uzalishaji zenye kutumia umeme achilia mbali malipo ya capacity charges? Nani anabisha kuwa kwa huu mkataba wa RICHMOND n.k Bwana Lowassa na Wenzake waliweka sahihi za kifo siyo kwa TANESCO tu bali pia cha kuvuruga maendeleo ya nchi yetu na kuendeleza umasikini?

Katika yote haya ambayo yamesemwa, Bwana Lowassa na wenzake wajue kuwa kama watanzania, we have a compelling moral case for complaining against him. There is also a compelling case that is in Tanzania’s self interest. Recently many trade agreements already have made the poorest countries worse off. Such agreement already have condemned to death thousands of our people . Corporations of whatever name do strip Tanzania of its natural resources leaving behind a trail of environmental devastation etc. This is done through very poor legal frameworks. Nimuhimu tukawa na viongozi waaminifu, waadilifu na wasema ukweli. Kwa haya yanayotendeka, something is fundamentally wrong with our government. Kwa kila maamuzi tunayoyafanya mara zote tuzingatie ni kwa maslahi ya nani; yale ya Taifa ni kipaumbele cha kwanza. Tuzingatie matumizi mazuri ya rasilimali zetu daima. Duniani ziko serikali nyingi tu ambazo zimevunja mikataba mibovu. Kwa ziara nyingi ambazo viongozi wetu wanafanya na baada ya wanahabari kupigia kelele RICHMOND, kwanini Lowassa huko nje hakutaka kujifunza namna ya kuvunja mikataba mibovu? Yaani umahiri wake uliishia mkataba wa maji Dar es salaam na kiwanja cha Mnazi Mmoja? Mikakati yetu ya maendeleo imekuwa haileti tija iliyokusudiwa moja ya sababu ikiwa a flawed vision of development. Successful countries have a broader vision of what development entails and a more comprehensive strategy for bringing it about. It is very unfortunate that in the majority of developing countries Tanzania included the nation – state has been weakened thoroughly! Haya maamuzi yanayofanywa na viongozi kama Lowassa ndiyo matokeo ya kutojua namna ya kuthibiti na kutumia kwa uangalifu fursa za kitu kinaitwa UTANDAWAZI.

Government that attempt to control capital flows find themselves unable to do so, as individuals find ways of circumventing the regulations. A county may want to raise the minimum wage, but discovers it can’t, because foreign companies operating there will decide to move to a county with lower wages. Situmeona jinsi waziri Chiligati ( waziri wa kazi wa wakati huo) alivyohenyeshwa na wakubwa – wawekezaji kukataa kulipa kima cha chini hapa Tanzania? Wengine wamepunguza kazi ndugu zetu na sasa ni katika kundi la Machinga! Waziri mkuu wa wakati huo Lowassa alisaidiaje? KIMYA! Dhahiri kinachoonekana hapo ni sense of powerlessness. Kwa kukumbatia matajiri na wakubwa wa nje, kupitia utanzawazi, baadhi ya viongozi wetu kama inavyojidhihirisha kupitia RICHMOND n.k. find their ability to act eroded. These days it is the order of the day for the electorate to see its government bending before foreigners wenye (mitaji). Day in day out democracy is being systematically undermined. When the electorate shouts through the media etc, no body listens! Wanataka sifa tu. The electorate feels being thoroughly betrayed. Whether we like it or not, it is perceived, quite rightly, I think the way globalization is currently managed is not consistent with democratic principles. Little weight is given to the concerns and voices of ordinary people and the poor! Kwa kiburi cha wakubwa kutosikia, kutopenda kukosolewa Tanzania inaendelea kubaki masikini. Lowassa na wenzake wangekuwa makini na mahiri katika kusikiliza waandishi wa habari mapema RICHMOND n.k isingetufikisha tulipo sasa ambapo kila siku tunapoteza fedha nyingi. Tusingekuwa na tume juu ya tume ambazo baadhi tunazibeza kwa kejeli hata kwa kutumia chama (CCM). CCM kweli tunasoma na kuzingatia kwa vitendo wajibu wa mwanachama wa CCM kifungu 15(3) na 15 (4) na 15(7) pamoja na ahadi za mwanachama wa CCM (3) na (4), na (8). Hivi CCM sasa ni mali na jina la mtu; kwamba hivyo mtu akikosolewa hamtaki kuona kakosa na mko tayari chama kife kwa ajili ya mtu mmoja au kundi dogo tu la watu? Nendeni Butiama mtupe majibu tafadhali. Uwezo, busara na nia vyote mnavyo. Ningekuwa Lowassa Butiama nisingeenda. Yeye kwenda huko ni kejeli kwa Baba wa Taifa.

BADO TUTAENDELEA KUWASEMA WENZAO KUHUSU MIKATABA YA HOVYO NA UKWAPUAJI WA RASILIMALI ZA NCHI HII. HOJA YA MWANASHERIA MKUU WA ZANZIBAR BWANA IDD PANDU HASSAN- “ Lowasa kutostahili kuitwa Waziri mkuu Mstaafu” ni muhimu ikazingatiwa sambamba na utata wa stahili za mafao. Haitoshi kuimba utawala wa sheria na kumbe inapofika kwa wakubwa tunakunja na kunyonga sheria zetu. Sheria ni Msumeno. Someni Pensions Ordinance cap 371 sambamba na kanuni za kudumu za utumishi wa umma toleo la (1994) kifungu F53 (d) na (e). Tusiwe na kigugumizi katika hili.Tujifunze yaliyojiri hapo jirani Kenya hivi majuzi.

Namalizia kwa kusema “Tuheshimu na kudumisha kitu UKWELI”. Kwa viongozi, zingatieni na kwa unyenyekevu heshimuni viapo vyenumnapokabidhiwa madaraka. Baba wa Taifa daima katika mkoba wake alibeba Bibilia na Azimio La Arusha. Nyinyi kwa kipindi hiki kigumu cha ufisadi na kukithiri kwa rushwa na mikataba mibovu; bebeni daima photo-copy za viapo vyenu pamoja na Bibilia au Koran pamoja na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mnazo dini zenu. Sikusikia yeyote akiapa kwa dini za asili kwa Rais au kwa Spika wa Bunge.

Nawashukuru watanzania, Mhe. Spika na Waandishi wa habari ambao wamekemea maneno ya Lowasa na wenzake baada ya kikao cha Bunge.

Namshukuru sana Mhe. William H. Shelukindo, Mwenyekiti wa Kamati ya Uwekezaji na Biashara kwa kuwasilisha hoja ya kuundwa kwa kamati ya kuchunguza Richmond na shukran maalum nazitoa kwa Dr. Mwakyembe na wajumbe wote walioshughulikia suala la Richmond na kuwasilisha taarifa Bungeni kwa uadilifu mkubwa sana.

Mwisho nawashukuru Watanzania wote na nchi za nje walionipongeza na kunipa moyo kuhusu makala zangu za kukemea ukwepuaji rasilimali za nchi BoT. yenye kichwa cha habari “Salaam kwa Mawaziri” Namshukuru Rais Kikwete. Namshukuru pia Mhariri gazeti la Rai namba 748 na 749.

Halmashauri kuu ya CCM inayokutana Butiama naitakia mafanikio makubwa katika maazimio watakayofikia . baada ya hapo muonekane mmedhamiria kutenda kwa kuleta maendeleo yenye kuzingatia uadilifu na uwajibikaji . viongozi wabovu wawajibishwe tu. Watanzania wengi leo bado wanamlilia Mwalimu J.K. Nyerere hasa kwa matatizo kama haya ya mikataba mibovu ya Madini, RICHMOND n.k. Wanasema sorry Mwalimu lived ahead of his time. Alituangazia kwa mengi, hakuna wa kutu tetea leo kwa matatizo yote haya.

Mungu Ibariki Tanzania. Mungu Ibariki Africa.

Samwel. H. Kasori
Katibu mstaafu wa
J.K.Nyerere
0754 372141



.............................LOWASA .........EDWARD..........NGOYAYE..........JAMBAZI SUGU LA TANZANIA!!..
 
Kumbuka haya maneno uliyoyaandika hapa. Kwamba hata kama magamba watatumia rushwa kuingia madarakani basi ndio washindi halali. Maneno haya kamwe hayawezi kuandikwa na mtu ambaye anaitakia mema nchi yetu. Mtu huyu yuko tayari kuona uchaguzi unavurugwa ili chama fulani kishinde na bado akayaita matokeo ya uchaguzi huo uliojaa rushwa kila kona ya nchi na wizi wa kura kuanzia chaguzi za Wabunge mpaka Rais ni matokeo halali. Eti Mzalendo halisi ambaye hana chama bali anatetea maslahi ya nchi!!!! Aibika Pasco!!!! Wengi tumeshakustukia siku nyingi tu.

Mkuu BAK, lengo la tendo la ndoa kwa mujibu wa mafundisho yote ya dini zote na jamii zote, was ment lifanywe ndani ya ndoa!. Lakini kabla tendo hilo halijafanyika, lazima kwanza umtafute umpendae, umpende, umpose, ndoa ifungwe ndipo ufaidi matunda ya ndoa!.

Hivyo hata kama CCM, walichakachua, walidanganya, walihonga, waliiba na kufanya kila mbinu, anayetangazwa na tume kuwa ndiye mshindi, anakuwa ni "mshindi halali"
.



Mkuu BAK, hili la njaa, nakubaliana na wewe, ni kweli njaa mbaya!. Ila pia nasisitiza kuwa niko kwa maslahi ya taifa na nina tatizo moja kubwa!, wengi humu jf ni wishful thinkers!, mimi ni realist, nikisema ukweli daima, no matter how ukweli huo ni mchungu, siupaki siagi na jam ili uwe mtamu!.
  1. Jee ni uongo kuwa Watanzania ndio wanaipenda rushwa na kuikumbatia?!.
  2. Jee kuna ubishi kuwa Watanzania walio wengi ni masikini wa kutupwa?!.
  3. Jee ni uongo kuwa rushwa its the order of the day kwenye uchaguzi wa CCM?!
  4. Jee ni uongo kuwa JK did nothing kuhusu rushwa ndani ya CCM zaidi ya kuelezea kukerwa kwake?!.
  5. Jee ni uongo kuwa wanaogaiwa pesa za rushwa, wanazifurahia na kumpigia kura mtoaji?!.
  6. Jee ni uongo kuwa hicho ndicho Wapiga kura wa Tanzania wanachokitaka?!.
  7. Jee ni uongo kuwa serikali ya CCM imetenga Sh. Bilioni 400 za ruzuku ambazo watazigawa kwa wananchi?!.
  8. Jee wananchi hao baada ya kugaiwa fedha hizo, hawataishukuru serikali yao kwa kuwajali?!.
  9. Jee shukrani hizo hazitakuwa reflected kwenye matokeo ya uchaguzi wa 2015?!.
  10. Jee ni uongo kuwa mimi nina waandaa members humu kwa ushindi wa CCM, 2015 ambao ndio reality hivyo kujikuta wako tayari wameandaliwa kisaokolojia kukubali matokeo!, kuliko kuwaacha wakiwa na "wishful thinking" za "great expectations kuwa 2015 mambo yatabadilika", na ikitokea mambo yake yale, watu wale wale, na chama kile kile, si wangeishia kwenye despair, frustrustion na psychoilogigal depression?!.

Kama hoja zozote kati ya hizo ni uongo, then nipinge kwa hoja na sio kuniita "mganga njaa" tuu!.
P.
 
Lowassa ndio mtu msafi kuliko wote barani africa!!! tapikeni basi!!!
na ndio Rais wa Tanzania wa Sasa na Baadae.
 
Kuna sababu kwa nini Bw.Lowasa anautaka Uraisi wa TZ kwa udi na uvumba hata baada ya kuengeuliwa na Chama chake bado hakubali na anakitaka Cheo hicho hata kupitia nje ya Chama hicho!

Sasa swali hapa ni Kwa nini?


Ni nini hasa kinamsukuma Bw.Lowasa kuutaka Uraisi kwa nguvu zote! Sababu kubwa ni moja tu, Mali!
Bw.Lowasa na marafiki zake wana madhambi makubwa sana na hivyo raisi ajaye ni lazima (waonavyo wao) atoke kwenye kundi lao ili awalinde wao na mali zao!

Na kama hili likitokea basi tujue ya kwamba TanZania yetu kama tuijuavyo itakuwa imebadilka kabisa na kuwa jamaii nyingine tofauti kwani hawa akina Lowasa, Rostam &Co. hawatakubali tena kuachia madaraka kwa watu wengine na watajenga tabaka moja tu la matajiri na Watawala na sisi wengine tutaishia kuwa Watumwa kwa Miaka 100 ijayo!

Hivyo wote Watz tuipongeze CCM kwa kuliona hili na kumzuia huyu Jamaa na genge la wezi wenzake kushika nafasi hiyo kubwa hapa nchini na nawasihi wana CHADEMA kama Bw.Lowasa na genge lake wakihamia kwenu basi kitoseni CHADEMA kwani mwisho wenu hautakuwa mzuri na mtatamani siku moja hata mrudi kwenye TanZania ya zamani ambayo itakuwa imekwishatoweka!!
 
Nyie wenyewe Ccm genge tu la walanguz n wanyan'ganyi kwan mnalipi jipya mlilofanya au kupitisha mikataba y gas n mafuta haraka msitufanye watto hii nchi cyo yenu peke yenu n watto wenu shwain kabisa
 
Back
Top Bottom